NMB Idara ya mikopo Rushwa imekithiri

NMB Idara ya mikopo Rushwa imekithiri

mkopo wa milioni moja, mkopo wa laki tano unaenda bank ya NmB, duh, watanzania wana shidaaaaa, hiyo hela si ungekopa hata kwa rafiki yako tu jamani. pengine nmb wameona ni hasara, mikopo midogo hiyo hawawezi kukuthamini kwasababu una faida kidogo sana kwao ndio maana unaona kama wanakuonea. nenda saccos au upatu wa mtaani huko au weka hela kwenye kibubu, laki tano haustahili kwenda kukopa bank. tuache utani jamani. hata milioni moja au mbili unaenda bank? hizo hata waendesha bodaboda wanazo majumbani mwao, kwanini mnapenda kunia madogo kiasi hicho, think big, act big....alaaa.
Unaweza kujiona Unajua kumbe hujui, vitu vingine bora kukaa kimya kuficha utupu wako.
 
NMB Tunduma kama unataka mkopo jua ya kwao ni ten percent hiyo haina mjadala tena hapo wewe ndio unawabembeleza na kuwapigia magoti.!
 
Habari wana Ukumbi,

Leo nimekuja hapa barazani kufikisha kero yangu kwa benki ya NMB tawi la Mbalizi road MBEYA.

Mwaka 2013 mwezi wa Nne (04) nilienda kwenye ofisi zao, kwa minajili ya kuomba mkopo. Nilipofika pale nilikutana na Loan officer alijitambulisha kwa jina la Kirungeme.

Katika hatua za awali niliweza pata ushirikiano wa kutosha kwa huyu mfanyakazi. Nilipokamilisha hatua zote ikiwemo ile ya kuja kunitembelea na kuangalia shughuli zangu. Bank iliamua kunipa mkopo wa Tsh. 500,000/- ingawa niliomba Tsh. 1,000,000/-

Kadhia ilianza hapa;

Niliombwa pesa ya mafuta ya gari kwa kuja kunitembelea niliwapa 15,000/- (ilinibidi kutoa maana nilikuwa na shida hasa na ule mkopo)

Akanielekeza kwa mwanasheria atakaye gonga Muhuri na kunitajia kabisa kiwango cha kumlipa (niliambiwa nikamlipe 50,000/-) hili sikulifanya maana, nilienda States attorney nikapigiwa muhuri kwa 10,000/- na kuzirudisha form Bank. Nilipo zikabidhi form za mkopo kwa loan officer huyu alianza kugomba kwanini sijaenda kwa mwanasheria aliyenitajia!

Nilifanikiwa kuchukua mkopo, na kufanya marejesho kila mwezi kama mkataba wetu ulivyokuwa umeelekeza. Baada ya kukamilisha Marejesho, na kufanikiwa kulipa mkopo wote nilienda tena Bank n kukutana na Kirungeme akaniambia yeye kapanda cheo, ila atanikabidhi kwa Mtu mwingine.

Alinikabidhi kwa Mdada anaitwa Alice (ana asili ya kichaga) huyu dada ndio sababu hasa ya kuja kuomba ushauri hapa.

Nilimwambia nahitaji mkopo wa Tsh. 1,500,000/- nilifanya hivi kwakua lengo hasa nilitaka mkopo wa 1M lakini nilijua wanaweza punguza kama walivyonifanyia mwanzo hivyo nikaona niongeze hii 500,000/-

Huyu dada alinizungusha sana, kila nikimpigia simu waje kunitembelea alikuwa haishi Sababu. Nikajua ni walewale wanaohitaji RUSHWA nilimtumia Tsh. 25,000/- ilikuwa ni J3 hiyo siku, wakaja kunitembelea J5.

Kama kawaida akanielekeza kwa Mwanasheria , sikufanya hivyo tena, nikaenda States Attorney. Na huu mkopo nimeumaliza.

Sasa nilipotaka mkopo mwingine nikaona kama kuna kukwepana sana , nikamtuma MKE wangu, yeye ni mtumishi wa Umma. (Mwalimu) nikamwambia aende akope 2M.

