Njia nyembamba (Simulizi mpya by SteveMollel)

Njia nyembamba -- 05


Mtunzi: SteveMollel






Tuseme Mungu hakuwa upande wao, wanaume wale waliomkwapulia gari waziri Talib, hawakufika mbali wakakamatwa. Walikuwa wakifanya jaribio la kutoroka nje ya jiji la Freetown. Walikuwa ndani ya gari lile lile walilolikwapua, na aidha hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya wao kukamatwa kwa upesi pale tu walipoonekana na wanajeshi ambao walikuwa tayari wameshapashwa habari.



Walijaribu kukimbia na gari hilo lakini hawakufanikiwa. Barabara zilizibwa wakaishia kugonga na kujijeruhi. Wanajeshi waliwatwaa na kuwatia lupango huku Talib akipashwa habari ya kwamba ‘watu’ wake wameshatiwa nguvuni. Isichukue muda mrefu, Talib akafika eneoni. Alitumia ndege ndogo ya abiria wawili.



Alifika hapo, majambazi hao wakiwa hoi tayari kwa kichapo cha haja walichokula. Walikuwa wanavuja damu wakiwa wametepeta kama kuku wenye midondo. Hata Talib mwenyewe ilimuwia vigumu kuwatambua na kuamini kama ndio wenyewe. Aliwajongea karibu akiwa anatabasamu upande mmoja, akasema kwa kebehi:
“Mlidhani mtafika wapi?”



Hakuna aliyejibu. Hakuna aliyekuwa na nguvu hiyo. Hata tu kumtazama ilikuwa shughuli.



Talib aliguna akabinjua lips zake.
“Nataka mniambie Amadu yupo wapi!” Alifoka Talib. Aliamini sasa watu wale watakuwa wana mahusiano na THE GHOSTS na kwa namna moja anaweza akapata taarifa muhimu ya kuwapata hao mahayawani, kama vile anavyoamini.



Aliuliza sana juu ya Amadu na wenzake lakini hakupata majibu alikuwa anayataka ama kuyategemea. Alikata tamaa, lakini pia hakutaka kuacha nafasi hiyo isimuachie harufu ya waridi. Kwa kujua ama kutokujua alijikuta anaamini majambazi wale watakuwa wametumwa na THE GHOSTS, na hata kama hawajakiri inambidi ainyonye fursa hiyo adhimu sana kwake.



Alimpigia simu bosi wake, Kessy, akiwa anatabasamu pana usoni. Simu ilipokelewa ndani ya muda mfupi tu, Kessy akakoroma na sauti yake nzito. Inaonekana wazi mwanaume huyo hakuwa anategema taarifa yoyote nzuri toka kwa Talib. Ila baada ya Talib kutia chumvi kisichostahili, kuremba mkaa kwa kuupaka rangi, basi Kessy akakenua kwa furaha.



“Hakikisha wanaongea!” Alisema. “Huo ndio utakuwa mwisho wao sasa.”
Baada ya simu hiyo kukatwa, Talib aliwaagiza majambazi wale wakubali ya kwamba wao ni washirika wa wakina Amadu kama kweli wanautaka uhai wao. La sivyo siku hiyo ndiyo itakuwa ya mwisho kwao duniani.



Unajisikiaje unapoambiwa jambo hujalifanya wala hulijui? Ndivyo ilikuwa kwa majambazi hao waliokamatwa. Japokuwa hawakuwa na uwezo wa kuongea, macho yao yaliyoa uchovu wa kipigo yalikuwa kwenye butwaa. Na kama kuna swali lililokuwa linawatatiza kichwani basi ni: Amadu ni nani?



Baada ya masaa kama matano mbele walipakiwa kwenye ‘karandinga’ wakirushiwa humo kama viroba vya mnafu. Walipelekwa moja kwa moja ikulu, huko wakapokelewa na Talib na Kessy.
“Ndio hawa?” Kessy aliuliza.
“Ndio wenyewe, mkuu,” Talib akajibu akiwatazama majambazi hao na macho ya kudai ahadi ile aliyowapa.
“Wako wapi wenzenu?” Aliuliza Kessy.



Ni majambazi wawili tu ndio walikuwa wanaonyesha dalili za uhai. Walikuwa wamelala chali wakihema kana kwamba wamekandamizwa na jokofu. Ni nguvu ya kuhema tu ndiyo walikuwa nayo, ilikuwa ni ajabu Talib na Kessy hawakuligundua hilo.



