Nitaka nianze mchakato wa talaka!

Kuna sababu nyingine za ugomvi huwezi mwanaume kujishusha maana ni hatari kwa maisha yako mpk ujue mwenzio Mungu amemkomboa sio kujishusha shusha tu utakufa mapema
Kama mke hataki kushuka,jifanye mjinga siku iishe utakuwa mjinga siku moja lakini utakuwa na furaha daima,Mungu hapendi kuachana

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimemsuspect tu kama ana relationship Nje. Ameshindwa kujitetea kawa mbogo anaomba tutengane nikaamua kuishi mbali nae. Lkn bado sijafika mahakamani. Kifamilia tumekaa hataki ndoa hivyo ndo nafikiria huyu Mungu atanihukumu vipi nikienda mahakamani?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa umri wako,kuacha mke,kupoteza mali,na watoto kutangatanga ni kukaribisha umasikini na mateso makubwa ya maisha yako huko mbeleni;ninachoweza kukushauri kama bado una nguvu ya ujenzi,tafuta mkoa uliotulia kama Arusha,jenga nyumba yako na usisikilize ushauri wa mkeo,baada ya hapo amia na kama bado unampenda mwenzi wako unaweza kumuita,akikataa unaweza kuwa na mchepuko unaojitambua huku maisha yakisogea.Huku ukiendelea kumiliki mali zako na watoto ukiendelea kuwasomesha.Na mwisho wa siku bi mkubwa atakufuata mwenyewe na kukuomba msamaha.Kukaa mazingira ya aina moja muda mrefu yanaweza kuharibu uhusiano.
 
Nini chanzo hasa? hebu eleza vizuri ili tukushauri vyema Mkuu!
 
Mlishakaa mkazungumza kuhusu tatizo lenu? Je mlishirikisha familia na viongozi wa dini ikashindikana?

Talaka inatolewa pale mke na mume watakapotengana zaidi ya miaka miwili pasipo suluhu kupatikana

Kumaliza mwaka mmoja ktk kutengana kwenu hakumaanishi kuwa talaka itakubaliwa manake mke ametengana na wewe au mume ametengana na mke ili hasira zitulie kwanza. Hiyo kisheria inakubalika.

Talaka siyo nzuri, hata mahakama hawakubali kirahisi, labda iwe na sababu zenye mashiko kama mume au mke kufungwa gerezani kwa muda mrefu, maradhi yasiyotibika( cancer) unyanyasaji wa kijinsia, ukichaa baina ya wanandoa.
Jaribu kuongea na mwenza wako tena kabla hamjafikia huko kupeana talaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana kwa changamoto hiyo Boss,,lakin pia kuw makin nae sana huyu mwanamke,,kuna hali ya hatarii ,,kuhusu kuachana kwakweli mm bado sijaona sababu ya msingi ya kufanya mpeane talaka
unasema kuw umehisi anamahusiano nje bt huna ushahidi kamili maana hujamfumania akiwa na mwanaume

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaka nashukuru Kwa ushauri wako. Ukweli kifamilia tumefika msimamo wake kutengana. Kwa Paroko hataki kabisa otherwise Mimi nikareport. Hiyo kwangu ngumu maana naona kama nitakuwa nalazimisha relationship. Ngoja niendelee kuvuta muda miaka 2 sio mbali.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo ya kanisa la ufufuo, Mashahidi wa Yehova, TAG, KKT, Moravian,RC au Kiislam? Hebu tueleze tatizo haswa linalofanya msilewane ni nn?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sishauri sana mpeane talaka, jaribu tena kwenda ofisi za ustawi wa jamii zilizo karibu yako nadhani suluhu itapatikana. Mtapewa marital counseling

Jaribu kujishusha kidogo ndoa ni changamoto mfano mume na mke wakiwa juu sana hamtasikilizana.

Madhara ya kutengana ni makubwa sana watoto watateseka na kukosa malezi ya wazazi wote , pia ni chukizo kwa Mungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yeye ndio aliyeomba mtengane ila wewe ukaona uishi mbali. Nadhani hapa wewe pia unakua umefanya maamuzi. Yeye aliyetaka mtengane angechukua hatua kuhusu huo utengano mpaka ambalo angekua tayari kwa hatua nyingine nikimaanisha kuachana kabisa au kurudiana.

Namaanisha una maamuzi tayari ila unatafuta justification.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa ndo umeondoka na mali zote umemwachia?

Kama inawezekana kaeni kifamilia, gawaneni mali pasu, halafu mwache aendelee na maisha. Usitoe talaka kwanza.

Akiishiwa atarudi, utaangalia status kama kumpokea au la. Lakini husisheni wanasheria kwenye kugawana hizo mali.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…