Nipe mawazo yako kuhusu hili

Shayu

Platinum Member
May 24, 2011
608
1,653
Hatuwezi kumaliza suala la madawa ya kulevya kwa nguvu peke yake. Matatizo ya kijamii ambayo tunayokabiliana nayo sasa ni lazima tuyaangalie katika mifumo yetu ya makuzi na malezi na mahusiano yetu. Lazima tuangalie katika tabia tunazozijenga kwa watoto wetu na vijana wetu. Kuwafunga watu kwasababu ya kutenda visivyo sahihi pasipo kuwa na mifumo mizuri ya malezi na makuzi ni kuendelea kila siku kuongeza gharama katika kujenga vituo vya polisi na jela wakati tunaweza kuzuia haya mambo kama tukiwa na malezi na makuzi mazuri. Na kama tutatoa elimu bora ya maadili kwa watu wetu.

Ni lazima tufanye hivi ili kupunguza uhalifu na matumizi ya hela nyingi kwenye kudhibiti uhalifu. Watoto wetu kama hawamjui Mungu hakuna tutachofanya kuwaokoa kutoka kwenye madawa ya kulevya na tabia nyingine zenye madhara kwa wao wenyewe na kwa jamii. Hakuna tutakacho kijenga. Hakuna kitakacho heshimiwa iwe ndoa au jamii.

We Must return to God.
 
Uhuru na Haki chini ya mwamvuli wa Demokrasia, ndio adui mkubwa katika hili. Tunahangaikia kufungua vinywa vyetu kumeza yaletwayo, tusijali udogo wake kulinganisha na mrija uletao. TUMEPOTEA.

Jamii changa kama zetu, tangu kwa watoto wetu hadi kwa watu wazima, hatuna budi KUFUNGWA nini tusikie, tuone, tutamke, tutende ama laa! Ati Uhuru wa watu! Na tutayari kurushiana mawe ili tubomoe Taifa, Ni Upumbavu.
Anaita sasa.
 
Uhuru na Haki chini ya mwamvuli wa Demokrasia, ndio adui mkubwa katika hili. Tunahangaikia kufungua vinywa vyetu kumeza yaletwayo, tusijali udogo wake kulinganisha na mrija uletao. TUMEPOTEA.

Jamii changa kama zetu, tangu kwa watoto wetu hadi kwa watu wazima, hatuna budi KUFUNGWA nini tusikie, tuone, tutamke, tutende ama laa! Ati Uhuru wa watu! Na tutayari kurushiana mawe ili tubomoe Taifa, Ni Upumbavu.
Anaita sasa.
Ndugu yangu,

Hatuwezi kusingizia demokrasia na utandawazi 100% kwenye kuharibikiwa kwa jamii yetu japo kuna baadhi ya mambo yanachangia... Kuna baadhi ya misingi ya malezi ambayo haijalishi unaishi kwenye nchi ya kidemokrasia au kidikteta lazima ifuatwe ikiwa tunataka kujenga jamii iliyo bora.

Ndio maana ukitazama nchi zilizoendelea na zilizo mbele kwenye masuala ya utandawazi na demokrasia utakuta kwamba kuna misingi fulani ya malezi wako juu kuliko hata sisi. Kwa mfano sio kila sehemu unaweza kukuta pombe zinauzwa kiholela, kuna maduka maalum yanayotambulika na hawauzi pombe kwa yoyote alie chini ya miaka 18 na kuna adhabu kali kwa wanaokiuka. Vivyo hivo kwenye kumbi za starehe wako strict kutoruhusu aliye chini ya miaka 18 kuingia. Mpita njia anaweza kukushitaki polisi akiona matendo yako yanahatarisha usalama na ustawi wa mtoto wako na ukachukuliwa hatua!

Kinyume chake sisi tumeingia kwenye utandawazi kichwa kichwa huku jamii ikiacha kusimama kwenye nafasi yake kama mdau wa kwanza kabisa kwenye matunzo na malezi ya watoto. Kila mtu anajifanyia mambo kivyake hakuna anayejali kinachoendelea kwa watoto halafu tunakuja kushangaa wakishaharibikiwa. Kuwafungia kwamba wasione wala wasisikie kinachoendelea huko nje ni kuahirisha tatizo. Utawafungia mpaka lini? sababu itafika siku wazazi wataondoka na kuwaacha watoto peke yao sasa watakabiliana vipi na dunia iliyojaa kila aina ya vurumai?

