Nipeni neno wenye hekima

Nipeni neno wenye hekima

Unauliza iweje wakati hutaki ushauri wa kuama?

Kanunue mafuta ya olive oil, salia na kufunika na damu ya Yesu kristo wa Nazareti

then paka popote kidogo kidogo huku unasalia yawe ndio ya kuvunja lolote linalotenda hayo na Mungu ayafumbue. Paka hata kiatu na linalobadilishwa

Weka imani juu haswa pia.

N.b. wanakujaribu ulalamike, upunguze imani wakumalize watakavyo. Ni kama haujui ulipo...nyumba za watu uficha siri nyingi.

Pole endelea kujenga imani, huku ukitafuta kwako. Natumaini unalipa chochote au hata kutoa pesa ya chakula kuchangia.
 
Ukigeuza hicho unachoita kapeti ya kiatu cha kushoto kitaingia vipi tena kwenye kiatu? Hujui kwamba ukigeuza itafanana na ya mguu wa kulia?
.
Mkuu kinageuzwa na kurudiswa tu kwa kulazimishwa kidogo.
d48ed7c8d2c75197e85836640100ecda.jpg
.

Kiatu chenyewe ndo hicho hapo.
 
.
Sasa hivi ndo nataka nilale na ndio nimevikagua viatu na kuhakikisha carpet yake ipo sawa japokuwa sio ndio nilivivaa leo wala jana. Nimefunga mlango na nishamshukuru Mungu kwa kunilinda katika siku.
Mimi nilikushauri utoe kabisa ili tuone inakuwaje ila tunasubir mrejesho mwenyez mungu akulinde
 
Hiyo carpet unaigeza mwenyewe usiku usingizini bila kujitambua..
 
Niposa safarini nchi jirani kibiashara na nimeshukia nyumbani kwa rafiki yangu. Nimepewa chumba changu na ninalala humo peke yangu. Cha kunishangaza kama wiki tatu zilizopita nimeamka asubuhi nikakuta kiatu ninachovaa cha mguu wa kushoto ile carpet ya kukanyagia ndani ya kiatu imegeuzwa ndani nje. Nikajiuliza maswali mengi bila kupata jibu. Mimi ni mkristo nisiyetishika na mauza uza ya kishirikina nilikipiga kiatu damu ya Yesu na kuondoa shaka lolote. Wiki mbili baadae nimekivaa kiatu kile na hapakuwa na dhara lolote. Ninachoshangaa ni kwamba juzi usiku kuamkia jana nimeamka asubuhi na kukuta kiatu kile kile cha mguu wa kushoto carpet lake la ndani limegeuzwa ndani nje. Nimejiuliza maswali mengi na sikupata jibu ila mimi kama mkristo thabiti nimetupilia mbali dhana zote zinazoaminiwa ktk uchawi na uganga. Msingi huu nimeujenga juu ya uthabiti wangu kwamba sikuwahi kumwamini mchawi wala kumpa usikivu wa namna yeyote ile na pia sikuwahi hata kushika wala kuamini katika hirizi ya namna yeyote ile.
Hebu wanye hekima wa Jf tushirikiane katika hili ni nani au nini kinageuza carpet ya kiatu changu usiku? Nia na dhumuni ni nini? Niko fiti mentally na physically na sijaruhusu kwa namna yeyote kujiathiri kisaikolojia.
Akili inakuambia hutshiki na ushirikina lkin kimsingi umeamini ushirikina.
 
Hahahaaa, unajua uchawi kitu cha ajabu sana, ni imani ndogo sana. kuna namna nyingi za ku disapoint hawa viumbe. Fanya moja kati ya yafuatayo.
1. Kama unasali kweli, kila ukivua viatu wakati wa kulala weka Rozali (kama wewe ni RC) au Bible kama mkristo wa kawaida au tazbi kwenye viatu.
OR.
2.Tafuta mfupa wa nguruwe au mtiwa mhogo uweke juu ya mlango halafu lala tu na hutopata shida (kama ni mpagani)
OR.
3. Ukiamka asubuhi ukakuta wamefanya huo mchezo, waite wenyeji wako, waambie unajua mchezo wanofanya na waache mara moja (kama wewe ni kauzu)
OR.
Ukiamka ukakuta wamefanya hivyo, kanunue kisu kipya dukani, uwe unakinoa ukiwa uani kisha unakianika, kisha unakinoa na kukianika tena kama mara kumi huku unaimba ule wimbo wa Remmy Ongalla, " Kifoo, Kifoo, Kifo hakina hurumaaa" (kama una asili yaugaidi)

CHAGUA NJIA MOJA WAPO HAPO KULINGANA NA IMANI YAKO, HAYO YOTE UKISHINDWA, BASI PANDA BASI URUDI KWENU MAANA HAUNA PESA YA KULIPIA HOTELI.

Regards
Kidudu.
 
Kwa jinsi tu unavyo ongea unaonesha ishara ya uoga
 
chukua chumvu uweke kwenye kiatu chako afu chumvi nyingine uweke kwenye maji ya kuoga uogee. kila kitu kitakaa sawa
 
Mkuu umesema umeenda kibiashara, je kama huyo jamaa yako asingekuwepo ungekaa wapi siku zote hizo? Unapokuwa na mashaka sehemu siyo vizuri kuendelea kuishi hiyo sehemu.
Kubwa zima bado linaenda kukaa kwa watu? Aibuuuu!! Kukaa kwa watu tena nchi ya ugenini, basi iwe siku 2 au 3 sasa lenyewe leo miezi liko kwa watu! Mfanyabiashara gani huyu ambaye hajajipanga huyu? Yaani unataka upate faida in the expense of others? Aibuuuuuuu!! Hama hapo kiongozi!!
 
Back
Top Bottom