Nitapataje hati ya nyumba?

Nitapataje hati ya nyumba?

farajakwangu

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2015
Posts
1,942
Reaction score
701
Kiwanja hakijapimwa lakini nimeshajenga, nataka kuanza kushughulikia hati kwa kutumia kampuni binafsi. Nataka kujua inachukua muda gani kupata hiyo hati na ni hatua gani inapitia mpaka kukamilika zoezi zima.

Ukijaribu kuwauliza wenyewe (kampuni binafsi) mara nyingi wamekuwa waongo hawasemi ukweli kuhusu muda utakaochukua kupata hiyo hati, wao wanasema lipa kwanza tuanze mchakato baada ya hapo ndipo tutajua itachukua muda gani, kitu ambacho naona hawataki kusema ukweli ila wanataka ukishalipia wanaanza kusema ooh ramani imeenda Dar haijarudi.

Wakuu nawasilisha, kiwanja kipo BUKOBA mjini.
 
Zipo kampuni ila sasa hiyo bei. Kama maeneo yaliyopimwa yapo yapo karibu kwa ajili ya kuchukua reference afadhali kiasi.
Miaka kama miwili kampuni moja iliniambia million 2.5
 
Unapeleka application kwa kujaza form, kwenda katika halmashauri idara ya ardhi! Wao wanajua cha kufanya, watatoa surveyors, lakini kiufupi wao huzingatia ukubwa wa eneo ili gharama zipungue!

Lakini fika idara ya ardhi ya halmashauri yako, au muone mwanasheria aliye karibu yako akupe muongozo! Usiogope kumlipa elfu 30 ya consultation!
 
Kwa aliyeko dar na anataka huduma hiyo kwa bei rafiki kabisa na bila usumbufu ani pm namba yake.
 
Tafuta Mwanasheri,ni rahisi sana ukiwa na mwanasheria.
Ila pia faham kwamba huu mchakato ni wa muda mrefu.Kama wewe uliweza kukaa muda mrefu bila hati basi ujue pia upatikanaji wake lazima uchukue muda kiasi.
Hizi ni taratibu za kawaida,na kule mafaili kibaoooo.
Tafuta mwanasheri atakupa wepesi juu ya hili,lakini kama ukiingia kichwa kichwa utapewa hati mwisho wake inatambulika mtaa wa Kongo.Mjini Mipango
 
Andika barua ya maombi ya kupimiwa eneo lako kwenda kwa mkurugenzi wa manispaa/halimashauli husika lakini iwe na viambatanisho vya hati za mauziano,barua toka kwa mjumbe/barozi wa nyumba 10,mwenyekiti wa mtaa,afisa mtendaji kata...hapo utaZipeleka manispaa kitengo cha Ardhi wao watakupa savear ambae atakuja kupima Kama eneo lako lipo sehemu stahili au umejenga kwenye eneo la open spece,au barabara?kama liko poa watakupa gharama utalipa watakupa mawe mtaenda kuyaweka site baada ya hapo kiwanja chak
 
Kiwanja Chako kitasubiri namba ambayo ndio itakuwa imefungua file la ofer then hati...nikutakie kila la kheri
 
Back
Top Bottom