Watu mko Dar mnaota Ndoto za Mchana, CC tunakomaa na M4C na michango yetu ya Ujenzi wa Chama huko Serengeti inajulikana na Record ziko Makao makuu, Kwa systeam ya sasa ya CHADEMA ili upate nafasi ya Kugombea ni lazima uwe na Record ya aina yake katika Kujenga Chama kupiga M4C na kujitolea kwa hali na mali, na si kukaa Mjini na kuota Ubunge, utausikia endapo hutakomaa kujenga Chama
Kwa sasa mambo mengine yatawekwa pembeni, Kama hushiriki kujenga Chama acha kujisumbua mkuu make utafyekwa wilayani, wanao Tangaza Nia kwa sasa wako Vijijini wanapiga M4C watu wanalaa kwenye mahema, wana tembea kwa Baiskeli, Pikipiki na hata Punda Ilimuradi kutoa elimu, sasa wengine wako Mjini wanakula AC and then wanaota Ubunge, Mkuu bila kupambana watu wakuone na Chama kikuone utakuwa unajidanganya Bure, kwa CHADEMA kwa sasa hakuna hilo bali ni juhudi pekee, wewe unazania wakina MAWAZO huko Kanda ya Ziwa wanacheza?