Nini na nani hasa chanzo cha mgawo wa umeme usiokwisha?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,516
Mimi ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam. Mahali ninapoishi, kwa siku hizi za karibuni ikiwemo jana, kumekuwepo na kukatika kwa umeme kuanzia asubuhi au mchana hadi usiku. Jana, umeme ulirudi, ukakatika na kurudi tena. Mgawo wa umeme ndani ya jiji la Dar es Salaam na sehemu nyinginezo za nchi limekuwa ni tatizo sugu.

Mawaziri wanaingia na kutoka lakini mgawo uko pale pale. Nilizipongeza na naendelea kuzipongeza juhudi za Serikali ya Rais Magufuli katika kuimarisha huduma ya umeme nchini. Moja ya juhudi kubwa ni kutenganisha iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini kupata Wizara ya Madini na Wizara ya Nishati ambayo ndiyo inayosimamia umeme.

Nilifarijika niliposoma:Serikali: Tatizo la umeme mwisho Desemba 15. Tarehe 15 iliyotajwa imepita na mgawo unaendelea. Nawakaribisha hata TANESCO tutafakari pamoja swali hili: nini na nani hasa ni chanzo cha mgawo wa umeme usiokwisha? Nini kinafanyika kumaliza kadhia hii?
 
Mkuu sizan kama ni mgao...mim pia nipo Dar es salam lakin kuna zaid ya week sasa umeme haujakatika...pengine itakuwa hitilafu zilizojitokeza kwa mvua zilizonyesha jana kwa baadhi ya maeneo...vuta subra mkuu...
 
Mimi ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam. Mahali ninapoishi, kwa siku hizi za karibuni ikiwemo jana, kumekuwepo na kukatika kwa umeme kuanzia asubuhi au mchana hadi usiku. Jana, umeme ulirudi, ukakatika na kurudi tena. Mgawo wa umeme ndani ya jiji la Dar es Salaam na sehemu nyinginezo za nchi limekuwa ni tatizo sugu.

Mawaziri wanaingia na kutoka lakini mgawo uko pale pale. Nilizipongeza na naendelea kuzipongeza juhudi za Serikali ya Rais Magufuli katika kuimarisha huduma ya umeme nchini. Moja ya juhudi kubwa ni kutenganisha iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini kupata Wizara ya Madini na Wizara ya Nishati amabyo ndiyo inayosimamia umeme.

Nilifarijika niliposoma:Serikali: Tatizo la umeme mwisho Desemba 15. Tarehe 15 iliyotajwa imepita na mgawo unaendelea. Nawakaribisha hata TANESCO tutafakari pamoja swali hili: nini na nani hasa ni chanzo cha mgawo wa umeme usiokwisha? Nini kinafanyika kumaliza kadhia hii?
Mkuu ungewatag na Tanesco ingependeza.

Mimi naona tatizo ni waziri mwenye dhamana. Kwa hali hii alitakiwa kuweka wazi tatizo halisi, wanakanusha hakuna mgao lakini unashuhudia umeme ukikatika si kwa bahati mbaya ni kama ratiba fulani.
 
Mkuu sizan kama ni mgao...mim pia nipo Dar es salam lakin kuna zaid ya week sasa umeme haujakatika...pengine itakuwa hitilafu zilizojitokeza kwa mvua zilizonyesha jana kwa baadhi ya maeneo...vuta subra mkuu...
Wewe uko maeneo gani Mkuu?
 
Nchi ambayo hata Top Most Executives hawafahamu vyanzo vya matatizo mbalimbali; katu haiwezi kuwa na solution ya matatizo hayo!!

Miaka miwili iliyopita JPM aliutangazia umma kwamba tatizo la umeme linatokana na watu kufungulia maji kwenye mabwawa ya uzalishaji umeme!

Kama kawaida yetu; akapigiwa makofi kwa uwezo wake "mkubwa" wa ku-identify problems!!

Ajabu ni kwamba, tangu watu waache kufungulia maji huko Mtera na Kidatu bado hamna jipya! Au bado hawa jamaa bado wanafungulia maji huko Mtera na Kidatu!!

We're good at identifying and handling petty problems while leaving behind primary problems!
 
Mimi ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam. Mahali ninapoishi, kwa siku hizi za karibuni ikiwemo jana, kumekuwepo na kukatika kwa umeme kuanzia asubuhi au mchana hadi usiku. Jana, umeme ulirudi, ukakatika na kurudi tena. Mgawo wa umeme ndani ya jiji la Dar es Salaam na sehemu nyinginezo za nchi limekuwa ni tatizo sugu.