Lazima turudi kwenye misingi ya malezi ya vijana wetu, tukae nao, tuongee nao, tuwasikilize, tujifunze kutoka kwao na wao wajifunze kutoka kwetu. Tusimame kwenye nafasi yetu kama wazazi na walezi, na muhimu zaidi tumtangulize Mungu.
 
Uhuru na Haki chini ya mwamvuli wa Demokrasia, ndio adui mkubwa katika hili. Tunahangaikia kufungua vinywa vyetu kumeza yaletwayo, tusijali udogo wake kulinganisha na mrija uletao. TUMEPOTEA.

Jamii changa kama zetu, tangu kwa watoto wetu hadi kwa watu wazima, hatuna budi KUFUNGWA nini tusikie, tuone, tutamke, tutende ama laa! Ati Uhuru wa watu! Na tutayari kurushiana mawe ili tubomoe Taifa, Ni Upumbavu.
Anaita sasa.
Huoni kwamba watu wanapaswa kuwa huru na sio kufungwa anachoona na achosikia? Je hii itamsaidia kuwa na nidhamu kwenye fikra zake au pengine kujenga tabia zake?
 
Uhuru na Haki chini ya mwamvuli wa Demokrasia, ndio adui mkubwa katika hili. Tunahangaikia kufungua vinywa vyetu kumeza yaletwayo, tusijali udogo wake kulinganisha na mrija uletao. TUMEPOTEA.

Jamii changa kama zetu, tangu kwa watoto wetu hadi kwa watu wazima, hatuna budi KUFUNGWA nini tusikie, tuone, tutamke, tutende ama laa! Ati Uhuru wa watu! Na tutayari kurushiana mawe ili tubomoe Taifa, Ni Upumbavu.
Anaita sasa.
Uhuru unaoulaumu ndio uliokufungulia mlango wa kusema uliyoyasema. Bila ya uhuru huo mawazo yako kakasi yasingepata upenyo wa kujibanza.
Kulaumu uhuru ni ufinyu wa tafakari. Kinyume chake uhuru ndio mwanzo wa maarifa ya sasa. POLE SANA.
 
Ndugu yangu,

Hatuwezi kusingizia demokrasia na utandawazi 100% kwenye kuharibikiwa kwa jamii yetu japo kuna baadhi ya mambo yanachangia... Kuna baadhi ya misingi ya malezi ambayo haijalishi unaishi kwenye nchi ya kidemokrasia au kidikteta lazima ifuatwe ikiwa tunataka kujenga jamii iliyo bora.

Ndio maana ukitazama nchi zilizoendelea na zilizo mbele kwenye masuala ya utandawazi na demokrasia utakuta kwamba kuna misingi fulani ya malezi wako juu kuliko hata sisi. Kwa mfano sio kila sehemu unaweza kukuta pombe zinauzwa kiholela, kuna maduka maalum yanayotambulika na hawauzi pombe kwa yoyote alie chini ya miaka 18 na kuna adhabu kali kwa wanaokiuka. Vivyo hivo kwenye kumbi za starehe wako strict kutoruhusu aliye chini ya miaka 18 kuingia. Mpita njia anaweza kukushitaki polisi akiona matendo yako yanahatarisha usalama na ustawi wa mtoto wako na ukachukuliwa hatua!

Kinyume chake sisi tumeingia kwenye utandawazi kichwa kichwa huku jamii ikiacha kusimama kwenye nafasi yake kama mdau wa kwanza kabisa kwenye matunzo na malezi ya watoto. Kila mtu anajifanyia mambo kivyake hakuna anayejali kinachoendelea kwa watoto halafu tunakuja kushangaa wakishaharibikiwa. Kuwafungia kwamba wasione wala wasisikie kinachoendelea huko nje ni kuahirisha tatizo. Utawafungia mpaka lini? sababu itafika siku wazazi wataondoka na kuwaacha watoto peke yao sasa watakabiliana vipi na dunia iliyojaa kila aina ya vurumai?

