Njia nyembamba (Simulizi mpya by SteveMollel)

Njia nyembamba (Simulizi mpya by SteveMollel)

[HASHTAG]#stevemollel[/HASHTAG] Asante sana endelea kutupa burudani ndugu


Asanteeeh

naisubiri kwa hamu

unanimissije bila story tivu halaf ratiba ipoje siku ipi na ipi

alhamisi leo natarajia mzigo utatoka steve

Baba nitag namimi

Tuko pamoja mkuu,

daaaaaaaa nashukuru mkuu aseeee

Hii hadithi nimeikubali sana mkuu naomba unitag ukishusha vitu

Daah story Ni Moto wa kuotea mbalii,,hongera Sana ndugu,,

Hn. Steve umenifanya nainze kuvutiwa tena kuwa karibu na phone yangu, pa1 xna ktk tag man, tunaisubiri.

Usinisahau Mzee babaa Kuni tawisee..!! [HASHTAG]#KuniTag[/HASHTAG]
Karibuni jamvini.




☆Steve
 
Asante mkuu ,,,sema naona Kama tunasubiri Sana kwann usingerusha hata mara3 kwa week ,,wazo tuu maana tunasubiri kunapoa mpk kunasahaulika
 
NJIA NYEMBAMBA --- 04





Mtunzi: Steve Mollel




No: 0685 758 123








****










Baada ya siku tatu tangu tukio la kutekwa kwa watoto lipate kufanyika, picha za Amadu, Talib na Chui zilitandazwa mitandaoni na kwenye kila chombo cha habari cha Sierra Leone huku dau nono likitangazwa kwa yeyote atakayefanisha kukamatwa kwa magaidi hao wa MDR.
Zaidi ya hapo, ikiwa ni kwa chini chini, serikali ya Sierra Leone kwa kupitia wakubwa wa jeshi wakawateua wanaume makomando saba kwa ajili ya tukio la kwenda kuvamia nchini Guinea kutafuta na kuvamia kambi ya waasi wa MDR. Makomando hao wakakutana na kupewa maelekezo. Wakahaidiwa kulipwa pesa nzuri kama wangelifanikisha kile walichotumwa.
Basi yakawa hayo. Ilipohitimu siku ya nne rasmi tangu watoto wa shule watekwe, makomando wakajitwika kila aina ya silaha wakaanza safari kuelekea walipotakiwa kwenda kutimiza walichoagizwa.
Huko nchini Guinea ndani ya kambi ya MDR, hakuna hata aliyeotea nini kitatokea siku hiyo ndani ya masaa machache yajayo. Shughuli zilikuwa zinaendelea kama kawaida, wengine wakifanya mazoezi na wengine wakifanya kazi kama vile kukata kuni, kuchimba mashimo ya choo na kadhalika. Amadu, Chui na Farah walikuwa pembezoni ya mto wakiwa wanafua nguo zao za kijeshi, mwilini walikuwa wamevalia nguo za kiraia, Amadu alikuwa kavalia bukta fupi ya kaki na shati jeupe jepesi, Chui alikuwa kavalia kaushi na bukta iliyokatwa toka kwenye suruali nyeusi ya kitambaa na Farah alikuwa kavalia kaushi nyeusi na suruali kavu ya jeans iliyochoka.
Wakati wakifua, walikuwa wanaongea habari za hapa na pale ila hasa juu ya ishu ya watoto wale waliotekwa. Amadu akionekana bado kutopendezwa na lile jambo.
“Mazoezi wanayowafanyisha wale watoto ni makali mno ukilinganisha na umri wao, nadhani general inabidi aambiwe.” Amadu alisema huku akifikicha nguo zake. Farah akatikisa kichwa.
“Unadhani italeta mabadiliko yoyote? … General anafahamu kinachoendelea. Na hakuna linalofanyika pasipo yeye kuruhusu.”
“Mmmh mmh. Lazima lifanyike jambo, Farah. Wale watoto wanakula mlo mmoja tu. Kuanzia asubuhi mpaka jioni wanafanya mazoezi, si kuuana huko? Tena mazoezi makali.”
“Ni kumshauri tu, general, anaweza akaelewa.” Chui alichangia.
“Tatizo ni kwamba, hakuna chakula cha kutosha stoo kuwalisha watoto wote wale. Najua hilo, sasa si tumeleta kuja kuwaua watoto wa watu!” Amadu alifunguka, akisema kwa mjazo.
“Tatizo mkuu ametaka kusolve tatizo kwa haraka bila kutazama kama anatengeneza tatizo jingine tena kubwa tu. Sasa hawa watoto watatufia huku. Jana tu yenyewe wamekufa watatu, ona.” Farah alisema.
“Sasa angefanyaje?” Chui aliuliza.
“Angetuliza kichwa zaidi. Hakutakuwa kukurupuka. Naona tunawaumiza tu wenzetu wasio hata na hatia. Huoni kama tunatengeneza mduara wa visasi?” Amadu aliuliza.
“Ni kweli.” Chui akajibu. Farah akaongezea;
“Unachokiongea kina ukweli ndani yake. Ila sasa hatuna la kufanya.”
“Hapana. Lazima liwepo. Ni kitendo cha muda tu.” Amadu alifafanua. Hakuna tena aliyeongea, malalamiko ya maji tu ya mto ndio yakawa yanasikika. Walimaliza kufua wakawa wanasuuza sasa. Na hapo ndipo wakasikia mlio wa risasi kwanguvu.
“Imetokea wapi hiyo?” Farah aliwahi kuuliza. Chui akanyooshea kidole muelekeo wa kambini na kusema;
“Watakuwa wanafanya mazoezi hao.”
“Mazoezi na bunduki za ukweli? Leo sio siku ya kulenga shabaha.” Amadu alieleza. Mara milio ya risasi ikaanza kufululiza kama matone ya mvua. Amadu na wenzake walificha nguo zao wakaanza safari kurudi kambini kwa tahadhari. Hawakuwa na silaha yoyote.
Kadiri walivyokuwa wanasonga kuelekea kambini, sauti za milio ya bunduki ndiyo ikawa inavuma kwanguvu. Wakaanza kusikia na vilio vya watoto! Walisogea na kusogea, mara wakamuona mwanaume mmoja akiwa ameshikilia bunduki.
“Tumevamiwa!” Amadu akasema kwa sauti ya chini. Walijibanza kwenye kichaka wakimtizama mwanaume yule aliyekuwa anarusha macho yake huku na huko akielekezea bunduki anapopatizama. Amadu akaokota jiwe kubwa akarusha na kumbamiza kwa nguvu mwanaume yule, ambaye pasipo jadili alikuwa ni komando wa Sierra, mwanaume yule akadondoka chini na kuzirai, Amadu akachukua bunduki wakasonga mbele, bado wakitembea kwa tahadhari kubwa.
Walipofika kambini wakakuta vita kubwa. Risasi zilikuwa zinarushwa huku na huko, na miili ya wafuasi wa MDR ikiwa imezagaa, michache ya makomandoo wa Sierra Leone. Chui na Farah nao wakatwaa bunduki, wakaendeleza mapambano. Walitumia utatu wao vyema kwa kujilinda na kushambulia. Walitengeneza kamduara wakipeana migongo, taratibu wakawa wanasogea huku wakishambulia.
Baada ya dakika kama thelathini, kukawa kimya. Milio ya bunduki ilipumzika. Makomando wote kumi wa Sierra Leone walikuwa chini. Kengele ya wafuasi wa MDR iligongwa, wote waliokuwa hai wakakutana eneo moja la makutano. Kessy akasimama mbele yao.
“Tumeshambuliwa na wanajeshi wa Sierra Leone, mpaka sasa tumepoteza wenzetu hamsini kamili. Ni loss kubwa mno. Zaidi ya hapo, tumepoteza watoto kumi na mbili kati ya arobaini walioletwa. Nayo pia ni loss kubwa. Tunachohitaji ni kuwa pamoja katika kipindi hiki kigumu, na tamko toka kwa mkuu litatolewa muda si mrefu. Kwa sasa, twende tukawapumzishe wenzetu.”
Baada ya tamko hilo, miili ya wafuasi wa MDR waliokufa ikabebwa na kwenda kuzikwa. Kama ilivyo ada wakati wa maziko, nyimbo za mapinduzi zikawa zinaimbwa. Machozi yalishuka kwenye baadhi ya macho ya wafuasi hao. Zoezi lilipokamilika, wote wakawapa migongo wafu na kuondoka zao.
Baadae mida ya jioni jua likielekea kuzama, Assessoko akaja kambini kukutana na General Kessy. Uso wake ulikuwa umejikunja, kabla hata hawajapeana salamu, alibamiza meza kwanguvu na ngumi yake kubwa. Kessy akaanza kuelezea;
“Ilikuwa ni shambulizi la kushtukiza, mkuu. Hakukuwa na jinsi.”
“Hakukuwa na jinsi hatutuokoa na kuangamia, Kessy! Ina maana mfumo wenu wa ulinzi haupo sawa. Inakuaje mnastukizwa na kuuwawa hivyo!”
Kessy akatizama chini asiseme jambo.
“Hapa unavyoniona nimetoka kuonana na raisi wa Guinea, hataki kutuona nchini kwake tena. Vyombo vyote vya habari vinaisakama serikali yake kwa kuwaficha waasi. Si siri tena! Hakuna tena mjadala, wote kesho tunahamia Kabala!”
“Sasa mkuu, vipi kuhusu hawa watoto? … Nao watapelekwa huko?”
“Hapana. Mateka tutakwenda nao, ila watoto watabaki huku chini ya jeshi la Guinea. Kessy, mpaka sasa hatujapiga hatua yeyote kuonyesha tunataka kuuchukua utawala wa Sierra Leone. Tumeganda pale pale, hatuna madhara kabisa! … Simaanishi madhara kama haya ya kuteka watoto, la hasha, madhara makubwa. Nadhani sasa ni wakati wa kuwa na madhara makubwa. Le tueurs wa Liberia wanatushinda. Mpaka sasa wameshaweka karibia nusu na robo ya Liberia, kwanini sisi tumeganda hapo hapo? Wafadhili wetu wamekuwa wagumu kutoa pesa kwakuwa hawaoni tena impact. Inabidi tuwape sababu ya wao kutuamini sasa.”
