Nini sababu ya kutojisikia kuwa na marafiki?

beevenom

JF-Expert Member
May 1, 2017
313
428
Aman iwe nanyi ndugu zangu,napenda kushare jambo langu binafsi katika maisha yangu ya kila siku. Sijajua ni tatizo au ni nini kwani tangu nikiwa bado mdogo kabisa(nikiwa shule ya msingi) sijawahi kuwa na rafiki kabisa mpaka umri huu wa thirties.

Lakini pia katika kupindi chote cha makuzi yangu nimekuwa ninaongea na kila mtu kwa sababu maalam yaani baada ya lengo langu kutimia hujikuta sitamani kuendelea kuongea na mhusika kabisa.
Pia kuna wakati huwa sijisikii kabisa kuongea na awaye yeyote labda kuchart kwa SMS tu.

Pia nina changamoto ya kutoamini MTU yoyote yule hivyo nikimkabidhi mtu kazi hujikuta nafuatilia kwa ukaribu haswaa kama vile na mie ninafanya kazi husika. Na mara nyingi nikijaribu kumuamini mtu tu lazima atazingua tu iwe kazi au mapenzi.

Sasa inafika wakati jamii inaniona nina dharau au jeuri kumbe sio kabisa kwani kuna wakati nikisalimia mtu huwa sijisikii kabisaa kuongea nae.

Jamani nisaidieni kuhusu hii hali maana kuna wakati hujikuta mpweke.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu mm sina majibu sawia ila ningekushauri ufanye mazoezi na watu wengi kama soka, mara nyng hali za kuwa peke yako huwa zinaondoka na inaweza kuwa mwanzo wa ww kuinteract na watu.

Ni muhimu sana kujuana na hao watu wanaokuzunguka 7bu binadamu siku ukipata tabu wanaweza kukuacha kabsa kwa kigezo tu "Huyo anajisikia sana":
 
Okey,nitajitahidi changamoto kubwa huwa siwaamini kabisa watu,kwa hiyo hata ikitokea nikapiga story nipo so much selective and limited na story ninazopiga. Yaani imenipelekea hata nikiudhiwa sipendi kuongea sababu huwa naamini nikikujibu utaamia zaidi yangu so huwa naugulia tu au kuamua kuondoka kabisa eneo la tukio
Pole sana mkuu mm sina majibu sawia ila ningekushauri ufanye mazoezi na watu wengi kama soka, mara nyng hali za kuwa peke yako huwa zinaondoka na inaweza kuwa mwanzo wa ww kuinteract na watu. Ni muhimu sana kujuana na hao watu wanaokuzunguka 7bu binadamu siku ukipata tabu wanaweza kukuacha kabsa kwa kigezo tu "Huyo anajisikia sana":

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni jambo au tabia ya kawaida kwa baadhi ya watu, so usijione kama una matatizo mkuu.

Kiongozi Paula Paul ebu pita hapa ushare kitu na mleta uzi.
Unajua nikiwa nasoma mada ya OP nikajikuta nawaza mbona huyu ni mimi? Nimeandika lini tena hii lol. Unajua ninachomaanisha Mla bata enh?

Hapa cha kumsaidia OP sina maana nina tatizo kama lake, labda apitie ule uzi mlionishauri atajifunza kitu.
 
Ni hali ya kawaida kama hukupata matatizo yoyote ya kisaikolojia ambayo pengine yangekufanya ujitenge na watu...

Vinginevyo jaribu kuwa karibu na watu wenye nature kama yako kiasi maana mtaongea lugha moja.ukienda vingine, utakuta unabadili lifestyle ambayo itakuletea stress zaidi
 
Ni hali ya kawaida kama hukupata matatizo yoyote ya kisaikolojia ambayo pengine yangekufanya ujitenge na watu...

