Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,600
- 217,999
Taarifa iliyotolewa na Chadema Mkoa wa Njombe inaeleza kwamba , miongoni mwa Watu 9 ambao ni wanakwaya waliopata ajali na kufariki huko Njombe , baada ya gari waliyokuwemo kugongana na Lori , ni wanachama wake , na kwamba CHADEMA NJOMBE IMEPATA PIGO KUBWA KWA KUONDOKEWA NA MAKAMANDA WAKE KATIKATI YA MAPAMBANO YA KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI .
Kwa niaba ya wanachadema wote duniani Na kwa vile kupigania Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi ni sawa na Kutenda Kazi ya Mungu , Basi nichukue nafasi hii kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai wa watu hawa aliyotupatia kwenye mapambano ya haki na namuomba Mwenyezi Mungu azipumzishe roho za Marehemu hao Mahali Pema Peponi , Amina .
Kwa niaba ya wanachadema wote duniani Na kwa vile kupigania Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi ni sawa na Kutenda Kazi ya Mungu , Basi nichukue nafasi hii kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai wa watu hawa aliyotupatia kwenye mapambano ya haki na namuomba Mwenyezi Mungu azipumzishe roho za Marehemu hao Mahali Pema Peponi , Amina .