Ntafikaje chuo cha mipango Dodoma?

Ntafikaje chuo cha mipango Dodoma?

salosalo

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2012
Posts
598
Reaction score
281
Nataka kwenda chuo cha mipango Dodoma nikitokea Arusha kwa magari ya abilia.
  1. Nitatakiwa nishukie kituo gani?
  2. Baada ya kushuka kuna umbali gani mpaka hapo chuoni ?
  3. kama safari itaenda vizuri, je ntafika mida gani kama nikiondoka Arusha saa 12 asubuhi?
  4. Je nitapata gari ya abiria ya kuelekea chuoni?
  5. Vipi kuhusu maeneo chuo kilipo, ntapata nyumba za kulala wageni?
Naombeni mwongozo tafadhali maana naenda kwenye interview ambayo itafanyika tarehe 13/08/2012. Hivyo nataka kujua ili nijipange siku ya kusafiri.
Je kama nikiondoka huku Arusha tar 12 ntaweza kuwahi usaili bila kulazimisha ?
 
Ukifika stand dodoma, uliza stend kuu ya daladala ya Jamatini. Hapo utapata daladala za kwenda chuo cha mipango. Pia hata ukipanda daladala za msalato au veyula utashukia kituo cha mipango. Chuo kipo barabarani kabisa. Nauli ya daladala ni tsh 300 na tax ni sh 6000. Ni bora uondoke ar trh 11, maana safar ni safar, hujui ya njiani. Guest jiran na mipango zipo ndio.
 
Kuna mabasi ya Arusha -Dodoma direct kama Abood, Hood na mengine ni safari ya siku moja ukiondoka AR saa 12 mkienda vizuri bila tatizo unawez kufika Dodoma same Day saa 3 au 4 usiku. Dodoma mjini guest kibao usihofu. Alternatively, kuna mabasi ya Arusha -Dodoma kupitia Babati na Kondoa nayo huondoka AR muda huo lakini yenyewe hufika mapema zaidi maana njia ni fupi zaidi. Ukipanda haya huna haja ya kufika Dodoma mjini maana basi linapita hapo hapo nje ya chuo ni suala tu la kuwaeleza wahusika wa basi wakuteremshe hapo. Ukiongeza na maelekezo ya Kaumza hapo juu utafika Chuo cha Mipango. Bon Voyage!
 
Hongereni sana kwa maelezo mazuri mliyompa Huyo jamaa, kwa kuongezea tu Kama yeye ni mvulana na usiku baada ya usaili akipenda kupumzika na kupata mrembo aende maeneo ya Chako ni Chako atapata mrembo
 
Ukifika stand dodoma, uliza stend kuu ya daladala ya Jamatini. Hapo utapata daladala za kwenda chuo cha mipango. Pia hata ukipanda daladala za msalato au veyula utashukia kituo cha mipango. Chuo kipo barabarani kabisa. Nauli ya daladala ni tsh 300 na tax ni sh 6000. Ni bora uondoke ar trh 11, maana safar ni safar, hujui ya njiani. Guest jiran na mipango zipo ndio.

Nasikitika sana kuchelewa kujiunga na Jamvi yaani najuta kuchelewa kulijua. Nashukuru sana bwana mkubwa, sasa najisikia nimekuwa mwenyeji wa Dom
 
Kuna mabasi ya Arusha -Dodoma direct kama Abood, Hood na mengine ni safari ya siku moja ukiondoka AR saa 12 mkienda vizuri bila tatizo unawez kufika Dodoma same Day saa 3 au 4 usiku. Dodoma mjini guest kibao usihofu. Alternatively, kuna mabasi ya Arusha -Dodoma kupitia Babati na Kondoa nayo huondoka AR muda huo lakini yenyewe hufika mapema zaidi maana njia ni fupi zaidi. Ukipanda haya huna haja ya kufika Dodoma mjini maana basi linapita hapo hapo nje ya chuo ni suala tu la kuwaeleza wahusika wa basi wakuteremshe hapo. Ukiongeza na maelekezo ya Kaumza hapo juu utafika Chuo cha Mipango. Bon Voyage!

Sajenti, hiyo salute hapo kwenye picha ni yako mkuu. Nashukuru sana. Kiukweli ushauri wenu umenifaa sana. Nimeelewa maana ya Bon Voyage.... so nashukuru sana. Nimeshindwa kukujibu kwa lugha hiyohiyo
 
Hongereni sana kwa maelezo mazuri mliyompa Huyo jamaa, kwa kuongezea tu Kama yeye ni mvulana na usiku baada ya usaili akipenda kupumzika na kupata mrembo aende maeneo ya Chako ni Chako atapata mrembo

:busu:busu:busu Tehe teheeeee! Nafurahi kweli, mimi ni kidume kweli na nadhani kwa namna hiyo ntapunguza stress za usaili au ntajipongeza kwa kufanya vizuri. Mimi ndo ntaamua kusuka au kunyoa. Hata kama kuna msichana ataenda naye apeleke bidhaa hapo chako ni chako(ni ushauri tu)
 
Jamani samahanini me ni mwanafunzi nimemaliza kidato cha nne na nimepata dvtin three ya 25 na sihitaji kwenda advance n napenda kwenda chuo lakini vyo vyenyewe napendelea kiwe udom au mipango naomba ushauri nikasomee couz gani ila nilisoma biadhara so nina d ya bkepng na comerce pamoja na c ya history, language na kiswahili pleas naombeni ushauri wenu
 
Jamani samahanini me ni mwanafunzi nimemaliza kidato cha nne na nimepata dvtin three ya 25 na sihitaji kwenda advance n napenda kwenda chuo lakini vyo vyenyewe napendelea kiwe udom au mipango naomba ushauri nikasomee couz gani ila nilisoma biadhara so nina d ya bkepng na comerce pamoja na c ya history, language na kiswahili pleas naombeni ushauri wenu
Mbona unaandika mwandiko mbaya,wewe umemaliza form four kweli????
 
Ndio maana umefeli,kwa huo mwandiko walimu walipata shida sana.jaribu wewe kusoma ulichokiandika hapo juu.
 
Sasa usipande abood au hood hizi zinapita morogoro na ni mbali, kata tiketi ya arusha express yanafika Dodona SAA 9 alasiri au saa nane mchana, inapita bahati, singida then Dodoma, stendi ya mkoa Dodoma na ya vifodi zipo umbali wa mita chache sana, panda vifodi vya st gema utashukia kituo cha mipango. By saa 10 jioni utakuwa mipango. Vyumba vipo vingi pale maeneo ya kanisani.
 
Back
Top Bottom