BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
WARAKA KUTOKA KWA MWENYEKITI WA CHADEMA NJOMBE, BIBI ROSE MAYEMBA KWENDA KWA ASKOFU MWAMAKULA.
Hello Bishop! Heshima yako!
Ninaitwa Rose Mayemba, Mwenyekiti wa CHADEMA Njombe. Leo tarehe 3 Septemba 2020, tumetoka gerezani hapa Njombe ambako tulikwenda kuwasalimia wenzetu, story zao zinatisha sana.Wanasema walipigwa na kuteswa sana huku wakilazimishwa wamtaje Mgombea wa Ubunge Emmanuel Masonga, Mwenyekiti wa Mkoa wa Njombe, Bi Rose Mayemba na Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe kuwa wamewatuma kufanya mauaji. Wanafuatilia simu zetu zote muda wote kututafutia makosa ya kutuweka ndani.
Walipelekwa kwa Mlinzi wa Amani wakiwa chini ya ulinzi mkali na kutishiwa kuvunjwa miguu kama watakataa kuhusika na mauaji hayo hivyo kila mahali walipohojiwa walilazimika kukubali ili kukwepa maumivu. Leo tulipowaona walikuwa bado wanachechemea huku wakilalamika kwamba uti wa mgongo bado una maumivu makali...
Lakini wanawasalimia sana wanasema wao wako imara. Wanaomba msife moyo. Wanaamini haya ni mapito tu hivyo iko siku yatakwisha.
Aliyekuwa anazungumza na sisi wawili (mimi na Mgombea Ubunge) ni George Sanga ambaye ni mtuhumiwa na pia Mgombea wa Udiwani katika Kata mojawapo na Katibu wa CHADEMA Jimbo la Njombe Mjini na alikuwa anawakilisha watuhumiwa wenzake. Lakini waliokuwa wanasikia ni wengi maana tuliingia pia na Mchungaji wa kanisa lake na mkewe na watu wengine wengi...
Hello Bishop! Heshima yako!
Ninaitwa Rose Mayemba, Mwenyekiti wa CHADEMA Njombe. Leo tarehe 3 Septemba 2020, tumetoka gerezani hapa Njombe ambako tulikwenda kuwasalimia wenzetu, story zao zinatisha sana.Wanasema walipigwa na kuteswa sana huku wakilazimishwa wamtaje Mgombea wa Ubunge Emmanuel Masonga, Mwenyekiti wa Mkoa wa Njombe, Bi Rose Mayemba na Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe kuwa wamewatuma kufanya mauaji. Wanafuatilia simu zetu zote muda wote kututafutia makosa ya kutuweka ndani.
Walipelekwa kwa Mlinzi wa Amani wakiwa chini ya ulinzi mkali na kutishiwa kuvunjwa miguu kama watakataa kuhusika na mauaji hayo hivyo kila mahali walipohojiwa walilazimika kukubali ili kukwepa maumivu. Leo tulipowaona walikuwa bado wanachechemea huku wakilalamika kwamba uti wa mgongo bado una maumivu makali...
Lakini wanawasalimia sana wanasema wao wako imara. Wanaomba msife moyo. Wanaamini haya ni mapito tu hivyo iko siku yatakwisha.
Aliyekuwa anazungumza na sisi wawili (mimi na Mgombea Ubunge) ni George Sanga ambaye ni mtuhumiwa na pia Mgombea wa Udiwani katika Kata mojawapo na Katibu wa CHADEMA Jimbo la Njombe Mjini na alikuwa anawakilisha watuhumiwa wenzake. Lakini waliokuwa wanasikia ni wengi maana tuliingia pia na Mchungaji wa kanisa lake na mkewe na watu wengine wengi...