Nisaidieni Waungwana!

Kalolo Junior

Member
Oct 20, 2011
81
27
Mwenzenu nimehamia Jijini Dar hivi karibuni baada ya kupata kibarua katika taasisi moja ya Serikali. Katika harakati za kutafuta makazi, nilibahatika kuunganishwa na mwenye nyumba ambaye pia ni mtumishi wa Taasisi niliyopo. Aliyeniunganisha na nyumba hii ni mtumishi mwenzangu ambaye tupo ofisi moja.
Nyumba niliyoipata ina sehemu za biashara kwa mbele na moja ya biashara hizo ni Kontena moja ambalo liliwekwa kwa ajili ya Grocery. wakati nahamia katika hii nyumba, hii grocery ilikuwa haifanyi kazi kwa kuwa aliyekuwa anaiendesha ni mwenye nyumba aliyehama. Kwa sasa Grocery inaendeshwa na yule mtumishi mwenzangu ambaye nafanya naye kazi ofisi moja.
Tatizo lililopo ni kwamba hii Grocery inavyoendeshwa imekuwa ni zaidi ya Bar kwa sababu ikifunguliwa mida ya saa 6 mchana unawashwa mziki mkubwa hadi itakapofungwa mida ya usiku mkubwa (saa 8 hadi 10). Hali hii imekuwa ikinikera na nashindwa nifanye nini maana kuhama nashindwa kwa kuwa nimelipa kodi ya mwaka na nimefanya ukarabati uliogharimu zaidi ya 1M.
Waungwana naombeni ushauri wa nini la kufanya!
 
ongea na huyoland loard wako in a gentle manner ukimwelezea concern yako juu ya hiyo hali. usikie eye atajibu nini tell the truth kuwa kelele zinakusumbua na uonyeshwe kukerwa nazo ila uwe makini san aisije ikawa unakereka lakini huo usiku wa saa 6 na wewe uko hapo bar unapata moja barid.

ikishindikana nenda kamwelze mtendaji wa kata ili apewe onyo ukion ahaitendeki nenda polis ukiwa na hiyo barua ya onyo as reference point. wengine watamalizia
 
Pole sana ndugu!Kuna kanisa moja limefunguliwa mitaa ninayoishi wakianza kupiga makelele wananikera sana!Hawa watu wanakera sana!
 
Pole sana mkuu, hili si tatizo lako peke yako watu wengi tunao kaa uswazi ndo shida kubwa. Ushauri wangu: hapo si kwako ni mpangaji tu ingekua kwako ndo ungefuata hizo taratibu kwenda kwa mtendaji au polisi, mtafute dalali yeye anaweza kuleta mtu mwingine mwenye kuyamdu hayo mazingira unampangisha unakata chako unatafuta nyumba kwingine.
 
jitahidi kopa bank nunua kiwanja jenga kakibanda ukae
mkataba wako unaweza tafuta mtu mwingine ukamkweka pale
as said ongea na landlord usikie atasemaje.
wakikaidi nenda mahakama ya jiji mwone kijumbe au Lwiza au Munga waeleze wao watafungua mshtaka
na mahakama itaweza kufunga hiyo grocery uishi kwa amani
 
jitahidi kopa bank nunua kiwanja jenga kakibanda ukae
mkataba wako unaweza tafuta mtu mwingine ukamkweka pale
as said ongea na landlord usikie atasemaje.
wakikaidi nenda mahakama ya jiji mwone kijumbe au Lwiza au Munga waeleze wao watafungua mshtaka
na mahakama itaweza kufunga hiyo grocery uishi kwa amani
Kwa hiyo ukishajenga nyumba halafu jirani akaweka baa na hiyo baa nayo ikawa na kelele unafanyaje? Au unajenga nyingine??!!!! Inabidi watanzania tufikie mahali tujue haki zetu, kuwa kwako mpangaji haina maana kuwa huna haki. Mimi nakushauri ufuate ushauri wa gfsonwin hapo juu
 
Back
Top Bottom