Nisaidieni jinsi ya kupunguza kupenda

careenjibebe

JF-Expert Member
May 28, 2020
1,604
1,646
Mimi ni mwanamke nimempenda mwanaume wangu kupita kiasi hata sijui nimempendea nini. Hili jambo linaniathiri sana kwasabu najua yeye hanipend kama ninavyompenda.

Huwa nabishana na mawazo yangu wakati mwingine kwa kuona kwamba ananipenda saana ila haniamini kwasababu anakauli yake kila siku anasema mimi nina mambo mengi bila kufafanua zaidi, huu umekua kama wimbo sasa masikioni mwangu.

Sasa nakuwa sielewi mambo mengi ni yap? Nachojua tu ana wivu sana. Sikai naye, yeye anakaa kwake na ameajiriwa Serikalini na mimi nakaa kwangu na nimejiajiri ila tupo Mji mmoja.

Nimeshajaribu sana kumuacha nimeshindwa basi angalau nipunguze tu. Nimefungua jina jipya kwasababu maalumu.
 
jikite zaidi na maisha yako, kua bize na mambo yako ya msingi,punguza kumtafuta inshort punguza mawasiliano naye na akikutafta akuulize mbona humtaft mwambie upo tight utamcheki kata sim endelea na mambo yako na usimcheki wala yan fanya kama vile hayupo hapa duniani na una mambo mengi ya kufanya
 
Mie ni mwanamke nimempenda mwanaume wangu kupita kias..hata sijui nimempendea nini...
Hili Jambo linaniathiri sana kwasabu najua yeye hanipend km ninavyompenda?
Huwa nabishana na mawazo yangu wakati mwingine kwa kuona kwamba ananipenda saana Ila haniamini kwasababu anakauli yake kila siku anasema mimi Nina mambo mengi bila kufafanua Zaid huu umekua Kama wimbo sasa masikioni mwangu....Sasa nakua sielew Mambo mengi ni yap? Nachojua tu Ana wivu saaana...
Sikai naye yeye anakaa kwake..na ameajiriwa serikalini na Mimi nakaa kwangu na nimejiajir Ila tupo mji mmoja..
Nimeshajaribu Sana kumuacha nimeshindwa bas angalau nipunguze tu...
Nimefungua jina jipya kwasababu maalumu...
Jibebe Careen
 
jikite zaidi na maisha yako, kua bize na mambo yako ya msingi,punguza kumtafuta inshort punguza mawasiliano naye na akikutafta akuulize mbona humtaft mwambie upo tight utamcheki kata sim endelea na mambo yako na usimcheki wala yan fanya kama vile hayupo hapa duniani na una mambo mengi ya kufanya
Mwisho wake ataniacha na Mimi sitaki kuachana naye
 

Similar Discussions

13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom