Nitapata wapi darasa la kujifunza kichina?

Nitapata wapi darasa la kujifunza kichina?

Drake

Senior Member
Joined
Dec 12, 2010
Posts
129
Reaction score
45
Habari wanajamii,
Natafuta mahali nipate kujifunza kichina, mtu anaye fahamu sehemu hiyo hapa dar anijuze
drake
 
Dah! Hata mimi napenda nijifunze hii lugha. Ukipata utaniambia.
 
hahahahahaha unanikumbusha mbali na siasa za kizushi za Tz hii lugha ilikuwa ikitumiwa na Mh Kitike alikuwa mgombea wa ubunge jimbo la Ubongo kwa tiketi ya Cuf 2000 ,baada ya fix kibaooo za kuomba kupewa KULA na kusema alisomea China utamckia akiongea kichina Nihomaa wafuac nao huitikia Nihoo
 
Tafuta marafiki wa kichina kwenye net watakusaidia japo kdogo mf: (kwadia=haraka) (sheshee=asante) (meyolaa=imeisha) (zai jian=kwaheri) baadhi ya maneno ya kichina
 
niliperuzi kwa haraka gazeti la mtanzania nikaona kitu kama hiki ila sikutilia maanani, sas naitafuta siipati,
washawasha: hayo maneno uliyotoa yana unganishwaje?

wana jamii,acheni utani dunia inaenda china, lazima ujianda kama wanauza maua kariakoo!kesho wako reception na marketing dept's kalia sit vizuri
 
Wasiliana na TANROADs watakuunganisha na makandarasi wa Kichina wanaojenga barabara zetu!
 
mikocheni karibia na shule ya east africa kuna shule utaona tangazo kuubwa linalosema "tunafundisha kichina". Ile barabara inayopita kiwanda cha cocacola na kutokea karibu na ofisi za clouds radio.
 
Tafuta marafiki wa kichina kwenye net watakusaidia japo kdogo mf: (kwadia=haraka) (sheshee=asante) (meyolaa=imeisha) (zai jian=kwaheri) baadhi ya maneno ya kichina

kuai yi dian=haraka, xie xie=asante, mei you=hakuna

Maneno hayo yameandikwa kwa Pinyin na sio chinese characters, pia kumbuka katika kutamka kuna tones mbalimbali na kila tone ina maana yake, kuna tone ya kwanza, ya pili , ya tatu na ya nne. So kwa maoni yangu kama unataka kujifunza ni vyema utafute shule kabisa inayofundisha kichina, kama ukitaka kufanya practice watu humu wapo kibao wanapiga kichina kile cha kufundishwa darasani, nakutakia mafanikio mema.
 
hahahahahaha unanikumbusha mbali na siasa za kizushi za Tz hii lugha ilikuwa ikitumiwa na Mh Kitike alikuwa mgombea wa ubunge jimbo la Ubongo kwa tiketi ya Cuf 2000 ,baada ya fix kibaooo za kuomba kupewa KULA na kusema alisomea China utamckia akiongea kichina Nihomaa wafuac nao huitikia Nihoo

Hii imeniacha hoi. Wabongo kucopy na kupaste wamo
 
Jamani natafuta mwalim wa kunifundisha lugha ya kichina au sehem wanayofundisha kichina jijini Arusha. Natanguliza shukurani

Cogito ergo sum
 
Ndugu wana JF naombeni mwenye kufahamu mahali ambapo kuna chuo au mwalimu ambae ataniwezesha kuongea vizuri,au kuongea fasaha Lugha ya Wachina,naomba hivyo nikiwa na maana mbili,MOJA....uchumi wao unakuwa kwa kasi sana kias kwamba miaka kumi ijayo yawezekana wakateka soko la kila kitu Dunian,na wao hawapo tayari kujifunza kingereza kwani wanasema siyo Lugha ya kibiashara,MBILI....kila nikutanapo na mchina kwenye Dili mala nyingi nakosa kaz au Dili kwa kutojua au kufahamu Lugha yap,pls mwenye msaada aliepo ndani ya JF naomba msaada juu ya hilo....!!
 
Udom wanafundish kichina.....yu just apply there,tena ujachelewa ndo wakati huu
 
Nashukuru mkuu Young warlock,mi ni mtumishi wa Shirika moja hapa Dar,uwepo wa Darasa UDOM ni mbali kwangu,natafuta kwa Dar es salaam....
 
nashukuru mkuu young warlock,mi ni mtumishi wa shirika moja hapa dar,uwepo wa darasa udom ni mbali kwangu,natafuta kwa dar es salaam....

Udsm ipo. Pia unaweza kujifunza mwenyewe kutumia DVDs za kufundishia lugha mbalimbali za dunia ambazo hubadilika tafsiri kadiri utakavyo. So ya Kichina unaweza kui- sett ikufunze kwa kizungu ama kiswahili.
Sijajua kama Tz zimefika but unaweza kuagiza toka Dubai.
 
Tunaulizia sehemu ya kusoma part time bila kuathiri majukumu ya kazi mfano hao wamachinga wa kichina waliojaa mitaani hakuna baadhi yao wenye tuition mitaani ili tukajifunze ? sasa mnatuambia UDOM na UDSM si unaanza ten a utaratibu wa kuaply mara maTCU NA MAMBO KADHA WA KADHA? Tuna hitaji zile za mitaani ili tunifunze kidogo kidogo NYI HAU MA?
 
Nenda UDSM ulizia taasisi ya Confucious, wanafundisha Kichina wale...
 
Umepata demu mchina nini?
+255 719 011 980
Piga hio namba utapewa maelekezo ya evening studies hapa hapa dsm posta
 
hodi, bwana Nyang
mimi ni msichana nchi ya uchina. ninajifunza kiswahili. nimejifunza kwa muda wa miezi sita hivi. labda tutaweza kusaidiana kwa kusoma lugha.
 
Back
Top Bottom