Wameomba LAKI TATU ili waweze kutoa huu mkopo. Huyu dada anayeitwa Elice akiwa ni Mmoja wao.
Naomba ushauri Ndugu zangu.

Naomba kuwasilisha.
Nakushauri kama ifuatavyo:
1. Chanzo cha yote hayo ni wewe mwenyewe kukubali kutoa Rushwa ili upate huduma,sheria ya kupambana na rushwa
inakutia hatiani.
2. Benki zote Tanzania zinagombania wateja,kama umetimiza masharti mkopo utapata,
3. Tafadhali wasiliana na ofisi ya kupambana na Rushwa pindi unapodaiwa rushwa kwenye huduma unayostahili
kuipata
 
Nmb karibia wote, mimi niliwahi omba laki tano bado wakaomba chochote, na wana kawaida ya kugomea, kuchelewa kutoa mkopo hadi uwape chochote. Wapo wanaoshirikiana na meneja wao, na pia meneja wengi wana kawaida ya kuficha uchafu unaofanywa na hawa vijana kuogopa kuchafua jina la benki. Ushahidi ninao, jina la meneja ninalo, jiba la loan ofiicer ninalo, jina la teller mwizi ninalo, jina la anayetangaza salio la wateja baa ninalo ila sina pa kulisemea, wote ni ndugu moja. Jirekebisheni, ushindani upo. Haiwezekani mimi naenda bar naambuwa na baameid salio langu halisi. Vijana wa siku hizi sijui tunaenda wapi.
 
Wewe ni muongo hakuna benki inatoa mkopo wa laki tano mpkaka milioni moja, tena eti umeweka hati a nyumba unajua gharama za kusajili hati ya nyumba ili ichukuliwe na bank we ni punga, utakuwa ulienda saccos ya wanyiha wenzio huko mbozi,
Lini mkopo wa laki 5 umefutwa huko NMB? Mkopo wa laki 5 upo achilia mbali hiyo 1m na marejesho yake ni miezi sita na endapo kumbukumbu zangu zipo sawa, marejsho ni sh. elfu themanini na tisa na hela fulani hapo juu!
 
Nenda Ofisi za PCCB hapo jirani, we umekalia chimpumu tu na ikyinde! Na usiwaambie kama ulishatoaga rushwa hapo awali wanaeza kukudaka manake nao sukihizi wananjaa kama polisi!

Ni walewale hakuna tofauti na Polisi au Mahakama.
 
Nakushauri kama ifuatavyo:
1. Chanzo cha yote hayo ni wewe mwenyewe kukubali kutoa Rushwa ili upate huduma,sheria ya kupambana na rushwa
inakutia hatiani.
2. Benki zote Tanzania zinagombania wateja,kama umetimiza masharti mkopo utapata,
3. Tafadhali wasiliana na ofisi ya kupambana na Rushwa pindi unapodaiwa rushwa kwenye huduma unayostahili
kuipata
Siwezi kumlaumu sana mdau kwa kulipa hiyo sh. 15,000/-( hela ya mafuta). Kwa mtu asiye ndani ya benki ni vigumu kufahamu kwamba Loan Officers wana fungu la kutembelea wateja. Loan Officers wengi huwa wanawatwishwa wateja mzigo wa kutembelea wakati kwa NMB kuna account inaitwa Business Travelling ambayo ndio inatoa fungu la usafiri kwa Loan Officers. Sasa wanachofanya, watamambia mteja agharamie usafiri lakini wakirudi ofisni wanaandika vocha ya Business Travelling na pesa wanaweka mfukoni!
 
