Habali zenu,
Mimi ni mwanamke mwenye miaka hiyo wakati nipo chuo nilikuwa na boyfrend baadae tukawa kama tunamis understantanding fulani hivi sijui ni kwasababu ya umbali anyway, basi mimi nikapata boy mwingine akaja home na akafata taratibu zote bahati mbaya kabla ya ndoa nikashika mimba kabla ya kufunga ndoa kuna mambo yakatokea katikati ikabidi nijifungue kwanza ndo tufunge ndoa.
Nikajifungua salama na maisha yakaendelea kama kawaida,ikiwa tunafanya process za ndoa sielewi nini kiliingilia kati yetu ukweli nashindwa hata kuelewa tulitofautina kwenye simu kama mnavojua mapenzi ya mbali basi yule bwana akakomoa kuwa basi na uhusiano uishie hapo kwa kweli sikuamini kilichotokea wazazi pande zote waliingilia kati wala hakutaka kunielew nilijitahidi kumpembeleza alikataa kata kata fikiria hapo na mtoto mdogo, basi ndugu zake wakawa wananifariji hatimaye nikawa normal.
Nikaendelea kulea mwanangu ila hakuacha kumjulia hali mtoto na kutoa support zote kama kunatatizo hata ndungu zake pia hasa wazazi wake hawa kuwa mbali na mimi kunijulia hali,basi nikazoea.
Sasa yule boyfrend wangu wa mwanzo kama 4yrs imepita akaanza kunitafuta nikamwambia kila kitu kinachoendelea baada ya kuniuliza social life yangu ya mapenzi nikamwambia kuwa na mtoto na blal blah nyingine alisikitika sana ila akakubali hali halisi baadae akawa ananiuliza vipi mbona upo home hujaenda kwako ikabidi nimwambie ukweli wote, akakaa kama miezi 6 then akanambia ooohh tuludie na nini na nin nikakataa badae akanisisitiza akaniambia usijari kuhusu mtoto siwezi kumuhukumu kutokana na historia yetu nikaona isiwe shida nikakubali ila nikamuuliza vipi kuhusu yeye akadai toka tulivoacha 4yrs ago hajaoa wala hana mtoto nikaacha kama yalivo.
Kweli nikaenda kwake hakukuwa kama siku mbili nikarudi alikuwa anaishi mwenyewe, sasa yupo kwenye process za kutaka kuja home ndo hapo utata ulipo nikapata habali ana mtoto nikamuuliza akasema ndiyo ila hakutaka kuniambia sababu ananipenda ningekataa kuoana naye.
nipo njia panda nataka kusitisha zoezi lake la kuja home kwanini hakuniambia hapo mwanzo hadi wengine wanambie?
Ushauri jamani tafadhali