Dennis Robert Shughuru
JF-Expert Member
- May 30, 2024
- 4,801
- 7,483
Deni la Taifa limekua sana na kila mtu analalamika kivyake lengo la uzi sio kutupia lawama sehemu yeyote ile bali kuja na siluhisho
Mimi nina mpango wa kuwa Rais wa Tanzania zifuatazo ni njia ntakazotumia Kupunguza ukuaji wa deni la Taifa
Mimi nina mpango wa kuwa Rais wa Tanzania zifuatazo ni njia ntakazotumia Kupunguza ukuaji wa deni la Taifa
- Kupunguza kodi (mfano VAT asilimia, corporate tax asilimia 8, individual income tax asilimia 5 flat rate/proportional tax)
- Kupunguza mishahara ya wabunge na kuwa million 7 take or leave it
- Kuondoa mikopo ya gari kwa wabunge wakitaka magari watanunua kimpango wao kama ilivyo kwa watumishi wengine
- Kupunguza misafara ya viongozi na kuwa midogo
- Ni kosa la jinai kwa watumishi wa umma kufanya kazi nje ya ofisi kwa malengo ya kufosi per diem lazima uwe na sababu za msingi
- Miradi yote mikubwa kama treni, barabara, flyover itafanywa na makampuni ya watanzania Hakutakuwa na compromise lengo kuhakikisha fedha yote inayotumika kwenye ujenzi ambayo ni nyingi sana inabaki Tanzania ili kubost Multiplier effects. Imagine zile Trillion 15 na zaidi zilizotumika kuwalipa makampuni ya nje zingebaki hapa Tanzania ni wazi zingeboost ukuaji wa uchumi
- Magari ya serikali yatakuwa yananunuliwa mara moja kila baada ya miaka 5 na sio kila mwaka kama ilivyo sahivi
- Serikali kufanya biashara, ukienda nchi za gulf moja ya mafanikio yao ya haraka sana ni pale Serikali zao zilipofanya biashara mfamo mashirika ya Emirates, etihad, oramco ceo wao ni wazungu. Kwa Tanzania mashirika kama ya TANESCO, MWENDOKASI, MIGODI N.K maceo wao watakuwa ni foreigner ambao watawekewa target lengo ni kuhakikisha yanakuwa na faida na inabaki hapa Tanzania