Novemba 12 Zanzibar inazidi kutumbukia kwenye mgogoro wa kikatiba

simplemind

JF-Expert Member
Apr 10, 2009
16,409
9,183
Pamoja na Dr Shein kuendelea kuwa Rais kwa kutumia kifungu tata cha katiba, Novemba 12 Zanzibar itazidi kutumbukia kwenye mgogoro wa kikatiba kutokana na kotokuwepo wawakilishi.

Kifungu cha 90(1) cha Katiba ya Zanzibar ya 1984 kinaeleza kwamba:

"90.(1) Wakati Baraza litakapovunjwa, Uchaguzi Mkuu wa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi utafanywa na mkutano wa mwanzo wa Baraza jipya utafanywa si zaidi ya siku tisini toka kuvunjwa kwa Baraza."

Baraza la Wawakilishi lililopita lilivunjwa tarehe 13 Agosti, 2015. Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa kifungu cha 90(1) cha Katiba ya Zanzibar, Baraza jipya linapaswa kuitishwa si zaidi ya tarehe 12 Novemba, 2015.

Kwa mujibu wa kifungu cha 29 na 92(2) cha Katiba hiyo, Baraza la Wawakilishi linaweza tu kuongezewa muda iwapo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakapokuwa kwenye vita.

Kwa msingi huo, sasa hivi hakuna Baraza la Wawakilishi ambalo ndiyo chombo cha wananchi wa Zanzibar kinachoisimamia Serikali yao, na Baraza jipya linapaswa kuitishwa si zaidi ya siku tisini tokea Baraza lililopita lilipovunjwa.

Kwa maana hiyo, ifikapo tarehe 12 Novemba, 2015 ni lazima Baraza jipya lililochaguliwa tarehe 25 Oktoba, 2015 liitishwe na lisipoitishwa, nchi yetu itaendelea kutumbukia kwenye mgogoro mkubwa zaidi wa kikatiba na kiutawala.
 
Kwani wewe huone kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iko kwenye vita na Wazanibari?

Kwanza ni kuyapinduwa matakwa yao kwa kutumia Jeshi.

Nani hajui kama Jecha alilazimishwa kwa kutumia Jeshi, ? Kama alikuwa huru mbona hakwenda moja kwa moja ukumbini ambo Observers na Wanahabari walikuwa wanamsubiri kutangaza.

Ni nani aliyekuwa hajuwa kama Makamo mwenyekiti alichukuliwa na Jeshi na Usalama wa taifa na Observers wote walishuhudia?

Jee hili Jeshi na Vifaru vilivyoenea mitaani Zanzibar Mzima vinafanya nini kama haya si Mapindizi ya Kijeshi?

Ni Tanzania nu ndiko ambako kwenye Chombo cha Sheria (Bunge) anasimama mtu anasema Serikali haitolewi kwa vikaratasi bila ya kuchukuliwa sheria wela kuhojiwa na yeyote wakakati Serikali inatumia mabillioni ya mapesa kuamndaa uchaguzi huu, pesa ambazo pesa nyingi kati ya hizo ni za wafadhili.

Wengi wanasema kuwa huu mgogoro ni wa Zanzibar, lakini tuelewe Zanzibar haieleweki Kimataifa.

Kama tunakumbuka wakati huu wa Kampeni Serikali ya Marekali kwa kupitia Mpango wa Millenium iliidhinisha $ 478 Mill kwa Tanzania, Masharti yalikuwa Uchaguzi uwe wa Huru na Haki.

Kama Mgogoro wa Zanzibar hautotatuliwa Haraka hizi Pesa Hazitoki na huo ndio ukweli wenyewe.

Kuna project chungu mzima Ambazo Tanzania hivi sasa inasubiri Mkopo kutoka Worldbank, pia hizo project zitayayuka.

Kuna hizo Badget zetu ambazo kwa asilimia kubwa zinategemea Wafadhili, hapo tutakapoisoma Namba.

Naka kama kweli Wao wataamua kwamba Mgogoro wa Zanzibar Tanzania hauwahusu, Zanzibar wakafungua Kesi ya Kikatiba kwenye mahkama za Kimataifa, hio itakuwa ni wazi, Tanganyika waiitangazia Zanzibar uhuru wake.
 