“Sawa, mkuu. Nimekuelewa.”
Assessoko alishusha pumzi ndefu akakuna kidevu chake.
“Kuna vijana wangu watatu nimewaona kwenye runinga wanatafutwa. Wako wapi?”
“Wapo mahemani mwao.”
“Naweza nikawaona. Inaelekea ni watu wa kazi sana. Maelezo yao yanayotolewa kwenye vyombo vya habari yanaonyesha wana uwezo mkubwa.”
“Acha niwaite.”
Punde, Amadu, Chui na Talib wakawepo ndani ya makao. Assessoko akawapongeza kwa kazi waliyoifanya lakini pia akawapandisha vyeo na kuwafanya wawe makamu wakuu, watu ataokuwa anaonana nao baada ya General Kessy.
“Unaju mtu akifanya jambo kubwa lazima apongezwe. Huyu Kessy mnayemuona hapa, yeye ndiye alikomboa uhai wangu toka kwenye mikono ya mshenzi mdhalimu Louis Diarra. Alikubali kujitolea uhai wake, akakaa mbele yangu akiwa na bunduki akawamaliza maadui. Bila yeye nisingalikuwepo hapa. Na ndio mana nikaamua kumpa hii nafasi aliyopo sasa. Anastahili. Na nyie nimeona juhudi zenu. Mnastahili. Na mkifanya makubwa zaidi ya haya, mtapata mengi zaidi. Sawa?”
“Sawa, mkuu.”
Amadu na wenzake wakaondoka na kumuacha Kessy na Assessoko ambaye naye punde aliaga akaondoka zake. Mkutano ukaitishwa wa wafuasi wa MDR, maamuzi yote ya kikao cha Kessy na na Assessoko yakaekwa wazi.
Jua lilpochomoza, ndani ya nchi ya Sierra Leone, kukaitishwa kikao. Watu wale wale waliopanga kuvamia Guinea kwa kutumia makomando, walikutana kwa mara nyingine.
“Kuna taarifa yoyote jamani?” Mwanaume aliyevalia suti aliuliza.
“Hakuna, mkuu. Tangu tulipopata maelezo kwamba wameshafika eneo la tukio, hatujapata kingine mpaka sasa.” Mjumbe mmoja akachangia.
“Watakuwa wameshauwawa.” Mwingine naye alisema.
Mwanaume ndani ya suti akashusha pumzi ndefu.
“Hilo ni tatizo sasa. Haiwezi ikaleta ngwengwe huko Guinea endapo ikijulikana ni wa Sierra?”
“Hapana, sidhani.” Mwanamama wa kikaoni alisema.
“Kwanini?” Mmoja wa wajumbe akauliza.
“Kwasababu endapo wakifanya hivyo, watatengeneza headline. Swali litakuja, kwanini wanajeshi wa Sierra waende huko. Na itazidi kuongeza nguvu kwenye mwangwi wa taarifa kwamba kuna kitu Guinea, na hata kukamata attention ya vyombo vya habari vya nje.”
“Vipi kama raisi wa Guinea ataliongelea katika sura ya uchokozi wa kivita?” Mjumbe akauliza. Mjumbe mwenzake akajibu;
“Hawezi. Anajua kama akianza mashambulizi dhidi yetu, ulimwengu mzima utakuwa upande wetu. Hawezi akashinda!”
“Ok … Ok … Embu tuachane na hayo. Jana maombi yalikuja mezani kwa raisi yakitokea Liberia. Wanaomba msaada wetu wa kijeshi, wamezidiwa na kundi la waasi la Le tueurs. Mnalionaje hili?” Mwanaume mwenye suti alifungua uzi mpya.
“Hatuwezi kuwasaidia kwa sasa japokuwa kweli wana mahitaji. Kumbuka na sisi tupo katika wakati mgumu pia.” Mjumbe mmoja alichangia, wenzake wote wakamuunga mkono ya kwamba haiwezekani.
“Sawa, nadhani sasa ni wakati muafaka wa kujadili nini cha kufanya kwa muda huu na hali tuliyopo. Nakaribisha mawazo yenu.”
“Mkuu, nadhani huu ni muda muafaka kwa mheshimiwa kuomba msaada mataifa ya magharibi. Endapo kama tutafaulu katika hilo, tutakuwa tumeukata mzizi wa fitna kabisa.” Alisema mjumbe.
“Tatizo kuomba msaada kwa hayo mataifa inakuwa ngumu kwetu kutokana na njia ambayo raisi wetu ameingilia madarakani. Marekani na uingereza wanamuona Diarra kama gaidi kwao. wapi unadhani tutapata msaada?” Mjumbe mwingine alitia neno.
“Kama marekani na waingereza hawapo tayari, mi naona tuwafuate warusi tu. Wanaweza wakatusaidia. Naamini hilo.” Mjumbe mwingine akachangia.
“Sawa. Nitayafikisha mawazo yenu.” Mwanaume aliyevalia suti alinena. Kikao kikafungwa.
Usiku ulikuwa tayari umeshaingia.
Wasaa ulikuwa ni saa nne inayoitafuta saa tano ya usiku. Amadu alikuwa amejilaza kitandani kwake yeye na Chui. Usingizi ulikuwa umempitia lakini Chui yeye alikuwapo macho. Alikuwa anatizama dari kama vile kuna jambo fulani analitafakari.
Baada ya muda kidogo, Amadu alipata njozi. Alijiona akiwa msituni yeye pamoja na Chui, Farah, Mou, Ussein na Ulsher. Walikuwa wakikimbia wakielekea kaskazini huku nyuma yao milio ya risasi ikirindima. Ila ghafla, bomu lilishuka mbele yao na kuwalipua vibaya mno. Wengine wote walichanwa na kupasuliwa na bomu akabaki yeye tu tena akiwa chini anagugumia maumivu ya hatari. Alikuwa hawezi kusogea maana miguu imeharibika. Damu zilikuwa zinamvuja mno. Mara, General Kessy akatokea mbele yake akiwa kabebelea bunduki. Alisogea karibu akanyooshea mdomo wa bunduki kwa Amadu. Alipofyatua, Amadu akashtuka toka usingizini!
“Nini Amadu?”
Chui aliuliza kwa tembe ya hofu. Amadu baada ya kutizama kushoto na kulia kwake, akashusha pumzi ndefu na kutikisa kichwa.
“Nimeota ndoto ya ajabu!”
“Ndoto gani?”
Amadu alitulia kwanza kama vile anatafakuri. Alijifuta jasho na kiganja chake, akamtizama Chui.
“Nimeota tupo mahali tunatoroka mimi na wale wenzetu tulioenda nao ile mishe ya Liberia pamoja na yule mdada mateka. Tukiwa njiani bomu likarushwa nisijue hata limetokea wapi, likatusambaratisha vibaya mno. Wakati nikiwa najikongoja kuamka, akatokea general akaninyooshea bunduki. Ile kufyatua tu ndo’ kushtuka!”
“Mmmh … Mbona ndoto yako inantisha? … Tulikuwa tunaenda wapi?”
“Hata sijui wapi tulipokuwa tunaelekea. Sielewi! Unadhani itakuwa ina maana gani hiyo ndoto?”
“Sijui!”
Amadu alinyanyuka akatizama saa yake ya mkononi akaona ni saa sita kasoro vidakika kadhaa. Alitupia shuka kando akaufuata mlango wa hema lao.
“Wacha ninyooshe miguu, naenda chimbo mara moja.” Amadu alimuaga Chui kisha akatoka na kuelekea zake chimboni. Alimkuta Ulsher amelala, na hata mzee Buruwani pia. Ila vishindo vyake vya miguu vikamshtua mzee Buruwani, akaamka na kutizama. Amadu akafungua mlango na kuingia ndani.
“Unaendeleaje, mzee?”
“Naendelea vyema.”
“Umekula leo?”
“Ndio, nimekula baba.”
Amadu aliketi chini akamtizama mzee Buruwani.
“Umetokea wapi, mzee? Na ulikuwa unafanya nini?”
“Nimetokea Kankan na shughuli yangu ni ukulima, baba.”
“Una familia?”
“Ndio. Mke na watoto watatu. Wote wanaishi huko Kankan huku huwa nakuja kwa ajili tu ya kilimo.”
“Ilikuwaje ukaingia katika haya matatizo?”
“Nilikuwa tu namsaidia yule binti. Nilisikia kwenye karedio kangu kwamba kuna zawadi kwa atakayetoa taarifa.”
Amadu alitikisa kichwa chake kwa masikitiko akatizama chini. Alitizama kushoto na kulia kwake akamwambia mzee Buruwani.
“Ukitoka hapa unaweza ukaenda mpaka nyumbani kwako?”
“Ndio! Naweza!”
“Utaufunga mdomo wako huko utakapokwenda?”
“Nakuahidi kwa roho yangu. Sitasema jambo!”
Amadu alimtizama mzee Buruwani kwa macho ya huruma. Akatoka nje na kutizama pande zote zimzungukazo. Alipoona ni shwari, akarudi chimboni na kumfungulia mzee Buruwani.
“Pita njia hii ya mashariki. Kwa mbele kidogo utaona imekata kona, usiende nayo, wewe nyoosha mpaka ufike mtoni na uendelee na safari yako. Ukipita mbali na maelekezo yangu utaakutana na walinzi, utauwawa.”
“Sawa.”
“Angalia wanyama wasikudhuru.”
“Ahsante. Nakushukuru sana mwanangu.”
Mzee Buruwani akashika njia na kuondoka. Amadu alimtizama mpaka anapotelea kisha akarudi zake hemani. Alimkuta Chui kalala, naye alipojilaza tu kitandani Chui akaamka.
“Nimemwachia yule mzee aondoke.”
“Buruwani?”
“Ndio.”
Chui kusikia hivyo akanyanyuka na kuketi kitako.
“Kwanini?”
“Sijaona haja yay eye kukaa humo. Ana familia inayomtegemea na anatakiw awe nayo.”
“Vipi akienda kutoa taarifa?”
“Hatosaidia chochote. Kesho wote tunaenda Kabala, Sierra Leone. Taarifa yake itasaidia nini?”
Ukimya ukashika anga kwa sekunde kadhaa. Chui akauvunja kwa kuuliza;
