Shida kubwa ni kuwa anaogopa kueleza ukweli lakini binafsi namuonea huruma sana na hasa baada ya kukutana na wengine kama yeye na kuongea nao.SI JAMBO JEPESI hasa kwa kijana mdogo.Huyu mwanzoni alikuwa anatueleza jinsi baba yake alivyoitwa kwa DSO na dhahama nyingine nyingi lakini hatujui alikumbwa na nini mpaka akageuka wenziwe.Kuna mambo mawili makubwa ambayo naaamini yalimkuta,VITISHO na AHADI KUBWA.
Alikuwa njia panda,aamue kueleza yote kwa umma na akose yote au aunge mkono angalau aambulie kidogo,hakika ni njia panda.
Bado ni kijana na kuna nafasi ya toba katika maisha naamini kuna siku atatueleza na tutamuelewa na inawezekana tukamhurumia.Kila la heri Elia.