Mimi binafsi naamini kutapeliwa ni jambo unalolipanga mwenyewe. Hivi kweli umehangaika miaka mingi kutafuta pesa halafu leo mtu tu from no where anakutapeli?!.
Viwanja vilivyopimwa kwa Dar kwa mfano ni aghali sana na watu wanataka rahisi. Hii kazi ya kuuza viwanja kwa Dar ina changamoto sana na si rahisi kihivyo. Mimi ninakutana na mteja anataka kiwanja cha milioni tano halafu maeneo anayokutajia anataka huwezi kupata hata cha milioni 15, ukimtajia wapi atapata hicho cha milioni 5 anaona unamdanganya. Kuna maeneo hapa kiwanja tu si chini ya milioni 100. Kama wasemavyo watu siku zote vizuri ni gharama.
Ni kweli utasisitiza kiwanja kiwe na hati lakini watakaomudu bei yake ni wachache sana na kwa mazingira ya sasa huwezi kwani sehemu kubwa ya ardhi haijapimwa. Kuna ofisi za ardhi ngazi ya kijiji/mtaa hadi wizara ya ardhi hapa hapa, ni rahisi kwa mkazi wa Dar kufuatilia mwenyewe binafsi kimya kimya na kufanikiwa kutambua iwapo kiwanja kina mgogoro au la, huwezi kutoka mwanza leo kwa kutumia tangazo la jf moja kwa moja unaenda kununua kiwanja Dar! utatapeliwa tu, chukuwa muda na peleleza vya kutosha kabla.
Nadhani wengine waendelee kuchangia hatua za kufuatwa iwapo utaamua kununua chenye hati au kisicho na hati kwa manufaa ya sisi sote.