Nitarudi tena nchini Kenya

Nitarudi tena nchini Kenya

Basi unaweza kupata ticket Sirari upande wa Kenya, ni 1,000/= mpaka Nairobi nauli. Kutoka Sirari mpaka Nairobi siyo chini ya masaa 7.

Option ya pili ni kwenda mpaka Migori ukachukua Shuttle zile zinabeba abiria 16 tu na bei ni sawa. Faida ya shuttle ni kwamba zinaenda moja kwa moja kwasababu wanajaza abiria fasta na wanaenda na muda.

Kuna Galaxy ndiyo anipenda sana kutoka Migori wana magari yanatoka kila baada ya masaa matatu kwenda Nairobi. Ya mwisho inaondoka saa tatu usiku inafika Nairobi saa 10 alfajiri.
Mikoani Kenya ni kuzuri kuliko mikoani Tanzania?..
 
Pia sehemu ya maendeleo hayo uliyoyaona ni matokeo ya katiba mpya ambayo iliwapa serikali ya majimbo (County governments) kila county inajipangia na kutekeleza miradi yake ya maendeleo na mfumo ule umehakikisha kwamba kila mwaka bajeti ya serikali lazima itenge siyo chini ya asilimia 15 kwenda kwenye county, hii ni tofauti na makusanyo ya ndani ya county zenyewe hivyo hela inashuka mpaka .
Hapa tuone sasa umuhimu wa katibu mpya itakayo tuletea maendeleo si katika swala la uchaguzi tu. WAKA......
 
Hapa tuone sasa umuhimu wa katibu mpya itakayo tuletea maendeleo si katika swala la uchaguzi tu. WAKA......
Tz Bado Sana Mana tuko bize kwa propaganda na usubwada wa kuhamishahamisha mijadala ili kuwapumbaza Wadanganyika...tunahitaji muda Sana kuifikia Kenya socially, economically and politically.

Ny..
 
sirari-nairobi nafika mitaa ya mai mahiu alfajiri naanza kuhaha kutafuta sehemu ya kuswali, nawauliza wenyeji na kiswahili chao kibovu wakaniambia ahaa muskiti!? enda pale juu utapatana nayo.

nafika nakuta bonge la kanisa nikageuza gari, inaonekana kule kwenye ile county uislamu haujafika kabisa mbona nilitandika shuka la kimasai nikaswali sheli.
 
Kwa taarifa tu ndugu mleta mada unatakiwa utambue kwamba Wajaluo ni wapinzani na hawakuwahi kuwa na uhusiano mzuri na serikali mpaka mwaka 2018 baada ya Raila kujiapisha na mkoa wote wa Nyanza kugomea uchaguzi wa marudio 2017.

Hawakuruhusu vifyaa vya uchaguzi kuingia mkoani humo. Sasa hayo unayosema kuhusu ukosefu wa nyumba za nyasi kwa wajaluo ni suala la historia.

Nyumba za nyasi zikikuwepo sana tu sema kwasababu wajaluo ni watu wa misimamo mikali na hawajui kubembeleza waliamua liwalo na liwe toka enzi za Kenyatta alipomzingua aliyekuwa makamu wa kwanza wa Rais Jaramogi Oginga Odinga, baba yake Raila Amollo Odinga na Oburu Odinga. Wanasema (Jaluo oksechi) mjaluo habembelezi au Jaluo Jeuri.

Sasa kutokana tifu ilokuwepo kati ka Kenyatta na Oginga Odinga, mkoa wote wa Nyanza ulitengwa kimaendeleo sana. Wao kwa jeuri wakasema hamna shida, wakaamua kuwekeza kwenye elimu. Walisomesha watoto kama hawana akili nzuri ndo maana wajaluo wana jeuri sana, kuna kipindi bungeni wakati bado kulikuwa na uhasama kati ya Raila na Uhuru, walikuwa wanasema chama cha jubilee kina mtaji wa watu wengi ila ODM kina mtaji wa akili wakimaanisha wasomi.

Sasa baada ya watu kupata elimu, ikabidi ajira zipatikane, wajaluo wakaamua kuondoa Nyumba za nyasi. Wakaja na kitu kinaitwa semi-permanent, ukuta tope ila paa limepigwa bati. Siku hizi wanazipiga na plasta usipoangalia vizuri unaweza kudhani ni nyumba ya matofali kumbe semi-permanent.

