NSSF kuiokoa serikali Mtwara...? Kujenga kiwanda cha Korosho

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,999
[h=3]NSSF kujenga Kiwanda cha Korosho[/h]


Na Queen Lema, Arusha

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), unatarajia kujenga kiwanda cha kubangua zao la korosho mkoani Mtwara ambacho ujenzi wake utagharimu dola za Marekani milioni 35 hadi 40.

Ujenzi huo utaanza mara moja baada ya mazungumzo ya uwekezaji huo kukamilika kwani zao hilo lina soko kubwa ndani na nje ya Tanzania ili kukuza uchumi wa mikoa ya Lindi na Mtwara.

Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo, Dkt. Ramadhan Dau, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wadau wa NSSF katika mkutano wa tatu unaoendelea jijini Arusha.

Alisema hivi sasa mfuko huo unaangalia jinsi ya kuwasaidia wananchi wa mikoa hiyo ambao wanajihusisha zaidi na zao
hilo lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu
wa kiwanda cha kubangua korosho ili kukuza kipato chao.

“Wakulima wa zao la korosho mkoani Mtwara wanapata shida
kwa sababu ya ukosefu wa kiwanda cha kubangua zao hili hivyo
kama tutawekeza kwa kujenga kiwanda ni wazi kuwa thamani ya
zao hili itaongezeka.

“Tunahitaji ushirikiano wa wadau ili tuweze kufanikisha ujenzi
huu pamoja na uongozi wa Wilaya ya Tandahimba ili lengo letu liweze kufanikiwa kwa wakati,” alisema Dkt. Dau.

Katika hatua nyingine, Dkt. Dau alisema uwekezaji huo utakuwa na faida kwa sababu wakulima wa zao hilo waliopo mikoa ya Lindi na Mtwara, watauza korosho zao kwa bei kubwa kuliko ilivyo sasa.

“Hivi sasa wanauza korosho zao kwa dola moja ya Marekani hivyo kusababisha wapate hasara...uwekezaji huu ukikamilika watauza dola saba baada ya kubanguliwa hivyo kunufaika zaidi,” alisema.

Kwa upande wao, wadau wa mfuko huo walisema umefika wakati wa NSSF kuona umuhimu wa kuwekeza katika viwanda hususani vilivyokufa kwa kuvifufua ili kutoa ajira kwa vijana, kukuza
uchumi wa Taifa na kupunguza umaskini nchini.

Walisema hivi sasa, Tanzania kuna viwanda vingi ambavyo vimekufa na vinatumika kama maghara ya kuhifadhia mizingo
na vyakula vya watu binafsi hivyo mfuko huo unaopaswa kubuni
mbinu mpya ya uwekezaji katika viwanda.

“Mifuko ya kijamii ina nafasi kubwa sana ya kufufua viwanda vyetu vilivyokufa kwa mfano...kiwanda cha kubangua korosho kilikuwepo Pwani lakini kilikufa na wakulima kupata shida hivyo zao hilo kukosa ubora unaotakiwa,” alisema.

MAJIRA
 
NSSF kujenga Kiwanda cha Korosho




Na Queen Lema, Arusha

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), unatarajia kujenga kiwanda cha kubangua zao la korosho mkoani Mtwara ambacho ujenzi wake utagharimu dola za Marekani milioni 35 hadi 40.

Ujenzi huo utaanza mara moja baada ya mazungumzo ya uwekezaji huo kukamilika kwani zao hilo lina soko kubwa ndani na nje ya Tanzania ili kukuza uchumi wa mikoa ya Lindi na Mtwara.

Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo, Dkt. Ramadhan Dau, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wadau wa NSSF katika mkutano wa tatu unaoendelea jijini Arusha.

Alisema hivi sasa mfuko huo unaangalia jinsi ya kuwasaidia wananchi wa mikoa hiyo ambao wanajihusisha zaidi na zao
hilo lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu
wa kiwanda cha kubangua korosho ili kukuza kipato chao.

"Wakulima wa zao la korosho mkoani Mtwara wanapata shida
kwa sababu ya ukosefu wa kiwanda cha kubangua zao hili hivyo
kama tutawekeza kwa kujenga kiwanda ni wazi kuwa thamani ya
zao hili itaongezeka.

"Tunahitaji ushirikiano wa wadau ili tuweze kufanikisha ujenzi
huu pamoja na uongozi wa Wilaya ya Tandahimba ili lengo letu liweze kufanikiwa kwa wakati," alisema Dkt. Dau.

Katika hatua nyingine, Dkt. Dau alisema uwekezaji huo utakuwa na faida kwa sababu wakulima wa zao hilo waliopo mikoa ya Lindi na Mtwara, watauza korosho zao kwa bei kubwa kuliko ilivyo sasa.