Lazima turudi kwenye misingi ya malezi ya vijana wetu, tukae nao, tuongee nao, tuwasikilize, tujifunze kutoka kwao na wao wajifunze kutoka kwetu. Tusimame kwenye nafasi yetu kama wazazi na walezi, na muhimu zaidi tumtangulize Mungu.
Mkuu, ninakupata vilivyo kabisa. Nilichosema hapo juu ni kuwa, Vinywa vyetu ni vidogo mno kupokea bomba la Uhuru na Haki kama lilivyoundwa. Demokrasia yaweza kuwa ni Jambo sahihi kabisa, lakini nina hakika kabisa kwa Mtu mweusi halipo kwa Wakati Sahihi.

Demokrasia si ya kuitazama kwa mawanda mafupi, hili ni dubwasha kubwa sana. Umetoa mfano kwa wenzetu nje na sheria zilindazo maadili ya watoto wao, Je, tunaweza kujiuliza kwanini kwetu inashindikana?

Mkuu, amini ninakuambia, huko kichwakichwa tulikoingia chanzo ni ULIMBUKENI WETU WA KUJILAZIMISHA KUISHI DEMOKRASIA, kwa madai ya kutafuta HAKI NA UHURU.
Nilikozaliwa vilinge vya pombe vilikuwa vinafunguliwa Jumapili tu, leo ni mpaka muda wa kazi, nini kilipoteza maadili yetu kama sio huo Uhuru? Serikali imepiga marufuku baa kufunguliwa muda wa kazi, je tunziona laana na lawama zitolewazo? Bado Uhuru ni jambo la kupiganiwa kwa watu aina hiyo?

TURUDI KWENYE MISINGI YETU, ambayo iliamua wazi Nini useme au usikie na nini usiseme au usisikie. NI LAZIMA TUFUNGWE. HUU SI WAKATI WA KUPIGANIA UHURU, NA SIFIKIRI KAMA UNAPIGANIWA.
Anaita sasa.
 
Huoni kwamba watu wanapaswa kuwa huru na sio kufungwa anachoona na achosikia? Je hii itamsaidia kuwa na nidhamu kwenye fikra zake au pengine kujenga tabia zake?

Mkuu, siku zote Uhuru si mjenzi mzuri wa Nidhamu, lakini Nidhamu ni mjenzi mzuri wa Uhuru. Na ni Nidhamu ambayo i miongoni mwa silaha bora kabisa katika kujikwamua na Umasikini. Je, tunakubaliana hilo? Tatizo kubwa la Taifa kwa wakati huu, ni Kukosekana kwa Nidhamu, ambayo ni miongoni mwa nguzo ya Ukombozi wetu. Je, tunaweza kujenga nidhamu kwa Kuropoka? Je, ni kweli tunafikiri Vinywa vyetu vinatoa maoni na si uropokaji?
Anaita sasa.
 
Uhuru unaoulaumu ndio uliokufungulia mlango wa kusema uliyoyasema. Bila ya uhuru huo mawazo yako kakasi yasingepata upenyo wa kujibanza.
Kulaumu uhuru ni ufinyu wa tafakari. Kinyume chake uhuru ndio mwanzo wa maarifa ya sasa. POLE SANA.
Nashukuru ndugu.
Mimi nabaki kusimama hapa "Utii bila Uhuru ni Utumwa, na Uhuru bila Nidhamu ni Uwendawazimu " J. K. Nyerere.

Je, tunatumia Uhuru wetu kwa Nidhamu? Ndio swali la kujiuliza? Binafsi siioni hata hako kanafasi kadogo ka kutumia Uhuru wetu kwa Nidhamu. HUU SI WAKATI WA KUPIGANIA UHURU, TUJENGE NIDHAMU KWANZA.
Anaita sasa.
 
Uhuru na Haki chini ya mwamvuli wa Demokrasia, ndio adui mkubwa katika hili. Tunahangaikia kufungua vinywa vyetu kumeza yaletwayo, tusijali udogo wake kulinganisha na mrija uletao. TUMEPOTEA.