“Lakini vipi mkuu akijua?”
“Hatoweza kujua. Hata kama akijua, nitawajibika kwa nilichokifanya kwani naamini ni sahihi.”
Walilala usiku ukapita. Taa ya mungu ilipomulika kengele ikagongwa na wafuasi wote wa MDR waliobakia wakakusanyika. General Kessy akasimama mbele ya umati na kutangaza siku ile ni siku ya kuondoka kwenda mji wa Kabala, hivyo wote wakajiandae kufanya zoezi hilo, umati ukatawanyika.
Baada tu ya muda mfupi yalikuja magari manne aina Fuso yasiyo na namba za usajili, yakapaki kwenye uwanja wa kambi. Magodoro, mahema, vyombo na mabegi yakapakiwa humo, hata watoto waliotekwa nao wakaswagwa humo chini ya uangalizi wa wanajeshi kadhaa. Watu walijiweka tayari, wakapanda kwenye magari ya mapambano ya MDR wakawa wanangoja tu amri toka kwa mkuu waende. Amadu pamoja na Chui wao walijipaki kwenye lile basi lao.
General Kessy alitoka kwenye hema lake akiwa anaongozana na mfuasi wake mmoja aliyekuwa amebebelea bunduki begani. General alionekana ameghafirishwa na jambo, uso wake ulieleza kwa ndita na hata matendo yake aliyokuwa anafanya pindi anaongea.
“Nyie mlikuwa wapi?”
“Tulikuwa lindoni kama kawaida, mkuu.”
“Sasa mateka anatorokaje kizembe hivyo?”
“Sisi wenyewe hatujui, mkuu. Hatujui ametokaje ndani ya chimbo.”
“Hamjui! Kazi yenu ilikuwa ni nini? Kuzurura?”
“Hapana, mkuu!”
“Kwa huo uzembe tutashika dola kweli?”
Kimya.
“Na mtoto wa waziri?”
“Huyo yupo, tumeshampaki kwenye gari.”
“Ok. Twendeni! Ila mkifika lazima muwajibishwe.”
Mpaka wanamaliza hayo maneno walikuwa tayari wameshayafikia magari. General alipanda gari lake binafsi akiwa na dereva wake, safari ya kuelekea Kabala ikaanza.
Baada ya mwendo wa masaa matano wakawa tayari wamekwishaingia mji wa Kabala, nchi ya Sierra Leone baada ya kuteketeza kilomita 255 njiani. Walipokelewa na wenzao kwa shangwe na nderemo. Mizigo ilishushwa, makazi ya mahema yakatengenezwa kwa ajili ya wakazi wapya.
Siku moja ikapita.
Siku iliyofuata, mkutano uliitishwa na General Kessy akahutubia umati kuwaweka wanajeshi wake katika utayari wa mashambulizi makubwa kuanzia siku ile kamili. Hakuna tena muda wa kupoteza, ni wakati wa kuleta madhara makubwa katika nchi ya Sierra Leone. Baada ya mkutano huo, General Kessy akawaita Amadu na Chui ofisini kwake, akawapa kazi;
“Jeshi la Sierra Leone limefungua kambi dogo maeneo ya Makeni. Wamefanya hivyo kwa ajili ya kurahisisha kazi yao ya kuurudisha mji wa Kabala. Sasa nataka mkafanye kazi huko kwa kuteketeza kambi hiyo ndogo yenye vifaa vya kila aina. Chagueni wenzenu mkaitende hiyo kazi sasa hivi.”
Amadu na Chui wakaridhia. Walichagua watu wao watatu na muda ukapangwa wa kwenda kufanya tukio, saa nne za usiku.
General akamuita Talib ofisini, naye akampa kazi yake;
“Ndani ya siku ya leo, nataka muende Magburaka. Kazi yenu kuu ni kutekeza tu, kuanzia ofisi za serikali, mpaka watu! Hakuna kuleta huruma, nataka nisikie taarifa ya habari leo za mauaji. Nataka leo serikali ya Sierra ijue ni jinsi gani tuna maanisha. Chagua watu wako, mkaitende kazi.”
Talib akaridhia. Alichagua watu wake kumi na mbili na muda ukapangwa wa kwenda kufanya tukio, saa kumi ya jioni.
Sasa ilibakia saa tu kuamua mambo hayo mawili. Ilipofika saa tisa ya jioni, magari manne yakatoka kambini yakiongozwa na Talib kuelekea Magburaka. Saa moja ya usiku ilipohitimu, yakatoka tena magari mengine mawili yakiongozwa na Amadu kuelekea Makeni, ndaniye walikuwepo Ussein, Mou, Farah na Chui.
Kila kitu kilienda kama kilivyopangwa. Kambi ya Makeni iliteketezwa na hata silaha zikabebwa. Wakina Talib waliteketeza kila ofisi na walimimina risasi za kumwaga mitaani wakaua watu mia moja na mbili, wakiwemo wamama na watoto. General alifurahishwa sana na hayo mafanikio. Mipango mingine ikaanza kusukwa.
“Soko kuu na ofisi za mji wa Bo, pamoja na mji wa Kenema vinatakiwa kufanyiwa mashambulizi ndani ya kesho kutwa. Hatuna muda wa kupoteza. Mtajigawa makundi mawili, moja litakwenda Bo na lingine Kenema. Kundi la Kenema litaanza kushambulia kwanguvu, wakati majeshi ya Sierra yakitumwa kwenda Kenema, kundi la Bo litaanza nao kushambulia kwanguvu, sawa?”
General alimpa maelekezo Talib na wenzake kumi na mbili. Wakapokea maelekezo na kwenda. Amadu na Chui wakaitwa.
“Keshokutwa nataka muende Freetown. Kazi yenu kubwa ni kuhakikisha mnateka maofisa wa serikali, nataka mniletee mawaziri ama manaibu waziri hapa, ama mkuu wa mikoa. Tumeelewana?”
“Ndio, mkuu.” Amadu na mwenzake wakaitika.
Baada ya siku moja kupita, ikafika siku ya tukio. Talib na wenzake walijitwika kwenye magari yao, safari ya kuelekea kwenye maeneo ya matukio ikaanza. Walijigawa makundi mawili kama walivyopangwa. Wakina Amadu wao walinyooka na njia kwenda Freetown.
Mpaka muda ambao jua lataka kupumzika, makundi yote yakawa yameshawasili maeneo yao ya kazi. Amadu akiwa na wenzake wa kazi walifikia nyumba moja ya mapumziko huku Amadu na Chui wakiwa wamevalia kofia na miwani kuficha nyuso zao. Wakiwa hapo chumbani wakaanza kupanga mipango yao ya mashambulizi. Waliamua kuanza na ofisi ya mkuu wa mkoa. Waligawana majukumu, na kila tukio likachorwa kwenye karatasi.
“Mou utakwenda na kuingia ofisini. Utabebelea bahasha na kudai una mahitaji toka kata yako na wilayani wamekuambia uende ofisi ya mkoa. Hakikisha unakuwa serious na unahakikisha unaonana na mkuu wa mkoa na unamweka kwenye himaya yako. Muda huo wote utakuwa unawasiliana na sisi kwa kupitia micro mic tutakayokufungia.” Amadu alieleza.
“Sawa.” Mou akajibu.
“Taarifa zako ndizo zitatupa sisi nafasi na jinsi ya kujipanga.”
“Haina shida.”
Baada ya kupanga, wakapumzika kwa usingizi. Amadu yeye alikuwa macho. Alifungulia runinga akawa anatizama. Kwenye kituo kimoja cha runinga akawa anaona matangazo moja kwa moja juu ya kinachotukia huko mji wa Kenema, wananchi mia mbili na ushee wameuwawa na watuhumiwa ni kundi la MDR.
Amadu alinyanyuka akaa kitako apate kuona vizuri. Macho yake yote yalitilia maanani akionacho na punde tu yakaanza kujaa machozi. Aliona maiti zikiwa zimezagaa, watoto wakilia kwa kupoteza wazazi na hata watu wazima pia wakilia kwa kupoteza familia zao. Moja kwa moja akaanza kukumbuka machafuko yaliyowahi kuikumba nchi ya Sierra Leone, jinsi alivyopoteza wazazi wake na dada yake. Kila aliyemuona runingani akiwa anaongea huku analia akajiona ni yeye ndiye analonga. Hata sauti hakusikia tena, alisikia sauti ya Ulsher ikimuita na kumshutumu ya kwamba ni muuaji wala si mwanamapinduzi. Alihisi kuchanganyikiwa, mwishowe alizima runinga akalala.
Asubuhi ya saa moja inayoitafuta saa mbili, Amadu aliamshwa na Chui akatakiwa ajiandae kwa ajili ya tukio walilopanga jana. Amadu akaamka na kuuliza;
“Mou amekwisha kwenda?”
“Ndio!” Chui alijibu, “amekwishaingia kwenye jengo la mkoa, anasubiria sasa mapokezi. Ametuambia kuna ulinzi mkali.”
“Umemwambia asiue mtu?”
“Si tulishakubaliana tokea jana. Sasa amka ujiandae tuondoke. Kwa sasa tunatakiwa tuwe maeneo ya karibu na ofisi ya mkoa.”
Amadu alikuwa kama mtu mwenye bumbuli la mawazo. Picha za mauaji alizoziona jana kwenye runinga bado zilikuwa zinamtafuna akili. Farah alimpiga kofi la mgongo kumshtua.
“Mbona kama una mawazo?” Farah aliuliza.
“Vipi, haupo sawa?” Ussein naye akaongezea.
Amadu alitikisa kichwa chake kujirudisha fahamuni. Alinyanyuka akaenda kunawa uso, ni yeye peke yake ndiye aliyekuwa yupo nyuma kwa kujiandaa. Aliponawa walitoka ndani ya chumba wakajipakia kwenye gari lao na kusogea maeneo ya karibu na ofisi ya mkuu wa mkoa. Wakaendelea kuwasiliana na Mou aliyekuwepo ndani.