"Hivi sasa wanauza korosho zao kwa dola moja ya Marekani hivyo kusababisha wapate hasara...uwekezaji huu ukikamilika watauza dola saba baada ya kubanguliwa hivyo kunufaika zaidi," alisema.

Kwa upande wao, wadau wa mfuko huo walisema umefika wakati wa NSSF kuona umuhimu wa kuwekeza katika viwanda hususani vilivyokufa kwa kuvifufua ili kutoa ajira kwa vijana, kukuza
uchumi wa Taifa na kupunguza umaskini nchini.

Walisema hivi sasa, Tanzania kuna viwanda vingi ambavyo vimekufa na vinatumika kama maghara ya kuhifadhia mizingo
na vyakula vya watu binafsi hivyo mfuko huo unaopaswa kubuni
mbinu mpya ya uwekezaji katika viwanda.

"Mifuko ya kijamii ina nafasi kubwa sana ya kufufua viwanda vyetu vilivyokufa kwa mfano...kiwanda cha kubangua korosho kilikuwepo Pwani lakini kilikufa na wakulima kupata shida hivyo zao hilo kukosa ubora unaotakiwa," alisema.

MAJIRA

hili porojo la gasi ...kuwa Mtwara watapata investment hii na ile ambayo haitokani na moja kwa moja na mauzo ya gasi...jee nauliza hio gasi haitakua na mapato ? ...hao wawekezaji...hawatapata mapato yoyote? jee faida yetu ni hiyo ya kuzalisha umeme tu ? kama ndio hizo Qatar wasingefika walipo..nchi yenye utajiri wa gasi tu......
ujinga mwengine bwana ,,,,,, bora Zanzibar wachimbe wenywewe hayo mafuta lakini ....kwa hawa jamaaa....kama hawana radhi..
 
Kwanza wamechelewa sana, hii ndo tunataka, si kuwekeza tu kwenye Government Securities, Majengo Makubwa na Kuikopesha serikali kwa riba ndogo kwa miradi kama ya UDOM yenye mianya ya rushwa!
 
mfa maji haachi kutapatapa...hapo ni serikali inatapatapa katika kuangalia namna ya kuwapoza wananchi wa mtwara waliokaa tamaa kwa serikali yao iliyowatelekeza toka uhuru....
swali la kujiuliza ni kuwa...kwa nini viwand vyote vilivyokuwepo huko mtwara na lindi vilikufa mara baada ya kubinafsishwa?...ilikuwa hujuma ya wahindi ili kushusha thamani ya korosho hapa tz na kupeleka ajira kwao india ili watu wao wapate fursa ya kubangua korosho manually? au viwanda vya kubangua korosho havilipi na ndio maana vyote vilikufa?
anyway...kila la kheri NSSF ila muwe makini na hela zetu hizo msije mkaboronga katika uwekezaji wenu huo na mkatuambia kuwa kupata hela zetu kibarua kikikoma mpaka tutimize miaka 80!
 
Kama unashirikisha kumbukumbu na akili yako vizuri utagundua kitu kimoja; kuondoa kauzibe kalikokuwa kanaletwa na POAC ili kuendeleza ufujaji huru wa pesa na rasilimali za umma. Kwa nini wenye hizi pesa za kwenye mifuko ya hifadhi za Jamii tusishinikize kutungwa kwa sheria ya ushirikishwaji na uwazi katika kuidhinisha uwekezaji wa mafao yetu? Pesa zetu zinawekezwa kisiasa, zinafia huko, hatujui na hakuna anayewajibika.

Hivi kwa nini tunaendesha nchi, Taasisi na Mashirika yake bila dira? Kila leo wanadai Serikali kujitoa katika masuala ya kufanya biashara sasa kama wanajenga kiwanda kitakuwa mali ya nani na nani atahusika kukiendesha? Kwa nini Serikali inaweka mikono kwenye mazao ya biashara pale tu mnyororo unapofika hatua ya mazao kuingia sokoni kama kweli tuna dira ya soko huria?
 
