Niulize maswali kuhusu software ya Adobe After Affect & Adobe Premiere Pro

Niulize maswali kuhusu software ya Adobe After Affect & Adobe Premiere Pro

Nina video ambayo ina background noise kiasi fulani(sababu ya camera ya quality ndogo),naweza kutoa background noise na premier pro??? Na je tool ipi ni bora zaidi kutoa background noise kwenye vids??
 
Nina video ambayo ina background noise kiasi fulani(sababu ya camera ya quality ndogo),naweza kutoa background noise na premier pro??? Na je tool ipi ni bora zaidi kutoa background noise kwenye vids??

neat video
 
Maana nilikuwa na google hapa,wanasema hiyo pia inaweza kuwa plugin kwa video editors kama premier pro etc.... storyteller
 
Last edited by a moderator:
Nina video ambayo ina background noise kiasi fulani(sababu ya camera ya quality ndogo),naweza kutoa background noise na premier pro??? Na je tool ipi ni bora zaidi kutoa background noise kwenye vids??

sijawi kukutana na case kama hiyo,ila nitajitahidi kukusaidia.suluhisho lake sidhani kama linaweza tatuliwa na premiere pro peke yake.

bila shaka wewe ni mtumiaji wa AE,naomba nikushauri upeleke hilo file ktk AE,then tumia masking tool ku-mask hiyo video uki-pay attention ktk movement ya subject ambayo unataka ibaki ktk video.

baada ya hapo create layer mpya na uiweke chini ya ile layer ya kwanza ambayo ina video ambayo umei-mask.

chukua ile video ambayo hujai-mask,i-drag ktk layer ya chini.baada ya hapo nenda ktk effect and preset window,tafuta effect/tool inaitwa fast blur(inapatikana pia ktk adobe premiere pro),apply fast blur tool ktk video yako ambayo hujai-mask.

fungua effect control window,shuka chini kidogo ya fast blur effect,kuna kibox kimeandikwa repeat edge pixels,tick hicho kibox,adjust fast blur effect from 00 to 100+.nenda tena kwenye effect and preset window,chukua effect inaitwa linear wipe(inapatikana pia ktk adobe premiere pro).apply linear wipe ktk video ambayo ulii-mask,adjust vizuri linear wipe ili kuondoa uhalisia ktk border. bila shaka mpako hapo utakuwa umeondoa BG noise kwa asilimia 70 au zaidi na unaweza kuirudisha video ndani ya premiere ili uendelee na editing.

matokeo yanaweza kuwa kama hivi ktk picha.

kabla ya ku-apply chochote.
1.jpg

wakati wa kufanya masking.
2.jpg




baada ya masking na baada ya ku-apply fast blur and linear wipe effects.
4.jpg

angalizo:maelekezo haya ni yangu mimi,mwingine anaweza kuwa na maelekezo tofauti lakini yenye matokeo mazuri zaidi.karibuni.
 
Mkuu mm pia niko interested na kujifunza graphics design, nn natakiwa nianze nacho kabla sjahamia kwenye izo software.
Thanks
 
Mkuu mm pia niko interested na kujifunza graphics design, nn natakiwa nianze nacho kabla sjahamia kwenye izo software.
Thanks
ni bidii tu kaka.la msingi na la kuzingatia ni kufanya maamuzi shahihi ya app unayotaka kujifunza,sababu apps zipo nyingi.ukisha fanya machaguzi la app gani unataka kujifunza,kitakacho fata ni kuweka bidii ya kuisoma app hiyo na kufanya majaribio ya kimazoezi mara kwa mara kadili utakapo pata nafasi.
 
Mkuu mm pia niko interested na kujifunza graphics design, nn natakiwa nianze nacho kabla sjahamia kwenye izo software.
Thanks

Anza na Adobe Photoshop> Adobe Illustrator> Adobe Premier>Adobe After Effect

Ukizijua hizo zote unakuwa umewiva kwa kiasi fulani, unaweza ukaanza kuongezea na nyinginezo eg. Cinemax 4D, Final Cut,etc


#Mtazamo tu
 
heri ya pasaka.....leta swali kama unalo.

Naonaga kwenye film nyingi za kutisha, kwenye labda scene za mtu kuyeyuka au kubadilika kuwa mbuzi au whatever ,bado kuna faking ya jinsi picha zinavyounganishwa, yani unaona kabisa apa wameunganisha picha mbili tofauti, nini kifanyike ili kuzuia hyo hali na kutengeneza believable scene? Au ni program ipi sahihi inayotumika kucheza na hzo ishu?
 
