je kati ya hawa vijana, masonga,lulandala, nyagawa, kazimoto na rose mayemba, nani atanguzruma kupitia chadema 2015. Maoni yenu nani anafaa ni muhimu pia.ni katika jimbo la njombe mjini.
Why, sijajua ni kwanini umekuja na uchambuzi huu...of course si lazima mtoa mada yeyote humu jukwaani watu wajue kwanini ametoa mada husika. Lakini ni machache ya kuzungumza kwa faida yako na wengine wenye mtazamo kama wako kuhusu Njombe Kusini.
1. Kwsasa si wakati wa kuwajua na kuchambua wataopeperusha bendera ya CHADEMA Njombe Kusini, wakati wa kujenga na kuimarisha Chama katika ngazi ya Kata na Vitongoji hadi Misingi. Ikiwa ni mkazi wa Jimbo hilo unatakiwa kufahamu kuwa kuna vitongoji CCM kimekuwa kama chama cha ukoo.
2. Majina ya wagombea kupitia CHADEMA yatajulikana na kupigiwa kura 2015 na wanachama wenyewe: Yakijumuisha majina yale ya wale walioonyesha nia na kutuma CV zao Makao Makuu pamoja na wale watakaoibuka wakati ukifika huko huko Njombe. Ndipo wanachama watachambua nani anafaa. Kigezo kimojawapo tutawapima katika michango yao kwenye ujenzi wa Chama. Mara nyingi si mara zote, asiyeshiriki ujenzi huwa haumizwi akiambiwa unakiua chama, hufanya anayotaka yeye.
3. Mtindo wa kujitangaza mapema unamfanya muhusika kuwa target nzuri kwenye kuangushwa na CCM. Msifikiri wanalala....muulizeni Nyagawa (Alatanga ) japo kwa ufupi namna propaganda na mbinu chafu dhidi yake zilivyotumiwa na timu ya Makweta (R.I.P.) na ya Deo Sanga (Jah People). Halafu kajifunze zile za Njombe Magharibi.
4. Iko wazi kuwa Deo Mwanyika (yule wa Barrick Gold) anataka kugombea Ubunge kupitia CCM. [Kumbuka 2010 Makinda na waliomuweka Makinda walimwambia zamu yake nu 2015]. Sasa timu yake Mwanyika inakazana sana kupenyeza mamluki na kutaka kujua nani atakuwa tishio kwao. Hivyo vi tisheti wanavyovalishwa vijana wa Njombe sasa na vimisaada uchwara si bure. Kuna karata zinachangwa. Msiwe wepesi wa kuonyesha silaha zenu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.