Tungeweza sema labda walikuwa wanafanya makusudi.
Baada ya kuona hakuna kinachoendelea, majambazi wale walirudishwa kwenye karandinga wakaenda kunyongwa hadharani tena wakihusishwa na kundi la THE GHOSTS. Talib aliamua hivyo, na hivyo Kessy. Na walikuwa wanawaaminisha watu hivyo wao walivyokuwa wanaamini.



Miili ya majambazi hao ilining’inizwa kwenye vitanzi. Na hata hawakupapatika kutetea uhai wao, bali kungojea kifo. Ni kama vile walikuwa wamepumzishwa toka kwenye mateso ya maumivu waliyokuwa wanayapata.
Ilipohakikishwa hawapo hai, walitolewa kwenye vitanzi wakapakizwa kwenye karandinga lililowaleta wakaenda kufanywa chakula cha mbwa wa jeshi!




***




Ilikuwa ni wasaa wa jioni ya saa kumi na moja wakati mwili mzuri unaovutia wa Rose ukiwa juu ya kitanda kikubwa sita kwa sita.



Mwanamke huyo alikuwa amelala akiwa amevalia nguo nyepesi isiyombana. Nakuambia kama usingemtazama vema basi ungejikuta unakufuru kwa kumuita malaika. Alikuwa ni yule yule Rose ila kila unapomuona anakuwa mpya kama kifo.



Aliamka baada ya simu yake kuita kwa muziki laini. Ilikuwa mbali kidogo na yeye hivyo akanyoosha mkono kuidaka akiwa amefungua jicho moja. Alitazama nani anampigia akakuta ni Kessy! Aliamka upesi akasafisha koo lake na kupokea simu.



“Nimekuta missed calls zako, mrembo. Kuna shida?” Sauti ya Kessy ilinguruma ndani ya simu.
“Ndio ipo.” Rose akasema kwa sauti moja hivi tamu yenye uwezo wa kuvunja ukuta wa Berlin. “Naona hutaki kuniona kabisa,” alilalamika.
“Hapana mama, kazi zinabana.” Kessy akaroroma kuelezea. “Ila leo nimelenga kukuona kabisa, sidhani kama nitakosa hyo fursa mpenzi.”
“Mie ni mhanga wa kiu kwenye jangwa lako, nitakataaje?” Alisema Rose.



Baada tu ya muda mfupi alikuwa ameshajipara na amependeza hatari akiwa amejivika gauni lililofeli kabisa kuzuia kuonekana kwa maungo yake ya kutesa macho. Pia bila kusahau kipochi chake alichoweka zana yake ya kufanyia kazi, sumu kali ya taratibu.



Alijipulizia marashi matam akatembea kama asiyegusa chini kwenda nje ya nyumba aliyomo. Huko akakuta range rover sport nyeupe ikiwa inamsubiria. Aliingia ndani ya gari, chombo kikaondoka. Baada tu ya robo saa akawa amefika ndani ya eneo la ikulu.



Yani ni tatizo moja tu lipo ikulu, hata kama panapendeza vipi, kile kitendo cha watu waliobebelea bunduki kutembea tembea huku na huko kinaweza kukutoa kwenye ‘mood’ kabisa. Ila hilo lilikuwa kinyume kwa Rose, yeye hakuwa na shida nalo, alitembea kwa maringo kumkuta Kessy aliyekuwa amesimama kibarazani akimtazama mwanamke huyo kwa jazo la huba.



Walikumbatiana wakaingia ndani. Talib alikuwa naye ameketi sebuleni, na macho yake yalivyomtazama tu Rose akili yake ikamkumbusha ni wapi alionana na mwanamke huyo. Kulee klabu! Tena alimshika na kalio. Alijikuta moyo unampasuka na anahangaika kutafuta pumzi.
Rose alimkonyeza mwanaume huyo kana kwamba hakumbuki kitu. Talib asiweze kudumu hapo akaamua kuaga.



“Talib, yani shemeji yako ndio amekuja na wewe unaondoka?” Alisema Kessy.
“Hapana, mkuu. Kuna kazi tu nataka nikamalizie,” alijitetea Talib.
“Sawa. Umefanya kazi nzuri sana leo. Natumai utaendelea hivi mpaka uwakamate wale mahasidi!”
Talib akaondoka.



Kessy alianza kunyonyana ndimi na Rose wasahau kabisa kama wapo sebuleni. Walikuja kukumbuka hilo baadae Kessy akambeba mwanamke huyo kumpeleka chumbani. Rose asisahau mkoba wake, aliushikilia kwanguvu akaenda nao huko chumbani na kuutupia kitandani.



Kessy alimsaula nguo zote mwanamke huyo akambakiza nguo za ndani tu. kwa papara zote, kana kwamba hajawahi onja kwa mwaka mzima, alimparamia mwanamke huyo aliyemponyoka akimpiga chenga ya mwili, akatoka kitandani.



