Anyisile Obheli
JF-Expert Member
- Dec 13, 2009
- 3,398
- 319
Nitayasema haya,
Bila kuyaonea haya,
Tuuche umalaya,
Utatupeleka kubaya.
Viwili Mola aliumba,
Kutimiza yake namba,
Mme alipomuumba,
Na mke pia akamuumba.
Ni vipi wewe wataka,
Tena tamaa kuwaka,
Rijali umejiweka,
Eti kila mke wataka.
Mwanamme akaweko,
Kasha mke akaweko,
Mwanaume hakuweko,
Na kisha wake kuweko.
Ni kweli kichwa kimoja,
Hubeba ndoo moja,
Ni vipi kichwa kimoja,
Ndoo zaidi ya moja.
Umalaya hulka chafu,
Utatufanya wafu,
Tuenende kwa hofu,
Tena tusiwe vipofu.
Bila kuyaonea haya,
Tuuche umalaya,
Utatupeleka kubaya.
Viwili Mola aliumba,
Kutimiza yake namba,
Mme alipomuumba,
Na mke pia akamuumba.
Ni vipi wewe wataka,
Tena tamaa kuwaka,
Rijali umejiweka,
Eti kila mke wataka.
Mwanamme akaweko,
Kasha mke akaweko,
Mwanaume hakuweko,
Na kisha wake kuweko.
Ni kweli kichwa kimoja,
Hubeba ndoo moja,
Ni vipi kichwa kimoja,
Ndoo zaidi ya moja.
Umalaya hulka chafu,
Utatufanya wafu,
Tuenende kwa hofu,
Tena tusiwe vipofu.