Nyanya ipi hybrid isiyo na bei gali lakini inafanya vizuri shambani?

Thesi

JF-Expert Member
Aug 8, 2010
997
282
Habari ya asubuhi ndugu zangu. Ninahitaji mbegu ya nyanya isiyo na bei ghali lakini inafanya vizuri na kutoa mazao bora.

Moja ya changamoto kubwa ya wakulima wa nyanya sasa hivi ni bei kubwa ya mbegu. Kampuni zinazozalisha mbegu sasa hivi zikiona mbegu yao inafanya vizuri tu wanaacha kuziweka kwenye package za uzito (gram/kg) na kuziuza kwa hesabu ya mbegu.

Wanauza mbegu 500 kwa Tsh. 30,000.00 mpaka 40,000.
Kwa mkulima anayetaka kulima kuanzia ekari 1 inayochukua miche kuanzia 12,000 ni changamoto kubwa sana kununua mbegu hizi. Kama unalima ekari 2 pesa ya mbegu tu unatakiwa kuandaa kuanzia Tsh.1,500,000.00 kwa ajili ye mbegu tu bado gharama zingine.

Naomba wale ambao wamelima mbegu tofauti za hybrid watupe uzoefu wao wa mbegu zinazofanya vizuri lakini hazina bein ghali sana.

Mbegu kama Kipato F1 inafanya vizuri katika mbegu zisizokuwa ghali lakini kuna uwezekano kuna mbegu uliyolima ikafanya vizuri ukaifurahia inaweza kuwa bora zaidi.
Karibuni.
 
Daaahhh, huu uzi ungekuwa ungekuwa kwenye jukwaa pendwa ungekuwa n kurasa hata mia
 
Unajua mbegu ya nyanya inaitwa Assila?, hii ndo mbegu iliyo ghali zaidi katika list ya mbegu za nyanya. Sasa kwa kuptia kampuni ya East West wamekuja na mbegu yenye character kama za Assila inaitwa IMARA F1 lakini wamepooza bei iko vizuri inakupa kitu unachotaka kwa gharama nafuu 25g kwa sh 130,000 tu! Kumbuka pia hiyo 25g inatosha one acre. Ukiitaji just nicheki tu!
 
Unajua mbegu ya nyanya inaitwa Assila?, hii ndo mbegu iliyo ghali zaidi katika list ya mbegu za nyanya. Sasa kwa kuptia kampuni ya East West wamekuja na mbegu yenye character kama za Assila inaitwa IMARA F1 lakini wamepooza bei iko vizuri inakupa kitu unachotaka kwa gharama nafuu 25g kwa sh 130,000 tu! Kumbuka pia hiyo 25g inatosha one acre. Ukiitaji just nicheki tu!
Mbegu ghali hapa nchini ni jarrah
 
Unajua mbegu ya nyanya inaitwa Assila?, hii ndo mbegu iliyo ghali zaidi katika list ya mbegu za nyanya. Sasa kwa kuptia kampuni ya East West wamekuja na mbegu yenye character kama za Assila inaitwa IMARA F1 lakini wamepooza bei iko vizuri inakupa kitu unachotaka kwa gharama nafuu 25g kwa sh 130,000 tu! Kumbuka pia hiyo 25g inatosha one acre. Ukiitaji just nicheki tu!
Upo wap Kaka.
 
Unajua mbegu ya nyanya inaitwa Assila?, hii ndo mbegu iliyo ghali zaidi katika list ya mbegu za nyanya. Sasa kwa kuptia kampuni ya East West wamekuja na mbegu yenye character kama za Assila inaitwa IMARA F1 lakini wamepooza bei iko vizuri inakupa kitu unachotaka kwa gharama nafuu 25g kwa sh 130,000 tu! Kumbuka pia hiyo 25g inatosha one acre. Ukiitaji just nicheki tu!
tunaomba mawasiliano plz kama unaweza nitumie inbox
 
Niliwahi kuishi kijiji fulani cha wakulima wa nyannya. Walichokuwa wanafanya ni kukamua mbegu kutoka nyanya walizolima, na maisha yalikuwa tanaendelea sikuwahi ona wanaenda dukani.
Kampuni zinapropaganda kubwa ya kuwakataza wakulima wasitumie mbegu mara mbili mi naona kama ujanja tu ili waendelee kuuza mbegu zao.
Juzi nimekutana na mkulima wa vitunguu amenielekeza A-Z jinsi ya kupata mbegu, anajiandalia mbegu na hio mbegu amepata junia 110 kwa heka.
Hebu tujaribu njia mbadala ndugu zangu hasa kama huna mtaji wa kununua mbegu dukani.
 
Niliwahi kuishi kijiji fulani cha wakulima wa nyannya. Walichokuwa wanafanya ni kukamua mbegu kutoka nyanya walizolima, na maisha yalikuwa tanaendelea sikuwahi ona wanaenda dukani.
Kampuni zinapropaganda kubwa ya kuwakataza wakulima wasitumie mbegu mara mbili mi naona kama ujanja tu ili waendelee kuuza mbegu zao.
Juzi nimekutana na mkulima wa vitunguu amenielekeza A-Z jinsi ya kupata mbegu, anajiandalia mbegu na hio mbegu amepata junia 110 kwa heka.
Hebu tujaribu njia mbadala ndugu zangu hasa kama huna mtaji wa kununua mbegu dukani.
Hizo mbegu za hybrid wakulima wanakamua na kulima hizo hizo ni zinaiva vizuri tu bila shida Kama zikipata samadi ya kutosha hakun shida yoyote.
 
Back
Top Bottom