Kwa nchi za kiafrika mgogoro wa kikatiba hakuna,Ingekuwa ni nchi zilizoendelea sawa watu wangeshaumiza vichwa mno ila kwa siasa zetu, tunaweka katiba pembeni, tunatumia kanuni!!! Yaani kanuni inakuwa zaidi ya sheria na katiba, ikishindikana kanuni tunatumia BUSARA!! Juzi hukumsikia polepole eti anakwambia suala la zanzibar haliitaji katiba wala sheria, kulitafutia ufumbuzi bali ni busara tu??!!!!! Yaani ni Tanzania tu mtu amesomea sociology anawafundisha wanasheria masuala ya sheria!!! Tena anakuwa mkali kweli hadi mwanasheria anarudi nyuma!! Sasa huyu pole pole kwenye siasa, uchumi, sheria, majanga, usafirishaji yumo tu!!! Na anavyopewa airtime na tv,
 
Kwa nchi za kiafrika mgogoro wa kikatiba hakuna,Ingekuwa ni nchi zilizoendelea sawa watu wangeshaumiza vichwa mno ila kwa siasa zetu, tunaweka katiba pembeni, tunatumia kanuni!!! Yaani kanuni inakuwa zaidi ya sheria na katiba, ikishindikana kanuni tunatumia BUSARA!! Juzi hukumsikia polepole eti anakwambia suala la zanzibar haliitaji katiba wala sheria, kulitafutia ufumbuzi bali ni busara tu??!!!!! Yaani ni Tanzania tu mtu amesomea sociology anawafundisha wanasheria masuala ya sheria!!! Tena anakuwa mkali kweli hadi mwanasheria anarudi nyuma!! Sasa huyu pole pole kwenye siasa, uchumi, sheria, majanga, usafirishaji yumo tu!!! Na anavyopewa airtime na tv,

kweli mkuu huyu jamaa yeye anajua kila kitu na huwa anashupaa kweli anajiona yeye ni zaidi ya watanzania wote
 
Kwa nchi za kiafrika mgogoro wa kikatiba hakuna,Ingekuwa ni nchi zilizoendelea sawa watu wangeshaumiza vichwa mno ila kwa siasa zetu, tunaweka katiba pembeni, tunatumia kanuni!!! Yaani kanuni inakuwa zaidi ya sheria na katiba, ikishindikana kanuni tunatumia BUSARA!! Juzi hukumsikia polepole eti anakwambia suala la zanzibar haliitaji katiba wala sheria, kulitafutia ufumbuzi bali ni busara tu??!!!!! Yaani ni Tanzania tu mtu amesomea sociology anawafundisha wanasheria masuala ya sheria!!! Tena anakuwa mkali kweli hadi mwanasheria anarudi nyuma!! Sasa huyu pole pole kwenye siasa, uchumi, sheria, majanga, usafirishaji yumo tu!!! Na anavyopewa airtime na tv,

kale kajamaa kanajifanya kuwa ni ka "Much Knowledgeable Others - M.K.O"

 
Kwani wewe huone kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iko kwenye vita na Wazanibari?

Kwanza ni kuyapinduwa matakwa yao kwa kutumia Jeshi.

Nani hajui kama Jecha alilazimishwa kwa kutumia Jeshi, ? Kama alikuwa huru mbona hakwenda moja kwa moja ukumbini ambo Observers na Wanahabari walikuwa wanamsubiri kutangaza.

Ni nani aliyekuwa hajuwa kama Makamo mwenyekiti alichukuliwa na Jeshi na Usalama wa taifa na Observers wote walishuhudia?

Jee hili Jeshi na Vifaru vilivyoenea mitaani Zanzibar Mzima vinafanya nini kama haya si Mapindizi ya Kijeshi?

Ni Tanzania nu ndiko ambako kwenye Chombo cha Sheria (Bunge) anasimama mtu anasema Serikali haitolewi kwa vikaratasi bila ya kuchukuliwa sheria wela kuhojiwa na yeyote wakakati Serikali inatumia mabillioni ya mapesa kuamndaa uchaguzi huu, pesa ambazo pesa nyingi kati ya hizo ni za wafadhili.

Wengi wanasema kuwa huu mgogoro ni wa Zanzibar, lakini tuelewe Zanzibar haieleweki Kimataifa.

Kama tunakumbuka wakati huu wa Kampeni Serikali ya Marekali kwa kupitia Mpango wa Millenium iliidhinisha $ 478 Mill kwa Tanzania, Masharti yalikuwa Uchaguzi uwe wa Huru na Haki.

Kama Mgogoro wa Zanzibar hautotatuliwa Haraka hizi Pesa Hazitoki na huo ndio ukweli wenyewe.

Kuna project chungu mzima Ambazo Tanzania hivi sasa inasubiri Mkopo kutoka Worldbank, pia hizo project zitayayuka.

Kuna hizo Badget zetu ambazo kwa asilimia kubwa zinategemea Wafadhili, hapo tutakapoisoma Namba.

Naka kama kweli Wao wataamua kwamba Mgogoro wa Zanzibar Tanzania hauwahusu, Zanzibar wakafungua Kesi ya Kikatiba kwenye mahkama za Kimataifa, hio itakuwa ni wazi, Tanganyika waiitangazia Zanzibar uhuru wake.


