Nisamehe kama nakufuru, nahitaji kufahamishwa

officialBossmtoto

JF-Expert Member
Jul 1, 2019
369
1,178
Mimi ni Mkristo Mkatoliki na napenda sana dini yangu. Ila zaidi napenda sana kujifunza hasa pale ambapo panakua na ugumu ama mkanganyiko.
Narudia tena, nitaomba mnisamehe kama nakosea ila nina swali nahitaji kufahamishwa.

Tunaambiwa kwenye Biblia kwamba Mungu alimtuna Musa(Moses) akawakomboe wana wa Israel kutoka mikono ya Farao(Pharaoh) na akampa maelekezo namna ya kufanya ili Farao aweze kumuelewa. Lakini Mungu pia akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu asikubaliane na ujumbe wa Musa. Sasa swali langu ni kwamba, Je? Mungu alikua anatafuta sababu ya kumuangamiza Farao? Maana pengine asingefanya moyo wa Farao kua mgumu, pengine Farao angekubali tu kwamba sawa enendeni maana Mungu wenu amewataka muende nchi ya ahadi.

Tunaambiwa Mungu wetu anaruhusu Free Will yaani Ruksa ya kufanya maamuzi mwenyewe, je mbona aliingia maamuzi ya Farao? Mbona aliufanya moyo wa farao kuwa mgumu?
 
Mkuu,Swali zuri sana?Je nini maana ya FREE WILL?Je Unafikiri Free will inakupa uhuru wakwenda nje ya Mpango wa Mungu au kumzidi Mungu Ujanja?Je unafikiri Free will inakupa uwezo zaidi ya MUNGU?Tumtazame Farao na Musa sasa.Je unafikiri Musa na Farao walikuwa ndani au nje ya Mpango wa Mungu?Je unafikiri Matukio yaliyotokea wakati wa Musa na Farao yalisimuliwa kabla au baada?

Napenda ufahamu kwamba katika maandiko ya Biblia unayoyaona yalisimuliwa baada ya kutokea na sio kabla ya kutokea na kuna uwezekano kabisa kwamba mwandishi hakuwa Musa bali ni mtu mwingine kabisa.Kwa mantiki hio basi unaposoma maandiko haya lazima uongozwe na Roho wa Mungu ili uelewa hasa mantiki ya andiko.

Waisrael walikuwa watumwa Misri kama ambavyo Waafrika walitawaliwa na Wakoloni.Katika hali ya kawaida unajua kwamba katika harakati za kutafuta ukombozi wakoloni hawakukubali kirahisi vivyo hivyo Pharao hakukubali kirahisi.So ni kweli Mungu alimfanya awe na Moyo Mgumu ashindwe kuelewa kwamba anatakiwa awape hawa watu uhuru wao kwa sababu ya kupenda kuwanyonya.SO kwa ufupi kabisa NDIO MUNGU HURUHUSU TUWE NA MIOYO MIGUMU ILI TUONE UKUU WAKE NA HIO NI SEHEMU YA FREE WILL NA SIO INTERFERENCE YA MUNGU.

MAISHA NI MACHAGUO.

Ubarikiwe
 
Kwenye imani zetu hizi ili kuweza kumuelewa Mungu kupitia maandiko kisawasawa kuna umuhimu wa kusoma vizuri, kuelewa na kupata muda wa kutafakari.

Mimi ninavyoelewa ni kwamba Mungu aliufanya moyo wa Farao kuwa mgumu ili aendeleze ubishi kwa taifa la Israeli aishie kupewa mapigo kupitia Musa

Ni kama pale Mungu alipomwachia mnadhiri wake Samsoni kwenda kumuoa Delilah mfilisti huku akijua yatakayotokea mbeleni. Ukisoma biblia utaona kuna sehemu Samson aliambiwa asimuoe mfilisti yule Delilah, ila ukweli ni hawakujua kwamba "Wazazi wake hawakujua kwamba huo ulikuwa mpango wa Mwenyezi-Mungu ambaye alikuwa anatafuta kisa cha kuchukua hatua dhidi ya Wafilisti. Wakati huo, Wafilisti waliwatawala Waisraeli" Waamuzi 14:4

Hicho kidogo ndio mimi nnachokielewa officialBossmtoto ila pia sipendi sana hizi maada za imani sababu naamini mimi sijabobea
 
Uo moyo mgumu sio alipewa na Mungu sasa apo tumlaumu farao au aliye mpa moyo mgumu farao
Hili sio swala nani wa kumlaumu,Unawajibika na machaguo unayofanya ndio maana ya FREE WILL.You can take or do anything,But once taken it is taken.Ugumu uko wapi?Au hupendi kuwa na Free will?Je ni bora kwako usingekuwepo kabisa?
 
Mungu alifanya moyo wa kijana Farao ili ishara zake ziwe nyingi kwa wana wa Israel, ili wapate kumumini Mungu katika uwezo na ishara zake, kwasababu Mungu alijua ambayo watakuna nayo wana Israel huko mbeleni. Kwa zile ishara ilikuwa kuwahengea kujiamini kwamba wane Mungu, na ndio maana utaona kuna baadhi ya nchi ( jamii ) waliposikia jamaa wanapita walikuwa wakinyaa kwasababu walisikia yale ambayo Mungu aliwatenda wa Misri. Ila angepiga tukio moja tu, Israel kuamini kwao kulikuwa tia maji tia maji
 
Kwa hiyo farao hakuwa na kosa, ni kama Mungu alikuwa anamfanyia fitna farao ili yeye (Mungu) akubalike na Waisrael. Kwa lugha ya kisasa tunaita kiki.
Mungu hahitaji KIKI wala hafanyi FITNA unakosea sana kufikiri hivyo.MUNGU amekupa uhuru wa kuchagua na kuwajibika kwa machaguo yako na anajua kwamba una njia ya laana na njia ya BARAKA ni wewe uchague tu.
 
Hili sio swala nani wa kumlaumu,Unawajibika na machaguo unayofanya ndio maana ya FREE WILL.You can take or do anything,But once taken it is taken.Ugumu uko wapi?Au hupendi kuwa na Free will?Je ni bora kwako usingekuwepo kabisa?

It is not free will because he was driven to do so. Alilazimishwa kufanya vile. Kumbuka Mungu ndo aliutia ugumu moyo wa Farao sio matendo ya Musa.
 
Unawezaje kusema nina uhuru wakati Mungu anaweza kuamua niwe mbakaji ili nifungwe jela kwa manufaa ya watu anaowataka yeye?
Mungu kakuruhus wewe uwe mbakaji au usiwe mbakaji.Na ukiwa mbakaji unaweza ukafungwa jela au usifungwe jela.Ndio maana ya Free will,Uhuru usio na mipaka ila kila mtu anawajibika kwa matendo yake
 
Mungu alifanya moyo wa kijana Farao ili ishara zake ziwe nyingi kwa wana wa Israel, ili wapate kumumini Mungu katika uwezo na ishara zake, kwasababu Mungu alijua ambayo watakuna nayo wana Israel huko mbeleni. Kwa zile ishara ilikuwa kuwahengea kujiamini kwamba wane Mungu, na ndio maana utaona kuna baadhi ya nchi ( jamii ) waliposikia jamaa wanapita walikuwa wakinyaa kwasababu walisikia yale ambayo Mungu aliwatenda wa Misri. Ila angepiga tukio moja tu, Israel kuamini kwao kulikuwa tia maji tia maji

Hivo basi Why are we told that there is free will na wakati looking at it countless times imekua broken
 
Back
Top Bottom