Nmb karibia wote, mimi niliwahi omba laki tano bado wakaomba chochote, na wana kawaida ya kugomea, kuchelewa kutoa mkopo hadi uwape chochote. Wapo wanaoshirikiana na meneja wao, na pia meneja wengi wana kawaida ya kuficha uchafu unaofanywa na hawa vijana kuogopa kuchafua jina la benki. Ushahidi ninao, jina la meneja ninalo, jiba la loan ofiicer ninalo, jina la teller mwizi ninalo, jina la anayetangaza salio la wateja baa ninalo ila sina pa kulisemea, wote ni ndugu moja. Jirekebisheni, ushindani upo. Haiwezekani mimi naenda bar naambuwa na baameid salio langu halisi. Vijana wa siku hizi sijui tunaenda wapi.
Kama una ushahidi fikisha NMB House/HQ... trust me, baada ya hapo tulia wiki moja au mbili kisha fuatilia kuhusu hao jamaa kama hujaambiwa wamehama kumbe ndo washachinjiwa baharini! Tatizo letu ni kwamba huwa tunalalamika bila kuwa na tangible evidence... lakini pale ilipo, habaki mtu hapo lakini usitoe malalamiko kwa Branch Manager... hakuna kitakachofanyika... si kwamba hao mameneja wanapenda huo uchafu but trust me, kuchukua maamuzi ambayo unajua huyu mtu atafukuzwa kazi si jambo dogo... inahitaji ujasiri na moyo wa chuma hasa ukizingatia kwamba hawa watu wanaishi na kula pamoja!!!
Lakini ukipeleka malalamiko HQ, they don't care coz' huko hawawafahamu personally hao watu (staffs) kwahiyo inakuwa ni kama kumkoma nyani gladi!
 
Unaweza kujiona Unajua kumbe hujui, vitu vingine bora kukaa kimya kuficha utupu wako.
Watu wengine si wa kuwajibu... binafsi nilitaka kumjibu huyo mbwiga lakini nilijua ningemtolea maneno machafu kwahiyo nikaamua kuachana nae na kumpuuza manake anakera zaidi kiwango cha kukera kinachokubalika! Mijitu kama hiyo ni ile mipuuzi iliyopata vikazi vyenye kamshahara nafuu juzi juzi kwahiyo ndo basi tena wanajiona wameshapatia maisha.
 
mkopo wa milioni moja, mkopo wa laki tano unaenda bank ya NmB, duh, watanzania wana shidaaaaa, hiyo hela si ungekopa hata kwa rafiki yako tu jamani. pengine nmb wameona ni hasara, mikopo midogo hiyo hawawezi kukuthamini kwasababu una faida kidogo sana kwao ndio maana unaona kama wanakuonea. nenda saccos au upatu wa mtaani huko au weka hela kwenye kibubu, laki tano haustahili kwenda kukopa bank. tuache utani jamani. hata milioni moja au mbili unaenda bank? hizo hata waendesha bodaboda wanazo majumbani mwao, kwanini mnapenda kunia madogo kiasi hicho, think big, act big....alaaa.

heri yako wewe ulienazo. Lakini chunhanga ulimi.
 
Weeee Wewewewe, vijamaa vya kariakoo vinaomba rushwa balaa, niliwahi kuvishitakia kwa meneja wao mwanamke akasema atawaonya baadaye file likatupwa nje, NMB Riba yao mkombozi lakini kupata mkopo bila rushwa bora ukalale utupu barabarani. lakini siku hizi vi-benki vyote viko hivyo kasoro ACB ndio wamekomesha, kuna Advance, ACCES Lumumba hawa balaa, matangazomengi lakini rushwa wako mbele, ukichukua mkopo wanatoka nje kukuwinda pale Riki hotel, alafu wanajifanya mkurugenzi anataka maji ya kunywa , kikawauliza kiasi gani eti laki mbili nikawapa 150,000 kwa kupata 1,500,000.00 mwezi uliofuata nikachelewesha siku moja makusudi, simu zilipigwa kama mvua.

Hapa ndio mahali pake weka mtandao wote hapa washawishi na wengine.
 
Lini mkopo wa laki 5 umefutwa huko NMB? Mkopo wa laki 5 upo achilia mbali hiyo 1m na marejesho yake ni miezi sita na endapo kumbukumbu zangu zipo sawa, marejsho ni sh. elfu themanini na tisa na hela fulani hapo juu!

katika hiyo lakini tano...elfu hamsini lazima umwachie afisa mikopo, bila hivyo hupati. That is NMB woking value.
 