Waliokula hi yo pesa ya kutoa tenda ya kusafirisha gesi, hata haishuki kooni jinsi wananchi walivokomalia. Ingwezekana kuitapika nahisi wangeitapika kitamboooo.
Nchi hii tunakoelekea mtu hata akidokoa inabidi kwanza asile alichodokoa, akibane maana watu wanakaba hadi penalty
 
Ngoja kwanza wakishajenga, na kika-operate profitably ndio turudi kuongea.., sababu hizi ndoto za alinacha na tutafanya hiki na kile zimeshakuwa kama hadithi ya "A Boy who Cried Wolf"
 
Mwanakijiji,wananchi wa mtwara wanachoitaji sio kiwanja,wanaitaji bei kubwa ya korosho kabla haijabanguliwa hilo tu ndio hoja yao ya msingi.Kimsingi viwanda vya kososho vipo ambavyo ni chungu kwa hao wananchi,swali la msingi viwanda hv vimewasaidiaje hao wananchi kwa upande wa bei?,Je bei bora kwa inawezekana au ipo kwa tabaka la wafanyabiashara wachache yaani ngozi nyeupe tu ndio wenye haki ya kununua kwa bei ndogo inayosimamiwa na serikali na kisha kuuzwa kwa bei kubwa ambayo pia inasimamiwa na serikali.
 
Kama unashirikisha kumbukumbu na akili yako vizuri utagundua kitu kimoja; kuondoa kauzibe kalikokuwa kanaletwa na POAC ili kuendeleza ufujaji huru wa pesa na rasilimali za umma. Kwa nini wenye hizi pesa za kwenye mifuko ya hifadhi za Jamii tusishinikize kutungwa kwa sheria ya ushirikishwaji na uwazi katika kuidhinisha uwekezaji wa mafao yetu? Pesa zetu zinawekezwa kisiasa, zinafia huko, hatujui na hakuna anayewajibika.

Hivi kwa nini tunaendesha nchi, Taasisi na Mashirika yake bila dira? Kila leo wanadai Serikali kujitoa katika masuala ya kufanya biashara sasa kama wanajenga kiwanda kitakuwa mali ya nani na nani atahusika kukiendesha? Kwa nini Serikali inaweka mikono kwenye mazao ya biashara pale tu mnyororo unapofika hatua ya mazao kuingia sokoni kama kweli tuna dira ya soko huria?

Kuhusu gesi asilia ya Mtwara, hatudanganyiki ng'ooooooooooooooooooooooooooooooooooooo sisi tunajua faida ya kuwa na gesi na tunajua mtwara ya miaka 15 had 20 ijayo itakavyokuwa kutokana na utajiri wa gesi. ccm hii gesi wameikosa, tunasubiri CDM ushike utawala na sera mzuri ya majimbo tuanze kuvuna gesi na mafuta yetu. hivyo mjuwe tunamafuta pia ambayo visima vyake vimeanza kufanyiwa kazi . GESI KWANZA UHAI BAADAYE
 
Hata kama NSSF watajenga hicho kiwanda bado hawataweza kuwasaidia wananchi wa kawaida ambao ndio walio wengi kwenye.kubangua korosho,wananchi wanachohitaji ni bei ambayo itawanufaisha wao na si vinginevyo?,Vipo viwanda vya korosho vya orlam lakini je malalamiko ya bei kutoka kwa wananchi yameisha au yapo palepale?,
 
Ni lini hii mifuko ya kijamii itaanza kutupatia gawio la faida itokanayo na miradi hii?
 
DR RAMADHANI DAU AKIMWAGA DATA KWENYE AGM YA NSSF HUKO ARUSHA



 
Last edited by a moderator:
Poleni sana mnaolazimishwa kuchangia hii mifuko.

Maana ukimsikiliza huyu jamaa unaona ni jinsi gani hii mifuko ilivyokuwa na little room to utilize their capital na jinsi gani serikali ilivyokuwa aina mikakati ya uhakika ya kutekeleza sera zake za muda mrefu. Watu hawawezi kutoa ahadi bila ya kuwa na mbinu za kuzifikia wakitegemea wengine wawekeze that is not how capitalism work nor how political decisions are made, you are supposed to create the environment that creates opportunities to many, lakini si kulazimisha wengine wawekeze and giving them the monopoly advantage (no wonder they dont see their bad anti capitalism development policies) anyway i always thought baba Ndulika ni kilaza that is 'Benno Ndullu' for you.

Halafu huyo Dr. lazima aelewe watu hawawakopeshi bali wana invest (they expect their return in time) na si kusumbuana. Tatizo mifuko ya jamii imekuwa ni kama monopolies tu (hata kama ina majina tofauti) kitendo cha watu kutupiwa tu pa kulipa their future pensions plans without their consent ni uonevu. Na haya yote ni matokeo ya serikali kushindwa kuja na mbinu za maendeleo ikitegemea hii mifuko ilipe fadhila ya kuwekeza inavyotaka wao kwa upande fulani.

kuna uozo mkubwa sana kwenye secondary and tertiary production ndani ya nchi lakini to what extent and for how long the pension funds are going to bail the government inayoshindwa kuja na sera za kuchochea maendeleo katika hizo sector. Hivi vitu haviwezi shamiri bila ya elimu ya jamii yenye kulenga kuwapa mbinu za ku-exploit their resources and offering cheap loans.

