NSSF Arusha mnatunyanyasa

NSSF Arusha mnatunyanyasa

jec2001tz

Member
Joined
Sep 10, 2010
Posts
15
Reaction score
3
Kumekuwa na hali ambayo haieleweki, watu tumefungua madai ya Mafao tangu November mwaka jana, lakini hadi sasa tunakaribia mwezi April ukienda unapigwa tarehe tu, mimi mwenyewe binafsi sasa ni mara ya nane napigwa tarehe, ukiomba kwenda kwa Meneja wanakukatalia, na hii inaonekana ni usanii wa ofisi nzima kwani katika ofisi zote hamna mlango unaoonyesha kwa Meneja.

Hivyo kama mtu uliacha kazi kwa malengo yako ya kujiajiri malengo hayawezi kutimia kutokana na muda.

Wengine wanasema eti NSSF hawana hela kwani hela zimechukuliwa na serikali. Mwenye habari zaidi na ushauri nini tufanye kuhusu mafao yetu plz atusaidie.
 
Pole sana ndugu,hiyo ndio Tanzania niijuayo.
Jichangishe uwape bahasha au nenda pccb wakope fedha za moto usikilizie wahusika, uone kama haijachukua siku mbili.
 
Mbali ya kupigwa tarehe,fedha wanayokupitishia bank inaweza kuwa pungufu.ukienda unafungua madai upya na unapewa mwezi mmoja kusubiri na danadana zinaendelea kama kawaida.
 
Nashukuruni kwa ushauri mkuu, leo kama kawaida niko hapa, kuna bwana mmoja ni mfanyakazi wa Nssf, mrefu ana makengeza sijui position yake ila anachokifanya ni kuzunguka akiona anayelalamika kidogo anajifanya kumsaidia ila anatengeneza mazingira ya rushwa. Ngoja nielekee PCCB, ila sijui kama kutakuwa na msaada maana kwa Tanzania ofisi usiyomjua mtu, Ofisi hiyo ni sawa na imefungwa.
 
Nashukuruni kwa ushauri mkuu, leo kama kawaida niko hapa, kuna bwana mmoja ni mfanyakazi wa Nssf, mrefu ana makengeza sijui position yake ila anachokifanya ni kuzunguka akiona anayelalamika kidogo anajifanya kumsaidia ila anatengeneza mazingira ya rushwa. Ngoja nielekee PCCB, ila sijui kama kutakuwa na msaada maana kwa Tanzania ofisi usiyomjua mtu, Ofisi hiyo ni sawa na imefungwa.
ofisa wa PCCB utakaemkuta mkatie kitu kidogo ili akushughulikie chapchap.
 
Hili la kuzuia kumuona meneja naliafiki, yaani hawataki kabisa uende kwa meneja, sijui kuna siri gani pale
 
Back
Top Bottom