“Naweza nikakusaidia shida yako?” Mwanamke mmoja mnene mweusi alimuuliza Mou aliyekuwa kwenye benchi.
“Nataka kuonana na mkuu wa mkoa.”
“Hata mimi naweza kukusaidia. Naomba unijuze shida yako.”
“Nimesema nataka nionane na mkuu wa mkoa. Mara ngapi nimekuja hapa na hamkusaidia? Nataka kumuona mkuu wa mkoa nimueleze shida ya kata yangu macho kwa macho.”
“Kwani wewe ni nani, kaka?”
“Diwani.”
“Sasa si ungeenda wilayani kwanza.”
“Nimeshaenda mara kibao, wazembe tu. Nalalamika kila uchwao kuhusu swala la maji naona sieleweki. Nimekuja kwa mkuu wa mkoa mwenyewe.”
“Unatoka kata gani?”
“Mbona maswali mengi, dada? Nataka kuonana na mkuu wa mkoa. Nataka anieleze kwanini wakina mama kwenye kata yangu wanapata shida ya maji hivi? Watoto hawaogi, hawaendi shule, watu wanakufa kwa kiu!”
Watu wengine waliokuwa wamekaa karibia na Mou wakamuunga mkono. Walionekana kuguswa na anachokiongelea Mou, diwani feki.
“Ila kaka, unajua matatizo ambayo yanayoikumba serikali kwa sasa, pesa na rasilimali nyingi zimeelekezwa kupambana na waasi. Kununua masilaha na kuwapa wanajeshi motisha.” Mwanadada alieleza.
“Kwahiyo watu wafe?” Mou aliuliza.
Maongezi yote hayo wakina Amadu waliokuwepo kwenye gari wakawa wanayasikia. Walikuwa wametulia tuli wakiacha masikio yao yafanye kazi kwa umakini. Gari lao lilikuwa umbali wa kama hatua thelathini za mtu mzima toka ofisi ya mkuu wa mkoa. Walikuwa wamelizima kabisa ili wapate kudaka kila habari.
Miongoni mwa wanajeshi waliokuwa wanalinda eneo la ofisi ya mkuu wa mkoa walilitizama gari la wakina Amadu na kulitilia shaka. Si kwamba halikuwa na namba ya usajili, la hasha. Ila kuwapo kwake pale maeneo ya ofisi kubwa kama ile bila ya kuonekana na shughuli yoyote kulizua hofu.
“Embu katizame lile gari pale, afande. Naona limekaa kwa muda na sioni mtu yeyote akishuka wala kufanya lolote.”
Alisema mwanajeshi mmoja akimuambia mwenzake. Mwenzake akatii, akiwa kabebelea na kushikilia bunduki yake akasogelea gari la wakina Amadu na kugonga kioo. Kong! Kong! Kong!
Kioo kilishushwa uso wa Ussein ukajitokeza.
“Ndio, afande.”
“Una ajenda gani hili eneo?”
“Kuna mtu namngoja.”
“Nani?”
“Mheshimiwa diwani, ameingia huko ofisini.”
“Upo na nani ndani ya gari?”
“Peke yangu, afande. Kuna tatizo?”
“Embu nione.”
Ussein alishusha vioo vyote mwanajeshi akapepesa pepesa macho yake ndani, aliporidhika akasema;
“Huyo mtu unayemngoja anatoka saa ngapi?”
“Sijajua, afande. Sijui michakato gani anayopitia huko.”
“Hili ni eneo muhimu la serikali. Haitakiwi kuonekana onekana kwa magari yakiwa yamesimama simama bila ya taarifa. Sasa nakupa dakika kumi tu, kama huyo diwani wako atakuwa hajatoka inabidi utoke hii sehemu. Tumeelewana?”
“Ndio, afande.”
Mwanajeshi alijigeuza akarudi kumkuta mwenzake na kumpasha habari alizozipata. Amadu, Farah na Chui walitoka chini ya viti vya gari wakarusha rusha macho yao kutazama usalama.
“Sasa itakuaje? … Mou amekupa taarifa yoyote?” Farah aliuliza.
“Hapana, ila amekwishaingia ofisini kwa mkuu wa mkoa.” Ussein alisema kisha akatoa earphone ya sikio la kulia akampachikia Farah sikio la kushoto.
“Inabidi afanye upesi. Hatuna tena muda wa kukaa hapa.” Amadu alisema. Ussein akasogeza mic ndogo mdomoni mwake;
“Mou fanya upesi, hatuna muda.”
Baada tu ya dakika tangu Ussein atume huo ujumbe, sauti ya Mou ikasika kwanguvu.
“Ingia! … Ingia! … Nimeshamuweka mkuu wa mkoa chini ya ulinzi!”
Haraka Ussein aliwasha gari, kwa mwendokasi mkali wakavamia geti, Amadu, Chui na Farah wakatokezea madirishani na kuanza kumwaga vyuma vya risasi wakiwalenga wanajeshi waliokuwa lindo.
“Usiue raia yoyote! Usiue raia yoyote!” Amadu alipaza sauti huku naye akishughulika kuwamiminia walinzi risasi. Gari lao lilizunguka jengo zima huku risasi zikirindima kisha kila upande wa jengo akashuka mtu mmoja kufanya kazi: Upande wa mbele alishuka Amadu, wa nyuma alishuka Chui na wa pembeni akashuka Farah. Mou alitoka akiwa kamkaba mkuu wa mkoa amemkandamizia bunduki, wanajeshi hawakuweza kumshambulia, waliweka bunduki chini wakanyoosha mikono yao juu. Mkuu wa mkoa aliwekwa ndani ya gari, wakina Amadu wakawamalizia wale wanajeshi kwa risasi, wakapasua na matairi yote ya magari yaliyokuwepo yale maeneo kisha wakaondoka.
Hata taarifa zilipokuja kusambaa kuhusu utekaji, wakina Amadu walikuwa wapo mbali mno. Walikuwa wanabadili gari kila baada ya muda mchache kwa usalama wao, walimfunga mkuu wa mkoa kamba na kumziba mdomo wakawa wanamuweka kwenye buti kwenye kila gari walilolitumia mpaka wanafika Kabala. General Kessy aliwapokea kwa mikono mikunjufu na tabasamu pana. Ila Amadu hakuwa na furaha, baada tu ya kumkabidhi mateka, aliondoka zake.
“Vipi, kuna tatizo?”
General Kessy aliwauliza Chui, Farah, Mou na Ussein.
“Hapana. Hamna!” Farah alijibu.
“Mbona Amadu ameondoka na anaonekana hana furaha?”
Wakina Chui walitazamana, Farah akajibu;
“Hatujui kwanini.”
General Kessy aliwaruhusu waondoke, Chui akamfuata Amadu hemani. Alimkuta akiwa ametulia, uso wake mkunjiko ukiwa umeelekea chini.
“Amadu, shida nini?”
Amadu alishusha pumzi ndefu kwa kutumia matundu ya pua yake kisha akamtizama Chui.
“Sisi si wanamapinduzi bali wauaji.” Alisema kwa sauti iliyobeba hisia.
“Kwanini unasema hivyo?”
“Kwanini? … Huoni, husikii jinsi MDR inavyoua watu wasio na hatia: wanawake kwa watoto? Wametufanya kosa gani? Je tutakapoingia madarakani hawatakuwepo wakina sisi wengine wakidai damu za ndugu, jamaa na marafiki zao? … Jana nilitizama taarifa ya habari kule tulipopumzikia, niliona jinsi maiti zilvyozagaa, watoto na watu wazima wakilia huko Kenema na Bo. Nikajikumbuka mimi kabisa. Nikakumbuka yale niliyoyapitia.”
Chui alikaa kitako kitandani akatulia kwa muda, alimshika Amadu bega akamuambia;
“Pole sana. Najua unachokiongea, ni ukweli mtupu. Lakini sasa tutafanyeje?”
Amadu alinyanyuka akatizama dari. Machozi yalianza kumbubujika kama maji. Aling’ata lips zake akamuambia Chui:
“Nitakuambia nini cha kufanya. Kwanza, naenda kwa general na kumweleza msimamo wangu.”
Chui hakupata nafasi ya kutia neno kwani Amadu alitoka upesi hemani akaelekea upande ilipo ofisi ya General Kessy. Chui alitoka nje ya hema akamtizama Amadu anavyoishia, alishika kiuno akatikisa kichwa chake. Akabakia palepale aone nini kitatukia. Baada ya muda mfupi, sauti ya General Kessy ilisikika ikiita wafuasi wa MDR waliokuwa wamekaa nje ya hema. Wafuasi wakaingia ndani upesi na mara wakatoka na Amadu huku wamemshika mikono wakimburuza. Amadu alikuwa anatapatapa lakini wanaume wanne waliokuwa wamemshikilia walimmudu.
“Wauaji wakubwa! Nani kasema nyie ni wanamapinduzi? Mnaua watu wasio na hatia kwanini? … Hata Mungu hatosimama upande wenu. Nyie ni wadhalimu tu kama wafuasi wa Diarra!” Amadu alikuwa anafoka. Wanaume wale wanne walimpeleka mpaka ilipo chimbo wakamtupia humo. Chui alinyanyua miguu yake akasogelea chimbo kumtizama Amadu. Humo chimboni alikuwamo Amadu na mkuu wa mkoa wakati upande wa pili ukiwa umetenganishwa na miti alikuwepo Ulsher.
“Nini umefanya, Amadu?” Chui aliuliza kwa sauti ya chini. Amadu akamtizama kwa macho yanayomimina machozi.
“Ni bora nikakaa humu, Chui, kuliko kuwa sehemu ya wauaji wa watu wasio na makosa, kuliko kumwaga damu ya watu wanaoumia na kuteseka kama sisi. Sikujiunga MDR kuua watu masikini wasio na msaada bali kuwasaidia kwa kuwakomboa na kuwaweka katika mikono tunayodhani ni salama. Ya nini tumwage damu ya wanawake na watoto ingali si wao walioiingiza nchi machafukoni? Ni bora nikakaa humu nijue moja ya kwamba wakati wanafanya maovu yao, nilikuwa kifungoni.”
