AdvocateFi
JF-Expert Member
- Jan 15, 2012
- 11,492
- 5,050
Kichefuchefu................!
Pumbavu.........
Pumbavu.........
![]()
huyu dada ana ujasiri mkubwa. jinsi alivyohutubia jana pale dodoma, inaonesha uwezo wake ni mkubwa. anasema chdm kuna mfumo dume. tusimshambulie kwa kauli yake. tuifanyie kazi. hivi kweli katibu mkuu wa chdm dr slaa ni mbabe? katika gazeti la rai la leo amekiri kuwa ubabe anao kwa kiasi fulani. hamuoni kuwa anakubaliana na juliana?
juliana akipitishwa na ccm kugombea ubungo, anaweza kumtoa kamasi na kumgaragaza mnyika. la kufanya ni mnyika kujipanga vizuri. tusiwe na utamaduni wa kudharau watu. juliana anatisha awapo jukwaani
![]()
hoja ya kwamba juliana alikua amefukuzwa chdm haina mashiko. hata dr slaa alikua mbunge wa ccm. alipo angushwa kwenye kura ya maoni ndiyo akakimbilia chadema. kuna watu hawajui historia ya slaa. vijana wengi wanadhani alianzia chdm.
Huyu binti kumbe havijui vijizehe vya Magamba!!
Si mnaona wenyewe alivyozongwa na hivi vizee vya CCM! Check alivyojiegemeza kwa kijibabu Kikwete?Hivi unafikiri vijizee vya Magamba vitamuacha salama kweli??? Lazima aliwe uroda tu atake asitake.
Afanya mchezo nini,thubutu yake!!!
Juliana Shonza aliyetimuliwa CHADEMA na kujiunga na CCM jana amelalamikia CHADEMA kuwa kuna mfumo dume na kwamba hakuna mwingine anayetoa kauli zaidi ya viongozi wa juu wa chama hicho.
Shonza alitumia fursa hiyo kumtumia salamu Mbunge wa Ubungo John Mnyika (CHADEMA) na kumtaka ajiandae kwa mapambano katika uchaguzi wa mwaka 2015.Shonza amesema mjini Dodoma kwamba mwaka huo ndiyo utaamua kati yake na Mnyika ni nani zaidi Ubungo
Akihojiwa na gazeti la Mwananchi Mbunge wa Ubungo John Mnyika amemtaka Shonza amuombe Mungu kwanza ili apitishwe na CCM kugombea na mengine yatafuatia.
Source:Tanzania Daima/Mwananchi.
Hakuna kilichofanyika kwenye jimbo la Ubungo zaidi ya kumuona mbunge wetu Mnyika akiruka sarakasi zake bungeni ambazo hazitusaidii chochote sisi wananchi.
Juliana Shonza atapata ubunge bila ya wasiwasi.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
huyu ni Rais wa Nchi! onesha heshima we dogo!
- una maana hawa wazee watafanya kama alivyo fanya mzee slaa kwa rose kamili na josephine mke wa mtu?
- una maana hawa wazee watampa juliana cheo kama mzee slaa alivyompa cheo rose kamili. rose ni mbunge viti maalum chdm. inasemekana alipewa ubunge ili aachane na mambo ya kuingilia mahusiano ya slaa na josephine.
chezea mzee slaa wewe!!!!!!!!! mzee ana uchu!!!
Utakuwa mnafiki kama hutoeleza sifa alizonazo j.shonza dhidi ya j.mnyika hususan katika masuala ya jimbo la ubungo, ni kitu gani au uwezo gani alionao shonza dhidi ya mnyika ili kufanya apewe kura na wanaubungo? kwa taarifa yako mnyika ni zaidi ya mbunge wa ubungo, hoja na maoni ayatoayo bungeni kwa asilimia kubwa ni za kitaifa zaidi kuliko za kijimbo jimbo, yeye ni mzalendo mjenga taifa!hivi kila mbunge akisimama bungeni awe anadai maslahi ya jimbo lake tu, je ni nani atatetea yale ambayo ni maslahi ya taifa kwa ujumla? mathalani ikiwa bei ya mchele ni nafuu sana jimboni kwa mbunge fulani wakati sehemu nyingine ni bei ghali sana unataka mbunge akae kimya kisa kwake ni bei rahisi, vipi kuhusu masuala ya rushwa, ufisadi, uzembe, kutowajibika n.k ndani ya serikali, je hayo ni masuala ya mbunge wa jimbo gani?
Kweli. Nikiona wanawake na watoto wanavyohangaika kutafuta maji. Badala ya kutoa solution anahamasisha nguvu ya umma ndio ishindikize tupate maji. Huku hatuna maji tuache kutafuta maji twende maandamano. Tukirudi na jasho maji hakuna vilevile na virungu tumepata. Kwa hili kaka Jimbo la Ubungo halina mwenyewe 2015Hakuna kilichofanyika kwenye jimbo la Ubungo zaidi ya kumuona mbunge wetu Mnyika akiruka sarakasi zake bungeni ambazo hazitusaidii chochote sisi wananchi.
Juliana Shonza atapata ubunge bila ya wasiwasi.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums