Omokora Nyangi
Member
- Apr 5, 2012
- 58
- 66
Ndg Wanajamii-Forum,
Mimi ni mdau wa masuala mbalimbali ya kimaendeleo na kwa sasa naishi Serengeti. Kwa miaka 6 sasa nimekuwa nafanya utafiti kubaini fursa anuai ambazo zinapatikana ktk jimbo letu la Serengeti lakini ambazo CCM na serikali yake wameshindwa kuzitumia kwa makusudi.
Hali hii imeendelea kusababisha maisha ya watanzania wa Serengeti kuwa duni katika maeneo yote, yaani; Barabara, Maji, Afya na kubwa zaidi ELIMU.
Mwaka 2010 nilitaka kuingia kwenye kinyang'anyiro hiki lakini nilirudi nyuma kwa sababu sikuwa nimefanya utafiti wa kina ili kujiridhisha kwamba CHADEMA inaibwaga CCM vibaya ktk uchaguzi huo.
Lakini tangu hapo, nimezunguka kwenye kata 29 za Wilaya ya Serengeti na kubaini mambo mengi ya msingi. Nailaumu CCM na serikali yake kwa mambo manne makubwa ya msingi ambayo nitayaleta humu jamvin baadaye na hatimaye nitayaweka kwenye makala yangu kupitia Raia Mwema siku chache zijazo.
Kwa ufupi, mimi ni mwana Serengeti na tayari nishaanza kutengeneza mtego na mtandao makini ambao utaitafuna CCM na serikali yake pamoja na vibaraka wake ambao wametanguliza matumbo yao mbele na kuuweka mustakabali wa jimbo letu tajiri na mustakabali wa taifa letu, "REHANI! NATANGAZA NIA"!!,
Nilihitimu Serengeti Sekondari miaka 19 iliyopita, nikaendelea na masomo IDM MZUMBE na kwingineko.
Nina msimamo usio badilika ktk mambo ya msingi, ni mfuatiliaji na mshiriki kwenye mijadala mbalimbali lakini zaidi, mimi ni miongoni mwa watanzania tunao amini katu, pasipo kuiondoa CCM madarakani..... maisha ya watanzania hususani wana serengeti, yataendelea kuwa hivi hivi, na wao CCM watabaki kuwa na uwezo na ulafi huo huo ilhali raslmali zetu zikiendelea kutafunwa na watu hawa hawa wa CCM na kuwanufaisha wao marafiki zao na watoto wao!
Mimi ni mdau wa masuala mbalimbali ya kimaendeleo na kwa sasa naishi Serengeti. Kwa miaka 6 sasa nimekuwa nafanya utafiti kubaini fursa anuai ambazo zinapatikana ktk jimbo letu la Serengeti lakini ambazo CCM na serikali yake wameshindwa kuzitumia kwa makusudi.
Hali hii imeendelea kusababisha maisha ya watanzania wa Serengeti kuwa duni katika maeneo yote, yaani; Barabara, Maji, Afya na kubwa zaidi ELIMU.
Mwaka 2010 nilitaka kuingia kwenye kinyang'anyiro hiki lakini nilirudi nyuma kwa sababu sikuwa nimefanya utafiti wa kina ili kujiridhisha kwamba CHADEMA inaibwaga CCM vibaya ktk uchaguzi huo.
Lakini tangu hapo, nimezunguka kwenye kata 29 za Wilaya ya Serengeti na kubaini mambo mengi ya msingi. Nailaumu CCM na serikali yake kwa mambo manne makubwa ya msingi ambayo nitayaleta humu jamvin baadaye na hatimaye nitayaweka kwenye makala yangu kupitia Raia Mwema siku chache zijazo.
Kwa ufupi, mimi ni mwana Serengeti na tayari nishaanza kutengeneza mtego na mtandao makini ambao utaitafuna CCM na serikali yake pamoja na vibaraka wake ambao wametanguliza matumbo yao mbele na kuuweka mustakabali wa jimbo letu tajiri na mustakabali wa taifa letu, "REHANI! NATANGAZA NIA"!!,
Nilihitimu Serengeti Sekondari miaka 19 iliyopita, nikaendelea na masomo IDM MZUMBE na kwingineko.
Nina msimamo usio badilika ktk mambo ya msingi, ni mfuatiliaji na mshiriki kwenye mijadala mbalimbali lakini zaidi, mimi ni miongoni mwa watanzania tunao amini katu, pasipo kuiondoa CCM madarakani..... maisha ya watanzania hususani wana serengeti, yataendelea kuwa hivi hivi, na wao CCM watabaki kuwa na uwezo na ulafi huo huo ilhali raslmali zetu zikiendelea kutafunwa na watu hawa hawa wa CCM na kuwanufaisha wao marafiki zao na watoto wao!