Pili, ile barabara uliyoitumia kutoka Sirare mpaka sehemu inaitwa Kakrao kabla ya kuingia kwenye ukanda wa mashamba ya miwa Uriri, Awendo (kuna kiwanda cha sukari hapa kinaitwa South Nyanza Sugar Company -Sony) mpaka Rongo ilijengwa na serikali ya Tanzania ikiwa ni sehemu ya makubaliano katika jumuiya ya Afrika madhara mimi. Kampuni iliyoinjenga inaitwa Kojifa, hii barabara inatokea Tarime na inapitiliza mpaka Kakrao kama nilivyokwisha kusema.

Kipande kinachotoka Kakrao mpaka Kisii kimejengwa juzi tu hata hakina miaka mitano. Hii ni kama matokeo ya serikali ya umoja wa kitaifa iliyoundwa mwaka 2008 baada ya varangati la 2007. Raila akiwa waziri mkuu alihakikisha anajenga miundombinu Nyanza ndo maana ukiwa Kisumu, barabara ni kama za Dar, Raila ni engineer na alikuwa waziri wa ujenzi na barabara kipindi cha nyuma hivyo alihusika katika kupanga miundombinu ya barabara.

Pia sehemu ya maendeleo hayo uliyoyaona ni matokeo ya katiba mpya ambayo iliwapa serikali ya majimbo (County governments) kila county inajipangia na kutekeleza miradi yake ya maendeleo na mfumo ule umehakikisha kwamba kila mwaka bajeti ya serikali lazima itenge siyo chini ya asilimia 15 kwenda kwenye county, hii ni tofauti na makusanyo ya ndani ya county zenyewe hivyo hela inashuka mpaka chini.

Kuhusu wanawake, nakuachia.
Nakubaliana na wewe! Hiyo barabara FUNDER alikuwa mmoja na CONTRACTOR mmoja. Ila cha ajabu upande wa Kenya barabara ni pana sana na upande wa TZ barabara ni nyembamba. Hii maana yake ni kwamba TZ tulichukua 10%!
 
Kwa taarifa tu ndugu mleta mada unatakiwa utambue kwamba Wajaluo ni wapinzani na hawakuwahi kuwa na uhusiano mzuri na serikali mpaka mwaka 2018 baada ya Raila kujiapisha na mkoa wote wa Nyanza kugomea uchaguzi wa marudio 2017.

Hawakuruhusu vifyaa vya uchaguzi kuingia mkoani humo. Sasa hayo unayosema kuhusu ukosefu wa nyumba za nyasi kwa wajaluo ni suala la historia.

Nyumba za nyasi zikikuwepo sana tu sema kwasababu wajaluo ni watu wa misimamo mikali na hawajui kubembeleza waliamua liwalo na liwe toka enzi za Kenyatta alipomzingua aliyekuwa makamu wa kwanza wa Rais Jaramogi Oginga Odinga, baba yake Raila Amollo Odinga na Oburu Odinga. Wanasema (Jaluo oksechi) mjaluo habembelezi au Jaluo Jeuri.

Sasa kutokana tifu ilokuwepo kati ka Kenyatta na Oginga Odinga, mkoa wote wa Nyanza ulitengwa kimaendeleo sana. Wao kwa jeuri wakasema hamna shida, wakaamua kuwekeza kwenye elimu. Walisomesha watoto kama hawana akili nzuri ndo maana wajaluo wana jeuri sana, kuna kipindi bungeni wakati bado kulikuwa na uhasama kati ya Raila na Uhuru, walikuwa wanasema chama cha jubilee kina mtaji wa watu wengi ila ODM kina mtaji wa akili wakimaanisha wasomi.

Sasa baada ya watu kupata elimu, ikabidi ajira zipatikane, wajaluo wakaamua kuondoa Nyumba za nyasi. Wakaja na kitu kinaitwa semi-permanent, ukuta tope ila paa limepigwa bati. Siku hizi wanazipiga na plasta usipoangalia vizuri unaweza kudhani ni nyumba ya matofali kumbe semi-permanent.