Anza na Adobe Photoshop> Adobe Illustrator> Adobe Premier>Adobe After Effect

Ukizijua hizo zote unakuwa umewiva kwa kiasi fulani, unaweza ukaanza kuongezea na nyinginezo eg. Cinemax 4D, Final Cut,etc


#Mtazamo tu
mtiririko mzuri wa kujifunza,japo sio muhimu sana.unaweza anza na AE au na yeyote kati ya hizo kama kichwa chako ni chepesi kuelewa kwa uharaka.

kwa mazingira ya sasa,ni muhimu sana kuwa "multi tasked".uweze kucheza na software zaidi ya moja au mbili.
 
Naonaga kwenye film nyingi za kutisha, kwenye labda scene za mtu kuyeyuka au kubadilika kuwa mbuzi au whatever ,bado kuna faking ya jinsi picha zinavyounganishwa, yani unaona kabisa apa wameunganisha picha mbili tofauti, nini kifanyike ili kuzuia hyo hali na kutengeneza believable scene? Au ni program ipi sahihi inayotumika kucheza na hzo ishu?

zipo advanced techniques mbalimbali za kufanya hivyo,hapa nazungumzia kwa zile big budget films.lakini pia kuna njia za kawaida tu zisizo na gharama.njia hii mtu yoyote anaweza fanya,hata wewe hapo ulipo ukifata maelekezo vizuri unaweza fanya,ila tu hakikisha unacheza na light vizuri ili usipoteze uhalisia wa kimazingira.
 
Kwa kweli hii adobe premiere pro ili nitoa kamasi sijajua hata nianzie wapi maana ili bidi niitoe tu nirudi kwa corel na powerdirector..

ila upo vizuri mkuu sijawaona kina kadoda11, wickerman na wengine..
 
Kwa kweli hii adobe premiere pro ili nitoa kamasi sijajua hata nianzie wapi maana ili bidi niitoe tu nirudi kwa corel na powerdirector..

ila upo vizuri mkuu sijawaona kina kadoda11, wickerman na wengine..
mkuu pole sana kwa usumbufu unao upata kwenye adobe premiere pro.labda tushirikashane maswali,wapi unatatizika na premiere?.uliza tu,tutasaidiana.nipo online saa hii na nimefungua adobe premiere.
PP.jpg
 
Mimi nna interest sana na hii kitu ila ciijui hata kidogo nmetumia photoshop lakini nayo kwa
kuunga unga youtube sasa nataka nianze kuijua AE unanisaidiaje
kwa kuwa mjadala wetu unafanyika online,msada pekee ninao weza kukusaidia kwa sasa ni kuniuliza swali,nami nita jitahidi kadili ya uwezo kukujibu kwa kukupa maelekezo.halikadhalika,nina video tutorials za kutosha za AE ambazo ni very useful for beginners.jisikie huru kunitafuta kama utazihitaji.

adobe after effect tutorials.
attachment.php
 
Kama kuna yeyote aliyekwisha fanya kazi yoyote na hizi tools atuwekee link tuone mfano kuna jamaa fulani mTz anafanya graphics "luiarts" yupo youtube,mnaweza muona
 
Mim swali langu, ni kwanin material ninayoedit ktk premier pro huwa ni mazito sana na nikipunguza uzito quality ya video Inapotea, naomba msaada
 
Mim swali langu, ni kwanin material ninayoedit ktk premier pro huwa ni mazito sana na nikipunguza uzito quality ya video Inapotea, naomba msaada

pole kwa usumbufu unao upata na asante kwa swali lako.
moja ya sababu inayo sababisha uzito wakati wa ku-edit videos ktk premiere pro, ni kukosea kufungua sequence yenye properties ambazo hazirandani na videos ambazo ume-import.

tunapo ongelea video properties,tunaongelea vitu kama aspect ratio,frame rate,video type(mpeg,mov,avi nk),image size na display resolution( probably HD videos).

tukirudi kwenye case yako,nakushauri ujaribu kusoma properties za videos zako,pia uende ndani ya premiere pro,fungua sequence mpya yenye properties zinazo fanana na videos zako.

drag video moja kwenye timeline,halafu tazama juu ya timecode,inakupa rangi gani,red au yellow.ikikupa red color ina maana bado hukufungua sequance sahihi,itakuwa nzito wakati wa editing.ikikupa yellow color,jibu ni kwamba sequence ni sahihi na haitakuwa nzito wakati wa editing na rendering.hautakuwa na sababu ya ku-transcode videos nje ya premiere pro,kwani madhara ya kufanya hivyo ni kushusha ubora wa picha.

sequence zipo nyingi,hutakiwi kuvunjika moyo.jaribu kadili uwezavyo mpaka upate sequence sahihi.

nakuwekea screenshots hapa chini.bila shaka zitakupa muongozo wa maelezo yangu.asante na karibu tena.

video properties/descriptions
properties.jpg

sequence types and settings
sequence descriptions.jpg
red timeline
timeline.jpg
yellow timeline

timeline yellow.jpg
 
Back
Top Bottom