Nyalandu: Ripoti ya Lembeli uongo mtupu

Nyalandu: Ripoti ya Lembeli uongo mtupu

Kama ni kweli ametamka au kuonyesha wasiwasi huo, basi namuunga mkono Nyalandu kwenye hili.

Na sijui ni kwa nini wengi mnakimbilia kumshutumu yeye ili tu ibaki kuwa kuna ukiukwaji wa haki za biinadamu wa kiwango kile ulifanyika....mnanufaika na nini ripoti ikiwa vile ?...na hata kama kuna ukiukwaji (siwezi kuwaamini watendaji wote kwa asilimia mia moja) lakini kwa ripoti ilivyo nadhani imepitiliza.

Ni uwezo gani wa ki taaluma ambao walikuwa nao wanakamati kuweza kuwahoji wahanga na kuridhika kwa yale wanayoongea ?

Watanzania tuna asili na vipaji vya kuzusha na kuongea uongo na tuna mifano lukuki.... ni juzi tu tumeambiwa kwamba samaki ameingia tumboni.....tuliwahi kuambiwa kuna mtu kageuka chatu.....tumewahi kusikia eti mbwa kazaa watoto wa nguruwe...ni wanainchi haohao ukipiga mbinja kijijini au mtaani kwamba bibi fulani ni mchawi watakupa ushirikiano wa hali ya juu wa kumuangamiza kikatili...ukiwaambia kuna babu anatibu ukimwi nchi nzima inahamia huko bila hata kujiuliza mara mbili n.k.

Ni wabongo nyie nyie mnaojitahidi kuiaminisha jamii kuwa mashahidi waliopelekea babu Seya kufungwa walipikwa...iweje kwenye hili uwezekano huo mmeutupilia mbali na wala hamtaki kusikia ? kuna nini hapa ?

Nitafurahi sana nikisikia kutoka kwa wale wote walioshiriki kwenye zoezi hili nao wakitoa maelezo yao....najua hawatokosekana waliokiuka maadili ya kazi lakini kamwe si kwa kiwango hiki.

Twajua kuna NGO zinazonufaika kwa uwepo wa sintofahamu hizi kwani wameshapeleka ripoti kwa wakubwa na wasingependa ipatikane ripoti tofauti na ile.
 
LEMBELI ALIDANGANYA KWA FAIDA YA NANI? jE YEYE NI JANG-HIL LA TEMBO?

Lembeli au kamati kama wanasiasa wengine walikwenda kutenda hii kazi wakiwa tayari na majibu waliyoyatarajia...na waliamini kuwa ripoti itakapokuja kama shutuma zilivyokuwa zimeanza basi ishu nzima na kamati husika itakuwa HIT.

Ni sawa na wanahabari wetu wanapoenda kumuhoji muhanga wa kuunguliwa duka moto..utamsikia anasema ana mikopo ya benki ili hali siku kadhaa nyuma ni huyohuyo alikuwa analalamikia ukosefu wa mikopo.
 
Nadhani wanataka kutujuza kuwa deal la kuua tembo na kuuza meno yake huwa limepangwa,
tujiulize kipindi meghji akiwa waziri wa wizara hii magogo ya miti ya asili iliyokamatwa kwa jina lake iliishia wapi!
 
Wakati inasomwa hiyo ripori Nyalandu hakuwepo Bungeni?
Mbona hakunyanyuka kuyasema hayo?
watu wengine ni wanafki.!!!

Sidhani kama kuna uwongo kwenye ripoti hiyo,ila ni njia ya kujaribu kujiosha taka.namuone huruma sana kwani wakati wa kuwadanganya watanzania umekwisha.Pili viongozi wa serikali hawapendi kuambiwa ukweli na pia hawapendi kuona serikali inatupiwa mawe na ukweli ukajulikana.

Nyalandu nae anatakiwa awe ameshaachia ngazi nashangaa anasubiri nini kwa sababu nae alikuwa ni kiongozi kwenye wizara ya maliasili.

Tangu apewe kukaimu, dogo anadhani ndo muda wa kuinua jina ili apewe Wizara. Lakini kiufahamu, hata yeye ni out. Waziri hawezi kutenda hovyo, yeye akawa nyota. Labdabkwa uzembe wa mteuaji.

Kila siku anaropoka jipya! Ngoja tusubiri kujikomba kwake.
 