Chui hakusema tena kitu. Alitoka akaelekea zake hemani akajilaza kitandani.
Katikati ya usiku wa manane, Amadu alikuwa macho. Alikuwa kaegemea ukuta wa chimbo huku amekunja magoti ambayo juu yake alilaza kichwa chake. Mkuu wa mkoa alikuwa amelala na kukoroma kabisa: kitambi chake kilikuwa kinapanda na kushuka. Ghafla Amadu akiwa hapo alisikia sauti ya kike ikimuita. Aligundua ni sauti ya Ulsher. Aliamsha kichwa chake akaitika.
“Wewe ni nani, Amadu? … Umetokea wapi?” Sauti ya Ulsher iliuliza.
“Naitwa Amadu Laurent, nimetokea Freetown. Mtoto wa masikini aliyejitolea kulipiza kisasi kwa wote waliowaumiza na kuwaliza wana Sierra Leone: wakiwafanya vilema, wapoteze ndugu na wazazi, na hata uhuru wao.”
“Pole sana, Amadu. Meli uliyoipanda kukufikisha huko si yenyewe.”
“Naam. Sasa natambua, najionea huruma nafsi yangu na hata wananchi wenzangu.”
Baada ya hiyo kauli kaukimya kalipasua anga kwa sekunde nne kisha Ulsher akatia neno:
“Jana jioni alikuja yule mwanaume aliyenitoa kifungoni na kwenda kujaribu kunibaka. Alikuja kunidhihaki na kunitania, alikuja akiwa amelewa akaniambia wamemuua baba yangu huko Kenema: sasa nimekuwa yatima kamili.”
“Anaitwa Talib. Kama sijakosea.”
“Simjui jina lake, ila kamwe sitosahau matendo yake, yeye ndiye alipelekea kifo cha mama yangu, na akaenda kumuua na baba yangu. Hawezi akatoka kichwani mwangu.”
“Pole. Ila baba yako amemwaga sana damu za watu wasio na hatia.”
“Najua, Amadu. Ila bado haibadilishi ya kwamba ni baba yangu aliyenizaa.”
Amadu hakusema kitu. Alitizama tu chini.
“Amadu, je harakati zako zimeishia hapa?”
“Kamwe, labda tu nife ila kama nipo hai sitoacha kuwateteta wana Sierra Leone wala kuwakomboa.”
“Nakuomba, utakapopata nafasi unipe nami fursa ya kufuta makosa ya baba yangu. Unipe nami mwanya wa kuandikwa katika vitabu vya historia vya nchi hii kwa kutetea wasio na nguvu.”
Amadu hakujibu kitu. Alitulia akisikilizia kama vile ambaye hakutegemea kauli hiyo toka kwa Ulsher. Alichokifanya ni kutabasamu kwa mbali na kukaa kimya. Punde wakaja wafuasi wawili wa MDR chimboni. Walifungua mlango wa chumba anachokaa Ulsher wakamtoa binti kwanguvu. Ulsher alilalama hataki kwenda na wamuache lakini wanaume wale wawili hawakumsikiliza wala kumjali, waliendelea kumsomba.
“We Mudy! Mudy! Mnampeleka wapi?”
Amadu alipaza sauti yake kuuliza ila hakuna aliyehangaika naye. Ulsher alibebwa akatokomea. Amadu alibakia akiduwaa na kujiuliza. Baada ya lisaa Ulsher alirudishwa chimboni akiwa hoi asiye na nguvu.
“Wamekufanya nini? ... Enh?” Amadu aliuliza. Ulsher alikuwa tu analia. Baada ya muda aliponyamaza ndipo akasema:
“Ananibaka.”
“Nani?” Amadu aliuliza kwa haraka.
“Mkuu wenu.” Ulsher akajibu, “Si mara ya kwanza wala ya pili. Usiku wa wa manane huwa ananitoa mara kwa mara na kwenda kunibaka ofisini kwake. Tokea tupo Guinea.”
Amadu alitikisa kichwa chake kwa masikitiko. Alisonya akatizama ukuta umtenganishao na Ulsher akasema kwa sauti ya taratibu:
“Pole kwa unayoyapitia, mwanamke.”
Ulsher aliitikia kwa kilio. Alilia na kulia mwishowe usingizi ulimpitia akalala. Siku inayofuata mida ya jioni, Chui na Mou walikuja chimboni kuleta chakula na kumpasha habari Amadu. Wakamuambia yaliyojiri kwenye mkutano ulioitishwa asubuhi na General Kessy.
“Wanajeshi wa Guinea wanakuja kesho kuja kusaidia MDR. Wanakuja kwa lengo la kuhakikisha MDR inakamata dola ndani ya juma hili. Watakuja wanajeshi si chini ya elfu mbili pamoja na vifaa vizito.” Mou alieleza taarifa. Chui akaongezea:
“Vita itakuwa very serious. Ndani ya jeshi la Sierra Leone kuna vibaraka wa MDR, wanaleta kila kinachoamuliwa huko makao yao.”
Baada ya hyo taarifa, Amadu aliwashukuru wenzake ila naye akapata kuwaeleza jambo:
“Mimi si mfuasi tena wa MDR. Sitotumia tena nguvu wala akili yangu kusaidia wauaji. Ila lengo langu la kuwakomboa wana Sierra Leone lipo pale pale. Naamini naweza kutimiza malengo yangu nje ya MDR bila kuwatesa wakina mama na watoto wasio na hatia. Kwa yeyote anayeona anakubaliana na ninachokisema naomba aniunge mkono.”
Mou na Chui walitizamana kama watu wanaojiuliza, waliaga wakataka waende kufikiria walichoambiwa.
Baadae ndani ya usiku mzito, wanaume wanne wa MDR wakiwa wamebebelea bunduki walikuja wakamtoa Amadu chimboni na kumpeleka msituni. Walimpigisha magoti na kumtaka asali sala zake za mwisho kwani sekunde chache mbele anaenda kuuwawa. Amadu akauliza:
“Nani amewatuma?”
Wanaume wale ambao walikuwa wamefunikwa na giza wakamdhihaki:
“Ya nini ujue na unaenda kufa?” Kisha wakacheka na kukoki bunduki zao, wakamnyooshea Amadu. Amadu alitizama juu machozi yakamtoka. Ghafla milio ya risasi ikanguruma. Amadu alijitizama ajabu hakuona jeraha lolote. Alipowatizama wale waliomleta kule msituni akawaona wanadondoka chini na punde wakatokea wanaume wengine wanne: Chui, Farah, Ussein na Mou. Walimnyanyua Amadu wakamkumbatia.
“Tupo pamoja. Eidha tufe ama tufanikiwe tukipambana.”
Amadu alitabasamu. Macho yake yalilenga chozi. Aliwakumbata wenzake kwanguvu huku akiwashukuru. Baada ya kupongezana na kupeana shukurani, walianza kuteta:
“MDR sio ulimwengu wetu tena, hatuna budi kupotea eneo hili. Ila wapi tunakwenda?” Mou aliuliza.
“Hatujui wapi pa kwenda, ila tuondoke hapa. Tutajua huko mbele kwa mbele.” Farah alijibu.
“Ila tunafanya nini kwa sasa na tumeachana na MDR?” Mou aliuliza.
“Kwani kati yetu kuna ambaye dhamira yake imekufa na MDR?” Amadu aliuliza, wenzake wakawa kimya, akaendelea kunena:
“Kabla ya kufanya lolote yatupasa tusemezane dhamira yetu ni ipi. Hatuna familia, hatuna lolote zaidi ya sisi wenyewe. Je tutakufa tukipigania nini?”
“Mimi nitakufa nikipigania mapinduzi ya kweli.” Farah alijibu.
“Na mimi pia, nitakufa nikipigania mapinduzi.” Ussein akasema.
“Nitakufa kwenye mapinduzi ya kweli.” Mou naye alichangia, akabakia Chui. Wote wakamtizama.
“Hii ndio njia niliyoichagua. Nitakufa nikiipigania.” Chui naye akatia neno. Wenzake wakatabasamu.
“Basi kama tumeamua, tuwe na dhamira ya kweli. Hii ndio sehemu kundi letu lilipozaliwa. Tutapigania mapinduzi na hiyo ndiyo dhamira yetu na sababu yetu ya kifo.” Amadu alisema. Wote wakajibu:
“Ndio!”
“Kuanzia leo tutafuata njia yetu. Hatutajali uchache wetu kwani tunajiamini na kujitosheleza. Hatutamuacha mwenzetu yeyote nyuma hata pale risasi zitakapokuwa zinapita pembeni ya masikio yetu.”
“Ndio!” Wote wakajibu.
“Kuanzia leo tumezaliwa upya. Tunavua gamba la MDR na kujivika utawala mpya, tutajiita GHOST, kwa kuwa hatutaonekana wala kuzuilika.”
“Ndio!” Wote wakajibu.
“Kama tumekubaliana, tutakula kiapo huko tutakapokwenda. Ila kwa sasa turudi kambini.”
“Kufanya nini, Amadu?” Farah aliuliza.
“Kumkomboa Ulsher, binti waziri. Naye pia anataka hii nafasi.”
“Huoni kama atakuwa mzigo?” Ussein aliuliza.
“Hapana. Kumbuka wazazi wake wote wamekufa. Mama yake pia baba yake huko mjini Kenema kutokana na mauaji ya MDR. Kila siku anabakwa na Kessy, hatuwezi kumuacha. Tumpe nafasi, tukimuacha hapa si punde atauwawa.”
Wakakubaliana.
“Na vipi kuhusu wale watoto?” Farah aliuliza. “Je tunawaacha?”
“Kwa sasa hatuwezi kuwapeleka popote: wapo wengi. Itakuwa ngumu kutoroka.” Amadu alijibu.
“Kweli.” Mou akadakia. “Labda kwa huko mbeleni.”
“Sawa, twendeni!” Farah alisema kwa sauti. Amadu alichukua bunduki moja ya wale wafu wakaanza kuenenda kufuata ilipo kambi. Ndani ya muda mchache wakawa wameshafika nyuma ya chimbo, walimuona mfuasi mmoja wa MDR akiwa lindo. Amadu alimnyatia mwana MDR huyo akamkaba na kumziba mdomo, akamvunja shingo kisha akafuata mlango wa Ulsher na kuufungua, akamtoa Ulsher wakapotea eneoni.