Kessy alimtazama mwanamke huyo kwa macho yanayoteswa na uchu mkavu. Rose alimtazama Kessy na macho yasiyojiweza, akasema kwa kupitia puani:
“Mie wako tu usiku mzima wa leo, utanila utakavyo.”



Rose alipomaliza kusema hivyo, alianza kuzungusha kiuno chake kwenda kushoto na kulia taratibu akicheza wimbo usiosikika. Mapaja yake mekundu yalivutia kutazama, kiuno pia na kifua chake kilichokuwa kinatikisika kipindi akitenda.



Alifanya nguo ya ndani ya Kessy ihamie sehemu moja yote.



Aliporejea kitandani alimfunga mikono mwanaume huyo kwa kutumia shuka, kisha akamvua nguo ya ndani, na kabla hajafanya kitu na anjoli ya Kessy aliiweka katikati ya mapaja yake ya moto na malaini akiwa amemlalia mwanaume huyo kifuani akichezea nywele zilizojaa eneo hilo.



Kessy alijihisi anakata roho kwa kungoja. Laiti kama angelijua lile lilikuwamo kichwani mwa Rose, wala asingetubutu kuendelea kufumba macho kwa raha aliyokuwa anapata. Yani pale hata angeambiwa ahonge Sierra Leone, angekubali pasi na kinyongo.



Rose alikuwa anasugua mapaja yake taratibu akimtazama Kessy. Ila mara kwa mara, kwa kuibia, akawa anatazama pochi yake na kuuvuta kisirisiri. Ilifikia kipindi sasa pochi ukawa upo karibu anavyotaka na ameshaufungua, na hapo ndio Kone akapewa gharika la utamu.



Rose alizunguka kiuno chake aking’ata lips zake tamu. Kiuno kilienda kwa migandisho kisha kasi … kilitulia kama kinasusa, alafu kikaenda tena kama kinakimbizwa. Kone akaachama mdomo kwa raha.



Mwanamke huyo alidumbukiza mkono wake ndani ya pochi akatia kidole chake ndani ya kichupa kilichokuwemo humo kabla hajatoa kidole upesi kikiwa na unga mweupe mithili ya sembe. Wakati huo alikuwa ananyonya sehemu ya chini ya sikio la Kessy huku akikisusa kiuno chake kwa kusua kama kina mafua.



Pasipo kujua, Kessy alisogezewa kidole chenye dawa puani. Alinusa akapiga chafya. Rose alimpa pole na kuendelea kumpa mambo jambo juu ya mtambo asimpatie mwanaume huyo hata muda wa kuwaza. Walipomaliza walipumzika mpaka kesho Rose alipoondoka pasipo kujulikana adhma yake wala afya ya Kessy kuwa na mushkeli.



Rose alimpigia simu Kone akamweleza kila kitu. Walikubaliana wakutane ‘maeneo yao’ muda si mrefu. Kweli wakafanya hivyo.


“Umehakikisha kweli?” Kone aliuliza akiwa na hamu pomoni ya kujua. Rose, mwanamke asiye na papara, akala kwanza sambusa yake akitafuna kwa madaha.



“Huniamini au?” Aliuliza akirembua.
“Nakuamini Rose ndio mana nikakupa hii kazi.”
“Basi jua nimeshamaliza.”
Kone akajikuta anatabasamu pasipo jitihada.
“Sawa,” alisema Kone kwa uso wenye bashasha. “Pesa yako taslimu utapewa punde tu tutakapopata taarifa ya kifo chake.”
“Sawa,” akajibu Rose akipandisha mabega yake juu. “Ila si ntapata advansi?”
“Pasipo shaka utapata. Tukitoka tu hapa.”



Walimalizana, Kone asipoteze muda ndani ya Sierra Leone akakwea ‘pipa’ kwenda Guinea. Huko alipanga kuonana na Raisi lakini pia vilevile kuimarisha ndoa yake kwakuwa kazi imeshakwisha sasa.



Alienda nyumbani kwake akapumzika kwa masaa matatu kisha akajiweka kwenye gari kwenda ukweni, huko alipodhani mke wake na watoto watakuwepo. Alipoteza masaa mawili barabarani kabla hajafika mbele ya geti la saizi ya kati rangi ya udongo. Alipiga honi hapo mara mbili, geti likafunguliwa.



Aliingia ndani akamkuta mkwewe, mama yake Fatma, pamoja na watotowe, lakini mke wake hakuwepo.
“Ni siku ya pili sasa sijui yupo wapi?” Alilalama mkwe. “Hapatikani hewani na sijui ameenda wapi.”



