NMB Idara ya mikopo Rushwa imekithiri

NMB Idara ya mikopo Rushwa imekithiri

Wewe ni muongo hakuna benki inatoa mkopo wa laki tano mpkaka milioni moja, tena eti umeweka hati a nyumba unajua gharama za kusajili hati ya nyumba ili ichukuliwe na bank we ni punga, utakuwa ulienda saccos ya wanyiha wenzio huko mbozi,
 
Nenda Ofisi za PCCB hapo jirani, we umekalia chimpumu tu na ikyinde! Na usiwaambie kama ulishatoaga rushwa hapo awali wanaeza kukudaka manake nao sukihizi wananjaa kama polisi!

Hapo penye red imenipasua mbavu!
 
wahame hao km vipi!nenda kungine
mbona wa mtwara hawako hvyoo?!
 
mkopo wa milioni moja, mkopo wa laki tano unaenda bank ya NmB, duh, watanzania wana shidaaaaa, hiyo hela si ungekopa hata kwa rafiki yako tu jamani. pengine nmb wameona ni hasara, mikopo midogo hiyo hawawezi kukuthamini kwasababu una faida kidogo sana kwao ndio maana unaona kama wanakuonea. nenda saccos au upatu wa mtaani huko au weka hela kwenye kibubu, laki tano haustahili kwenda kukopa bank. tuache utani jamani. hata milioni moja au mbili unaenda bank? hizo hata waendesha bodaboda wanazo majumbani mwao, kwanini mnapenda kunia madogo kiasi hicho, think big, act big....alaaa.

acha dharau. Wewe huyajui maisha. Unakula ugali wa bure kwa dingi yako na kukupa vijisent unakuja kuleta dharau. Mkopeshe wewe hapo ulipo hata mia huna mfukoni kazi kubwabwaja2.
 
Nenda Ofisi za PCCB hapo jirani, we umekalia chimpumu tu na ikyinde! Na usiwaambie kama ulishatoaga rushwa hapo awali wanaeza kukudaka manake nao sukihizi wananjaa kama polisi!

Hao PCCB unawaamini?
 
Wewe ni muongo hakuna benki inatoa mkopo wa laki tano mpkaka milioni moja, tena eti umeweka hati a nyumba unajua gharama za kusajili hati ya nyumba ili ichukuliwe na bank we ni punga, utakuwa ulienda saccos ya wanyiha wenzio huko mbozi,

Hulijui ulisemalo ndugu yangu, ama nawe ni mmoja wa hawa wanaonizungusha?
Kwa kukusaidia tu,
Awamu hii nilipoenda walidai ili niupate huo mkopo nahitaji kufungua A/C mpya Bank na Shilingi laki Mbili deposit kwa mkopo wa 2M au laki moja kwa 1M.
 
Nenda Ofisi za PCCB hapo jirani, we umekalia chimpumu tu na ikyinde! Na usiwaambie kama ulishatoaga rushwa hapo awali wanaeza kukudaka manake nao sukihizi wananjaa kama polisi!

Ahsante kwa Ushauri, ila hivyo viywaji situmii Mkuu.
 
Tawi la Kariakoo kuna jamaa anaitwa Julius
Weeee Wewewewe, vijamaa vya kariakoo vinaomba rushwa balaa, niliwahi kuvishitakia kwa meneja wao mwanamke akasema atawaonya baadaye file likatupwa nje, NMB Riba yao mkombozi lakini kupata mkopo bila rushwa bora ukalale utupu barabarani. lakini siku hizi vi-benki vyote viko hivyo kasoro ACB ndio wamekomesha, kuna Advance, ACCES Lumumba hawa balaa, matangazomengi lakini rushwa wako mbele, ukichukua mkopo wanatoka nje kukuwinda pale Riki hotel, alafu wanajifanya mkurugenzi anataka maji ya kunywa , kikawauliza kiasi gani eti laki mbili nikawapa 150,000 kwa kupata 1,500,000.00 mwezi uliofuata nikachelewesha siku moja makusudi, simu zilipigwa kama mvua.
 