Vinginevyo jaribu kuwa karibu na watu wenye nature kama yako kiasi maana mtaongea lugha moja.ukienda vingine, utakuta unabadili lifestyle ambayo itakuletea stress zaidi
hilo ni tatizo la kisaikolojia. tatizo la dunia ya sasa ni kwamba tumekua na tabia ya kuremba matatizo yaonekane kama sio matatizo. naona watu wengi humu wanasema ni hali ya kawaida. no sio hali ya kawaida. mpaka mtu anakuja kuandika uzi ameona kabisa kuna tatizo sehemu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
N vzr ukatafta wataalamu wa kisaikolojia wakusaidie kawazo maana kukaa bila
Rafik nayo n ngumu

god is good
 
Write your reply...walikufanyia kitendo gani cha kinyanyasaji ulipokuwa mdogo ? naomba usifiche useme ukweli usaidiwe

au ukiona aibu unaweza nieleza pm mi ni daktari wa saikolojia mkuu
 
Kitu muhm ni kwamba je unaenyoj na uko comfortable na hali hii?? Kama uko comfortable na una enjoy naona haina shida! Ila kama hali hata na ww hupendezwi nayo hapo ndo kuna tatizo..
 
We utakua bonge la introvert, em kaonane na psychologist muelezee matatizo yako yote uanze kupata lessons kidogo jinsi ya kuinteract na watu.

Sahihisho kidogo "kuchat na watu" sio "kuchart".
 
Kama hali hiyo uifurahii bali jirekebishe,

Mimi pia nikishamsalimia mtu huwa sitamani tena kuendelea na maongezi na mpaka nikusabahi ujue kuna kaukaribu nahata hivyo sipendi Salam ndefu na salamu yangu sio nisimame au nikae nitakusalimia huku naendelea namambo yangu au safari yangu. Nahali hii nafurahia sijawahi kuumiza kichwa kama wewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hilo ni tatizo la kisaikolojia. tatizo la dunia ya sasa ni kwamba tumekua na tabia ya kuremba matatizo yaonekane kama sio matatizo. naona watu wengi humu wanasema ni hali ya kawaida. no sio hali ya kawaida. mpaka mtu anakuja kuandika uzi ameona kabisa kuna tatizo sehemu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndio maana nikasema "ni tatizo kama alipitia vitu vyenye kumletea shida kisaikolojia hadi kujitenga na watu"..

Vinginevyo atakuwa introvert na kwa nchi kama zetu ambazo kila mtu anatakiwa kuwa the same na tofauti yoyote ni tatizo. Bhasi mtu wa hivi huchukuliwa negatively na mwisho wa siku anatengenezewa tension inayomla mwenyewe

Kingine si vyema mtu kuwa alone lakini kwa type hii ya mtu ni lazma awe makini maana Mtu mmoja atakaemuelewa ana thamani kuliko 20 ambao hawatomuelewa. Sababu kubwa ni frustration,

Atapojaribu kufit_in, wengi watamkumbusha kuwa yupo tofauti na atatengeneza inner insecurities zaidi unless abadili uhalisia wake kitu ambacho kitamcost. Yupo at 30's kumbuka, si mtoto wa primary school

Hiki ndicho nilimaanisha kwa ile comment fupi kama hukuelewa sehemu flani
 
Hilo ni tatizo linalo wakumba watu wengi wenye uwezo wa kifedha hao hata ukiwa jiran yao anakupita hata bila salamu (baadhi yao lakin)
Huwez ukawa hauna kitu na usiongee na watu utakufa njaa

Sent using GunTrigger
 
Aman iwe nanyi ndugu zangu,napenda kushare jambo langu binafsi katika maisha yangu ya kila siku. Sijajua ni tatizo au ni nini kwani tangu nikiwa bado mdogo kabisa(nikiwa shule ya msingi) sijawahi kuwa na rafiki kabisa mpaka umri huu wa thirties.

Lakini pia katika kupindi chote cha makuzi yangu nimekuwa ninaongea na kila mtu kwa sababu maalam yaani baada ya lengo langu kutimia hujikuta sitamani kuendelea kuongea na mhusika kabisa.
Pia kuna wakati huwa sijisikii kabisa kuongea na awaye yeyote labda kuchart kwa SMS tu.

Pia nina changamoto ya kutoamini MTU yoyote yule hivyo nikimkabidhi mtu kazi hujikuta nafuatilia kwa ukaribu haswaa kama vile na mie ninafanya kazi husika. Na mara nyingi nikijaribu kumuamini mtu tu lazima atazingua tu iwe kazi au mapenzi.

Sasa inafika wakati jamii inaniona nina dharau au jeuri kumbe sio kabisa kwani kuna wakati nikisalimia mtu huwa sijisikii kabisaa kuongea nae.

Jamani nisaidieni kuhusu hii hali maana kuna wakati hujikuta mpweke.