Kone akalemewa na mawazo. Aliketi akitafakuri. Aliaga watoto na mkwe wake akaondoka zake. Alizunguka kwa ‘mashoga’ zake Fatma na ndugu wote anaowajua, kote huko hakumkuta. Alijaribu kupiga simu nayo haikupatikana.



Alichoka akarudi nyumbani kwake. Alilala akiwaza na kuwazua. Hakupata kabisa usingizi.
“Fatma upo wapi mama?”




***




Baada ya siku mbili, ikiwa ni majira ya jioni, Al Saed toka Liberia alifanya ziara kuja nchini Sierra Leone kukutana na rafiki yake, bwana Kessy.



Kama zawadi, alibeba mvinyo mmoja wa ghali sana. Wakiwa wanakula chakula juu ya meza kubwa mno iliyojaa kila aina ya chakula ambavyo vingine hata havikuguswa, walikuwa wanateta mambo yao ya kiutawala, haswa namna ya kuimarisha ulinzi ndani ya tawala zao wasipate shurba.



Walipomaliza kula walitembeatembea ufukweni mwa bahari huko kwenye hewa safi. Kwa mbali walinzi wao wawili walikuwa wanawafuata kuhakikisha usalama wao.



Waliteta mengi, Kessy akiwa mshauri. Ila jipya sana lililochomoza ni maneno ya Al Saed akimtaarifu Kessy ya kwamba kuna nchi za huko ughaibuni zimemuahidi kumsaidia kwenye utawala wake, lakini wamempa masharti.



Masharti ambayo kwa namna moja ama nyingne ndio sababu kubwa iliyomfanya aje kuomba ushauri.
Kessy alijikuta ana hamu kubwa sana ya kujua hayo aliyokuwa anataka kuambiwa. Alimtazama Al Saed usoni akiwa amempa umakini wote. Lakini Al Saed akiwa anaongea, taratibu Kessy akaanza kupoteza uwezo wa kuona.




Aliyafikicha macho yake akidhani atakuwa poa, lakini haikuwezekana na hali ilizidi kuwa mbaya zaidi!
Kama haitoshi akaanza kuhisi kichwa kinauma vibaya mno. Al Saed alistaajabishwa na hilo. Walinzi walisogea karibu wakamsaidia kiongozi huyo kupata usafiri wa haraka, ‘ambulance’, akawahishwa hospitali.
Al Saed, Talib na kiongozi mwingine wa juu walikuwepo pia eneo hilo. Walikaa wakiwa wamestaajabu ni nini kimetokea. Ulinzi wa eneo hilo ulikuwa mzito sana kiasi kwamba hakuna hata mbu aliyepita.




Baada ya kukaa hapo kwa muda wa lisaa limoja tu, daktari alikuja kuwapa taarifa ya mgonjwa. Alimtazama Talib kisha Al Saed, akameza mate. Ni kana kwamba alikuwa anahofia kuongea. Na ni kweli kwa namna alivyokuwa anatazamwa, alikuwa ana haki ya kuogopa. Talib alikuwa ametoa macho kama nyanya mbichi wakati Al Saed akiwa amekunja uso mithili ya tambara la kikongwe.




.***




☆Steve
 
*Njia nyembamba -- 06



*Mtunzi: SteveMollel











Baada ya kukaa hapo kwa muda wa lisaa limoja tu, daktari alikuja kuwapa taarifa ya mgonjwa. Alimtazama Talib kisha Al Saed, akameza mate. Ni kana kwamba alikuwa anahofia kuongea. Na ni kweli kwa namna alivyokuwa anatazamwa, alikuwa ana haki ya kuogopa. Talib alikuwa ametoa macho kama nyanya mbichi wakati Al Saed akiwa amekunja uso mithili ya tambara la kikongwe.




“Nasikitika kuwaambi …”
“Amekufa?” Talib aliwahi.
“Hapana, hajafa.” Daktari akajibu kwa sauti ya upole. Talib alishusha pumzi akadaka kiuno chake.
“Raisi ni aidha amekula ama amepewa sumu kali sana. Ni bahati kwake kuwa hai mpaka muda huu. Tunaweza tukauita muujiza.”




Jambo hilo likawachanganya Talib na Al Saed kwa mawazo. Kessy amekula sumu muda gani, na hivyo basi nani kampa? Japokuwa waliteta na kuulizana sana kuhusu hilo swala hawakupata jibu wakaishia kutegemea labda Kessy atakapopata uwezo wa kufungua kinywa basi utajulikana upi ni mchele na upi ni pumba.