Wajanja wajanja wa mjini na wapiga deal ndo wenye kuongoza maamuzi ya serikali. Who is Nyalandu,? Katokea wapi mpaka kufikia hapo alipo? Ni nani aliye nyuma yake? Na, je Ni juhudi zipi anafanya kujipatia nafasi anazozitafuta? Mimi sijui, ila nahisi naye Ni JANGA la Taifa.

Naye misheni town tu! Elimu fake ya chuo cha US. Kajidai kunyoosha shule kwa kupitia shirika la dini akipozi kama mulokole fulani. Kumbe fake tupu!
 
Sijawahi kumkubali huyu mtu na.kama ni madaraka anapata ya uteuzi! !!!!!!
Hii nchi ina taabu sana na viongozi hawa!!!!!

Anaongea leo as if kaletwa na mafuriko hivi kazi tarajiwa haifanyiki basi hata kuheshimu ufahamu wetu pia ni ngumu????!!!!
Sawa kaka,nyalandu ni opotunist na fisadi wa kati,huyu kule singida kaskazini kwa umaskini wao wanamuona wa maana.Hana personality na uongozi
 
kwani nyarandu yeye anaona wananchi kunyanyaswa? au ndo anataka full uwaziri?
 
Tangu apewe kukaimu, dogo anadhani ndo muda wa kuinua jina ili apewe Wizara. Lakini kiufahamu, hata yeye ni out. Waziri hawezi kutenda hovyo, yeye akawa nyota. Labdabkwa uzembe wa mteuaji.
Kila siku anaropoka jipya! Ngoja tusubiri kujikomba kwake.

Usije ukapata stroke ndugu yangu,chochote chawezekana kwenye siasa ya nchi yetu.Mzembe,mwizi,mla rushwa na fisadi ndiyo nguzo kuu za uongozi,so usijeshangaa.
 
Lazima wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Mazingira na Maliasili wakiongozwa na James Lembeli wachukuliwe hatua za kinidhamu ili kukomesha tabia ya kudanganya umma na kuleta uchochezi kwa viongozi. Wajumbe hao pamoja na wabunge wengine yaonyesha walikuwa na maslahi binafsi
 
nlivyosikia anamsalandia faraja kota nikajua kumbe na yeye ni mtu wa mabebez kama le big show!

kazi yake ni kujibu maswali mjengonitu, anatafuta uwaziri huyo hana lolote mbona hakuomba mwongozo kama lukuvi. Nimeipenda hiyo ya mtu wamabebez wakaleee kama le mutuz ha ha ha
 
Yaan vile nlikuwa namheshimu sikutegemea aongee huu upuuzi...
 
huyo tangu ile tuhuma ya mke wake faraja kota kugawa rushwa jimboni kwa jina la mkopo , simwamini kwa lolote .
 
Sipati picha wizara inapokuwa mbovu na matatizo kibao kisha uniambie eti waziri peke yake ndo alikuwa mbovu, hawakushirikiana na naibu wake, katibu wa wizara je? They are all party and percel of rubbish!!!
 
Tembo 60 wameshauawa baada ya kusitishwa operesheni? ... ina maana basi hizi operesheni hazina umuhimu kwa kuwa zikiisha tu, kazi inaendelea.
 
Amuulize Bosi wake?Mi nashangaa kwanini bado yupo!kwani wizara zao si zimetenguliwa na JK....wanajifanya hamnazo

Lembeli akipewa kazi anafanya kazi hana muda wa kumpamba mtu hata mh. Maige alisema kaonewa lakini ukweli haukubadilika simshangai Lazaro kusema hivyo, hata hivyo kazi hiyo hakuifanya Lembeli peke yake Mzee Shekifu Henry ni mmoja wa wajumbe hao waseme uwongo kwa kumkomoa nani? Wananchi ndiyo waliotendewa hayo.
 
Unakamata wawinda panya buku na digidigi unatarajia tukusifie unafanya kazi.., wakati tembo 60 wametolewa meno hujakamata hata jangili mmoja.

S.t.u.p.i.d.i.t.y
 
Mwandishi wa habari hii hakutimiza kazi yake vizuri. Labda alikuwa na maslahi binafsi na Nyalandu. Nilitegemea baada ya kusikia toka kwa Nyalandu angewasiliana na uongozi wa bunge au Lembeli mwenyewe ili kupata maelezo yake.
 
Back
Top Bottom