Pili, ile barabara uliyoitumia kutoka Sirare mpaka sehemu inaitwa Kakrao kabla ya kuingia kwenye ukanda wa mashamba ya miwa Uriri, Awendo (kuna kiwanda cha sukari hapa kinaitwa South Nyanza Sugar Company -Sony) mpaka Rongo ilijengwa na serikali ya Tanzania ikiwa ni sehemu ya makubaliano katika jumuiya ya Afrika madhara mimi. Kampuni iliyoinjenga inaitwa Kojifa, hii barabara inatokea Tarime na inapitiliza mpaka Kakrao kama nilivyokwisha kusema.

Kipande kinachotoka Kakrao mpaka Kisii kimejengwa juzi tu hata hakina miaka mitano. Hii ni kama matokeo ya serikali ya umoja wa kitaifa iliyoundwa mwaka 2008 baada ya varangati la 2007. Raila akiwa waziri mkuu alihakikisha anajenga miundombinu Nyanza ndo maana ukiwa Kisumu, barabara ni kama za Dar, Raila ni engineer na alikuwa waziri wa ujenzi na barabara kipindi cha nyuma hivyo alihusika katika kupanga miundombinu ya barabara.

Pia sehemu ya maendeleo hayo uliyoyaona ni matokeo ya katiba mpya ambayo iliwapa serikali ya majimbo (County governments) kila county inajipangia na kutekeleza miradi yake ya maendeleo na mfumo ule umehakikisha kwamba kila mwaka bajeti ya serikali lazima itenge siyo chini ya asilimia 15 kwenda kwenye county, hii ni tofauti na makusanyo ya ndani ya county zenyewe hivyo hela inashuka mpaka chini.

Kuhusu wanawake, nakuachia.
Congratulations sana Mkuu!
Unaonekana unaijua sana Republic of Kenya, vip kuhusu biashara hasa ya Mahindi.Masoko yake yakoje?
 
Congratulations sana Mkuu!
Unaonekana unaijua sana Republic of Kenya, vip kuhusu biashara hasa ya Mahindi.Masoko yake yakoje?

Una mahindi? Mimi nipo kwenye mchakato wa kusajili kampuni Kenya itakayohusika na biashara ya nafaka kama una dili tutaongea
 
JF nadhani ilipata shambulio kidogo maana nilikuwa naandika naona inagoma
 
Basi unaweza kupata ticket Sirari upande wa Kenya, ni 1,000/= mpaka Nairobi nauli. Kutoka Sirari mpaka Nairobi siyo chini ya masaa 7.

Option ya pili ni kwenda mpaka Migori ukachukua Shuttle zile zinabeba abiria 16 tu na bei ni sawa. Faida ya shuttle ni kwamba zinaenda moja kwa moja kwasababu wanajaza abiria fasta na wanaenda na muda.

Kuna Galaxy ndiyo anipenda sana kutoka Migori wana magari yanatoka kila baada ya masaa matatu kwenda Nairobi. Ya mwisho inaondoka saa tatu usiku inafika Nairobi saa 10 alfajiri.
Nashukuru sana mkuu,je ofisi za uhamiaji kwa upande wa Tanzania kwa ajili ya kupata kibali cha kuvuka boda zipo wazi mpaka weekend?
 
Sasa huyi demu wa kimataifa umeipotezea story?
 
Nashukuru sana mkuu,je ofisi za uhamiaji kwa upande wa Tanzania kwa ajili ya kupata kibali cha kuvuka boda zipo wazi mpaka weekend?

Kama alivyoeleza mtoa mada, ukitaka kibali kile cha muda inabidi uende wilayani ambayo ipo Tarime, siyo Sirare watakurudisha Tarime.

Utahitaji nyaraka muhimu kama kitambulisho cha NIDA ili upewe hicho kibali.
 
Kenya hata nyumba za kupanga ni za hovyo sana yan chumba ukiweka tu kitanda mlango unafunguka robo kama una kitambi haupiti utalala nje
Nafkiri kwasababu ya uhaba wa ardhi
 
Kenya bhna 😋 mi niko kwa mpaka yao hapa Kilimanjaro
 
Back
Top Bottom