Lakini zaidi ya hapo hilo swala pia likaonekana gumu baada ya muda kidogo daktari kuja na kuwapa taarifa ya kwamba hana uhakika ni kwa muda gani Kessy atakuwa kitandani mpaka aje kupata fahamu zake kwani sumu aliyotumia bado haijajulikana ni ipi ili basi wafahamu namna ya kuikabili.




“Kwahiyo daktari unataka kusemaje?” Talib alikunja sura.
“Mi – mie sina usemi mheshimiwa. Laki …”
“Lakini kitu gani? … kwani wewe kazi yako ni nini? Unavyotuambia haujajua ni sumu gani sisi ndio tutajua?”
“Tutajitahidi mheshimiwa kwa kadiri ya uwezo wetu. Tunaomba tu utupatie muda.”
“Daktari, kaa ukijua ya kwamba; akifa nawe utazikwa naye.”




Hilo tisho likafunga maongezi kati ya Talib na daktari aliyeondoka upesi kuelekea ndnai ya chumba maalum alipolazwa kiongozi mkuu wa nchi.
Baada ya muda mchache mbele, Al Saed akaaga anaondoka kurudi Liberia, lakini akiahidi kuendelea kumjulia hali rafiki yake huyo aliye taabani. Talib alimsindikiza kiongozi huyo mpaka uwanja wa ndege, akaondoka zake.




Wakati Talib akirejea kurudi hospitalini, bado kichwa chake kilikuwa kinachakata swala la Kessy. Mambo yalikuwa magumu lisilionyeshe dalili ya kung’amulika. Ila kwa namna moja ama nyingine akili ya Talib ikaanza kuelekea kwa Al Saed ya kwamba yeye ndiye anaweza kuwa mtuhumiwa wa tukio hilo. Alijitahidi kukataa lakini bado akili yake ilitokea kuamini hivyo.




Al Saed ndiye mtu wa mwisho kuwa na Kessy, kwa siku zote hizo za nyuma Kessy alikuwa mzima. Al Saed alikuwa ndiye mtu wa mwisho kula na Kessy, na pia kwa mujibu wa maelezo yake, Al Saed alimletea Kessy mvinyo kama zawadi.




Ila afanye hivyo kwasababu gani ingali hawakuwa na ugomvi wowote? Kama wangekuwa na tofauti yoyote basi Talib aliamini angekuwa anaifahamu.




Alijitahidi kuitafuta sababu ya Al Saed kutenda hilo tendo, akakosa kabisa. Sasa basi akili yake ikawa inaamini yule ndiye mtenda lakini pia kwa wakati huohuo tena akiwa anajikosoa.




Kufa kufaana lakini, waswahili walinena. Japokuwa Talib alikuwa kwenye rundo la mawazo, alijikuta anapata tabasamu katikati yake baada ya kujigundua ya kwamba ni yeye peke yake sasa ndiye atakaimu kiti cha uongozi wa Sierra Leone mpaka pale Kessy atakapopona. Na kama je asipopona?




Kabla hajapata jibu alikuwa ameingia ndani ya hospitali pamoja na msafara wake. Aliendea karibu na chumba alicholazwa Kessy akaketi karibu.





***





Zilipita siku tatu.




Siku inayofuata, yaani ya nne, ilikuwa ni mahususi kwa THE GHOSTS kutoka ndani ya jiji la Freetown waende kutafuta mahali tulivu na papekee kwa ajili ya kujiandaa kama kikundi na hata pia kuongeza idadi ya watu baada ya kuona kuna haja hiyo.




Hilo halikuwa shida, bali watatokaje nje ya jiji hilo ukizingatia wanajeshi wameambaa huko kwenye barabara, njia za maji na hata uwanja wa ndege? Mipango ilihitajika, tena mipango thabiti ya kukwepa vikwazo. Mipango itakayowawezesha kuwakwepa wanajeshi lakini kwa wakati huohuo wasafirishe silaha na wajisafirishe na wao pia.




Hivyo basi kwa usiku mzima walipanga namna ya kutenda ili kukwepa. Asubuhi ilipodamka, gari kubwa, canter nyeupe iliyofunikwa na shuka kubwa la ngozi, lilitoka ndani ya nyumba hiyo na kushika barabara ya lami. Mwendo wake ulikuwa wa wastani na vioo vyake vilikuwa vimejiveka rangi nyeusi usiwaone waliomo ndani.




Gari hilo lilielekea upande wa kusini wa jengo lilimotokea. Baada ya muda mfupi likaingia kwenye barabara kuu na kuanza safari ya kuelekea upande wa mashariki. Halikudumu sana katika barabara hiyo kuu, likachepuka na kwenda upande wake wa kushoto. Huko lilikaa kwa muda wa masaa matatu likafika mahala kulipokuwa na msururu wa magari yakingojea zamu ya kukaguliwa.




