Nitawakingaje wanangu wasitumie madawa?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
13,718
14,150
Pamoja na kuchanganyika na kucheza pamoja lakini sio watoto wote mtaani wanatumia madawa ya kulevya. Wako watoto ambao hawavuti hata sigara ya kawaida ingawa wanaishi pamoja kwenye nchi, mkoa, wilaya, tarafa, kata, kijiji/mtaa au hata kitongoji au nyumba moja na watoto wengine ambao wanatumia madawa ya kulevya.

Hivi, ni sababu zipi zinazosababisha watoto watumie au wasitumie madawa ya kulevya?. Ni nini nafasi ya familia, shule, taifa katika kuzuia au kusababisha mtoto atumie au asitumie dawa za kulevya? Maana kinga ni bora kuliko tiba.

Wale wazazi wenye watoto ambao hawatumii dawa za kulevya naomba elimu/mbinu (kama ipo) ya jinsi ya kuwafanya watoto wangu wasipende kutumia madawa ya kulevya.
 
Hao watoto wako wameshaanza kutumia dawa za kulevya!? Wanaumri gani na wanatumia dawa gani?
 
mlezi wa mtoto ni Mungu...pekeee!!
omba sana shirikisha Mungu kwenye kila kitu!

Wapo watoto wana tabia njem ila wametoka kwenye walezi wabovu vibaya mnoo...

wapo waliotoka kwenye malezi mazuri baba, mama wachamungu Ila watoto hovyooo kabisa...

yote kwa yote umaskini ndo chanzo kikuu cha hizo mambo!
 
Kuwa karibu na wanao waeleze ukweli wafanye kuwa rafiki kwako mana itakuwa ni rahisi sana jua mienendo yake, pia watoto hujifunza toka kwa wazazi kama wewe ni mlevi uwezekano wa WAo kuwa walevi ni mkubwa pia vile vile kama ni mvuta sigara

Mimi nimekuwa kwenye jamii ambavyo inawalevi na wavuta bangi haswaa lakini sikuwahi hata onja hata siku moja mana kwenye familia yangu tangu niwe mtoto sijawahi ona MTU akivuta sigara

Shule ndo huchangia sana haribu watoto especially boarding schools

Huko mi ndo niliona ulevi wa kila rangi lakini namshukuru mungu sikuwahi hata fikiria jaribu radha na hivo vitu
 
mlezi wa mtoto ni Mungu...pekeee!!
omba sana shirikisha Mungu kwenye kila kitu!

Wapo watoto wana tabia njem ila wametoka kwenye walezi wabovu vibaya mnoo...

wapo waliotoka kwenye malezi mazuri baba, mama wachamungu Ila watoto hovyooo kabisa...

yote kwa yote umaskini ndo chanzo kikuu cha hizo mambo!
umaskini!!! mbona yuko mtoto wa profesa mmoja anatumia?
 
Watoto wadogo hivyo ushaanza kuwawazia mabaya hata muda wa balehe bado
16464440_234060670397386_8213001068032819200_n.jpg
sana,wewe mzazi wa aina gani
Hawajaanza bado ni wadogo miaka 5 - 10
 
Watoto wadogo hivyo ushaanza kuwawazia mabaya hata muda wa balehe badoView attachment 472472 sana,wewe mzazi wa aina gani
nikikosea sasa nitakosea hata baadae na kesho pia. Sasa hivi ni wakati wangu wa kudunduliza elimu kwaajili ya akiba kwa matumizi ya baadae watakapofikia balele unayosema wewe.
 
Nimekaa na marafiki wavutaji bangi tena maskani moja lakini tokea nizaliwa mpaka hivi sasa siijui bangi wala pombe

Mwanao akili yake tu je ni mtu wa kufuatisha mkumbo ,na hata ukimlinda ni consciousness yake tu..nimesoma o level na msichana ambaye alikuwa analindwa sana na baba yake lakini alikuwa kicheche balaa

Mpe counseling na awe anajitambua 99% wamejiingiza kwenye madawa sababu ya peer pressure ,marafiki na mkumbo tu

Mbinu pekee kijana wako ajitambue ,je marafiki zake wakiwa wanavuta wakampitishia kipisi atakata na akikataa ataonekana mshamba na bwege,atavuta asionekane mshamba??

Awareness tu ndio njia pekee
 
"MLEE MTOTO KATIKA NJIA IMPASAYO NAYE HATAIACHA HATA AKIWA MZEE" read the BIBLE
 
Kuwa karibu na wanao waeleze ukweli wafanye kuwa rafiki kwako mana itakuwa ni rahisi sana jua mienendo yake, pia watoto hujifunza toka kwa wazazi kama wewe ni mlevi uwezekano wa WAo kuwa walevi ni mkubwa pia vile vile kama ni mvuta sigara

Mimi nimekuwa kwenye jamii ambavyo inawalevi na wavuta bangi haswaa lakini sikuwahi hata onja hata siku moja mana kwenye familia yangu tangu niwe mtoto sijawahi ona MTU akivuta sigara

Shule ndo huchangia sana haribu watoto especially boarding schools

Huko mi ndo niliona ulevi wa kila rangi lakini namshukuru mungu sikuwahi hata fikiria jaribu radha na hivo vitu
Ni kweli mkuu.. Tengeneza urafiki na watoto wako... Wafanye kama washikaji zako.. Some tym jifanye kuwaomba hata ushauri wa kimawazo kutoka kwao.. Watoto watatulia tuli hawachomokiiiii
 
Akili ya mtoto haichungwi na mzazi bali inaongozwa kwa utaratibu maalum. Ni watoto wangapi geti kali lakini matendo yao hayaendan na ulinzi walionao,ni wangapi wamelelewa kwa misingi ya dini lakin akili zikawatuma vingine.

Wanao pia ni binadamu,wana rithi tabia kama ulikua nazo za kufuata mkumbo wa marafiki basi lazima uwe na wasi wasi.
nikikosea sasa nitakosea hata baadae na kesho pia. Sasa hivi ni wakati wangu wa kudunduliza elimu kwaajili ya akiba kwa matumizi ya baadae watakapofikia balele unayosema wewe.
 
Ni sawa na kuomba ushauri watoto wako wasijekuwa wazinzi, wakati misambwata imejaa mitaani.


Ndukiiiii
 
ukitambua jinsi ya kuwafanya wanao wajitambue na wawe na hofu ya Mungu, ndio jinsi yakuwafanya wasije tumia mihadarati
 
Dunia kwa sasa ipo kwenye.kiganja. kuwa karibu na watoto wako kuwa malezi bora kuwashirikisha.mambo ya Imani yaani ibada na pia uwe rafiki badala ya kuutwa ufalme au ubaba. Zaidi sana kumtanguliza Mungu wako kuilinda.na kuingoza familia yako. Yaani hapa ndipo napochukia haya mabadiliko ya ulimwengu kwa mawazo yangu zamani mambo haya yalikuwepo lakini sio kwa kiwangl hiki
 
Back
Top Bottom