******



☆Steve
 
sante tivu

Ntakuwa na udhulia mpaka mwisho nijue


tuko pamoja steve haina kulala hiyo

Asante mkuu ,,,sema naona Kama tunasubiri Sana kwann usingerusha hata mara3 kwa week ,,wazo tuu maana tunasubiri kunapoa mpk kunasahaulika

[HASHTAG]#stevemollel[/HASHTAG] Asante sana endelea kutupa burudani ndugu


Asanteeeh

naisubiri kwa hamu

Tuko pamoja mkuu,

daaaaaaaa nashukuru mkuu aseeee

Hii hadithi nimeikubali sana mkuu naomba unitag ukishusha vitu

Pamoja sana mkuu
Karibuni sana.




☆Steve
 
*NJIA NYEMBAMBA -- 05*





*Mtunzi: StevieMollel



No: 0685 758 123




****





Magari makubwa ya kivita yakiwa yameongozana na yamebebelea wanajeshi yaliingia kwenye kambi ya MDR. Yalikuwa magari kumi kila mojawalo likiwa na wanaume wasiopungua thelathini wenye mabegi migongoni. General Kessy alipokea wageni hao, mmoja wa wageni akaongozana naye mpaka makaoni, wakakaa na kuteta:
“Tumekuja hapa kwa oda ya mkuu wetu wa majeshi. Tupo hapa kwa ajili ya kuwasaidia kukamata dola ya Sierra Leone. Haitozidi wiki tatu tutatakiwa kurudi Guinea.”
“Vipi kuhusu vifaa?”
“Navyo vi njiani vyaja. Ndani ya muda mfupi vitakuwapo hapa. Bunduki, silaha nzito, mabomu na kadhalika. Hatutakuwa na muda wa kupoteza, kila siku tutafanya tukio kutimiza dhamira.”
“Sawa. Lakini jua kwamba jeshi lako litakuwa chini yangu. Oda na amri zote zitatoka kwangu, sawa?”
“Sawa. Hii ni nchi yako.”
General Kessy alichukua ramani akaitandaza juu ya meza, akaanza kuelekezana na mwenzake.
“Kesho utaenda Freetown wewe pamoja na wanajeshi wako kadhaa na wa MDR.”
“Sawa. Nini misheni yetu?”
“Kuvamia na kuharibu wizara ya ulinzi. Hakikisheni mnaharibu kila kitu, mnachakaza kila mtu. Kuna taarifa wana kikao kesho huko wizarani kujadili usalama wa nchi ya Sierra Leone, waziri na makatibu wote watakuwepo huko. Kikao kitafanyika saa nne ya asubuhi.”
“Sawa.”
“Wanajeshi wako wengine wataenda na wanajeshi wa MDR kuziba barabara kuu toka mji wa Kenema hata kushambulia, inasemekana kuna kundi la wanajeshi watatoka kuja maeneo ya karibu na Kabala kuzuia nguvu yetu ya mashambulizi.”
“Sawa.”
“Nadhani yote hayo yataenda vyema endapo tutapata pia hivyo vifaa. Kwa sasa unaweza kwenda na kuwapasha habari wenzako.”
“Sawa.”
Mwanajeshi wa Guinea alinyanyuka akatoka nje ya makao. General Kessy alitabasamu akalamba lips zake. Alifunga mlango wake kwa funguo akatoa simu yake kumpigia mtu aliyetunzwa kwa jina la Bakary. Simu iliita mara mbili ikapokelewa.
“Tayari wameshafika, kuanzia kesho misheni zinaanza kutekelezwa … Usihofu kabisa kuhusu hilo … Nchi itakuwa chini yangu muda si mrefu … Vipi huko Liberia? …”
Mara ngo! ngo! ngo! Maongezi yakakatishwa na hodi mlangoni, general ikabidi aage:
“Tutaongea baadae.”
Aliuendea mlango akaufungua akakutana na Talib.
“Nini Talib?”
“General, Amadu pamoja na wenzake hawaonekani.”
General aliufungua mlango kwa upana zaidi Talib akaingia ndani na kuketi.
“Ina mana Amadu hajauwawa?”
“Hapana! Tumekuta wakina Agu wamekufa, na Amadu pamoja na wenzake: Mou, Farah, Ussein na Chui hawapo!”
“Shiiit!” General alibamiza meza. Alitikisa kichwa chake kwa masikitiko akauliza:
“Mbona mnakuwa wazembe kiasi hiki?”
Talib kimya.
“Mmeruhusu vipi hao watu wakaondoka?”
“General, mimi mwenyewe nimeshangazwa na hizo habari. Isitoshe wametoroka na mateka, binti waziri.”
“Pumbavu kabisa! … Mpaka wanafungua chimbo nyie mlikuwapo wapi?”
“Alikuwepo mtu mmoja lindo, ila kauwawa!”
“Talib, unaweza kazi huwezi?”
“Naweza, mkuu!”
“Nenda katafute hao watu sasa hivi! Sasa hivi! Potea!”
Talib alitoka nje akawaita wafuasi kumi akapanda nao gari na kutoka eneo la kambini kwenda kuwatafuta wakina Amadu. General Kessy alifunga mlango wake akarudia kupiga simu yake ya hapo awali.
“Ndio … Hakikisha ndani ya wiki hii mnafanikiwa kila kitu, kama mkikwama mtanitaarifu … Bakari, inabidi sasa muache habari za kupigana misituni kama masokwe ni wakati wa kuingia ndani ya mji, Liberia hawana usaidizi wowote kwa sasa si unajua utawala wake uliingia kwa mabavu … Nasubiria kusikia toka kwenu Bakari, kama sio sasa, basi ni kamwe.”









****










Ndani ya ofisi moja kubwa iliyonakshiwa na meza ya kioo, viti vyenye viuno vyembamba na picha kubwa za watu maarufu weusi kama Nelson Mandela, Steve Biko na Nkurumah Kwame, alikuwa ameketi bwana Assessoko akiwa amevalia kaunda suti nyeusi, pembeni yake alikuwa ameketi mwanaume mmoja mnene mweusi mwenye kiwaraza kikali, mwili wake ulikuwa umevikwa suti nyeupe kama yangeyange. Juu ya meza kulikuwepo na glasi zenye maji pamoja na chupa zake. Bwana Assessoko alikunya fundo moja la maji, akamtizama mwenzake.
“Nimefurahi sana kusikia hivyo, hakika sasa njia ni nyeupe.”
Mwanaume yule mweusi alitabasamu na kusema:
“Sasa ni muda wa kusaini mkataba bwana Assessoko.”
Alitoa faili toka kwenye mkoba wake akaliweka juu ya meza na kulifungua.
“Inabidi sasa usaini mkataba ili tupate kuishi kwa amani.”
“Kwani hamuniamini bwana Kolo?”
“Hamna, Assessoko. Mambo siku hizi hayaendi hivyo. Inabidi utie sahihi yale tuliyokubaliana ili kila mmoja wetu awe ana sauti kwa mwenzie.”
Assessoko alivuta faili karibu naye akapitisha macho kurasa baada ya kurasa, alipomaliza aliweka faili juu ya meza akashusha pumzi ndefu.
“Kuna shida yeyote, bwana?” Mwenzake aliuliza. Assessoko akatikisa kichwa. Mwanaume yule mweusi akatoa peni yake mfukoni na kumkabidhi Assessoko. Assessoko akapokea peni na kumwaga wino juu ya karatasi mojawapo ya faili, kisha akalirudisha faili kwa mwanaume yule mweusi aliyelitizama na kutabasamu.
“Sasa kazi imekwisha, mheshimiwa. Nashukuru sana kwa maridhiano.”
Mwanaume yule mweusi alirudisha faili lake kwenye mkoba kisha akaaga na kuondoka.
“*** Guinea!” Assessoko aliropoka. Aling’ata meno yake kwanguvu huku akigosha vidole vyake.
“Wanadhani wao ni wajanja sio? … Nitawaonyesha!” Assessoko aliendelea kuongea mwenyewe. “Mimi ndo’ Assy. Hakuna anayeweza kushindana na mimi. Tutaona mwisho wa siku nani atakayekuwa mwanaume pekee anayesimamia miguu yake.”
Alinyanyua glasi yake ya maji akabugia. Punde sauti ya mwanamke atangazaye habari ikamfikia masikioni, alirusha macho yake juu ukutani kwenye runinga akamuona mwanamke mmoja mzungu mtangazaji wa shirika kubwa la habari la uingereza akiwa anatangaza habari ya machafuko ya Sierra Leone. Assessoko alitabasamu kwa kebehi, akageuzia kiti chake vizuri kutizama habari.
“Kwa sasa tunaongea moja kwa moja na katibu mkuu wa wizara ya ulinzi ya Sierra Leone apate kutuambia wamejipangaje kuhakikisha machafuko yanakoma nchini mwao na je watadhibiti vipi kundi la waasi la MDR … mheshimiwa karibu.”
Mara runinga ikagawanyika mara mbili, sehemu moja akawa anaonekana mtangazaji wakati sehemu ya pili akiwa katibu wa wizara ya ulinzi ya Sierra Leone.
“Ndugu muandishi hatuwezi tukaweka wazi ni nini tumepanga kufanya, ila tungependa kuchukua wasaa huu kuwatoa hofu wana Sierra Leone kuwa serikali yao haijalala na inalifanyia kazi lile linalotukia ili tuwahakikishie usalama”
“Lakini muheshimiwa, watu wanazidi kufa. Mpaka hapo mtakapochukua hatua hamuoni kwamba mtakuwa mmechelewa?”
“Ndugu muandishi, huwezi kukurupuka na kufanya maamuzi. Hili swala wote tunafahamu madhara yake. Sisi kama serikali tunaguswa sana na mauaji hayo, lakini hatujakaa kimya, la hasha! Tunajiapanga kufanya jambo la uhakika.”
“Mheshimiwa, unaonaje sasa serikali yako ikakaa meza moja na kundi hili la waasi mkafanya majadiliano na hata mwishowe mkaelewana?”
“Kwa sasa hatuwezi tukafanya hilo jambo, ndugu muandishi. Kufanya hivyo ni kudhihirisha udhaifu na kuwatangazia ushindi MDR. Tutapambana na tunaamini tutashinda.”
“Mheshimiwa, je mnaongeleaje ukimya wa AU (African Union) katika hili swala lenu? Hamuoni kama wamewatekeleza?”
“Ndugu muandishi ni mapema sana kusema hilo. Ila tunafahamu ya kwamba katika mkutano wa AU mwezi ujao mojawapo ya agenda kuu ni usalama wa Sierra Leone.”
“Na je vipi kuhusu umoja wa mataifa?”
“Nadhani halina haja ya kwenda huko, tutalimaliza sisi wenyewe.”
“Mheshimiwa, unaongeleaje kauli ya raisi wa Marekani kwamba endapo vita ikiendelea na suluhisho halitopatikana, basi wataleta majeshi yao Sierra Leone?”
“Ningependa kumwambia raisi wa Marekani ahangaike na mambo yake, hatuhitaji msaada wake wowote maana hatukuuona tokea serikali imeingia madarakani.”
“Huoni sababu ni kuingia kwenu kwa mabavu serikalini, mheshimiwa? Na hali hii imepeleka kutoungwa mkono na baadhi ya washirika?”
“Sidhani.”
“Na je, unasemaje kuhusu ushiriki wa Guinea katika hali mliyopo kwa sasa?”
“Tunatambua ya kwamba nchi ya Guinea inawasaidia MDR kimali na hali japokuwa wamekuwa wakikanusha hili kwanguvu zao zote. Tuna ushahidi wa kutosha wa picha na hili swala litapewa kipaumbele pia kwenye mkutano wa African Union.”
“Nashukuru mheshiwa kwa taarifa. Tunakutakia siku njema.”
“Nawe pia.”
Assessoko alizima runinga akacheka kwanguvu. Alicheka mpaka akatoa machozi, alijifuta na leso akasema huku akitikisa kichwa:
“Usilolijua ni usiku wa giza. Kikulacho ki nguoni mwako, katibu.” Baada ya kusema hayo maneno akaendelea kucheka zaidi.