Kulikuwa kuna wanajeshi sita kwa macho ya haraka. Wote walikuwa wamebebelea bunduki ndefu mikononi mwao na kwa kugawana walikuwa wanakagua magari, huyu akishika hili basi yule lile.




Taratibu magari yalienda, na mpaka ukafikia muda ambapo Canter lilikuwa la pili kwenye msururu. Basi kutokana na ukubwa wa gari hilo na kufanya ukaguzi uwe wa kiufanisi zaidi, wanajeshi watatu walilidaka ambapo mmoja alisimama upande wa dereva wakati wengine wakiwa wanalitazama kiubavu.




“Shukeni chini,” ilitoka amri. Alikuwa ni yule mwanaume rasta, mwanaume aliyekubali kuungana na Amadu pasipo shuruti.




Alishuka akatia mikono yake mfukoni. Rasta zake zilikuwa zinamtekenya mabega, na uso wake haukuonyesha hofu yoyote.




“Umebeba nini humu?” Aliuliza mwanajeshi kwa uso kakamavu.
“Nimebeba nyama. Nawapelekea wazazi wangu kijijini,” akajibu Rasta.




Aliamriwa aonyeshe nyama hiyo, akaenda nyuma ya gari na kufungua shuka lililofunika gari. Humo ndani kulikuwa kuna ‘dude’ kubwa rangi nyeusi lenye pembe nne. Rasta aliamriwa alifungue hilo dude kionekane kilichomo ndani. Akasita.
“Samahani, nina aleji na nyama. Nitapata matatizo endapo nitanusa harufu hiyo.”




Basi mwanajeshi mmoja akajitolea kwenda kutazama. Alifungua dude hilo na kukuta mfuko mweupe ukiwa umefunika nyama iliyokuwa inanukia vilivyo. Alipekua nyama hiyo asikute kitu. Waliporidhika hamna jambo, walieleka na kwa dereva wakapekua, napo hawakukuta kitu hivyo wakamruhusu Rasta aende zake. Gari likaenda.




Ilipita kama dakika kumi na tano, mwanajeshi yule aliyepekua nyama, pamoja na yule mwenzake, wakaanza kuwashwa miili. Walijikuna kama hawana akili nzuri. Mwasho ulizidi kuongezeka sambamba na muda, sasa wakawa kama vichaa. Walipiga kelele kali na kuzua tafrani, walitokwa na vidonda kwa kujikuna wakawa wanavuja damu. Wenzao walisitisha zoezi la ukaguzi wakawajongea kuwatazama kwa bumbuwazi.




Walitaka kufanya utaratibu wa kuwawaisha hospitali ya karibu kwa kutumia usafiri wao, lakini kabla hawajatenda hivyo wakaliona gari la wagonjwa. Na kwenye ubavu wa gari hilo kulikuwa kumeandikwa jina la hospitali iliyo karibu. Basi kwa haraka wanajeshi wakawasaidia wenzao kuingia kwenye gari la wagonjwa wapate kwenda kupata tiba. Na kwa msaada zaidi, mwanajeshi mmoja mzima, sajenti, akaongozana na wenzake.




Hakukuwa na muda wa kukagua gari hilo la wagonjwa, wanajeshi wagonjwa walipakiwa na chombo kikaondoshwa kwa kasi kuelekea hospitali. Dereva alikuwa ni Chui akiwa sambamba na Ulsher. Walikuwa wamevalia kofia nyeupe za nailoni na miwani ya macho. Walifika mbele Ulsher akachomoa bunduki na kumtwanga yule mwanajeshi mzima kisha akatoa simu ndani ya mfuko wake na kupiga.
“Muda ndio huu.”




Kisha akakata alafu akampisha Ulsher ashike usukani kabla hajaenda kutwaa ‘redio koo’ na kuitumia kuwasiliana na wanajeshi waliobakia kule kwenye kitengo cha upekuzi. Aliwapa taarifa ya kwamba kuna ujio wa gari kubwa hapo, canter ya kijivu, akalitaja na namba zake za usajili. Taarifa ni kwamba gari hilo linatakiwa kupita upesi.




Isipite muda mrefu, wanajeshi watatu waliobaki kwenye ukaguzi wakaliona gari hilo. Baada ya kujiridhisha ndilo lenyewe, gari hilo likapita wasijue ndaniye yapo mabaki ya wana THE GHOSTS.