Umechangia vizuri sana na kuweka matukio mengi yanayodhirisha kuna ukiukwaji mkubwa wa ki sheria na haki za binadamu ila kuna kitu umekisahau kuweka hapa ilitujadiliane kwa uhuru na uzalendo kwa ajili ya nchi yetu. VIPI MBONA HAUJALIWEKA SUALA LA MSAKA TONGE MAALIM SEIF KUJITANGAZIA USHINDI WA URAIS KABLA YA TUME YA UCHAGUZI
 
Umechangia vizuri sana na kuweka matukio mengi yanayodhirisha kuna ukiukwaji mkubwa wa ki sheria na haki za binadamu ila kuna kitu umekisahau kuweka hapa ilitujadiliane kwa uhuru na uzalendo kwa ajili ya nchi yetu. VIPI MBONA HAUJALIWEKA SUALA LA MSAKA TONGE MAALIM SEIF KUJITANGAZIA USHINDI WA URAIS KABLA YA TUME YA UCHAGUZI
ji

Hili hapa jibu lako: Tume ilikua imeyatangaza majimbo yote kwa kubandika matokeo yote ya Urais, uwakilishi,udiwani,ubunge na Urais wa Muungano tangu tar:25 jioni walipomaliza kuhesabu kura za kila mgombea kila jimbo, na matokeo yalibandikwa na kujulikana na matokeo kila mtu aliyajuaMaalim alitoa mapendekezo Yale tar27.
 
Ninachoamini hawa watawala hawana aibu kabisa maana next step nahisi itakua ya aibu zaidi usishangae kuona Shein anaapishwa kabla ya 12.nov tena kwa mbwembwe zote baada ya hapo kila atakaepinga atakua muhasi kamili anaepambana na serikali ilioko madarakani.
 
Naomba Mh. Rais aniwie radhi nimwite kama Mwl. Nyerere alivyokuwa anawaita akina Malecela na Kawawa. Hapa John anatakiwa awe mkakamavu, aseme "kama noma na iwe noma" huu mgogoro autatue kama hana akili nzuri aseme sasa yatosha na wamwapishe Maalim Seif Sheriff Hamad kuwa Rais wa Zanzibar. Akiwachekea akina Jakaya, Ali na mwenzao Benjamin itakula kwake!! Yeye ndo serikali itamdodea wenzake wakimchekea kwenye mashavu! SHAURI YAKEE!! Hataweza kuongoza serikali isiyokuwa na hela za miradi, hazina yenyewe Mkwe.re kaiacha tupu sasa ataponea wapi?

Hapo anatakiwa avae miwani ya mbao ili asiwaone hawa jamaa asifikiri wanampenda kama wanavyojionesha kwenye nyuso zao. Hivi anafikiri Mkwe.re alikuwa anamtaka? Hivi anafikri Myao alikuwa anamtaka? Thubutu yake!!
 
Mkuu tunamuapisha Maalim kuwa Rais mpya wa SUK Zanzibar kabla ya hio Novemba 12 wee tulia.
Atakuwa Rais wa Jamuhuri ya Pemba(kama ipo) ila kwa Zanzibar sifikirii kama waunguja watakubali..Kibaya zaidi wapemba wamewekeza zaidi Unguja kwao wameacha magofu..ndio kusema mziki ukianza pale watakaotafuta pa kujificha ni wapemba..usipime jombaa
 
Umechangia vizuri sana na kuweka matukio mengi yanayodhirisha kuna ukiukwaji mkubwa wa ki sheria na haki za binadamu ila kuna kitu umekisahau kuweka hapa ilitujadiliane kwa uhuru na uzalendo kwa ajili ya nchi yetu. VIPI MBONA HAUJALIWEKA SUALA LA MSAKA TONGE MAALIM SEIF KUJITANGAZIA USHINDI WA URAIS KABLA YA TUME YA UCHAGUZI

Nawe tujulishe. Vipi kuhusu Makamba kumtangaza Magufuli mshindi na mpaka kutaja siku ya kuapishwa kwake kabla hata zoezi la kuhesabu kura halijahitimishwa na tume? Vipi kuhusu wana CCM kudai kuwa CCM haitotolewa madarakani kwa vikaratasi? Vipi kuhusu Tume kumtangaza Magufuli mshindi kwa kutumia kura za Zanzibar ambazo uchaguzi wake umefutwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar?
 
kwa hali ya zanzibar ilivyo hata wafadhili watuzuie tu kupewa misaada...

Hawatazuia watasihi na kuomba mgogoro utatuliwe. Wao wameshaambiwa Uamsho ni AlShabab na ISIS na watarudi kwa mgongo wa CUF.
Subiri utakuja kuona. Propaganda iliyopo si ndogo!
 
Hii miaka 5 iliyopita taratibu, sheria na katiba vimebakwa hadharani. Tafsiri sahihi ni ile wanayotaka wao
 
..... VIPI MBONA HAUJALIWEKA SUALA LA MSAKA TONGE MAALIM SEIF KUJITANGAZIA USHINDI WA URAIS KABLA YA TUME YA UCHAGUZI[/QUOTE said:
Omba radhi kijana kwa kumuita Maalim Seif kuwa ni msaka tonge. He is a liberator!
 
Back
Top Bottom