We pwapwasa acha kuchafua majina ya watu kidwanzi!hiyo 25000 hukuombwa na ndio mana umeshindwa sema sababu ulizokuwa unapewa hadi ukafikiria unazungushwa sana na kwamba wote ni walewale wanaotaka rushwa.
Pili,mikopo ya biashara na ya watumishi inashughulikiwa na maafisa mikopo tofauti,onesha alice ANAHUSIKAJE kwenye kuombwa rushwa mkeo ambae ni mtumishi na wewe ni mfanyabiashara.
Tatu,wewe ni mnafiki sana!wasema TRA uliwatengea kabisa pesa ya rushwa,sasa hapa umekuja kufanya nini wakati ndio 'michezo' yako?
Usivyo na haya unadiriki kutaja hata jina la mtu eti alikuomba unachokiita rushwa ya 15000 ya mafuta,mwaka mmoja na nusu uliopita!!unajielewa wewe kweli?
Jitazame sana wewe pwapwasa!
 
nmb kote hawachekani tawi la kigoma alikuwepo anaitwa oliva mwanaume nami ni mtumishi niliomba m4 alchukua laki 2 urasimu huo upo na bado unaendelea kwani mara nyngne huhusisha hadi branch manager sijui tukimbilie wap jamaani
 
We pwapwasa acha kuchafua majina ya watu kidwanzi!hiyo 25000 hukuombwa na ndio mana umeshindwa sema sababu ulizokuwa unapewa hadi ukafikiria unazungushwa sana na kwamba wote ni walewale wanaotaka rushwa.
Pili,mikopo ya biashara na ya watumishi inashughulikiwa na maafisa mikopo tofauti,onesha alice ANAHUSIKAJE kwenye kuombwa rushwa mkeo ambae ni mtumishi na wewe ni mfanyabiashara.
Tatu,wewe ni mnafiki sana!wasema TRA uliwatengea kabisa pesa ya rushwa,sasa hapa umekuja kufanya nini wakati ndio 'michezo' yako?
Usivyo na haya unadiriki kutaja hata jina la mtu eti alikuomba unachokiita rushwa ya 15000 ya mafuta,mwaka mmoja na nusu uliopita!!unajielewa wewe kweli?
Jitazame sana wewe pwapwasa!

Ungesoma kwa umakini ungejiona wewe ndio pwapwasa.
 
tusifichane idara za mikopo karibu mabenk yote na branches zake zinanuka rushwa shida ya staffs wa NMB wanaomba rushwa hata kwa wasiokuwa na uwezo wa kutoa rushwa
 
We pwapwasa acha kuchafua majina ya watu kidwanzi!hiyo 25000 hukuombwa na ndio mana umeshindwa sema sababu ulizokuwa unapewa hadi ukafikiria unazungushwa sana na kwamba wote ni walewale wanaotaka rushwa.
Pili,mikopo ya biashara na ya watumishi inashughulikiwa na maafisa mikopo tofauti,onesha alice ANAHUSIKAJE kwenye kuombwa rushwa mkeo ambae ni mtumishi na wewe ni mfanyabiashara.
Tatu,wewe ni mnafiki sana!wasema TRA uliwatengea kabisa pesa ya rushwa,sasa hapa umekuja kufanya nini wakati ndio 'michezo' yako?
Usivyo na haya unadiriki kutaja hata jina la mtu eti alikuomba unachokiita rushwa ya 15000 ya mafuta,mwaka mmoja na nusu uliopita!!unajielewa wewe kweli?
Jitazame sana wewe pwapwasa!

Hopeless.
 
nmb kote hawachekani tawi la kigoma alikuwepo anaitwa oliva mwanaume nami ni mtumishi niliomba m4 alchukua laki 2 urasimu huo upo na bado unaendelea kwani mara nyngne huhusisha hadi branch manager sijui tukimbilie wap jamaani

kama mimi sikupi
 
Back
Top Bottom