Jamii changa kama zetu, tangu kwa watoto wetu hadi kwa watu wazima, hatuna budi KUFUNGWA nini tusikie, tuone, tutamke, tutende ama laa! Ati Uhuru wa watu! Na tutayari kurushiana mawe ili tubomoe Taifa, Ni Upumbavu.
Anaita sasa.

Ndugu, kama hiyo dhana yako ina uhusiano wowote na ukweli basi kabla ya kuileta hapa ungetambua hilo janga lilikuwepo kabla ya Demokrasia kukanyaga bara la Afrika.
 
Hatuwezi kumaliza suala la madawa ya kulevya kwa nguvu peke yake. Matatizo ya kijamii ambayo tunayokabiliana nayo sasa ni lazima tuyaangalie katika mifumo yetu ya makuzi na malezi na mahusiano yetu. Lazima tuangalie katika tabia tunazozijenga kwa watoto wetu na vijana wetu. Kuwafunga watu kwasababu ya kutenda visivyo sahihi pasipo kuwa na mifumo mizuri ya malezi na makuzi ni kuendelea kila siku kuongeza gharama katika kujenga vituo vya polisi na jela wakati tunaweza kuzuia haya mambo kama tukiwa na malezi na makuzi mazuri. Na kama tutatoa elimu bora ya maadili kwa watu wetu.

Ni lazima tufanye hivi ili kupunguza uhalifu na matumizi ya hela nyingi kwenye kudhibiti uhalifu. Watoto wetu kama hawamjui Mungu hakuna tutachofanya kuwaokoa kutoka kwenye madawa ya kulevya na tabia nyingine zenye madhara kwa wao wenyewe na kwa jamii. Hakuna tutakacho kijenga. Hakuna kitakacho heshimiwa iwe ndoa au jamii.

We Must return to God.

Nakubaliana nawe kuwa njia zaidi moja lazima itumike ili kuweza kukabiliana na kulishinda janga la madawa ya kulevya. Mkazo umewekwa kwenye Sheria na Nguvu kwa sasa lakini njia nzuri zaidi ni kuhusisha roho na fikra za wanajamii. Naunga mkono kuwa mchango wa mafundisho ya kumcha Mungu (dini) na malezi bora ni silaha nzuri sana kwenye hii vita.
 
Ndugu, kama hiyo dhana yako ina uhusiano wowote na ukweli basi kabla ya kuileta hapa ungetambua hilo janga lilikuwepo kabla ya Demokrasia kukanyaga bara la Afrika.

Sijakuelewa labda, kuwepo kwa Tatizo kabla ya ujio wa Demokrasia Afrika, kunahalalishaje utakatifu wa Demokrasia katika hili?

Je, tunaposema Dhana nzima ya Soko Huria namna tunavyoiishi ni kichocheo cha Unyonyaji kwa Afrika, tutakuwa tumekosea kwa sababu tu Unyonyaji ulikuwepo hata kabla ya ujio wa dhana ya Soko Huria?

Msingi wa kanusho lako ni upi?

Naunga mkono hoja ya kuhusishwa kwa Fikra na Roho za wanajamii katika hii vita, kwa maana kwamba, humo ndimo mwa kupandikiza Vifungo vya Kujenga Fikra na Roho chanya dhidi ya Madawa.

Dini na Jamii zina wajibu wa Asili na Uhuru wa kusimamia Malezi Bora, wamefanya nini hadi sasa? Jahazi linazidi kuzama, wamebatilisha nafasi zao na na kuwa hasi kwa msaada wa Uhuru wao. NI LAZIMA TUFUNGWE, TUFUNGWE NA MISINGI YENYE USAWA NA SAHIHI. Watadai Uhuru wao na kudai ni haki yao, WANAFIKI.

Anaita sasa.
 
Sijakuelewa labda, kuwepo kwa Tatizo kabla ya ujio wa Demokrasia Afrika, kunahalalishaje utakatifu wa Demokrasia katika hili?

Je, tunaposema Dhana nzima ya Soko Huria namna tunavyoiishi ni kichocheo cha Unyonyaji kwa Afrika, tutakuwa tumekosea kwa sababu tu Unyonyaji ulikuwepo hata kabla ya ujio wa dhana ya Soko Huria?

Msingi wa kanusho lako ni upi?

