BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,020
Kwanini UIDHULUMU nafsi yako jinsi unavyompenda huyo jamaa? Bila ya shaka kuna kitu kinachokufanya umpende kiasi hicho. Mapenzi si sawa na fungu la kitunguu au nyanya kwamba akikupa kilo moja basi nawe umpe kilo moja. Endelea kumpenda kiasi hicho hicho labda kuna siku atakuelewa otherwise it his LOSS. ID yako ya siku zote iweke kwenye PM yangu
Mimi ni mwanamke nimempenda mwanaume wangu kupita kiasi hata sijui nimempendea nini. Hili jambo linaniathiri sana kwasabu najua yeye hanipend kama ninavyompenda.
Huwa nabishana na mawazo yangu wakati mwingine kwa kuona kwamba ananipenda saana ila haniamini kwasababu anakauli yake kila siku anasema mimi nina mambo mengi bila kufafanua zaidi, huu umekua kama wimbo sasa masikioni mwangu.
Sasa nakua sielewi mambo mengi ni yap? Nachojua tu ana wivu sana. Sikai naye, yeye anakaa kwake na ameajiriwa Serikalini na mimi nakaa kwangu na nimejiajiri ila tupo Mji mmoja.
Nimeshajaribu sana kumuacha nimeshindwa basi angalau nipunguze tu. Nimefungua jina jipya kwasababu maalumu.