Canter hilo lilitembea kwenda kukutana na ambulance pamoja pia na canter nyeupe ya mwanzoni. Tayari wanajeshi wale wawili, waliokuwa wanawashwa, walishakufa kwenda kukutana na mwenzao aliyeuwawa kwa risasi. Wote walivuliwa nguo zikapuliziwa dawa kabla ya kuvaliwa na Fredy na rafiki yake Rasta, Thomas, sasa wakaonekana ni wanajeshi.




Walijipaki wote kwenye canter ya kijivu huku sehemu ya dereva na mwenza wakiwepo wanaume hao ndani ya sare. Sehemu ya nyuma palipokuwa pamezibwa, pakawa pamehifadhi silaha na wengineo wana THE GHOSTS.




Canter hiyo ilisonga kwa muda wa masaa matatu mbele kabla ya kukutana na kizuizi cha mwisho watoke ndani ya Freetown. Kwa muda wote huo Chui alikuwa anaisikiliza redio koo kwa umakini ili wapate kujua kama kuna namna yoyote mpango wao upo hatarini. Lakini mpaka wanafika kwenye kizuizi cha mwisho, walikuwa salama.




Kwenye kizuizi hiki hakikuwawia vigumu, wanaume wale waliokuwa wameketi mahali pa dereva walitumia nguo za za jeshi vema kuwalaghai wapekuzi na kisha kwenda zao sasa nje ya Freetown. Kwenda huko msituni wapate kujikoboa kwa mafunzo, lakini pia kujiongeza.




Kukaa ndani ya Freetown kungewanyima fursa hiyo ya ‘kujiachia’ wapendavyo. Kwa namna iliyopendeza machoni, kutumia mfumo wa MDR kwa kuketi mbali na mkono wa serikali, lakini pia karibu na raia, ulikuwa ni mpango mtamu zaidi kufikisha malengo.





***




Japokuwa ilikuwa ni mchana kamili, Kone alikuwa amechoka na yu kitandani akiwa hajafanya lolote tangu asubuhi, hata kunawa uso.
Alikuwa amejifunika shuka mpaka kiunoni. Mara moja moja bado alikuwa anafunga macho yake kwa usingizi na kisha akiyafungua tena. Ni dhahiri shairi alichelewa kulala, alafu hakuwa anatakata kulala tena.




Alitafuta simu yake ya mkononi, akaikuta kitandani. Aliitazama kama kuna habari yoyote kwenye kioo, hakukuta. Alisonya kisha akatafuta jina la Rose aliloliita akiiweka simu sikioni. Baada ya muda mfupi simu ikapokelewa, na sauti ya kike ikanena upande wa pili.




“Vipi umepata taarifa zozote za Kessy?” Kone aliuliza.
“Hapana,” sauti ikamjibu.
“Inakaribia juma sasa, Rose. Kweli ulimpatia sumu?”
“Bila shaka.”
“Mbona hamna majibu?”
“Sijajua kwanini. Nitajitahidi kufuatilia.”




Kone alikata simu akairushia mbali. Kwa namna moja aliona ulimwengu umeamua kumfanya asiwe na amani. Ni siku kadhaa sasa anawinda habari njema na hazipati, si kwa mkewe wala huko Sierra Leone. Alijiona yupo kwenye jehanamu ndogo. Aliona kana kwamba watu wa ulimwengu wamekaa kando wakifurahia anavyotaabika.




Alijinyanyua toka kitandani alipatie tumbo lake chochote kitu. Alijiiandalia chakula cha upesi: cornflakes na maziwa, kisha akaketi mahala pa kulia chakula. Alijitahidi kula lakini alishindwa, hakuwa na hamu kabisa japokuwa alihisi njaa. Alijikuta anasogeza bakuli la chakula kando na kushika tama.




Mke wake, bi Fatma, alitawala kichwa chake. Na hata pale alipompa ahueni, basi Kessy akachukua zamu. ‘shift’ hiyo ilimnyima raha. Alihama kila kona ya nyumba mpaka jioni ikawasili. Wakati sasa akiitafuta usiku, alikuwa sebuleni akitazama taarifa ya habari. Alitamani aone habari ya msiba wa Kessy lakini kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga, matumaini yakawa yanafifia.




Akiwa hapo bado anakodoa, alisikia mlango wa mlango wa sebuleni unafungwa. Upesi aligeuka kutazama akamwona mke wake, bi Fatma, akiwa amevalia dera na anatembea kwa kuyumba. Alikuwa amelewa!




Kone alisimama akamfuata mkewe akimwita jina. Fatma alimpuuza mumewe na hakutaka kuzozana juu ya hali yake. Hakusema wapi ametokea wala wapi alipokuwa siku zote hizo. Mdomo wake ulikuwa unanuka mvinyo wa bei ghali. Alikuwa mkali kama mbogo akisisitiza asiguswe.