Naunga mkono hoja ya kuhusishwa kwa Fikra na Roho za wanajamii katika hii vita, kwa maana kwamba, humo ndimo mwa kupandikiza Vifungo vya Kujenga Fikra na Roho chanya dhidi ya Madawa.

Dini na Jamii zina wajibu wa Asili na Uhuru wa kusimamia Malezi Bora, wamefanya nini hadi sasa? Jahazi linazidi kuzama, wamebatilisha nafasi zao na na kuwa hasi kwa msaada wa Uhuru wao. NI LAZIMA TUFUNGWE, TUFUNGWE NA MISINGI YENYE USAWA NA SAHIHI. Watadai Uhuru wao na kudai ni haki yao, WANAFIKI.

Anaita sasa.

Hakuna uhusiano wa wa moja kwa moja kati madawa ya kulevya na Demokrasia. Pili hakuna uhusiano wa "unyonyaji" na madawa ya kulevya. Tatu kuna uhusiano kati ya ujinga na unyonyaji kama vile ilivyo kwa madawa ya kulevya.

Ujinga wetu na ubinafsi ndio sababu kubwa ya sisi Waafrika kunyonywa. Hao wanyonyaji sana sana wametumia fursa tulizowatengenezea kwa hayo mawili.

Kwa mfano:- zamani tulizoea kusikia Wazungu/Westerners ndio wanyonyaji lakini leo Wachina ni wanyonyaji wabaya kuliko hao Westerners. Leo tuna viongozi wa Kiafrika ambao ni wanyonyaji wabaya kuliko Westerners. Leo tunao ndugu, jamaa na majirani wenzetu ambao ni wabaya na wanyonyaji kuliko hao Westerners. Ndio maana sikukubaliana na kisingizio cha Demokrasia.

Madawa ya kulevya ni tatizo pana lenye kuhusisha maisha kamili ya mtu i.e. roho yake, nafsi yake, akili zake, mwili wake, jamii yake, mazingira na mambo yenye kufanana na hayo. Huwezi kuishinda vita ya aina hiyo kwa kutumia silaha za aina moja au mbinu ambazo kimsingi ni za aina moja. Ni vita inayopiganwa na kushinda kwa kutumia "all armors".
 
Madawa ya kulevya ni tatizo pana lenye kuhusisha maisha kamili ya mtu i.e. roho yake, nafsi yake, akili zake, mwili wake, jamii yake, mazingira na mambo yenye kufanana na hayo. Huwezi kuishinda vita ya aina hiyo kwa kutumia silaha za aina moja au mbinu ambazo kimsingi ni za aina moja. Ni vita inayopiganwa na kushinda kwa kutumia "all armors".

Mkuu, ni kipi hapo juu unachofikiri hakifungwi na dhana ya Uhuru na Haki chini ya mwamvuli wa Demokrasia? Je, ni roho zetu, ama nafsi zetu? Je, ni mazingira yetu ama jamii zetu? Je, ni miili yetu, ama akili zetu leo hii?

Unakiri kuwa sisi ni wajinga na wabinafsi, unashindwaje kuona athari za Kuachwa Huru kwa mtu mjinga na mbinafsi kutumia ujinga na ubinafsi wake?

Bado nasisitiza, HATUNA BUDI KUFUNGWA. Na natambua wazi kuwa, mara tu baada ya vifungo sahihi kuanza kufanya kazi, Ni sisi tena tutakaotafuta wa kumburuza barabarani, kwa hoja za Kunyimwa Uhuru wa kutumia Ujinga na Ubinafsi wetu. Na Mataifa yataunga mkono...

Sisi si Wajinga na Wabinafsi kiasi hicho, Vipo Vifungo, kuvisema sio Kufuru.

Anaita sasa.
 
Mkuu, ni kipi hapo juu unachofikiri hakifungwi na dhana ya Uhuru na Haki chini ya mwamvuli wa Demokrasia? Je, ni roho zetu, ama nafsi zetu? Je, ni mazingira yetu ama jamii zetu? Je, ni miili yetu, ama akili zetu leo hii?

Unakiri kuwa sisi ni wajinga na wabinafsi, unashindwaje kuona athari za Kuachwa Huru kwa mtu mjinga na mbinafsi kutumia ujinga na ubinafsi wake?