****









Ngo! Ngo! Ngo! Ngo!
Mlango wa makao ya General Kessy uligongwa. General alishusha glasi yake ya kilevi juu ya meza akapaza sauti:
“Ingia!”
Mlango ukafunguliwa Talib akaingia. Alipiga saluti kisha akaketi kitini baada ya kuruhusiwa na mkuu wake.
“Mkuu, hatujafanikiwa kuwapata. Tumewatafuta lakini …” Kabla kauli haijakwisha, Talib alizabwa kofi na General.
“Mshenzi wewe! Hamjafanikiwa nini? Mnajua hao watu watatugharimu kiasi gani endapo wakiwa huko mitaani? Wanatujua ndani na nje, ni hatari kwa usalama wetu!”
“Mkuu, sidhani kama kuna haja ya kuwahofia. Hawawezi kutufanya lolote, tupo na tutafanya kazi!”
General Kessy alimzaba kofi lingine Talib, akafoka:
“Mpumbavu wewe nyamaza! Unaujua uwezo walio nao hao watu? Amadu kuwa hai na akiwa hayupo upande wetu ni hatari. Unajua uwezo wake? Nimekuwa na hili kundi tokea limeanza, hakuna mwanajeshi mwenye uwezo wa Amadu. Kitendo cha kuachwa hai tena akiwa na wenzake ni jinamizi na halitoacha kututafuna, Talib.”
Talib alikunja sura, alinyanyuka akaondoka, General Kessy alimuita lakini hakugeuka, alitoka nje ya makao akabamiza mlango. General aliketi akamimina kileo pomoni kwenye glasi kisha akamwagia mdomoni mwake. Aliwasha msokoto wake wa bangi akawa anauvuta.
Siku ikaenda.
Jua lilipochomoza likachomoza na mipango ya MDR kama ilivyoanishwa. Wanajeshi walijigawa wengine wakaelekea Freetown wengine Kenema, miongoni mwa wanajeshi wa MDR walikuwapo pia watoto nane: walikuwa wamevalia nguo za kijeshi wakiwa wamebebelea bunduki kubwa, wengine walikuwa wamebebelea misokoto ya bangi midomoni mwao wakishea na wenzao, wakati wengine wakiwa wanashiriki kuvuta madawa na wanajeshi wa MDR.
Baada ya masaa kadhaa magari ya MDR yalikuwa tayari yameshafika ndani ya mji wa Freetown. Mbele ya wizara ya ulinzi magari ya MDR yalijikita na kutema wanajeshi ambao walianza mapambano papo hapo. Risasi zikarindima na kuvuma. Mtaa ukageuka kuwa uwanja wa vita. Kundi la MDR lilishambuliana na wanajeshi wa serikali ambao kiidadi hawakuwa wengi. Wafuasi wa MDR walilipua jengo la wizara kwa makombora mazito. Wanajeshi wa serikali walipoona wanazidiwa walitoa taarifa kwa wenzao wakiomba msaada haraka iwezekanavyo, bahati haikuwa kwao, wenzao wakiwa njiani kuja kuwasaidia walivamiwa na kundi la MDR lililotumwa kwenda Kenema baada ya taarifa ya ujio wao kudakwa. Sasa kukawa hakuna msada kwa wanajeshi wa serikali, wanajeshi wa MDR wakateketeza kila kitu, pale walipojiaminisha hakijasalia kitu, walijitwika kwenye magari yao na mengineyo waliyoyateka wakatokomea.
Halikuwa jambo dogo, vyombo vya habari vilitekwa na mkangamano wa habari ya uvamizi wa wizara ya ulinzi. Redio na runinga mbalimbali zilizowapa wananchi wa Sierra Leone fursa ya kuongelea hilo tukio, zilionyesha na kusimulia jinsi wananchi walivyokamatwa na hofu. Kama wizara ya ulinzi inaweza kufanywa tukio hilo, wananchi je wasio na ulinzi wowote? Lilikuwa swali kubwa. Mbali na hapo, baadhi ya wakuu wa nchi mbalimbali za Afrika na hata mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Afrika ya kusini, Senegal, Ghana na Tanzania nao walipewa uwanja wa kutema misimamo yao juu ya tukio hilo, wote wakikemea na kulaani vikali kile kinachoendelea kwa minajili ya usalama wa wana Sierra Leone. Lakini hakuna kiongozi hata mmoja aliyesema hadharani nchi yake itachukua hatua gani kurudufu hali ya Sierra Leone.
Nyuma ya kioo cha runinga, alikaa katibu mkuu wa serikali ya Sierra Leone, bwana Momka Tejan. Uso wake ulikuwa mtulivu na juu ya meza yake palikuwepo na glasi ndogo ya maji ya kunywa. Baada ya kusafisha koo, katibu mkuu alianza kusema dhamira yake, ama tuseme dhamira ya serikali:
“Tumesikitishwa sana na hali ya taharuki na sintofahamu kubwa ambayo imeivika nchi yetu pendwa kwa sasa. Sisi kama serikali tumeguswa kama wahanga wa kwanza na tumeteka fursa hii ya wazi kuwasiliana na wananchi wetu ili wapate kujua ni hatua gani stahiki ambayo tumeichukua. Tumekaa na kukubaliana kwamba, huu ndio muda, eidha tumechelewa au tumewahi, wa kukaa meza moja na kundi hili la MDR ili tuepuke kuwaumiza wananchi ambao ni ndugu, familia na jamaa zetu. Tunaomba sasa, sauti hii iwe kama sauti nyikani, na iwe mwanzo wa kutatua mgogoro huu unaofurukuta. Kiongozi wa MDR, atapata fursa ya kujadili na mkuu wa nchi mambo kadhaa ambayo yataepusha na hata pia kutupumzisha na vita hii. Tunatumai kwamba wito huu utakubaliwa na kuzingatiwa, na tutayamaliza haya yanayotukia. Nashukuru kwa kunisikiliza.”
Kwa General Kessy, alitabasamu baada ya kupata huo ujumbe. Kwake ilikuwa ni kama alama ya ushindi. Hakuna maagano yatakayokubaliwa kati ya wao na serikali. Ndani ya usiku huo, mpango wa kuvamia ikulu na eneo analoishi Mkuu wa jeshi la ulinzi ulisukwa. Talib alipewa jukumu la kuvamia ikulu na kumteka raisi, ambatano naye alipewa wanajeshi mia mbili, makombora na maguruneti. Kiongozi wa wanajeshi wa Guinea, akapewa kazi ya kuvamia na kumleta Mkuu wa jeshi la ulinzi akiwa hai au amekufa, naye akaambatanishwa na wasaidizi na vifaa. Tukio likapangwa kufanyika siku inayofuata wakati wa usiku.
Kutokana na matisho ya vita, hata barabara zilikuwa nyeupe. Magari yalikuwa machache au kutokuwepo kabisa si wakati wa usiku ama mchana. Hali hii general aliichukulia kama chochezi na kisaidizi cha kukamilisha mazoezi yao ya kuteka nchi.
Katika usiku huo huo ndani ya kambi ya kijeshi ya Sierra Leone amri ilitolewa toka kwa Mkuu wa jeshi la ulinzi kujiandaa kwa ajili ya kushambulia mji wa Kabala. Mashambulizi yatatumia njia ya anga kutokana na majiribio ya ardhini kushindwa kufua dafu. Japokuwa njia ya mashambulizi ya anga ni hatia kwa usalama wa wananchi, hakukuwa na jinsi kwa mujibu wa Mkuu wa jeshi la ulinzi. Ndege nne aina ya chopa zilishtushwa injini kuwekwa sawa kwa mashambulizi yaliyopangwa kutukia pale jua litakapochomoza. Lakini kabla ya usiku huo kukoma, taarifa hiyo ikafika mikononi mwa General Kessy. Simu ya mkononi iliita na sauti moja kavu mithili ya majani ya uwanda wa savana ikamtaarifu General mpango wa jeshi la Sierra Leone. Silaha za makombora ya kudungua ndege zikaandaliwa kwa ustadi na kuwekwa kwenye maeneo yazungukayo kambi na kati kati ya kambi pia.
Jua la siku iliyofuata lilikimbia na kufika utosini. Chopa nne ziliacha kambi ya jeshi zikifyatuka kwa kasi kubwa mno kuelekea upande wa mji wa Kabala huku marubani wake wakiwa wamejivika kofia ngumu zilizoshikilia miwani kubwa nyeusi zikiwa zimefunika vyema macho yao. Kutokana na kasi kubwa ya ndege hizo, haikuchukua zaidi ya dakika kumi kufika Kabala. Zikiwa zimerandana, marubani walitizamana na kupeana ishara ya kutikisa kichwa, ila kabla hawajabonyeza vitufe vya kuachia makombora, ghafla kombora moja likiwa linakimbia kwa kasi lilivamia chopa moja na kuibabua kwa mlipuko mkubwa. Kufumba na kufumbua, yalikuja makombora mengine matatu kwa kasi, chopa moja ikayeya na kukwepa huku zingine zikiishia kusombwa na mafuriko ya malipuko. Chopa iliyobakia ikageuza kama inarudi ilipotokea, kabla haijapotea, makombora manne yalitumwa kwa pupa, na huo ukawa mwisho wa rubani pekee aliyebakia, ndege ilisambaratishwa na kuwa vyuma chakavu vilivyodondokea chini.
General Kessy aliitisha umati wa wafuasi wake. Aliamuru uvamizi wa ikulu na nyumba ya mkuu wa jeshi la ulinzi ufanyike mara moja, ilikuwa ni fursa adhimu kufanya hilo tukio kwa muda huo. Kama walivyopangiwa majukumu siku iliyopita, Talib na kiongozi wa jeshi la Guinea wakatoka na vikosi vyao na kwenda maeneo yao ya matukio.
Masaa sita mbele, kila chombo cha habari kikatangaza kifo cha raisi na familia yake, pamoja na mkuu wa jeshi la ulinzi. Maiti zao zilionyeshwa zikiwa zinaburuzwa katika mitaa ya Freetown huku zikiwa uchi wa mnyama. Wafuasi wa MDR walitawala mitaa yote ya Freetown wakiwa wanashangilia ushindi kwa kuimba nyimbo zao za ukombozi huku wakiweka silaha zao angani. Miongoni mwao wakiwa watoto wadogo lakini wenye sura zilizokomaa na macho ya kuogofya. Watu walijifungia ndani ya nyumba zao, maduka na ofisi zilifungwa, hali hii ilipelekea jiji kuwa jeupe isipokuwa tu uwepo wa wafuasi wa MDR waliokuwa wakijimwaya na kujimwaga wanavyotaka. Wakivamia popote na kuchukua chochote, wakiiba vyombo vya usafiri na kuvitumia pasi na ustaarabu.








