La Quica
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 1,335
- 3,140
Wakuu habari za mda huu. Kwanza kabisa TGIF.
Naomba niende kwenye mada moja kwa moja bila kupoteza wakati. Mimi ni kijana bado yanki kidogo nimehitimu chuo kikuu mwaka juzi. Sasa tatizo langu lipo kuwa kuna mdada ambaye tulisoma nae chuo ambaye wakati tukiwa chuoni alikuwa mpenzi wa rafiki yangu wa karibu sana.
Yani rafiki wa karibu kiasi cha kutosha maana tullikuwa tuna share mambo yetu na hata kusaidiana kwa hali na mali. Huyu shemeji wameachana kwa mda sasa tokea tukiwa chuoni lakini juzi hapa amenitafuta akaniambia amenimiss anaomba tuonane.
Kweli tumeonana na katika kukaa kwetu akaanza vijitabia ambavyo sikuvielewa elewa (kurembua rembua na mikonyezo mingi) ila nikajiongeza kusingizia dharura nikaondoka. Baadae usiku akanitumia sms kuwa kwanini namfanyia makusudi sitaki kukaa nae sijui anaumia moyo, nikashtuka sana. Kiukweli kwangu mimi naona kama jambo la ajabu ukizingatia alishawahi kuwa mpenzi wa rafiki yangu japo ni miaka kama mitatu imepita tokea walipoachana.
Naona kama kitendo cha kuwa nae ni kama usaliti kwa msela wangu japo sijui kama yeye atachukulia vipi au jamii mnachukuliaje swala kama hilo. Huyu binti ananitafuta kila wakati sio asubuhi mchana wala jioni, kisingizio ni kuwa anasema najali na alinipenda mda tokea chuoni ila ni baada ya kuwa alishakuwa na rafiki yangu.
Anadai alipenda jinsi nilivyokuwa mcheshi, ninaejali na nimaejituma kwenye masomo kuanzia ngazi ya mimi mwenyewe hadi kwenye group ambalo tulikuwa nae group moja na mara nyingi nilikuwa namsaidia assignments hata kama hakuwepo chuoni nilimfanyia na mwisho akapata na yeye GPA nzuri tu.
Tatizo kubwa jingine linakuja kuwa anajiamini kuwa ataninasa kutokana na hali mbaya ya ajira na maisha kuwa magumu na yeye kwao ulimbo upo na hata hiyo degree alisoma tu ili apate kujua masuala ya usimamizi wa biashara za nyumbani kwao, hivyo anatumia nguvu ya ulimbo kuninasa maana mpaka sasa nipo mtaani natangatanga sina hata shilingi.
Wakuu hali hii kusema kweli imenifanya nizidiwe na msongo wa mawazo ukizingatia kuwa mimi naona kama nitakuwa nimemsaliti mwana alafu kwa upande mwingine naona kama ndio sehemu ya kujifariji maana sina hata demu kila ninaemtaka anaringa kisa sina hela. Wakati hapa mbele yangu naona kabisa kuna faraja lakini nikimfikiria msela nakosa kabisa la kufanya.
Naombeni ushauri wenu wakuu nifanyeje.
Naomba niende kwenye mada moja kwa moja bila kupoteza wakati. Mimi ni kijana bado yanki kidogo nimehitimu chuo kikuu mwaka juzi. Sasa tatizo langu lipo kuwa kuna mdada ambaye tulisoma nae chuo ambaye wakati tukiwa chuoni alikuwa mpenzi wa rafiki yangu wa karibu sana.
Yani rafiki wa karibu kiasi cha kutosha maana tullikuwa tuna share mambo yetu na hata kusaidiana kwa hali na mali. Huyu shemeji wameachana kwa mda sasa tokea tukiwa chuoni lakini juzi hapa amenitafuta akaniambia amenimiss anaomba tuonane.
Kweli tumeonana na katika kukaa kwetu akaanza vijitabia ambavyo sikuvielewa elewa (kurembua rembua na mikonyezo mingi) ila nikajiongeza kusingizia dharura nikaondoka. Baadae usiku akanitumia sms kuwa kwanini namfanyia makusudi sitaki kukaa nae sijui anaumia moyo, nikashtuka sana. Kiukweli kwangu mimi naona kama jambo la ajabu ukizingatia alishawahi kuwa mpenzi wa rafiki yangu japo ni miaka kama mitatu imepita tokea walipoachana.
Naona kama kitendo cha kuwa nae ni kama usaliti kwa msela wangu japo sijui kama yeye atachukulia vipi au jamii mnachukuliaje swala kama hilo. Huyu binti ananitafuta kila wakati sio asubuhi mchana wala jioni, kisingizio ni kuwa anasema najali na alinipenda mda tokea chuoni ila ni baada ya kuwa alishakuwa na rafiki yangu.
Anadai alipenda jinsi nilivyokuwa mcheshi, ninaejali na nimaejituma kwenye masomo kuanzia ngazi ya mimi mwenyewe hadi kwenye group ambalo tulikuwa nae group moja na mara nyingi nilikuwa namsaidia assignments hata kama hakuwepo chuoni nilimfanyia na mwisho akapata na yeye GPA nzuri tu.
Tatizo kubwa jingine linakuja kuwa anajiamini kuwa ataninasa kutokana na hali mbaya ya ajira na maisha kuwa magumu na yeye kwao ulimbo upo na hata hiyo degree alisoma tu ili apate kujua masuala ya usimamizi wa biashara za nyumbani kwao, hivyo anatumia nguvu ya ulimbo kuninasa maana mpaka sasa nipo mtaani natangatanga sina hata shilingi.
Wakuu hali hii kusema kweli imenifanya nizidiwe na msongo wa mawazo ukizingatia kuwa mimi naona kama nitakuwa nimemsaliti mwana alafu kwa upande mwingine naona kama ndio sehemu ya kujifariji maana sina hata demu kila ninaemtaka anaringa kisa sina hela. Wakati hapa mbele yangu naona kabisa kuna faraja lakini nikimfikiria msela nakosa kabisa la kufanya.
Naombeni ushauri wenu wakuu nifanyeje.