Sent using Jamii Forums mobile app
[/QUOTE
Pole sana kwa hali hii unayopitia! Kwangu ninaiangalia hali hii katika sehemu tatu ambazo ni makuzi yako, sonona (depression) na haiba yako (personality).

Inawezekana katika makuzi yako hasa ya utotoni kuna mambo ambayo uliyapitia ambayo yalikuingiza katika hali hii. Inawezekana wazazi/walezi wako walikuwa ni watu wenye misimamo mikali (strict) kama vile kukukataza kuchangamana na watoto wengine au kujichanganya na watu usio wajua! Hali hii, mara nyingine humfanya mtoto kushindwa kujiamini na kutoamini mtu. Inawezekana pia kuna jambo kubwa lililokutoea ambalo hukulipenda na kukufanya upate huzuni, hasira, nk. Matukio ya namna hii humfanya mtoto mbele ya safari kutokuamini watu.

Kujitenga na kupenda kuwa peke yako ni dalili mojawapo ya tatizo la sonona (depression).

Inawezekana pia ni haiba yako (personality) kwani wako watu ambao ni wakimya na ambao hupata energy yao kwa kuwa peke yao.

Kwavile uliandika kwa ufupi, siwezi toa conclusion kipi ni kipi!

Pole sana!
 
Sidhani kama ni tatizo,naona ni hali ya kawaida.kuna watu wanapenda kuongea na watu,wakikutana na mtu yeyote siku moja tu kashakuwa rafiki na mikusanyiko ya watu masherehe nk, yaani 'outgoing'. lakini watu wengine wao salamu inatosha wanakuwa hawana la kuongea au hawatamani kuendeleza maongezi.Pia kuwa kwenye mikusanyiko au watu wengi inakuwa shida.Binafsi sioni tatizo sababi binadamu tumeumbwa tofauti,tatizo ni wale wanaofikiri kuwa ivi ni kosa.
Tupo wengi kama wewe,naweza nikakaa peke angu mda mrefu bila mawasiliano na watu,na hali hii ikanipa 'peace' kubwa,na nikiwa na hamu kuongea na watu,ni wachache napenda kuongea nao hasa ndugu.Sina marafiki wengi,hao wachache tunajuana kwa miaka mingi sana,nao naweza nisiwapigie simu hata miezi 6,lakin siku tukiongea ni kama jana ake tulikuwa pamoja,na wengi wao hatujaonana karibu miaka mitatu.#SolidIntrovert.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni hali ya kawaida kama hukupata matatizo yoyote ya kisaikolojia ambayo pengine yangekufanya ujitenge na watu...

Vinginevyo jaribu kuwa karibu na watu wenye nature kama yako kiasi maana mtaongea lugha moja.ukienda vingine, utakuta unabadili lifestyle ambayo itakuletea stress zaidi
Yeah hapo kwenye kubadili lifestyle ni shida, Nakumbuka mama angu alikua ananipigia kelele sana kuhusu kusocialize na watu kama ndugu na majirani, lakini nikijaribu kila siku huwa naishia kuumiza hisia zangu kwa mambo yao na action zao, kifupi huwa sielew kabisa na naona kama ni complications tu kuwa karibu na kila mtu. Mim naweza kuwa karibu na watu wachache tu ambao nawaamini, hata nikiwa shule nilikua na rafiki mmoja tu, nikaja chuo nikawa nae mmoja tu, now sina rafiki kabisa naongea na mama angu(ndio kama rafiki kwangu) nawatu wengine itakapobidi kuongea. Hata sielew itakuaje natamani kusocialize ila huwa naona shida naacha.
 
Unajua nikiwa nasoma mada ya OP nikajikuta nawaza mbona huyu ni mimi? Nimeandika lini tena hii lol. Unajua ninachomaanisha Mla bata enh?

Hapa cha kumsaidia OP sina maana nina tatizo kama lake, labda apitie ule uzi mlionishauri atajifunza kitu.
Yeah at first,i thought nimerudia kusoma uzi wako then nikagundua ni mtu mwingine mwenye exactly the same same issue, nikaona ni vema nikuite labda kuna kitu mleta uzi anaweza gain kutoka kwako.

Anyway, would you mind kama utaweza kuattach link ya uzi wako hapa labda mleza uzi anaweza kupitia na kutoka na kitu.
 
Back
Top Bottom