Bado nasisitiza, HATUNA BUDI KUFUNGWA. Na natambua wazi kuwa, mara tu baada ya vifungo sahihi kuanza kufanya kazi, Ni sisi tena tutakaotafuta wa kumburuza barabarani, kwa hoja za Kunyimwa Uhuru wa kutumia Ujinga na Ubinafsi wetu. Na Mataifa yataunga mkono...

Sisi si Wajinga na Wabinafsi kiasi hicho, Vipo Vifungo, kuvisema sio Kufuru.

Anaita sasa.

Watu wenye hulka na mtazamo kama wako pia si haba kwenye utawala huu wa awamu ya tano.

Yaani wewe badala ya kumwelimisha mjinga (sio mpumbavu) wewe unamfunga!?!!? Yaani mawazo hayo hayo ndiyo Wakoloni walitumia na kuwafunga babu zetu na kuwauza kama mbuzi kwenye masoko ya utumwa. Ndio maana tuliona baadhi ya waadhirika (victims) wa dawa za kulevya wakiwekwa mahabusu badala ya kusaidiwa kwenye rehabs.

Bila shaka umewahi kusikia kuwa kuna wajinga wa "kutengenezwa", na nchi hii kwa sehemu inao wengi thanks to CCM policies. Ambayo inawachukulia (for granted) wananchi wa Tanzania kama properties & tools for their lusts. Ndio maana baadhi yetu tuliona na kuainisha kasoro katika mchakato mzima wa vita ya dawa za kulevya. It was not a genuine war but rather a contaminated political struggle for supremacy.
 
Watu wenye hulka na mtazamo kama wako pia si haba kwenye utawala huu wa awamu ya tano.

Yaani wewe badala ya kumwelimisha mjinga (sio mpumbavu) wewe unamfunga!?!!? Yaani mawazo hayo hayo ndiyo Wakoloni walitumia na kuwafunga babu zetu na kuwauza kama mbuzi kwenye masoko ya utumwa. Ndio maana tuliona baadhi ya waadhirika (victims) wa dawa za kulevya wakiwekwa mahabusu badala ya kusaidiwa kwenye rehabs.

Bila shaka umewahi kusikia kuwa kuna wajinga wa "kutengenezwa", na nchi hii kwa sehemu inao wengi thanks to CCM policies. Ambayo inawachukulia (for granted) wananchi wa Tanzania kama properties & tools for their lusts. Ndio maana baadhi yetu tuliona na kuainisha kasoro katika mchakato mzima wa vita ya dawa za kulevya. It was not a genuine war but rather a contaminated political struggle for supremacy.

Mkuu, sifikiri kama hoja ya watu wa awamu ya tano ama ya kwanza ni ya msingi humu. Pia sifikiri kama msingi wa hoja ni approach inayotumika na serikali wakati huu. Siwezi kuvijadili.

Unachofanya katika hoja ya ujinga ama upumbavu wa watanzania, ni kucheza na maneno tu kukwepa hoja ya msingi.

Ni kweli kuwa Mjinga ni mtu asiyejua jambo, hivyo Elimu kwake ni jambo sahihi kabisa. Je, Watanzania hatujui nini kuhusu Madawa ya kulevya? Ni athari zake au sheria zake? Je, ni muuzaji, msambazaji, ama mtumiaji? Nani hajui na hajui nini na anahitaji elimu ipi kuhusu madawa ya kulevya?

Mpumbavu ni yule ajuae kweli na bado akaamua kutenda kwa kufuata mihemko yake. Je, wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya na matumizi yake HAWAJUI WALITENDALO?

Kwangu Elimu ni Sawa, maana vizazi vinakua, lakini bado Wapumbavu ni wengi hawana budi KUFUNGWA. Wapo serikalini, kwenye nyumba za ibada, mashuleni, makazini, mitaani, n.k. Wengi ni wapumbavu, na sifikiri kuwa uliposema Wajinga ulikuwa na maana ya watu wasiojua mambo.

Pia, Elimu haiko nje na Vifungo vya Uhuru na Haki, na Elimu inapokosa vifungo sahihi ndio inapozalisha Wasomi Wapumbavu kama walio wengi leo.

Anaita sasa.
 
Back
Top Bottom