Mawaziri wanaingia na kutoka lakini mgawo uko pale pale. Nilizipongeza na naendelea kuzipongeza juhudi za Serikali ya Rais Magufuli katika kuimarisha huduma ya umeme nchini. Moja ya juhudi kubwa ni kutenganisha iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini kupata Wizara ya Madini na Wizara ya Nishati ambayo ndiyo inayosimamia umeme.

Nilifarijika niliposoma:Serikali: Tatizo la umeme mwisho Desemba 15. Tarehe 15 iliyotajwa imepita na mgawo unaendelea. Nawakaribisha hata TANESCO tutafakari pamoja swali hili: nini na nani hasa ni chanzo cha mgawo wa umeme usiokwisha? Nini kinafanyika kumaliza kadhia hii?

Mimi naona kama wanafanya makusudi kumuhujumu Mheshimiwa Waziri ili aje atumbuliwe huko mbele ya safari. Maana mimi haiininiingii akilini kwamba mgawo wa umeme tulikwisha sahau, halafu alll of a sudden unarudi miaka miwili baadaye, na wakati huo huo tunahitaji umeme kwa ajili ya uchumi wa viwanda. Mimi nashauri Mh. Waziri aliangalie swala hili kwa jicho pana, kuna kitu hapa, mtakuja kuniambia huko mbeleni
 
Mimi ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam. Mahali ninapoishi, kwa siku hizi za karibuni ikiwemo jana, kumekuwepo na kukatika kwa umeme kuanzia asubuhi au mchana hadi usiku. Jana, umeme ulirudi, ukakatika na kurudi tena. Mgawo wa umeme ndani ya jiji la Dar es Salaam na sehemu nyinginezo za nchi limekuwa ni tatizo sugu.

Mawaziri wanaingia na kutoka lakini mgawo uko pale pale. Nilizipongeza na naendelea kuzipongeza juhudi za Serikali ya Rais Magufuli katika kuimarisha huduma ya umeme nchini. Moja ya juhudi kubwa ni kutenganisha iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini kupata Wizara ya Madini na Wizara ya Nishati ambayo ndiyo inayosimamia umeme.

Nilifarijika niliposoma:Serikali: Tatizo la umeme mwisho Desemba 15. Tarehe 15 iliyotajwa imepita na mgawo unaendelea. Nawakaribisha hata TANESCO tutafakari pamoja swali hili: nini na nani hasa ni chanzo cha mgawo wa umeme usiokwisha? Nini kinafanyika kumaliza kadhia hii?
IPTL imekuwa frozen out bila ya kuwepo plan B.

huu ni uzwazwa wa magamba tu, hakuna namna nyingine ya kuielezea kadhia hii.
 
Mimi ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam. Mahali ninapoishi, kwa siku hizi za karibuni ikiwemo jana, kumekuwepo na kukatika kwa umeme kuanzia asubuhi au mchana hadi usiku. Jana, umeme ulirudi, ukakatika na kurudi tena. Mgawo wa umeme ndani ya jiji la Dar es Salaam na sehemu nyinginezo za nchi limekuwa ni tatizo sugu.

Mawaziri wanaingia na kutoka lakini mgawo uko pale pale. Nilizipongeza na naendelea kuzipongeza juhudi za Serikali ya Rais Magufuli katika kuimarisha huduma ya umeme nchini. Moja ya juhudi kubwa ni kutenganisha iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini kupata Wizara ya Madini na Wizara ya Nishati ambayo ndiyo inayosimamia umeme.

Nilifarijika niliposoma:Serikali: Tatizo la umeme mwisho Desemba 15. Tarehe 15 iliyotajwa imepita na mgawo unaendelea. Nawakaribisha hata TANESCO tutafakari pamoja swali hili: nini na nani hasa ni chanzo cha mgawo wa umeme usiokwisha? Nini kinafanyika kumaliza kadhia hii?
swali zuli......Mheshimiwa naomba kukujibu swali lako kama ifuatavyo kwanza katika ilani yetu ya chama hili jambo linashughulikiwa haraka ipasavyo ni kweli tumekuwa na changamoto hii ya kukatika katika kwa umeme ni kwa sababu tu ya jitihadaa ya Kiongozi wetu ,Amiri jeshi mkuu wa kuzingua VIwanda vingi sana hapa Nchini jambo ambalo linafanya mitambo yetu ya kufua umeme ielemewe zaidi....o_Oo_O Lakini nikutoe tu Hofu Mheshimiwa hilo suala tuna lishughulikia na ni juzi tu nikiwa studio nilimpigia MHeshimiwa Raisi simu na nikamjulisha hilo na akahaidi kutoa Bilion kadhaa point something hiv za kununua mitambo mipya ...Jamba la kuwaomba tu wananchi tuwe wavumilivu kama ilivyo kawaida yenu ,,ili hata Chama chetu kiendelee kuwa ni kile kile na Hatimaye ndiyo ghafra bin Vuuuu VIwanda Hivyooooooo..........:D:D:D:D:D:D:D
 
Nchi ambayo hata Top Most Executives hawafahamu vyanzo vya matatizo mbalimbali; katu haiwezi kuwa na solution ya matatizo hayo!!

