Nyalandu: Ripoti ya Lembeli uongo mtupu

Nyalandu: Ripoti ya Lembeli uongo mtupu

Cv yake tafadhali

Anamiliki kampuni ya utalii na vitalu vya uwindaji! Hapo mwanzo ilisemekana walikuwa hawakai zizi moja na bosi wake Kagasheki kwani walikuwa wakitoa lugha gongana kuhusu wizara yao! Ni mkali kwa totoz kwani jiko lake ni matunda ya uncle Lundenga! Ni miongoni mwa wanaotaka kukaa mahali patakatifu a.k.a Ikulu!
 
Awajibishwe lembeli kama unacho sema ww nyalandu ni cha kweli.ila kama lembeli alichosema ni kweli basi ww nyalandu uwajibike kwa kusema uongo.
 
huyu nyalandu kwani akwepo bungeni mpaka hayaseme hayo nje ya bunge kwani yeye awajui wanao wauwa tembo mbona pembe zilikamatwa zanzibar kesi aijaenda mahakamani na wachina wanaokamatwa awaruswa kuwataja aliyewapa huu ni usani wa serekali hivyo nyalandu asijifanye anapotosha watu wakati anajua kila kitu
 
kapalamsenga

Uko sahihi mkuu ila nadhani naibu waziri huyu alitakiwa aseme ina mapungufu badala ya kusema ni uongo mtupu.
Inawezekana Lembeli akawalinda wenzake kama alivyofanya Hosea wa akukuru kwenye issue ya richmond
lakini hapa mh.lazaro hakutakiwa kusema kuwa ni uongo bali alitakiwa ajazie pale penye mapungufu kama kweli yeye ni mkweli.

Nyalandu Mimi simuelewagi kwakweli....,kwa nini hakusimama kumtetea waziri wake? Na Badala ya kumtetea akanza kampeni Za kuupata uwaziri Kamiki.....Sasa news in circle zinaposema kuwa uwaziri wa utalii anapewa..Lembeli Ndio Anaanzisha kampeni dhidi yake? Tumueleweje...
 
Last edited by a moderator:
Anamiliki kampuni ya utalii na vitalu vya uwindaji! Hapo mwanzo ilisemekana walikuwa hawakai zizi moja na bosi wake Kagasheki kwani walikuwa wakitoa lugha gongana kuhusu wizara yao! Ni mkali kwa totoz kwani jiko lake ni matunda ya uncle Lundenga! Ni miongoni mwa wanaotaka kukaa mahali patakatifu a.k.a Ikulu!

Alikuwa pia hapatani na waziri wake alipokuwa wizara ya viwanda...he has always wanted to be a full minister...na hata akiupata labda asiwe na Naibu ..ni one man show type
 
Wakati inasomwa hiyo ripori Nyalandu hakuwepo Bungeni?
Mbona hakunyanyuka kuyasema hayo?
watu wengine ni wanafki.!!!

ana mfariji kagasheki kwamba , eee bwana!!!! zile dili zako mimi nitaendeleza tu mzee usihofu tupo pamoja . sabuni haisafishiki . eti hawa ndiyo wasomi . naamini sasa aliyoandika mmbwambo katika raia mwema iliyopita , hata baraza la mawaziri lipanguliwe hakuna jipya madam ni chama kile kile.
 
Kwa watu makini hii kauli ya Nyalandu ni unafiki uliopitiliza.Hivi huyu Nyalandu alikuwa wapi wakti Kamati ya Lembeli ikifanya uchunguzi hadi kuwasilisha ripoti yake Bungeni?
'
Nyalandu alikuwa wapi wakti watu wakiteswa,kupigwa,kubakwa,kuporwa mali zao na wengine kuuawa?Alikuwa wapi huyu kibuyu?Hivi kuna haki gani ya kumwajibisha Waziri peke yake na kumwacha Naibu wake kwenye Wizara iliyokumbwa na kashfa
???Nyalandu anatakiwa amfuate Kagasheki kwa kujiuzulu au Rais atengue Unaibu wake!
 
Wajanja wajanja wa mjini na wapiga deal ndo wenye kuongoza maamuzi ya serikali. Who is Nyalandu,? Katokea wapi mpaka kufikia hapo alipo? Ni nani aliye nyuma yake? Na, je Ni juhudi zipi anafanya kujipatia nafasi anazozitafuta? Mimi sijui, ila nahisi naye Ni JANGA la Taifa.

