Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama “HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA” katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za “The Dar es salaam School of thought” kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!

Hata mimi nimepata aibu sana huwa ninawafundisha wanafunzi wangu kuwa yule "Karl Peter" kwa jina lengine tunamuitaga "mkono wa damu" kutokana na ukatili wake.
 
Waarabu hawakuleta utumwa, walikuja kununuwa watumwa, babu zako wale waliokuwa kidogo wajanja, walikuwa wanawakamata babu zako wale waliokuwa dhaifu na wanawauza kwa vioo na shanga, kumbuka hilo.
Nakumbuka ndio walioleta kile kitabu cha mud
 
Tena licha ya Ikulu, Mjerumani kafanya kweli, reli ya kati mpaka leo.

Barabara karibu zote unazotumia leo ni zile zile za Mjerumani, sanasana tumezipanuwa na kuweka lami.

Nenda Tanga, moja katika miji ambayo imepangika vizuri na hiyo ni toka Mjerumani, si leo.

Ukweli ubaki kuwa ukweli. Natamani tungebaki kutawaliwa na Wajerumani hadi leo hii. Hatuwezi lolote.
Mkuu hizo sentensi mbili za mwisho ni za kwako kweli? Yaani hatuwezi kujitawala?
 
Tusiumize vichwa,hapa ni Mkoloni mweusi anamsifia mkoloni mzungu

Nia ya Mwalimu ilikuwa njema na laiti hawa waliomfuata wangeishi katika falsafa zake...ni mtu aliyezaliwa nje ya historia tu atakayebisha hili! Hapakuwa na sababu ya kuomba,ni kuamrisha tu upate mrejesho wako kutokana na rasilimali zenu kumnufaisha mhusika! Angetakiwa amtembeze kwenye zile familia na kanda zilizoadhirika zaidi na biashara ya utumwa ili nao wapate uchungu(kama wana hisia)
 
Tena licha ya Ikulu, Mjerumani kafanya kweli, reli ya kati mpaka leo.

Barabara karibu zote unazotumia leo ni zile zile za Mjerumani, sanasana tumezipanuwa na kuweka lami.

Nenda Tanga, moja katika miji ambayo imepangika vizuri na hiyo ni toka Mjerumani, si leo.

Ukweli ubaki kuwa ukweli. Natamani tungebaki kutawaliwa na Wajerumani hadi leo hii. Hatuwezi lolote.

I hope mkienda h*ja huwa mnawashukuru waarabu kwa kuwauza utumwani.
 
Faiza nadhani mababu zetu waliotangilia mbele ya haki wangeisikia kauli hii wangekuchuna ngozi,sema wewe na serikali yako ndo hamuwezi lolote hivyo basi wapisheni wanaoweza kazi hapo magogoni msaidiwe maana imeshawashinda!!!!Kwamba unasifia ukoloni kwamba wametujengea barabara na kutupangia mji wa Tanga hii mishahara mnaowalipa TOWN PLANNERS ni za nini???? haya mabilioni mnayoyatafuna hapo BOT yangetosha kujenga barabara ngapi zetu kama watanzania???Unyama uliofanya na kila TOM VON PRINCE na wengineo unausifia,historia tunaijua nashauri mkawadanganye huko vijijini wasiojua historia ya unyama wa wajerumani

Hii ndio sababu serikali ya ccm huwaabudu hawa wenye ngozi nyeupe ('wadhungu'). Sijasoma kwenye historia kama tuliwahi kuwa na chief wa kikwere
 
Mr.Kikwete amelitia taifa aibu ya mwaka.
jamani huu ukilaza wa ccm kumbe unaanzia kwenye level ya mwenyekiti wao?
....Hao CCM ukilaza wao ni wa muda mrefu sana, hawakukutana nao barabarani!!.

Hapo ndo tutajuuta kuwa na viongozi mbumbumbu wanaosifia ukoloni wakati nchi za kikoloni wenyewe mara nyingi wanaomba radhi kwa unyanyasaji na mambo yasiyofaa waliyowafanyia Waafrika na hawapendi kukumbukia lakini Proffesore anafurahia lol!!!
 
Acha uongo, jengo la ikulu ya Dar halikujengwa na Wajerumani, ni Waingereza. Hata ikulu ya Zanzibar walijenga Waingereza. Wakati walikuwa na system ikiitwa BOMA (British Overseas Management and Administration). Ilikuwa baada ya Wajerumani kuondoka

Kwa hiyo hata JK hakuwa analijua hili, including FF
 
Mkuu hizo sentensi mbili za mwisho ni za kwako kweli? Yaani hatuwezi kujitawala?

Amesahau hostoria huyo kuea wajerumani waliondoka baada ya kushindwa vita zote mbili na mwingereza sasa wangeendeleaje kuwa watawala wetu na huku uhuru tumeupata kws wsingeteza?.

Turudie historia tafadhali.
 
