Njoo uniunganishie dot tafadhali

Alilipa shilingi ngapi kwa mganga?

Unaweza kukuta hiyo simu ni huawei ascend y320 na halafu mganga amemuomba apeleke mbuzi mzima, kuku, mchele kilo tano, mkaa, pesa ya kiingilio jumlisha pesa ya kazi, nauli(unaweza kuta wanaishi mbali sana kwa kila mmoja), ongeza na hasara ya muda alioutumia kufuatilia hilo suala utaona ni zaidi ya gharama ya simu ilimfanya aende kwa sangoma.
 
Uchawi upo na unaconnection na waaminio....Mimi nahisi siwezi logeka kwa Imani yangu niliyonayo.
 
Kwakua nilikuwa natoka sikupata muda wakumdadis vizur, ila nikirudi nitamuulza ili anipeleke siku ukiniudhi nikugeuze popo

Basi sawa. Ila kama mganga ni jirani basi ujue aliichukua yeye na alijua huyo mshirikina lazima amfuate (labda ndo huwa anamuwangia kila mara)... akajichukulia chake mapema.... yani kama CCM vile
 
mimi nahisi mganga aliiba hiyo simu ili aende kupeleka hela halafu airudishe
 
Hiko kiinimacho...yeye anadhani anatumia simuyake kumbe kawekewa uume/nyeti za mtu
 
Ndio maana siamini kwenye nguvu za giza.

Full kudanganyana.

Kama umeibiwa simu basi mtafute mwizi, ukimkosa basi nunua nyingine.

Ila hii ya kwenda kwa mganga ni kujidanganya.

Wew acha uoga, kule wao wanagawa utajiri wakati wao maskini.
 
Waganga wengi kama siyo wote wanaodai kurudisha mali zilizoibiwa huwa ni wanamtandao wa vibaka. Ukipeleka shida yako atakuambia njoo kesho kisha huku nyuma anatuma kikosi kufuatilia na mali ikipatikana anafika bei na washikaji. Kesho yake ukija unapewa muda na mahali utakapoikuta mali yako na unamuachia chake kama kawaida.
Mademu wanaohisi wana gundu yaani hawatongozwi nao huwa wanaingizwa mjini kwa mfumo unaofanana na huo.
Ila watu wa CCM nao kwa kupenda mambo ya masangoma balaa.
 
Hapo ni kuwa Mganga anafanyiwa "promo" na muhusika ili ninyi msioamini mjue mganga ni mkali muende mkapeke fedha zenu na aliyewaonesha huko anapata 10%.
 

Waganga wana hila sana.

Mganga anaweza kukwambia mama yako mchawi na anakuroga.
 

Jamani kwani kwenda kwa mganga ni kesi hadi nitafute, support??? Anyway nimetoka mzuzu kuna waganga hata ukitaka kumgemza mtu nyoka unaweza. Miaka nenda rudi sionagi ukweli wao.

Nimeuliza nataka kujua tu wala si uwezavyo
 
Last edited by a moderator:

Sim ya laki na nusu ila wao nimesikia wanawaambia watu eti walinunua ni laki 5. Wakati ni visamsung uchwara.

Kesho lazima akapeleke shukrani.
 

Wew umeunganisha dot nilivyotaka mim, hili ndio hasaa nimelihisi, maana etii mganga alimuuliza "unahisi nani kachukua" mama ccm akawataja vijana wawali ambao wanaendaga sana kwake.
 
Basi sawa. Ila kama mganga ni jirani basi ujue aliichukua yeye na alijua huyo mshirikina lazima amfuate (labda ndo huwa anamuwangia kila mara)... akajichukulia chake mapema.... yani kama CCM vile

Mganga walenda mbali, kule ninakokaa sijawah sikia mganga.
 

Mmmh!!!! Kwa hyo mchawi na mganga ni sawa???? Bado hujaniunganishia dot, mganga alifikaje kumwambia kibaka arudishe sim! Haka kasehemu funguka kitaalam
 
Tabia ya makada wa sisiem kwenda kwa waganga hiyo sasa imewaingia kwenye damu
 
Mmmh!!!! Kwa hyo mchawi na mganga ni sawa???? Bado hujaniunganishia dot, mganga alifikaje kumwambia kibaka arudishe sim! Haka kasehemu funguka kitaalam

Mchawi anaharibu mganga anarekebisha... Waganga baadhi yao huwa na mawasiliano na Ulimwengu wa roho na kwa kutumia mapepo au mizimu au majini huweza kuamrisha chochote na kikafanyika
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…