****








Mazingira yalikuwa tulivu. Wanaume waliovalia nguo za jeshi zenye bendera ya Guinea mabegani walikuwa wanazunguka huko na huko wakiwa wamebebelea bunduki aina ya SMG. Nyumba iliyokuwa inalindwa ilikuwa kubwa mno yenye rangi nyeupe. Majani ya kijani kibichi yalikuwa yametapakaa yakizunguka nyumba hiyo kubwa, pia maua. Sehemu ya kuhifadhia magari ilikuwa ni kubwa na magari yaliyokaa hapo yalikuwa ni aina ya Rolls Royce, Mercedes benz, range rover, Ferrari na Lamorghini, zote zikiwa nyeusi kwa rangi.
Ndani ya nyumba hiyo kubwa, sehemu moja iliyokaa kama kichumba kidogo cha kikao, walikuwa wamekaa wanaume wawili: Assessoko na raisi wa Guinea kwenye viti viwili vikubwa vyekundu vyenye miguu ya dhahabu. Mbele yao walikuwepo wadada warembo wawili wakiwa uchi wa mnyama, walikuwa wanacheza mitindo mbalimbali huku wakiwatizama wateja wao. Raisi wa Guinea alinyanyua mkono akawaonyesha wadada ishara ya kuondoka, wadada wakatoka. Raisi wa Guinea akamtizama Assessoko na uso wa tabasamu, akasema:
“Hongera sana. Hakika unastahili pongezi kwa dhamira yako uliyoisimamia mpaka dakika ya mwisho.”
Walinyanyua glasi zao za vinywaji wakazigongesha klang! Kisha wakanywa fundo moja. Assessoko akasema:
“Siwezi kukushukuru vya kutosha kwa msaada wako. Ila nipo kuonyesha kwamba nathamini kila tone la juhudi yako uliyoitoa. Pasipo mkono wako, ni wazi kurudisha heshima yangu inagalikuwa vigumu mno.”
Raisi wa Guinea alitabasamu, akatikisa kichwa chake.
“Usihofu, Assessoko. Sisi ni wamoja, leo wewe kesho huenda ikawa mimi. Ila … Nadhani huu ni wasaa wa kutupia macho yetu kwenye utekelezaji wa mkataba tuliojiwekea kati yangu na wewe.”
“Aaahm … kuhusu hilo jambo la mkataba, siwezi kukupa jibu kamili kwa sasa mpaka pale nitakapojadiliana na mshirika mwenzangu, Kessy.”
“Hapana! Hapana! Hapana! … hayo hayakuwa makubaliano yetu. Nilifunga mkataba na wewe na si mtu mwingine. Naomba makubaliano yaheshimiwe.”
Assessoko aliria fundo moja la kinywaji. Alitulia kwa sekunde chache, akavuta pumzi kwa nguvu na kulonga:
“Sawa, mheshimiwa. Kila kitu kitaenda sawa tu, hakuna haja ya kuhofia. Ila naomba basi muda kidogo maana nchi yenyewe ndiyo kwanza nimeikwapua, bado sijatulizana na kutizama rasilimali katika jicho yakinifu.”
“Sawa.” Raisi wa Guinea alisema, “Unachokiongea ni hoja, nami niko radhi kukupatia muda.”
Waligongesha tena glasi zao, wakapeleka vinywaji mdomoni.
Wakati jua laelekea kuzama, Assessoko alikuwa karibu na General Kessy ndani ya nchi ya Sierra Leone. Walikuwa kwenye chumba fulani kikubwa wakiwa wamekaa kwenye viti vilivyotenganishwa na meza ya kioo ambayo juu yake kulikuwa na faili la mkataba. General alikuwa amevaa nguo zake za kazi: magwanda yasiyobeba bendera yoyote, wakati Assessoko alikuwa amevalia shati jeupe na tai nyembamba nyeusi iliyorandana rangi na suruali yake ya kitambaa.
“Unaonaje kuhusu hili swala la mkataba. Kessy?”
“Mkuu, kusema ukweli kutimiza yaliyoko humo ndani ni ngumu mno. Nimejaribu kuyarejelea, nimeona ni hasara kubwa tutakayobakiza endapo kama tukitoa maeneo hayo muhimu.”
“Ni kweli. Ila sasa tutafanyeje na alitusaidia?”
“Hatuwezi kukubali kutekeleza chochote kilichokuwemo ndani ya mkataba huo. Hata kama tukikataa, hawezi kuupeleka mkataba huu popote pale kwakuwa ni kithibitisho cha kwanza kwamba alitusaidia, kitu ambacho amekuwa akipinga kwanguvu zote mbele ya umma. Huu mkataba ni kama ghelesha tu, hautakuwa na madhara yoyote utakapokiukwa.”
“Vipi endapo ataamua kuanzisha vita baina yetu na yeye?”
“Hawezi. Anajua kwamba sisi pekee ndio washirika wake kwenye utunzaji wa siri yake ya kidhalimu. Ila hata kama atataka vita, tutapambana naye.”
“Nani atakuwa upande wetu?”
“Liberia.”
“Umejuaje?”
“Le tueurs wapo kwenye nafasi nzuri ya kushika dola sasa. Guinea hatokuwa na upande wa kumsaidia kutokana na shutuma zake za kuwasaidia waasi.”
Assessoko alitabasamu huku akitikisa kichwa. Alinyanyuka, General Kessy naye akanyanyuka wakakumbatiana.
“Mwishowe tumefanikisha, Kessy.” Assessoko alisema kwa furaha, akaongezea, “Sasa nenda kawaambie hao watu wa vyombo vya habari niko tayari kuhutubia wananchi.”
General Kessy alitoka akaufuata mlango ulioukuwa upande wao wa kulia. Alirudi mkono wake wa kulia ukiwa nyuma. Alipomkaribia Assessoko alimkumbatia akautoa mkono wake nyuma ukiwa na kisu, akamchoma Assessoko tumboni mara tatu chup! Chup! Chup! Assessoko alilalama kwa maumivu. Alikodoa macho yake yaliyogeuka kuwa mekundu haraka na kuvujisha machozi. Huku mdomo wake ukitetemeka, Assessoko alimuuliza General Kessy:
“Nini nimekukosea?”
General alibinua mdomo wake akajibu:
“Kosa ulilofanya ni kudhani nakufanyia kazi wewe muda wote huo. Samahani sana, mkuu. Na ahsante kwa mchango wako.”
Baada ya kusema hayo, General Kessy alimuachia Assessoko akadondoka chini kama mzigo wa kuni. Shati lake jeupe lilikuwa limetapakaa damu. Macho na mdomo vilikuwa wazi.
General Kessy alienda mbele ya kamera akahutubia umma. Alijitangaza yeye ndiye mkuu wa nchi kuanzia muda huo. Nchi itaongozwa kwa mujibu wa kanuni na taratibu atakazoziweka kwani yeye ndiye katiba halisi.
Si wafuasi wote wa MDR waliomuunga mkono General Kessy kuwa kiongozi wa nchi. Wafuasi kumi walijitenga na kusimamia msimamo wao wa kumtaka Assessoko ndiye akaimu madaraka. Taarifa zilipofikishwa kwa General Kessy, wafuasi hao walikamatwa na kupelekwa kwenye uwanja wa taifa, wakanyongwa papo. Kisha General akatoa tishio kuwa hilo ndilo litakalowakuta wale wote watakaokaidi na kupinga maamuzi yake.
Wakati General Kessy akiwa ofisini kwa mkuu wa nchi. Simu yake ya mezani iliita. Alipokea akakuta ni raisi wa Guinea anamtafuta. Huku akiwa anatabasamu kwa kebehi, General Kessy aliongea:
“… Halo! … General anaongea hapa … Assessoko? Ameshakufa, yupo kuzimu kwa sasa … mkataba gani? Mkataba uliweka na nani? … Ah! Ah! Siwezi nikafuata makubaliano ambayo sijayaweka ndugu yangu … Nikupe pole tu na nikutakie kazi njema.”
General Kessy alirudisha simu mezani akacheka. Upande wa pili wa Guinea ilikuwa ni manung’uniko na hasira. Raisi wa Guinea alikuwa amekunja sura. Alirusha chupa ya mvinyo kabatini huku akitusi. Alibamiza meza akasema huku akiwa ameng’ata meno:
“Naapa nitakufundisha somo, mshenzi wewe! Naapa kwa Mungu wangu!”







******









Baada ya mwezi mmoja tangu General Kessy aingie madarakani, nchi za Uingereza, Ufaransa na Marekani zilikata mahusiano na nchi ya Sierra Leone. Balozi za nchi hizo zilifungwa huku mawaziri wao wa mambo ya nje wakitupia maneno makali kwa utawala wa General Kessy kuingia na kutawala kwa mabavu, kunyima haki wananchi kueleza mawazo yao, kuvifungia vyombo vya habari, kukataza vyama na shughuli zozote za kisiasa. Akijibu hoja hizo, General alitumia runinga ya serikali akajibu kwa ufupi:
“Nchi yangu inaweza kujiongoza bila ya msaada wowote wa mtu mwenye ngozi nyeupe. Wanaingilia mambo ya nchi yangu, mimi nimegusa yao?”
Siku iliyofuata, Sierra Leone ikajitoa kwenye umoja wa nchi zilizowahi kutawaliwa na mwingereza, commonwealth. Katika siku hiyo hiyo, vipeperushi na matangazo yakabandikwa na kusambazwa mitaani yakiwa yamebebelea picha ya Amadu, Chui, Farah, Mou na Ussein. Zawadi nono kutolewa kwa yeyote atakeyetoa taarifa ya upatikanaji wao.







*******




☆Steve
 
Back
Top Bottom