Nipe bei ya 'CEMENT" eno ulipo

Nipe bei ya 'CEMENT" eno ulipo

Bakulutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2011
Posts
2,595
Reaction score
1,863
Leo maeneo ya Bunju, Boko, Tegeta na Goba cement Dangote/Twiga Extra 1500-16000/= na Plus 16000-19000/=

Nimenunua leo Dangote extra Goba uwanjani 16000/

Nasikia kiwanda cha Wazo hakifanyi kazi, bei ikipanda itarudi tena?
 
Mkuu umetembea kifua mbele kweli ?? Hizo ndo namba zinazotakiwa somwa na watanzania wote
 
Duh noma sana aisee cement nimenunua Jana 16,000..

Nenda kaulize na nondo mkuu uone maajabu,dah ujenzi ni noma sana
 
Jana nimenunua kwa 15500Tshs, Leo nimeenda nimenunua kwa 16000Tshs.
 
Kwa hali ilivo sasa hivi nadhani viwanda kama Nyati na Kilimanjaro walitakiwa wazalishe cement ya kutosha ili walikamate soko kwa bei reasonable
 
Nchi siyo simenti tuu, kuku, hakuna vifaranga, hakuna mafuta kabaki jiwe na mbwebwe, za the country is on the right track
 
Wasiwasi wangu itarudi kwenye bei yake? Tatizo Tanzania kitu kikipanda bei kwa dharura hakishuki tena mfano sukari, mafuta ya kupikia.
 
Naamini hivi viwanda vyetu vingine vya cement havijui maana ya biashara mana sasa hivi demand iko high while supply ni low.... Wanatakiwa kutake advantage ya soko like wazalishe cement nyingi na wauze kwa bei yao hiyo hiyo mana kupanda kwa bei ni kutokana na shortage ya mzigo madukani na si kupanda kwa operating cost. Ukizunguka sehem kubwa ya Boko maduka mengi hayana cement till kwa Msaki ambae ni Wakala wa Twiga.

Bado narudi kusema nyati,dangote na kilimanjaro cement hawajui biashara au hawajui kipindi gani cha kutake advantage ya soko
 
Hivi dangote amesitisha uzalishaji kabisa Kiwandani kwake?
 
hapa tarime mpakani sementi ni sh 22000 lakini upande wa pili kenya ni 14000 tu eti alafu huruhusiwi kununua cement ya kenya. inabidi uchague kusuka au kunyoa(ununue tanzania uchangie uchumi au ununue kenya uhujumu uchumi)
 
Back
Top Bottom