Nini Sababu za Mbowe na Lowassa kukwepa kongamano kumbukumbu ya Mwl.Nyerere?

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Nini Sababu za Mbowe na Lowassa kukwepa kongamano kumbukumbu ya Mwl.Nyerere?

Haijawahi kutokea kwenu ninyi kuonekana mkishiriki makongamano na midahalo ya wazi yenye kuzungumzia masuala ya utaifa na nchi kwa ujumla. Mara kwa mara Taasisi ya Mwalimu Nyerere imekuwa ikiandaa mada na hoja zenye kubeba changamoto za utaifa hususani maadili,miiko ya uongozi na vita dhidi ya rushwa. Mara kadhaa vingozi wastaafu kama Jaji Warioba, Dr.Salim, Mzee Butiku nk. Wamekuwa wazungumzaji wakubwa kwenye mada hizo.

Mbowe kama KUB amekuwa kimya kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, Lowassa kwa upande wake hata kwenye kampeni za uraisi mwaka jana hakuwahi kuongelea mikakati yake kudhibiti maadili ya uongozi na vita dhidi ya rushwa. Kinachoshangaza ni kuwa duniani kote vinara wa upinzani ndio huibana serikali na viongozi wa umma kuhusu masuala ya rushwa ila hapa kwetu angalau chama cha ACT-Wazalendo kwa siku za karibuni wameonyesha njia.

Ninaomba tujadili haya kwa mapana kwani hawa ni viongozi wetu, kama watakwepa kuzungumza na kukemea matatizo ya nchi yetu kupitia makongamano kama hili ya Mwl.Nyerere inatia shaka


Je ni kweli hawana cha kuzungumza jinsi gani Taifa letu linaweza kupiga hatua kwa kupiga vita rushwa na kzingatia maadili ya viongozi wa umma?


Je nao ni miongozi mwa tatizo katika jamii yetu hususan katika vita dhidi ya maadili mabovu,rushwa na ubadhirifu wa mali za umma?
 
Un assembly anakacha, muungano hataki kuukumbuka, UN habitat anatuma wawakilishi

Anza na haya mambo
Kijana unayumbayumba...hueleweki...umelewa nini asubuhi yote hii? jikite kwenye mada.
 
Anza na sababu za JPM kukacha shughuli ya kuuzima mwenge.
Urais ni taasisi, siyo mali ya mtu. Lakini nimsaidie mleta mada. LOWASSA kwenda Kongamano la mwalimu Nyerere ambalo linazumgumzia pamoja na mambo mengine UADILIFU pia, ni sawa na Mkatholiki kwenda kwa PADRE kuungama huku akiomba asamehewe dhambi ambayo ataitenda kesho na siyo aliyotenda jana.
 
Urais ni taasisi, siyo mali ya mtu. Lakini nimsaidie mleta mada. LOWASSA kwenda Kongamano la mwalimu Nyerere ambalo linazumgumzia pamoja na mambo mengine UADILIFU pia, ni sawa na Mkatholiki kwenda kwa PADRE kuungama huku akiomba asamehewe dhambi ambayo ataitenda kesho na siyo aliyotenda jana.
Punguza ukali wa maneno
 
Urais ni taasisi, siyo mali ya mtu. Lakini nimsaidie mleta mada. LOWASSA kwenda Kongamano la mwalimu Nyerere ambalo linazumgumzia pamoja na mambo mengine UADILIFU pia, ni sawa na Mkatholiki kwenda kwa PADRE kuungama huku akiomba asamehewe dhambi ambayo ataitenda kesho na siyo aliyotenda jana.
Iweje aseme "serikali yangu" na taasisi imekaa kimya!?
 
Hivi mtu akiwa anashutumiwa ni mwizi alafu aende kwenye kongamano alafu akaseme anapiga vita rushwa etc. Kuna mtu yeyote kati ya wale wanamtuhumu watabadili mawazo yao?? Mpelekeni Lowasa mahakamani kama mnataka aongelee vizuri masuala hayo.... vinginevyo hakuna atakachojiongezea. Vile vile sio kawaida ya nchi yetu vyama vya siasa kushindana hoja kwa njia ya makongamano... ukitaka style hiyo waambieni na CCM wakubali kuandaliwe makongamano alafu uone kama awatakimbi. Unakumbuka spidi ya polepole kabla hajawa mkuu wa wilaya?? Madaraka matamu unamuona anapiga tantarira zake... kabla hahawa somebody else. LOWASA akienda kwenye kongamano akaongea atakuja yule aliyepigwa chini Simanjiro kwenye media na kuanza kubwabwaja uongo na ukweli.
 
Hivi mtu akiwa anashutumiwa ni mwizi alafu aende kwenye kongamano alafu akaseme anapiga vita rushwa etc. Kuna mtu yeyote kati ya wale wanamtuhumu watabadili mawazo yao?? Mpelekeni Lowasa mahakamani kama mnataka aongelee vizuri masuala hayo.... vinginevyo hakuna atakachojiongezea. Vile vile sio kawaida ya nchi yetu vyama vya siasa kushindana hoja kwa njia ya makongamano... ukitaka style hiyo waambieni na CCM wakubali kuandaliwe makongamano alafu uone kama awatakimbi. Unakumbuka spidi ya polepole kabla hajawa mkuu wa wilaya?? Madaraka matamu unamuona anapiga tantarira zake... kabla hahawa somebody else. LOWASA akienda kwenye kongamano akaongea atakuja yule aliyepigwa chini Simanjiro kwenye media na kuanza kubwabwaja uongo na ukweli.
mbona unalia lia kijana?...jikite kwenye hoja kwanini wanakwepa makongamano?
 
mbona unalia lia kijana?...jikite kwenye hoja kwanini wanakwepa makongamano?
Walikuwa kwa watindiga, huko hutakiwi kwenda na kamera, wamejadili vya kutosha kabisa.

Ushapata jawabu tuhamie kwa JPM Mwigulu Kigwagwala na Makondya sasa.
TWENDE KAZI.

======UPDATE======
Kwanini JMP aliwakacha mabalozi pale ikulu
 
Back
Top Bottom