Naona anataka kutumia fursa ya unaibu aonekane anachapa kazi kumbe nguvu ya soda, Yeye anashutumiwa pia kumiliki vitalu vya uwindaji wakati ni naibu waziri hapo tayari kuna mgongano wa maslahi. Nadhani naye aondoke tu
 
Nyalandu alishaunda tume yake ambayo imebaini uongo wa ripoti ya tume ya bunge? Tume ya Rais haijaanza kazi huo uongo umebainika vipi? Ukiona kauli za namna hii zinaanza kutolewa jua kuwa mkakati wa kuficha ukweli na kuharibu ushahidi uko kazini. Usishangae wale waliobakwa pamoja na jamaa zao ama wakapewa fedha wakane ukweli au wakatoweka katika mazingira ya kutatanisha!Yaana wanahangaikia sifa ya nchi kwenye macho ya ulimwengu na sio kuhangaikia haki na usalama wa raia. Eti sifa ya nchi imeshuka kiutawala bora, kwani imeshuka leo? Tumuize Dr Ulimboka.
 
Mwandishi wa habari hii hakutimiza kazi yake vizuri. Labda alikuwa na maslahi binafsi na Nyalandu. Nilitegemea baada ya kusikia toka kwa Nyalandu angewasiliana na uongozi wa bunge au Lembeli mwenyewe ili kupata maelezo yake.

Jina la gazeti lenyewe sasa! "Chagadema Daima"
 
Yaani Kusema Ukweli Katika Mawaziri Na Manaibu Waziri Nyalandu Huwa Ni Mkweli Sana. Jamaa Atakuwa Sahihi Ila Tatizo Ni Heading Ilivyokuja.
 
Nyalandu: Ripoti ya Lembeli uongo mtupu

nyalandu1-300x169.jpg


NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, ameilalamikia Kamati ya Bunge ya Ardhi, Mazingira na Maliasili iliyoongozwa na James Lembeli kuwa taarifa iliyowasilisha bungeni na kuwang’oa mawaziri wanne ilikuwa ya uongo.

Nyalandu alitoa kauli hiyo juzi alipozungumza na viongozi wa taaluma mbalimbali pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dodoma na Manyara juu ya mgogoro wa mipaka kati ya hifadhi ya taifa ya Tarangire, Pori la Akiba Nkungunero na vijiji vya jirani uliofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara.

Alieleza kutokana na taarifa hiyo Tanzania kwa sasa imeonekana kushuka kwa kiwango kikubwa katika utawala bora ikiwa ni pamoja na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Alisema kuna taarifa ambazo zilionyesha kuwa wapo watu ambao walibakwa jambo ambalo halikuwa la kweli.

Hata hivyo, alisema kwa sasa Rais Jakaya Kikwete amekubali kuunda tume ya kimahakama ambayo itafanya uchunguzi juu ya kuwepo kwa matukio hayo na itakapabainisha kuwa kuna watu walipotosha ni wazi watachukuliwa hatua kali za kisheria bila kujali cheo cha mtu ambaye alihusika na uongo au ukiukwaji wa sheria.

Katika hatua nyingine, Nyalandu ametangaza kumsimamisha kazi ofisa wanyamapori mwandamizi katika pori la akiba la Maswa, Lawrence Kileo, kwa kutuhumiwa kupokea rushwa na kuwatoza faini wafugaji bila kuzingatia taratibu.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku chache tangu atangaze kusimamishwa kazi kwa watumishi 22 wa wizara hiyo.

Ofisa huyo anatuhumiwa kuwatoza faini wafugaji wanaoingiza mifugo yao katika pori hilo bila kutoa risiti za serikali, na hivyo fedha hizo kujinufaisha mwenyewe kinyume cha kifungu cha sheria namba 116[2]C cha sheria ya kuhifadhi wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009.

Nyalandu ametangaza kuanza kwa uchunguzi kwa Ofisa Wanyamapori wa Wilaya ya Kasulu, Benjamini Mkosamali, kabla ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa kuwaruhusu watuhumiwa wa ujangili kuondoka na nyara za serikali walizokamatwa nazo kabla ya kukamatwa tena kwa msaada wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Nyalandu alisisitiza kuwa serikali itaendelea kuchukua hatua zaidi kwa maofisa wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vyovyote vile vya kukiuka maadili ya kazi yao.