Miaka miwili iliyopita JPM aliutangazia umma kwamba tatizo la umeme linatokana na watu kufungulia maji kwenye mabwawa ya uzalishaji umeme!

Kama kawaida yetu; akapigiwa makofi kwa uwezo wake "mkubwa" wa ku-identify problems!!

Ajabu ni kwamba, tangu watu waache kufungulia maji huko Mtera na Kidatu bado hamna jipya! Au bado hawa jamaa bado wanafungulia maji huko Mtera na Kidatu!!

We're good at identifying and handling petty problems while leaving behind primary problems!
Lenyewe kwa mawazo yake eti kuwa msomi Ni kukariri Kumbe bureeee Na hovyo kabisa
 
Kitu cha msingi kwanza tukubali kuwa matumizi na mahitaji ya umeme yameongezeka kwa kiasi kikubwa sana kuliko uzalishaji na usambazwaji wa umeme nchini, shirika la Tanesco limehemewa na linahitaji msaada wa kuweza kulisaidia katika kutoa huduma zake, serikali ikaribishe kampuni binafsi ambazo zitaweza kutoa huduma hii ya umeme kwa njia mbadala za kuzalisha nishati ya umeme, tunaweza kutatua hili tatizo kwa kiasi fulani kama si hivyo viwanda vingi vitategemea umeme wa majenereta na kusababisha ongezeko la bei katika bidhaa zinazozalishwa na viwanda hivyo.
TANESCO pekee hawawezi kutatua hili swala kutokana na miundo mbinu yao mingi imechoka, na watu waliyotangulia wamelitia shirika kwenye matatizo ambayo mpaka sasa ni vigumu kuyatatua. Naona kabla ya kupata viwanda vya aina yoyote naona tuwekeze kwenye viwanda vya kuzalisha umeme.
 
Mimi nakubali kuwa TANESCO imeelemewa lakini tujiulize kwa nini imeelemewa? Na hasa hawa viongozi wetu wasiwe ving,ang,nganizi wa kushikilia mitazamo yao tu kuona wao ndio pekee wapo sahihi....Kwa sasa TANZANIA ilipo sio ya kuwa na Tegemeo moja tu la umeme yaani toka Tanesco.Kumbuka kuwa hata TTCL wangeendelea na mitazamo yao tu kuwa wabinafsi kuwa wawepo wao tu tanzania leo tusingekuwa na uhuru wa kuamua njia gani nitumie kwa mawasiliano.ikumbukwe kuwa mara TTCL ilipokubali kuruhusu wengine wenye uwezo waingie kwenye kutoa huduma hii ndipo tukaanza kuona kila mtz anaaamua achague kipi kulinganisha na uwezo wake....Sasa Tanesco hadi sasa hilo wazo hawataki na hadi sasa mimi sijui kwa nini hawataki?sijui ndio kuona sisi wananchi hatuna uwezo wa kuchambua mambo au ndio wanaogopa kwamba wakiruhusu hii itasababisha Tanesco kukimbiwa na wateja kwa sababu ya huduma yao mbovu....;);) Nachukia sana mimi kuona nipo mjini lakini kwa sasa niliamua kununua soral ili angalau niwe huru kupata umeme pindi ninapouhitaji na si hawa ambao pindi unahitaji umeme wao hawakupatii pindi ambapo wewe umelala ndipo umeme unapewa...sasa sijui uamke uanze kufanya kazi muda huo ili uendane sawa na mzee wa Tanzania ya viwanda...Aiseeee Mnaboa kweli hebu ruhusu Makampuni kuleta umeme bila masharti ya kusema lazima muwe chini ya Tanesco
 
Kuna tatizo kubwa kwenye sekta ya umeme ndio maana kila siku unasikia waziri anasogeza siku mbele za kumaliza tatizo. Sasa hivi ni ngumu kujua tatizo ni nini na litakwisha lini, maana kuna sifa ya kisiasa inatafutwa kuweka tatizo bayana inatafsiriwa kama kukosesha kura na kupunguza sifa ya rais ambaye wapambe wanasema ni chaguo la Mungu kumaliza matatizo yetu. Ila nadhani Msando yupo atakuja kutoa ufafanuzi, inaonekana kwa sasa yeye ndio kapewa jukumu la kujibu hoja kwani aliowakuta ccm wamefubaa kimawazo, na Jerry Muro yeye ni mipasho tu.
 
Back
Top Bottom