Niwazavyo mimi; ajira mkononi mwako; shida za watu ndo kazi yako

IPILIMO

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
1,819
799
Haya wakuu, hivi ndivyo niwazavyo mimi, dont qoute me wrong!

Fursa za kujiajiri zinatokana na gap la ufahamu/ujuzi kati yako na watu wengine katika jamii/taifa. Pia kila mtu kwa wakati fulani anakuwa na magumu anayopitia; yanahitaji ufumbuzi; na mengi ya mambo hayo hutatuliwa na watu wenye ufahamu/ujuzi huo!! mfano mimi ni consultant katika masuala ya maendeleo, miradi na resource mobilisation! Naamini wapo watu wenye shida fulani ambayo katika haya niyafanyayo ufumbuzi wake utatokea. Na pia ni vema watu wakajua tunategemeana kwa namna moja au nyingine. Hata kama ni msomi vipi bado nitahitaji ufumbuzi wa masuala yangu kwa watu/kampuni fulani. Cha msingi mtu binafsi lazima ujue strenght yako ni ipi!! Kila kazi duniani ni product ya haya ninayo sema!! Watanzania wasipende kutatuliwa matatizo yao bure, hata kama ni ushauri hasa wa kitaalamu!!! tukifanya hivyo vijana wengi wasomi watajiajiri. Naona wenye elimu ndogo au wastani ndo wanaweza sana hii kanuni; kuna carpenters, car wash etc, ili sisi wenye magari tupate ufumbuzi wa magari yetu kuwa safi kutoka kwao. Kama hutaki kuwalipa osha mwenyewe, ila hutafanya kwa ustadi, na wale vijana watabaki hawana kazi!!
 
Unaelekea kuwa SANGOMA siku si nyingi mkuu

Hata sangoma wamejiajiri kama nilivyo eleza hapo juu!! Mimi nitabaki na ya kwangu iliyo sajiliwa kwa sheria za nchi hii!! wenye shida na huduma yake kama kawaida wanapyembelea ofisini kwake!
 
Back
Top Bottom