Kauli hii imetolewa na JK mjini Kigoma wakati wa sherehe za miaka 36 ya CCM...." nitahakikisha nina kabidhi nchi kwa mgombea wa CCM na si vinginevyo"!
KAMA RAIS WA NCHI, SALAAM HIZI MAANA YAKE NINI?!!
Duh, lakini kwa kuwa alikuwa kwenye sherehe za CCM, anastahili kuongea hayo. Angeongea kama Rais wa nchi ingekuwa taabu kidogo kumuelewa
Hivi bwana swai una ndoto za chadema kushinda urais?? Kuwa mkweli huwezi kutegemea ukoo mmoja usambae nchi nzima na kupewa nchi. Kighoma wameshasema hawachezi tena midundiko ya wapinzani wanataka uongozi si kupewa viroba orijino kurushia watu mawe
Ndio Slaa anataka hivyo lakini watanzania wameshatambua hilo, 2015 mkipata wabunge watano mshukuru mungu.Maana yake tutegemee mauaji na amani kutoweka tanzania mwaka 2015. Ccm ni janga kwa taifa letu!!
Hapo zamani za kale mnamo mwaka 1995 niliamini kua huyu mtanzania ana uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko nchini.
Nililaani sana kitendo cha mwalimu kuliengua jina lake katika kinyang'anyiro cha kuelekea kushika hatamu.
Ni takribani miaka 18 imepita ndipo nimeanza kujua maana ya mwalimu kwa ule mwaka 1995.
Sasa nimeamini hapa duniani tuna chui waliojivika ngozi ya kondoo, pia, majuto ni mjukuu.