Nyalandu nisiyemfahamu

Nyalandu nisiyemfahamu

Mimi binafsi siomfuasi WA nyalandu ila kwahili nampongeza sana kaonyesha uzalendo(utu)kupita ninavyomfahamu
 
Nachelea kutoa pongezi, bora tu nitoe.

Nyalandu ni Mbunge wangu toka 2000 hadi sasa,

Mengine ya jimboni kwake ambayo ni madogo au makubwa yanasikitisha sana.

Sitaki kuyasema humu bali nawapeni uwanja msifie.

NB: Si kila furushi(robota) kubwa la nguo lililopambwa kwa kila aina ya pambo juu ndani yake lina nguo nzuri, mengine unawezakukuta ni midoli
 
Nimemsifia kwa makubwa ambayo wewe hukuyaona,nikosoe kwa kufukuwa nisiyoyajua lakini yawe KATIKA HILI.

Habeeb Marhan

Habeeb anayemponda Nyalandu katika hili msamehe bure. Laiti mngelijua ushiriki wa Nyalandu katika hili. Lakini Kama sifa au kama mnavyoita kutafuta Kiki zinatafutwa kwa kufanya alichofanya Nyalandu basi ameipata na jamii inamkubali.
 
Kafanya kazi kubwa ipi...!?

Tuelezee sio wote wanafahamu...!
Mengi amefanya kupitia Mgongo wa Serikali na Wahanga wenyewe wa Ajali, hivi ni nani angeshindwa kufanya aliyo yafanya....!?

Au ni kwa kuwa yeye aliwahi tu....!!?

Anyway.....PONGEZI NYALANDU..

Sent using Jamii Forums mobile app

Ungekuja huku Arusha na hizi pumba zako tungekugombea kama mpira wa kona. Better to shut up ur mouth than opening it and talk rubbish
 
Habeeb anayemponda Nyalandu katika hili msamehe bure. Laiti mngelijua ushiriki wa Nyalandu katika hili. Lakini Kama sifa au kama mnavyoita kutafuta Kiki zinatafutwa kwa kufanya alichofanya Nyalandu basi ameipata na jamii inamkubali.
Sifa za utendaji mzuri unaoondoa shida za jamii ndiyo miongoni mwa sifa za kiongozi wa watu,sifa bora kwa mabadiliko na maendeleo ya watu.

Habeeb Marhan
 
Hivi bado ni waziri yule?
Hapana,ila bado ni mbunge kama si wa Singida mjini basi maeneo ya Iramba huko,ila nafikiri pia Mwigulu ni Iramba,sijui kama kuna kanda za mashariki na maghari ila najua ni mbunge.

Habeeb Marhan
 
Mimi binafsi siomfuasi WA nyalandu ila kwahili nampongeza sana kaonyesha uzalendo(utu)kupita ninavyomfahamu
Mimi pia kama wewe,ila namsifu kwa mfululizo wa matukio.
Hata kuwa bize kufuatilia na kutujuza maendeleo ya vijana wetu si dogo,wangapi wanaandika ngono tu humu na mitandao mingine?

Habeeb Marhan
 
Salamu za jumapili kwa kila atakayesoma.

Nimeona nimpongeze Nyalandu kwa moyo wa dhati sana katika msaada kwa watoto walionusurika katika ajali ya LUCKY VICENT.

Mtaani watu wanaongea kama Nyalandu anatafuta sifa au mtaji wa kisiasa kwa jinsi alivyokuwa mstari wa mbele kusaidia matibabu kwa watoto walionusurika.

Mimi namtazama kama mtu mwenye huruma sana,mzazi mwenye uchungu,kiongozi asiye mbinafsi.Tukio halikutokra jimboni kwake lakini hakujali hilo,hapo anatafutaje kiki ya kisiasa?

Wapo wenye uwezo wa kuleta tofauti katika jamii kwa ushawushi wao tu(influence)lakini pasipo na jambo linalowaubganisha moja kwa moja huwa hawajitoi kufanya lolote,naamini NYALANDU angekuwa mbinafsi basi angekaa kimya tu,uwezo wa kula Jodari anao lakini hakuacha kufanya analoweza.

Hakufanya kwa maslahi ya kifedha,zaidi naamini atajuwa katika eneo fulani ametumia fedha zake,lakini wapo walionufaika na tukio lile.
Tuwatie moyo wenye moyo wa kujitolea,haki yake kumsifu kwa hili.
Naomba tumsifu pamoja,si lazima tueaze sawa,munaweza pia kuwaza muonavyo.

Habeeb Marhan

Umefanya kazi vizuri kwa weledi, umepata bei gani?
 
Nachelea kutoa pongezi, bora tu nitoe.

Nyalandu ni Mbunge wangu toka 2000 hadi sasa,

Mengine ya jimboni kwake ambayo ni madogo au makubwa yanasikitisha sana.

Sitaki kuyasema humu bali nawapeni uwanja msifie.

NB: Si kila furushi(robota) kubwa la nguo lililopambwa kwa kila aina ya pambo juu ndani yake lina nguo nzuri, mengine unawezakukuta ni midoli
Hakuna mwanadamu aliyemkamilifu kama mungu,na hatatokea.
Mitume walikuea ni wakosaji kwa mungu japo wao ndiyo tulikuwa tunawaiga kwa matendo yao,lakini walikuwa pia ni wenye kuomba toba sana kwa muumba wao kwa makosa ya KIBINADAMU.
Nyalandu ni binadamu wa kawaida ambae anakosea kama mimi na wewe,tunaangalia HILI LA Lucky Vicent.

Habeeb Marhan
 
kwa hili anastahili pongezi kwa kweli...kama huko ni kutafuta sifa ndio huko basi tunahitaji viongozi watafuta sifa........
ila alinishangaza alipowaweka watoto wake mbelembele kwenye shughuli ya kuwakaribisha watoto wale,
Samaki hukunjwa angali mbichi, na mtoto umleavyo ndivyo akuavyo, hao watoto wamejifunza kitu muhimu na kikubwa katika maisha ni umuhimu wa kujitoa kwa ajili ya wengine, labda kama nawe ni bunga hujui elimu kwa vitendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimelazimika kukubaliana na mtoa mada,Nyalandu kwenye hili big up/thumb up au vyovyote ikavyokuwa sawa.
Nilisikia kuwa ni mwenyekiti mwenza wa taasisi iliyoleta ndege ya kuwabeba.
HONGERA NYALANDU
Pongezi Nyalandu kuwa mwenyekiti mwenza tuliache tuendelee kupongeza kama mtoa mada atakavyo.
 
Jimbo lake lina matatizo ya kutosha, mbona hafanyi hivyo? sema siku hiyo ni wale wageni wakizungu ndiyo wamesababisha awe msitari wa mbele.
 
Pongezi Nyalandu kuwa mwenyekiti mwenza tuliache tuendelee kupongeza kama mtoa mada atakavyo.
Nongwa sasa hiyo!,nilimaliza kwa kusema "unaweza kufikiri tofauti",si lazima tufanane kwenye kuwaza mjomba,ila ukiacha kupongeza au kama huoni sababu basi unawrza kutujuza amekosea wapi.


Habeeb Marhan
 
Jimbo lake lina matatizo ya kutosha, mbona hafanyi hivyo? sema siku hiyo ni wale wageni wakizungu ndiyo wamesababisha awe msitari wa mbele.
Huyo siyo mgeni na wazungu,katika kusomasoma humu mtandaoni hadi nilikuta mahali mtu ameandika kuwa huyo ana DUAL CITIZENSHIP(sina uhakika),na pia ana marafiki wengi wazungu,Americans in particular.

Habeeb Marhan
 
kwa hili anastahili pongezi kwa kweli...kama huko ni kutafuta sifa ndio huko basi tunahitaji viongozi watafuta sifa........
ila alinishangaza alipowaweka watoto wake mbelembele kwenye shughuli ya kuwakaribisha watoto wale,
Nami nilishangaa kuona hilo. Utaratibu mzima ulikuwa wa ovyo. Watu walifika mpaka kwenye ngazi ikawa vurugu tu. Kwa nini wazazi/wababa hawakupewa haki yao badala yake wapewe watoto wa Nyalandu? Saying that haina maana hatumpongezi Lazaro kwa kushughulikia swala zima kama mtumishi wa umma. Hawakujiandaa kuwa na mkalimali wazungu wale walikuwa wanashangaa what's next kwenye kupewa zawadi. MC ndio kabisaaaaa ovyooo hata shule hawakuwa na utaratibu mzuri. All in all Tunamshukuru Mungu Watoto wamerudi wakiwa na afya njema thou Doreen bado ana safari ndefu Mungu azidi kumponya. Hivi waziri wa Afya hakualikwa Mbunge naye je?? Swali la kizushi!
 
Back
Top Bottom