mkopo wa milioni moja, mkopo wa laki tano unaenda bank ya NmB, duh, watanzania wana shidaaaaa, hiyo hela si ungekopa hata kwa rafiki yako tu jamani. pengine nmb wameona ni hasara, mikopo midogo hiyo hawawezi kukuthamini kwasababu una faida kidogo sana kwao ndio maana unaona kama wanakuonea. nenda saccos au upatu wa mtaani huko au weka hela kwenye kibubu, laki tano haustahili kwenda kukopa bank. tuache utani jamani. hata milioni moja au mbili unaenda bank? hizo hata waendesha bodaboda wanazo majumbani mwao, kwanini mnapenda kunia madogo kiasi hicho, think big, act big....alaaa.
Mkopo wa laki tano ukitolewa kwa watu elfu kumi wa kipato cha chini baada ya mwaka benki itapata faida si chini milioni miatano na hiyo ni baada ya kutoa gharama. Hao wateja wadogo wadogo unao wadharau Barkhesa ndo wanamfanya bilionea. Wake up ndugu yangu. Na pia wanaothink big hawazadharau hata senti kumi. Inaonyesha haupo katika wanaothink big
 
Mkopo wa laki tano ukitolewa kwa watu elfu kumi wa kipato cha chini baada ya mwaka benki itapata faida si chini milioni miatano na hiyo ni baada ya kutoa gharama. Hao wateja wadogo wadogo unao wadharau Barkhesa ndo wanamfanya bilionea. Wake up ndugu yangu. Na pia wanaothink big hawazadharau hata senti kumi. Inaonyesha haupo katika wanaothink big

aise ndugu umensaidia kumjibu huyu bwana.maana nilikuwa natafuta kiki ya kumtoa baru....anadharau wakopaji wadogo?hajui nchango wa microfinancing katika mapato ya banking sector?ngoja niishie hapa.alaf kadharau sana ..eti muwe great thinkers.....sTART SMALL..THINK BIG NDIO OPTION
 
Hii bank inalalamikiwa sina sy tawi hilo tu la mbalizi ila mpk matawi mengine
Wahusika fanyeni mabadiliko
 
Naomba ushauri nifanyaje, hata kama wataninyima lakini niweze kutumbua jipu la urasimu huu.

Nenda takukuru ofisi ya karibu waeleze watakusaidia kumuadabisha huyo mla rushwa, ila unaweza ukaanza na uongozi wa juu wa hapo Benji kuwaeleza kama ni viongozi wenye sifa watakusaidia pia
 
bank ya NMB nilipewa mkopo 15m rushwa nilitoa laki 5 ,
sasa nimeamua kuamishia majeshi bank ya post kule jamaa wako poa sana jamaa yangu kashepewa 10m na amewapa 40,000 tu

Dah! Tanzania iko kazi
 
mkkuu, fanya kitu kimoja, wale usipate nao shida hao staff wa nmb, na wala usiende kwa meneja wake, maana lao huenda likawa moja, fanya hivi, ingia kwenye website ya nmb, kuna sehemu imeandikwa ya kutolea maoni, weka maoni yako pale na taja jina la huyo staff, na branch hukika, moja kwa moja hayo malaliko yanaenda kwa wenye benk wazungu. Mda si mrefu atatimuliwa huyo mtu..... Maana tukiendekeza huu ujinga, watazoeya hawa watu, au ukiona vip wakiendelea, tutaweka hapa jamvini namba za zone meneger zao, maana hawa wana zone katika utawala.
 
mkkuu, fanya kitu kimoja, wale usipate nao shida hao staff wa nmb, na wala usiende kwa meneja wake, maana lao huenda likawa moja, fanya hivi, ingia kwenye website ya nmb, kuna sehemu imeandikwa ya kutolea maoni, weka maoni yako pale na taja jina la huyo staff, na branch hukika, moja kwa moja hayo malaliko yanaenda kwa wenye benk wazungu. Mda si mrefu atatimuliwa huyo mtu..... Maana tukiendekeza huu ujinga, watazoeya hawa watu, au ukiona vip wakiendelea, tutaweka hapa jamvini namba za zone meneger zao, maana hawa wana zone katika utawala.

Naufanyia kazi huu ushauri, nitarudi kwa mrejesho Mkuu.
 
Hiyo ni kila nmb ndivyo wanafanya. leo nilienda ludewa nashangaa afisa mikopo anaanzo ooo soda mara nn duu!
 
Back
Top Bottom