Hatimaye, alijifungia ndani ya chumba akimwacha mume wake mlangoni na mabumbuwazi.




“Fatma fungua!” Kone alibamiza mlango. Macho yake yalikuwa mekundu. Uso wake ulikuwa mweusi.
Alikaa hapo kama lisaa asifunguliwe mlango. Alimwendea mlinzi na kumuuliza juu ya ujio wa mke wake, mlinzi akamtaarifu ya kwamba aliletwa na gari kubwa, Toyota Prado nyeusi. Kone akachanganyikiwa kwa fundo la wivu.



Alirudi ndani akaenda kubwatukia maswali yake mlangoni mwa chumba alimo Fatma, lakini hakupewa jibu lolote. Fatma alikuwa amelala na inawezekana alikuwa hata hasikii linaloendelea.



Kone alikata tamaa akaenda zake kulala kwa matumaini ya kwamba kesho yake, pombe zikiwa zimemtoka Fatma, basi atapata majibu anayoyataka. Alijitahidi kupunguza jazba.



Ilimchukua kama masaa matatu kitandani kuupata usingizi. Alikuja kuamka muda wa saa mbili asubuhi, kesho yake, akaendea kile chumba kilichomficha mkewe.



Mlango ulikuwa wazi. Aliingia ndani akakuta kitanda cheupe, hakuna mtu! Alitafuta nyumba nzima asimuone mke. Alimwendea mlinzi akamuuliza, mlinzi akamhabarisha ya kwamba mwanamke huyo aliondoka kwenye majira ya saa kumi na mbili, na gari lililomleta jana ndilo limekuja kumtwaa.



Kone alirudi ndani aking’ata kidole chake kana kwamba anataka kukitemea chini. Alimpigia simu mkwe wake kumuuliza kama mkewe yupo huko, akakanusha. Aliwapigia na rafiki wa mke wake anaowajua, nao wote wakakanusha. Hakuna aliyempatia majibu zaidi ya kusema “sifahamu”.




***




Zinapita siku tano.




Talib akiwa nyumbani kwake anamkumbuka mwanamke yule aliyekutana naye klabu ya usiku ya Aces. Anakumbuka namna alivyoshika maungo yake na namna alivyomkonyeza akiwa na Kessy, basi akajikuta anatabasamu mwenyewe kama mwehu.



Alijikuta anatamani kumuona tena mwanamke huyo. Alijikuta ana kiu ya kutaka kumtia mikononi. Kessy alikuwa yu hoi kitandani, hivyo basi hakuna wa kuukata mkono wake mrefu unaotaka kumdaka mwanamke huyo.



Lakini kumbuka Talib hakuwa na namba ya simu wala hawakuwa anajua makazi ya mwanamke huyo, hivyo basi ilimlazimu kufanya namna ya ziada kumpata mwanamke huyo basi amfaidi kabla Kessy hajarudi fahamuni.



Alimtafuta dereva aliyemleta Rose ikulu siku ya mwisho kumuona mwanamke huyo, akampata. Zoezi hilo lilikuwa rahisi kwake kwasababu alikumbuka ni gari lipi lilitumika baada ya kuliona limepaki nje alipokuwa njiani kutoka ikulu siku ile. Lakini pia alikumbuka ilikuwa ni majira gani na gari lilifanya tukio gani.



Dereva alimweleza mahali alipomtoa mwanamke yule, basi Talib akaanza kuchukua hatua. Alijiweka kwenye gari akiwa na ‘kamsafara’ ka magari matatu mpaka eneo anapoishi Rose. Alimkuta mwanamke huyo akiwa amevaa sketi fupi nyeusi na blauzi rangi ya udhurungi ikiishia juu ya kitovu. Hakika alipendeza japokuwa haikuwa dhamira.



Talib alimsalimu na kumtaka waende mahali bora zaidi ya pale wapate kuteta. Rose alitaka kubadili nguo lakini Talib hakuweza kuvumilia, alimtaka waende vivyo hivyo kwani bado alikuwa anavutia sana.



Walijipaki kwenye gari wakaondoka. Rose alitabasamu akimtazama Talib, Talib akajiona yu peponi kwa wasaa.



Lakini kama angelijua ni nini Rose alikuwa anakiwaza kichwani, basi angemshusha mwanamke huyo aende zake ili apate kujinasua toka mtegoni.
Tabasamu la Rose lilikuwa zuri mno, hata macho yake pia. Lakini roho yake, hakuna binadamu anayeiweza zaidi tu ya yule aliyemuumba.





***




☆Steve
 
Back
Top Bottom