Watuhumiwa hao wa ujangili mkoani Kigoma ambao walikamatwa wakiwa wamebeba wanyama aina ya tohe 12, madume watano na majike saba wakiwa pia na insha wanne aina ya Oribi ambao hawakupaswa kuwinda kwa mujibu wa leseni yao ya uwindaji namba B59921 iliyotolewa Kigoma.

Alisema awali watuhumiwa hao walikamtwa na kikosi cha doria cha Kampuni ya Friedkin Conservation Fund na kumuita ofisa huyo kwa ajili ya kuchukua hatua zaidi ambapo alipofika na kuzungumza na watuhumiwa aliwaruhusu kuondoka na wanyama hao.

Nyalandu alisema Benjamini akiwa na taaluma ya kusimamia wanyamapori huku akifahamu majangili waliokamatwa wamekutwa na nyara za serikali na wamekutwa katika kitalu cha uwindaji sehemu ya Kibenge, baada ya kupata taarifa kwa wahusika, aliamua kwa makusudi kuwaruhusu majangili hao kuondoka.

“Hivyo nimeagiza mamlaka husika kukamilisha uchunguzi na kumchukulia hatua za kinidhamu na za kisheria haraka sana ofisa huyo,” alisema Nyalandu.

Alisema kuwa vita dhidi ya ujangili itaendelea kwa kasi na hata rais ameishaahidi kuwa operesheni ujangili awamu ya pili itarejea hivi karibuni baada ya kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika awamu iliyomalizika.

Alifafanua kuwa kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita baada ya kusitishwa kwa operesheni hiyo, tembo 60 waliuawa na majangili hao kitendo ambacho hakitakiwi kuvumiliwa.

Source:
Tanzania Daima (Tanzania Daima – Nyalandu: Ripoti ya Lembeli uongo mtupu)
Naona huyu jamaa ana kichwa cha panzi. Alishindwa kuyasema bungeni hadi watu wanawajibika. Kwanini aseme leo kuwa ulikuwa ni uongo? S
 
Hivi majuzi Naibu Waziri wizara ya Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alisema ripoti ya Operesheni Tokomeza Ujangili iliyowang’oa mawaziri wanne ilikuwa ya uongo. Nyalandu anadaiwa kutoa kauli hiyo alipozungumza na viongozi wa taaluma mbalimbali na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dodoma na Manyara kuhusu mgogoro wa mipaka kati wanavijiji na Hifadhi ya Tarangire.





Nyalandu alikaririwa akisema kutokana na taarifa hiyo kueleza wapo watu waliobakwa wakati siyo kweli. Tanzania imeonekana kushuka kwa kiwango kikubwa katika utawala bora kutokana na ukiukwaji haki za binadamu.

Kutokana na kauli hii ni wazi kuwa Nyalandu amemdhalilisha mheshimiwa Rais wa Jamhuri na anapaswa kumuomba radhi haraka sana na ikiwa ni pamoja na kufuta kauli yake kwa Umma. Nyalandu anataka kuuambia Umma kuwa mheshimiwa Rais alikurupuka kufanya maamuzi ya kuwatimua mawaziri wanne waliotuhumiwa katika ripoti hiyo.

Ikumbukwe ni Nyalandu huyuhuyu ndiye aliyesababisha Waziri wake Omari Nundu kuvuliwa Uwaziri yeye alipokuwa Naibu wake wizara ya Viwanda. Ni hatari sana kuwa na watu aina ya Nyalandu wanaotaka madaraka kwa kuwaharibia maboss wao ili wao waonekana wazuri.
 
Hili suala linapaswa kuchukuliwa kwa umakini sana. Ukweli ni kwamba watanzania tunasifa ya kusema uongo na si kwa nyalandu pekee. Vipi kuhusu zile cd za Mbowe kuhusu bomu la Soweto?
 
Hili suala linapaswa kuchukuliwa kwa umakini sana. Ukweli ni kwamba watanzania tunasifa ya kusema uongo na si kwa nyalandu pekee. Vipi kuhusu zile cd za Mbowe kuhusu bomu la Soweto?

Ungekuwa wa kike, mbowe angeshakuchumbia, watu wanajadili hili wewe unakuja na mbowe... shame
 
Kabla ya kuendeleaa na hii mada hebu tuambie ni lini Omary Nundu aliwahi kuwa Waziri waa viwanda na biashara???????
 
Halafu alituambia eti wamarekani wanampendekeza awe Rais ajae wa Jamuhuri. Sijui ni wabebabox wa wapi hao walimpamba hlvyo.
 
Back
Top Bottom