Nnaomba muongozo - TZ international driving licence

Nnaomba muongozo - TZ international driving licence

Bradha

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2017
Posts
8,786
Reaction score
45,268
Habari wakuu,

Ninatumaini sote ni wazima na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku pasi na mawaa yoyote.

Nimewahi kusikia kuna 'international driving licence' zinazotolewa Tanzania.Nimejaribu kucheki kwenye website ya TRA ila sijaona hii category.Kama hizi leseni zipo(au hazipo) ninaomba mwenye uhakika aconfirm plz.

Kama zipo:
Ninaomba kujulishwa utaratibu wa kupata leseni ya kimataifa ya kuendeshea gari la kawaida.Kwa wale waliokwisha kupata leseni hizi, nnaomba mnisaidie kujua gharama zake zikoje na taratibu za kufanya mitihani zikoje(mitihani mingapi, passing marks etc).


Pia, kwa wale waliojaribu kuzitumia(leseni hizi za kawaida au za kimataifa kama zipo) nje ya nchi, je kuna nchi ambayo hawazitambui?

Ntashukuru sana ukinisaidia uzoefu wako katika hili .......
 
Mi nazojua ni za Zamani zilikua ni kijitabu flani karma bado zipo kwa sasa zitakua in smart card format.
 
Mi nazojua ni za Zamani zilikua ni kijitabu flani karma bado zipo kwa sasa zitakua in smart card format.

Hizo unazozijua ni za kimataifa au ni zile za kitabu za kawaida ambazo hazitumiki tena?
 
Leseni yetu ya kawaida inakubalika katika nchi zote za SADC bila shida yoyote.Kwa nchi nyingine za nje ya Afrika utahitaji kwenda kufanya test na kupewa Provisional Driving License jwa matumizi ya muda kama itakidhi mahitaji yako au kufanya mtihani kupata leseni ya kawaida ya sehemu husika.
 
Hizo unazozijua ni za kimataifa au ni zile za kitabu za kawaida ambazo hazitumiki tena?
Ni za kimataifa ndugu. Maarufu kama (IDL) zilikua zinatolewa na THE ASSOCIATION OF AUTOMOBILE TANZANIA ofisi zao zilikua pale morogoro Rd fire
 
UK walikuwa wanaruhusu leseni ya kawaida ya Tanzania kutumika kwa mwaka mmoja sijui kwa sasa hivi, then uende DVLA Wembley kufuatilia learner umalize kusoma ukafanye written test then practical ukitoboa unapewa leseni yako
 
Ni za kimataifa ndugu. Maarufu kama (IDL) zilikua zinatolewa na THE ASSOCIATION OF AUTOMOBILE TANZANIA ofisi zao zilikua pale morogoro Rd fire
Zile ofisi nadhani bado zipo nilikuwa na gari ina namba za nje nikawa naenda kulipia vibali pale
 
UK walikuwa wanaruhusu leseni ya kawaida ya Tanzania kutumika kwa mwaka mmoja sijui kwa sasa hivi, then uende DVLA Wembley kufuatilia learner umalize kusoma ukafanye written test then practical ukitoboa unapewa leseni yako
Nna rafiki yangu ameniambia UK hawazikubali tena leseni zetu baada ya kuona kuwa waTZ wengi wanasababisha ajali.Sina official statement katika hili japo ...
 
Habari wakuu,

Nnatumaini sote ni wazima na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku pasi na mawaa yoyote.

Nimewahi kusikia kuna 'international driving licence' zinazotolewa Tanzania.Nimejaribu kucheki kwenye website ya TRA ila sijaona hii category.Kama hizi leseni zipo(au hazipo) nnaomba mwenye uhakika aconfirm plz.

Kama zipo:
Nnaomba kujulishwa utaratibu wa kupata leseni ya kimataifa ya kuendeshea gari la kawaida.Kwa wale waliokwisha kupata leseni hizi, nnaomba mnisaidie kujua gharama zake zikoje na taratibu za kufanya mitihani zikoje(mitihani mingapi, passing marks etc).


Pia, kwa wale waliojaribu kuzitumia(leseni hizi za kawaida au za kimataifa kama zipo) nje ya nchi, je kuna nchi ambayo hawazitambui?

Ntashukuru sana ukinisaidia uzoefu wako katika hili .......

Leseni ya udereva ya kimataifa hutolewa na nchi unayoishi pale unapotaka kwenda nchi ingine ambayo huna leseni yao ya udereva.

Kwa mfano ukienda Marekani au Uingereza na nchi zingine za Ulaya basi unaomba IDL ili ikisaidie kuendesha gari kwenye nchi hizo sambamba na leseni ya kawaida ya nchi yako.

Ukiwa mtembezi au visitor kwenye baadhi ya majimbo nchini Marekani unaweza kuomba leseni ya muda ili uitumie kukodi magari.

IDL inatumika sana pale unapotaka kukodi magari kwenye nchi unayoitembelea lakini ni lazima uwe na leseni zote mbili yaani leseni ya nchi husika na IDL.

IDL inatolewa na Automobile Association of Tanzania:

Utaratibu ni kama ifuatavyo:

Unatakiwa kuwa na leseni ya Udereva ya daraja lolote lile.

Pia unatakiwa kuipeleka leseni yako ofisi ya Mamlaka ya Leseni (T) TRA kwa ajili ya ukaguzi.

Baada ya Ukaguzi, Mamlaka ya Leseni (T) TRA itatoa barua rasmi kwenda kwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani(T) kuthibitisha uhalali wa leseni hiyo.

Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itakagua leseni hiyo pamoja na cheti cha Umahiri (Certificate of Competence) kuthibitisha uhalali wa leseni na cheti hicho cha umahiri.

Baada ya kuthibitisha uhalali wa leseni yako, Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itatoa barua rasmi kwenda Oisi ya Automobile Association Tanzania ambayo ndiyo asasi pekee hapa nchini yenye Mamlaka ya kutoa leseni za Kimataifa.

Ofisi za AAT zipo barabara ya Morogoro karibu na kituo cha mafuta cha Oryx karibu na Zimamoto.

Ukiweza basi jidamke mapema sabahi na uwahi huko.
 
Nna rafiki yangu ameniambia UK hawazikubali tena leseni zetu baada ya kuona kuwa waTZ wengi wanasababisha ajali.Sina official statement katika hili japo ...
Inaweza kuwa kweli Mkuu
 
Mkuu Wala usihofu kabisa. Hakuna leseni rahisi kupata Kama hii, hakuna huo mlolongo wote ulioambiwa huko juu. Nenda ofisi za AAT pale 'faya' opposite na kituo Cha mwendokasi ukiwa na vifuatavyo

1. Leseni ya udereva Tanzania
2. Kopi ya passport
3. Shilingi 235,000/=


Ni process ya dakika 10 maximum. Hakuna Cha TRA wala Polisi

Usidanganywe

Ukikwama niambie
 
Leseni ya udereva ya kimataifa hutolewa na nchi unayoishi pale unapotaka kwenda nchi ingine ambayo huna leseni yao ya udereva.

Kwa mfano ukienda Marekani au Uingereza na nchi zingine za Ulaya basi unaomba IDL ili ikisaidie kuendesha gari kwenye nchi hizo sambamba na leseni ya kawaida ya nchi yako.

Ukiwa mtembezi au visitor kwenye baadhi ya majimbo nchini Marekani unaweza kuomba leseni ya muda ili uitumie kukodi magari.

IDL inatumika sana pale unapotaka kukodi magari kwenye nchi unayoitembelea lakini ni lazima uwe na leseni zote mbili yaani leseni ya nchi husika na IDL.

IDL inatolewa na Automobile Association of Tanzania:

Utaratibu ni kama ifuatavyo:

Unatakiwa kuwa na leseni ya Udereva ya daraja lolote lile.

Pia unatakiwa kuipeleka leseni yako ofisi ya Mamlaka ya Leseni (T) TRA kwa ajili ya ukaguzi.

Baada ya Ukaguzi, Mamlaka ya Leseni (T) TRA itatoa barua rasmi kwenda kwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani(T) kuthibitisha uhalali wa leseni hiyo.

Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itakagua leseni hiyo pamoja na cheti cha Umahiri (Certificate of Competence) kuthibitisha uhalali wa leseni na cheti hicho cha umahiri.

Baada ya kuthibitisha uhalali wa leseni yako, Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itatoa barua rasmi kwenda Oisi ya Automobile Association Tanzania ambayo ndiyo asasi pekee hapa nchini yenye Mamlaka ya kutoa leseni za Kimataifa.

Ofisi za AAT zipo barabara ya Morogoro karibu na kituo cha mafuta cha Oryx karibu na Zimamoto.

Ukiweza basi jidamke mapema sabahi na uwahi huko.

Maelezo yamejitosheleza hayaitaji nyama wala mifupa

Labda ungetuwekea ata kipicha kimoja tu cha ushahidi
 
Habari wakuu,

Ninatumaini sote ni wazima na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku pasi na mawaa yoyote.

Nimewahi kusikia kuna 'international driving licence' zinazotolewa Tanzania.Nimejaribu kucheki kwenye website ya TRA ila sijaona hii category.Kama hizi leseni zipo(au hazipo) ninaomba mwenye uhakika aconfirm plz.

Kama zipo:
Ninaomba kujulishwa utaratibu wa kupata leseni ya kimataifa ya kuendeshea gari la kawaida.Kwa wale waliokwisha kupata leseni hizi, nnaomba mnisaidie kujua gharama zake zikoje na taratibu za kufanya mitihani zikoje(mitihani mingapi, passing marks etc).


Pia, kwa wale waliojaribu kuzitumia(leseni hizi za kawaida au za kimataifa kama zipo) nje ya nchi, je kuna nchi ambayo hawazitambui?

Ntashukuru sana ukinisaidia uzoefu wako katika hili .......
Leseni ya tz unaweza ku endesha popote pale hiyo hiyo unayo ijua
 
Mkuu Wala usihofu kabisa. Hakuna leseni rahisi kupata Kama hii, hakuna huo mlolongo wote ulioambiwa huko juu. Nenda ofisi za AAT pale 'faya' opposite na kituo Cha mwendokasi ukiwa na vifuatavyo

1. Leseni ya udereva Tanzania
2. Kopi ya passport
3. Shilingi 235,000/=


Ni process ya dakika 10 maximum. Hakuna Cha TRA wala Polisi

Usidanganywe

Ukikwama niambie


Ahsante sana mkuu, nafikiri hii ndio njia rahisi zaidi.Nitaifanyia kazi.Weekend njema!!
 
Leseni ya udereva ya kimataifa hutolewa na nchi unayoishi pale unapotaka kwenda nchi ingine ambayo huna leseni yao ya udereva.
.
.
.
Ofisi za AAT zipo barabara ya Morogoro karibu na kituo cha mafuta cha Oryx karibu na Zimamoto.

Ukiweza basi jidamke mapema sabahi na uwahi huko.

Ahsante sana Richard
 
Back
Top Bottom