Bravo! Na alishindwa kumwambia huyo Mzungu kuwa sehemu ya maendeleo yao inatokana na rasilimali wailizpora huku kwetu. Na wanao wajibu - na sio ombi,- wa kuturejeshea ili waondokane na lawama ya milele

Kweli wakenya huonekana wako vizuri kuliko waTZ, maana wazee wa Kenya walidai mrejesho wa upolaji wa wakoloni. Sisi tunasifia, kweli hizi ni pumba
 
Wakoloni waliwakuta mababu zote juu ya miti......wanaishi maisha ya kinyani pamoja na manyani,

Walitustaarabisha na kutupa elimu angalau tuonekane na sisi watu duniani. Na ndio maana mpaka leo baadhi ya

wazungu wakimuona Muafrika wanamwita nyani, huo ndio ukweli !! Tusibishe wala kukasirika, sisi ni manyani!!

sisi ni manyani!! Sisi ni Manyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaani !!

Sawa nyani Komiri, mimi ni Mtanzania hata bila mkoloni tungechomoza tuu. Tungeweza kuchelewa, lakini tungechomoza zaidi yatulivyo sasa ambapo ccm imetuingiza kwenye ukoloni mamboleo. kumbuka Mungu aliye hai hana upendeleo.
 
Kinachonishangaza siku hizi ni kila analofanya, analosema Rais wetu lazima tumkosoe, tumkejeli, tumdhalilishe,..., sijui huu ndio uzalendo mpya!

Wengine wanasema hata ule mkutano wa waandishi wa habari na mgeni wake alipaswa kuongea Kiswahili eti kwa kuwa mgeni wake aliongea Kijerumani!

Tukumbuke kuwa Rais wetu ni kioo na nembo maalum ya nchi yetu. Tunajitukana wenyewe kwa kumkejeli kila mara.
 
Kinachonishangaza siku hizi ni kila analofanya, analosema Rais wetu lazima tumkosoe, tumkejeli, tumdhalilishe,..., sijui huu ndio uzalendo mpya!

Wengine wanasema hata ule mkutano wa waandishi wa habari na mgeni wake alipaswa kuongea Kiswahili eti kwa kuwa mgeni wake aliongea Kijerumani!

Tukumbuke kuwa Rais wetu ni kioo na nembo maalum ya nchi yetu. Tunajitukana wenyewe kwa kumkejeli kila mara.

Kumpigia makofi mkoloni kwamba alitutawala vizuri ni sifa kwa taifa sio? Vioo vina sehemu ya kuwekwa!
 
Tena ninatamani aingie nao mkataba wa kuimarisha idara za serikali kama polisi. Kwamba Jeshi la polisi liwe chini ya serikali ya ujerumani kwa miaka kadhaa ili warudishe hadhi kama walioyoicha.

Na wewe ulikuwa unafundisha hayo kwa mtaala gani?

Lakini huwa unakumbuka kuwafundisha wanafunzi wako how ccm is under developing Tanzania?

Kushuka kwa elimu ya Tanzania ni sababu ya Wajerumani pia?

Kukithiri kwa matendo ya rusha na ufisadi napo ni ajili ya wajerumani?

Huduma mbovu za jamii, ukiukwaji mkubwa wa katiba na haki za binadamu nazo ni za wakoloni?

Matumizi mabaya ya raslimali za taifa na lack of accountability nayo ni wajerumani?

Ndiyo maana kuna shida kubwa sana kaika kuinua elimu ya Tanzania. Kumbe hata wizara ya elimu inatkiwa ibinafisishwe!.

Ninatamani sana kikwete aongee naye juu ya kubinafsisha jeshi la polisi na wizara ya elimu ili wajerumani wazichukue.
 
Hawa ma rais wawe wanapimea IQ kwanza ..kuna mambo wanaongea yanatoa kichefu chefu sana
 
Tena ninatamani aingie nao mkataba wa kuimarisha idara za serikali kama polisi. Kwamba Jeshi la polisi liwe chini ya serikali ya ujerumani kwa miaka kadhaa ili warudishe hadhi kama walioyoicha.

Na wewe ulikuwa unafundisha hayo kwa mtaala gani?

Lakini huwa unakumbuka kuwafundisha wanafunzi wako how ccm is under developing Tanzania?

Kushuka kwa elimu ya Tanzania ni sababu ya Wajerumani pia?

Kukithiri kwa matendo ya rusha na ufisadi napo ni ajili ya wajerumani?

Huduma mbovu za jamii, ukiukwaji mkubwa wa katiba na haki za binadamu nazo ni za wakoloni?

Matumizi mabaya ya raslimali za taifa na lack of accountability nayo ni wajerumani?

Ndiyo maana kuna shida kubwa sana kaika kuinua elimu ya Tanzania. Kumbe hata wizara ya elimu inatkiwa ibinafisishwe!.

Ninatamani sana kikwete aongee naye juu ya kubinafsisha jeshi la polisi na wizara ya elimu ili wajerumani wazichukue.

Mr. Prisident kama hana ID humu basi atakuwa anaingia kama mgeni,atasoma wazo lako na akiona linafaa atampelekea Rais mwenzie...ila akichelewa kumpelekea atapanda ndege amfuate!
 
Hatuwezi kuwashukuru wajerumani kwa kututawala kwa sababu
  • walitutawala kwa nguvu
  • walitupokonya ardhi
  • walitufanya manamba - forced labour
  • walituweka katika daraja la chini
    kwa hivo hata kama waliacha ikulu, barabara hata reli hii haitufanyi tuwasifu maana hawakutujengea bali walijijengea wao. Tunaweza kuwashukuru kwa misaada wanayotupa sasa au baada ya uhuru na si wakati wa utawala wao.
 
Back
Top Bottom