happiness win
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 2,461
- 1,384
Toka mwanzo nilijitahidi nisipende kwa lengo la kukwepa kuumizwa. Kuna walionipenda sana na waliishia kuumia maana sikuwa tayari kupenda. Niliwaacha wakiumia na kulia mimi niliendelea kuishi kwa raha bila majeraha ya mapenzi.
Mmoja kati ya hao niliowahi kuwaumiza alinifata tena kwa machozi, nilijikuta narudiana naye na nilibaini nimempenda kikweli. Shida ikawa hana imani tena na mimi, mara kwa mara hukumbushia niliyomfanyia siku za nyuma. Hata nisipojibu simu kwa wakati ni maneno, kwa kifupi mapenzi yamekuwa kero na nimeshindwa kujizuia nampenda sana. Sijielewi hata imekuwaje nikatekwa kwa mapenzi kiasi hiki. Imefikia hatua nimemuomba aniache maana haniamini, anasema hayuko tayari ila eti mimi niendelee kumvumilia maana nilimharibu nilipomtenda. Cha kutisha ni kwamba ananitishia maisha endapo nitamkimbia na kumuacha. Nisaidieni niwezetoka kwenye mapenzi haya na nisipende tena.
Mmoja kati ya hao niliowahi kuwaumiza alinifata tena kwa machozi, nilijikuta narudiana naye na nilibaini nimempenda kikweli. Shida ikawa hana imani tena na mimi, mara kwa mara hukumbushia niliyomfanyia siku za nyuma. Hata nisipojibu simu kwa wakati ni maneno, kwa kifupi mapenzi yamekuwa kero na nimeshindwa kujizuia nampenda sana. Sijielewi hata imekuwaje nikatekwa kwa mapenzi kiasi hiki. Imefikia hatua nimemuomba aniache maana haniamini, anasema hayuko tayari ila eti mimi niendelee kumvumilia maana nilimharibu nilipomtenda. Cha kutisha ni kwamba ananitishia maisha endapo nitamkimbia na kumuacha. Nisaidieni niwezetoka kwenye mapenzi haya na nisipende tena.