Inatakiwa hii mifuko ijielewe hipo kwa maslahi ya wanachama wao na si serikali (serikali kama mdhamini ndio ina haki ya kuakikisha kuna responsible investments lakini si kuwapangia, that is just pathetic) kisa ina sera zake ambazo inategemea jamaa wasaidie.

Aisee hii nchi ina matatizo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Vile viwanda walivyouziana vinafanya nini?

Yaani Serikali hii.!!!,viwanda waliuziana kinyemela,kwani Bodi ya korosho iliporwa?.Serikali ilipaswa kutaifisha hivi viwanda vilivyouzwa kinyemela kwa watu binafsi bila kujali maslahi ya wakulima na Taifa.
Wanajua,lakini hawataki kuchuka hatua.!!,hakuna sababu ya kutumia fedha ya mifuko ya hifadhi jamii katika kujenga viwanda,wakati viwanda vilivyokuwa chini ya Bodi ya korosho havijafanyiwa tathimini kama vinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.
 
Sioni tatizo kwa NSSF kujenga kiwanda cha korosho Mtwara provided ni viable investment. Nakumbuka miezi kadhaa iliyopita kulikuwa na Mkutano jijini Arusha ambao ulijumuisha mifuko ya hifadhi ya jamiii toka nchi mbalimbali za Afrika. Moja ya mada ambazo walizitoa NSSF Tanzania ni umuhimu wa kuangalia uwekezaji kwenye sekta ya kilimo....I am happy, wameamua kufanya ambacho walikihubiri!
 
Sioni tatizo kwa NSSF kujenga kiwanda cha korosho Mtwara provided ni viable investment. Nakumbuka miezi kadhaa iliyopita kulikuwa na Mkutano jijini Arusha ambao ulijumuisha mifuko ya hifadhi ya jamiii toka nchi mbalimbali za Afrika. Moja ya mada ambazo walizitoa NSSF Tanzania ni umuhimu wa kuangalia uwekezaji kwenye sekta ya kilimo....I am happy, wameamua kufanya ambacho walikihubiri!

Biashara inataka mitaji na NSSF wanapesa ya kutosha ya kufanya chochote itakacho kwa nchi masikini kama Tanzania kutokana na makusanyo yao na aina maana wao kuwekeza kwenye kiwanda cha korosho ni kosa hili kukuza pato lao na kuweza kutimiza majukumu yao.

Tatizo ni kwamba wanawekeza kama nani wanaingia kama wawekezaji wenye kutegemea kuchukuwa chao kwenye faida ama kiwanda kinakuwa chini ya usimamizi wao hundred percent (maana hii sasa inakuwa kama yale yale ya ukomonisti isipokuwa serikali imeshindwa) kama unataka kufanya industrialization people need the source of money and financial investors, lakini si financial powers tena wawekeze kutakuwa amna distribution of money else where.

Hawa NSSF nadhani hawa ruhusiwi kuwekeza kwenye venture capitals (makampuni ambayo yangewekeza kwa niaba yao kwenye miradi kama hii) uoni kama serikali inashindwa changamoto za dunia ya leo na kudumaza maendeleo kwenye sekta ya viwanda kwa sababu ya kutegemea makampuni machache na kuwaitia wazungu tu when so many of us need the funds to propel our growth.

When are Tanzanians going to be given the chance to propel their own economical growth, ikiwa financial providers wanaingia wenyewe direct kwenye viwanda au unadhani mabenki huko ulaya na pensions funds hawawezi kufanya biashara nyingi ambazo inawakopesha watu wawekeze?
 
Mwanakijiji,wananchi wa mtwara wanachoitaji sio kiwanja,wanaitaji bei kubwa ya korosho kabla haijabanguliwa hilo tu ndio hoja yao ya msingi.Kimsingi viwanda vya kososho vipo ambavyo ni chungu kwa hao wananchi,swali la msingi viwanda hv vimewasaidiaje hao wananchi kwa upande wa bei?,Je bei bora kwa inawezekana au ipo kwa tabaka la wafanyabiashara wachache yaani ngozi nyeupe tu ndio wenye haki ya kununua kwa bei ndogo inayosimamiwa na serikali na kisha kuuzwa kwa bei kubwa ambayo pia inasimamiwa na serikali.
tatizo viongozi wetu wanawezeshwa na hao wafanya biashara ya korosho, hivyo kumtetea mkulima ni ndoto, kelele kidogo wakati wa uchaguzi na kanga na kofia kidogo, hao wanapita
 
Back
Top Bottom