Nipo tayari kutoa ushauri wowote wa Kitaaluma juu ya fani ya Masoko na Uhusiano (Marketing and PR)

Burhani Omari

Member
Sep 27, 2022
8
10
Habari wanaJF!

Niwaombe radhi kwa kimya kirefu hapa JF tangu 2016, kwani nimiongoni mwa Wadau wakubwa wa jukwaaa hili. Awali nilikuwa natumia acc kwa jina Burhani Kassimu, ila kwasasa nina hii acc mpya.

Mnamo mwaka 2016, niliandika uzi hapa wa kuomba ushauri juu ya fani ya masoko na uhusiano yaani Marketing and Public Relations. Na nawashukuru wale wote waliotoa mawazo yao mseto yaan chanya na hasi lakini mwishowe niliamua moja, na chaguo langu liliangukia kwenye kwenye hii fani. Nilisoma toka 2016 mpaka 2019 nilipohitimu pale Chuo cha Taifa cha Usafirishaji, Mabibo.

●Uzuri na Ubaya wa kozi hii kwenye soko la ajira
Fani hii inauzuri na ubaya wake kama ilivyo kwenye kozi nyingine na ikumbukwe hii ni kozi ya biashara, hivyo inakuw na ushindani mkubwa kwenye soko la ajira. Kwanza ningependa kuangazia Uzuri wa kozi hii:

Mosi, uzuri wa kozi hii ni, imebeba fani mbili tofauti yaani Masoko na upande mwingine Mahusiano hivyo unaweza kuwa na chaguo (option) mwenyewe uende upande gani baada ya kumaliza masomo.

Pili, ni miongoni mwa kozi ambayo inaajira nyingi zinazotangazwa kwenye majukwaa ya ajira mfano mabumbe, ajira yako, ajira leo n.k, hivyo ni juhudi zako na umakini katika kuomba/kutafuta kazi.
Tatu, ni fani ambayo inatoa maarifa mengi sana hasa kwa wale ambao wamepanga baada ya kumaliza wajiajiri, kwani unajifunza biashara na masoko kwa ujumla.

Nne, ni kozi ambayo fani zake ni mara chache kukosa idara zake kwenye taasisi mbalimbali, hivyo inauwanda mpana kwenye soko la ajira.

Kwa mchache haya juu ya uzuri wa kozi hii, nihamie upande wa pili
kwa kuangazia changamoto/ubaya wa kozi hii:-

●Changamoto za Kozi hii kwenye soko la Ajira
Mosi, ni kozi ambayo inaushindani mkubwa kwani baadhi ya ofisi/mashirika/makampuni hususani ndogo/madogo na za/ya kati hazizingatiii sana mtu aliyesoma kozi hii kufiti kwenye nafasi, taasisi inaweza ikaopt mtu mwenye kozi nyingine inayoendana na hii na akafit kwenye nafasi mfano, Nafasi ya Marketing anaweza akafit pia mtu aliyesoma Business Administration kwani hata ukiangalia modules zao chuoni wanashare, sasa jiulize kuna vyuo vingapi vinatoa kozi za Marketing au Business Administration? Lakini pia ukiangalia kozi ya Public Relations nafasi yake anaweza akafit mtu wa Journalism au Mass Communications, je ni vyuo vingapi diploma au degree vinatoa kozi ya Journalism au Mass Communications?

Kwa leo ningependa kuishia, ila ningependa kukaribisha maswali au mjadala wowote ule. Ila angalizo ukibisha njooo na facts kwani ambaye utakayebishana nae (mimi) nimesoma hii course na nipo kazini kwasasa.

Ahsante,
Burhani Omari.
 
Nn tofauti ya marketing and public relations na marketing management
Je Kati ya hawa yupi ana soko la kupata ajira haraka zaidi
 
Marketing Management ipo ndani ya Marketing. Hivo Marketing ni General and Marketing Management ni module inasomwa kama somo ukiwa Mwaka wa pili inategemeana na muongozo wa taaluma wa chuo.
 
Mtu aliyesomea marketing anaweza kufanya kazi kama mhasibu?
Hapana hizo fani mbili tofauti mbili. Japokuwa huyu Marketing anasoma uhasibu kama somo lakini haifanyi kufanya kazi kama mhasibu. Uhasibu ni fani sensitive kama zilivyofani nyingi zinataka mtu aliyekamilika na kuwa na msingi wa masomo ya biashara hapa nazungumzia ECA ukiwa advance/A- level.
 
Marketing Management ipo ndani ya Marketing. Hivo Marketing ni General and Marketing Management ni module inasomwa kama somo ukiwa Mwaka wa pili inategemeana na muongozo wa taaluma wa chuo.
Kuna bachelor of marketing and public relations na bachelor of marketing management ndio na bachelor of business administration in marketing nakuuliza ipi nzuri.
 
Vigezo vya kusoma hiyo kozi ni vipi na je unamshauri mtu asome kozi ipi kati ya marketing na accountacy
 
Bila kusahau ndio kozi pekee ambayo kazi nyingi zinazopatikana ni za sales na mishahara huwa haizidi laki 3
 
Toa hio notion kabisa.

Kwanza, kazi ya sales anaweza fanya mtu yoyote haijalishi amesoma Marketing, Finance, Accountancy, Insurance and Risk Management nakadhalika.

Pili, Kazi za Sales si za kudharau hata kidogo ila swala linakuja pale je, unafanya katika taasisi ipi? Je, una uzoefu gani na mda gani? Mpaka nakueleza haya nimeshafanya uchunguzi na nina uthibitisho wa kutosha na nimeshafanya kazi za sales kadhaaa.

Na labda ni kusanue tu, kama nilivyokueleza kazi za sales si za kubeza kabisa. Kuna watu wanafanya kazi kwenye makampuni makubwa, taasisi kubwa, mashirika makubwa na wanapiga hela nyingi kuliko hao unaodhani kuwa wananafasi nzuri. Je, unafikiri yule mtu anayefanya kazi za sales pale TBL, Serengeti, Sportpesa nk wanalipwa hio 300k unayofikiri?

Ingia kwenye hii industry then utaijua kiundani kuna watu wanasale advertising spaces na wanakula commissions za mamilions kwa mwezi na wanakuwa na maendeleo kwa mda mfupi sasa we endelea kudharau kazi za watu hali ya kuwa hauna unachokifaham kwenye industry.
 
Vigezo vya kusoma hiyo kozi ni vipi na je unamshauri mtu asome kozi ipi kati ya marketing na accountacy
Marketing anaweza kusoma yoyote haijalishi umesoma combinations za science au arts lakini Accountancy, lazima uwe na msingi wa combinations za biashara aidha O level au Advance, kwa A level mara nyingi wamesoma ECA (Economics, Commerce and Account).
 
Back
Top Bottom