Nini mtazamo wako kuhusu mama wa kambo

Nini mtazamo wako kuhusu mama wa kambo

Ablessed

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2013
Posts
4,616
Reaction score
3,502
Habari wanaMMU,

Naomba leo tujadiliane kuhusu issue hii ya mama wa kambo. Naamini humu ndani ya jamvi kuna waliowahi kuishi na mama wa kambo au wao wenyewe wamejikuta wanaitwa mama wa kambo kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.

Pia naamini kua hakuna mama anaependa kua mama wa kambo. Na hakuna mwanamke anaezaliwa ili awe mama wa kambo. Kumbe mama yeyote anaweza kuwa mama wa kambo.
Sasa kuna sifa nyingi sana tumezisikia au kuziona juu ya wamama hawa nami nitaainisha chache tu kwani wanajamvi zingine mtanisaidia
  • Ukatili
  • Ubinafsi
  • Roho mbaya
Swali langu kwenu wanajamii hivi inakuaje mama anakua na tabia hizo kwani mbona hao watoto aliowakuta nae ni watoto wake tu . Kuna wengine watoto wao walipokua watu wazima waliwatelekeza wazazi wao na mtoto wa kambo ndio akawa msaada and vice versa.
Ninajua wewe ndugu yangu unayo mengi ya kushare hebu tueleze nini mtazamo wako juu ya hili
Nawakilisha

A%20S-fire1.gif
 
ni tabia na roho ya mtu kuna mama wa kambo wanalea watoto kama wake hata watoto wenye kutoona tofauti lakini wapo wengeni mmmhhh utajuta na pia watoto wanakuwa wamejiengea mawazo kuwa mama wa kambo sio mama wanakuwa na madharau na kutokuwa na heshima kwa huyo mama kwa hiyo haya mambo yanachanganya sana kwa familia .......mie limenikumba kwa mama kambo hata ujitahidi kufanya nini bado swala la kutengwa lilibaki pale pale mwisho wa siku nitazama namna nyingine ya kuishi
 
++
Ablessed
Mama wa kambo acheni aitwe mama wa kambo tu.
Wapo wa huruma Wapo wakatili.
++
 
Last edited by a moderator:
Amini usiamini, mama wa kambo hawezi kuwatreat sawa watoto wake na wa mke mwenzie, na hii ni kama vile inakuja naturally, haiwezekani binadamu akafeel the same love strenght kwa mtoto wa tumboni na wa mwingine.

Tuseme mama na mwanae wanakuwa na very strong invisible connectin ambayo haiwezi kusimamishwa au kukatwa.

Sasa mama wa kambo kazi yake kubwa ni kuizamisha chini hii feeling ili isi'raise up its head, na hapo ndipo hasa mama wa kambo anapoonyesha busara au kiburi.

Wamama wa kambo wengine huacha moyo utawale hii feeling, matokeo yake wanafanya upendeleo wa wazi kwa watoto wao wa kuwaza, huku wakithubutu hata kuwatesa watoto wa mama mwingne.

Hutokea aghalabu sana mwanamke ambaye ni mama. wa kambo, akaweza kuishinda nafsi yake akawatreat watoto wale kwa usawa.

Kwa upande ma mtoto pia , ile invisible bond inafanya kazi ileile kama kwa mama, ndiyo maana kwa wengi hawawezi kumheshimu mama yao wa kambo, na kila atakalolifanya watalipa jina.

Hayo ni kwa mujibu wa fikra zangu.
 
Mimi nimelelewa na mama wakambo me sijui kama hawa mama wakambo wanafanya wayafanyayo kwa kupenda au ni nature ya viumbe vyote. Ilinilazimu kusoma nikiwa mtu mzima sababu ya adha za mama wakambo nimeishia darasa la tano mwaka 1991 na sikuendelea hadi mwaka 2007 nilipo anza form 1 na nina subiri tokeo la 4m6 yote sababu mama hakunipenda sababu uwezo wangu kimasomo ulikuwa juu kuliko mtoto wake ila nachofahamu hata kuku hawez kulea kifaranga cha kuku mwenziwe
 
Inategemea
Mie ni mama wa kambo na niko poa tu mbona?
 
PakaJimmy, nimekua na kaka ambae sithubutu kumuita wa kambo. Na yeye pamoja na sisi hatukujua kama ana mama yake na siku tunaambiwa (nikiwa std 5 hivi) i was like what do you mean ni mamake kaka?!?!?!.

Mama wa kambo, kama alivyo baba wa kambo anaweza kukupa treatment nzuri tu! Mama wa kambo anahitaji ushirikiano kutoka kwa familia nzima ili awe mama.

Roho mbaya ni tabia ya mtu.Lakini mama wa kambo anaweza kukataa kwa njia nyingi kutokuwa mama wa kambo. Mfano mdogo tu ni pale unapomsapraizi mkeo na mtoto wa nje tena mdogo kuliko wanae na ukamlazimishia awe mama wa kambo. Hapo inakuwa ngumu kumesa. Na ndoa ikiwa haina amani tumeshuhudia humu watu wakisema; they took it out on the kids. Huenda mtoto wa kambo anaweza kuwa an easy victim?
 
Last edited by a moderator:
PakaJimmy, nimekua na kaka ambae sithubutu kumuita wa kambo. Na yeye pamoja na sisi hatukujua kama ana mama yake na siku tunaambiwa (nikiwa std 5 hivi) i was like what do you mean ni mamake kaka?!?!?!.

Mama wa kambo, kama alivyo baba wa kambo anaweza kukupa treatment nzuri tu! Mama wa kambo anahitaji ushirikiano kutoka kwa familia nzima ili awe mama.

Roho mbaya ni tabia ya mtu.Lakini mama wa kambo anaweza kukataa kwa njia nyingi kutokuwa mama wa kambo. Mfano mdogo tu ni pale unapomsapraizi mkeo na mtoto wa nje tena mdogo kuliko wanae na ukamlazimishia awe mama wa kambo. Hapo inakuwa ngumu kumesa. Na ndoa ikiwa haina amani tumeshuhudia humu watu wakisema; they took it out on the kids. Huenda mtoto wa kambo anaweza kuwa an easy victim?
 
Last edited by a moderator:
ni tabia na roho ya mtu kuna mama wa kambo wanalea watoto kama wake hata watoto wenye kutoona tofauti lakini wapo wengeni mmmhhh utajuta na pia watoto wanakuwa wamejiengea mawazo kuwa mama wa kambo sio mama wanakuwa na madharau na kutokuwa na heshima kwa huyo mama kwa hiyo haya mambo yanachanganya sana kwa familia .......mie limenikumba kwa mama kambo hata ujitahidi kufanya nini bado swala la kutengwa lilibaki pale pale mwisho wa siku nitazama namna nyingine ya kuishi
Oooh kwa hiyo kumbe tatizo wakati mwingine linakua kwa watoto. Najua dear kua kuna baadhi ya wamama wa kambo wazuri mno lkn kwanini hawa wengine wanakua na roho mbaya hivi.
 
++
Ablessed
Mama wa kambo acheni aitwe mama wa kambo tu.
Wapo wa huruma Wapo wakatili.
++
Hivi kwanini hawa wengine wana roho mbaya hivi hebu hapo chini kuna ndugu ametoa malamiko yake juu ya mama huyu na jinsi alivyorudishwa nyuma na mama huyo . Hawa wengine wanaweza kubadilika kweli na kuwa wema
 
Inategemea
Mie ni mama wa kambo na niko poa tu mbona?
Kwanza nikupe hongera na nimefurahi sana kusikia kutoka kwako . Najua ulipo ingia ulipata changamoto kidogo . Hata hivyo hongera sana sasa hawa wanaofanya vibaya ni kwa sababu gani wanakua na roho mbaya hivi.
 
PakaJimmy, nimekua na kaka ambae sithubutu kumuita wa kambo. Na yeye pamoja na sisi hatukujua kama ana mama yake na siku tunaambiwa (nikiwa std 5 hivi) i was like what do you mean ni mamake kaka?!?!?!.

Mama wa kambo, kama alivyo baba wa kambo anaweza kukupa treatment nzuri tu! Mama wa kambo anahitaji ushirikiano kutoka kwa familia nzima ili awe mama.

Roho mbaya ni tabia ya mtu.Lakini mama wa kambo anaweza kukataa kwa njia nyingi kutokuwa mama wa kambo. Mfano mdogo tu ni pale unapomsapraizi mkeo na mtoto wa nje tena mdogo kuliko wanae na ukamlazimishia awe mama wa kambo. Hapo inakuwa ngumu kumesa. Na ndoa ikiwa haina amani tumeshuhudia humu watu wakisema; they took it out on the kids. Huenda mtoto wa kambo anaweza kuwa an easy victim?
Nimekupata dear haya uliyosema yote yana ukweli lkn kuna wengine hata uwape ushirikiano wa vipi watakua na roho mbaya tu sijui kwanini . Halafu wanakua na ubaguzi wa wazi hadi inauma.
 
Sijalelewa na mama wa kambo na bado sijawahi kuwa mama wa kambo ila nimekuwa mama wa yatima.
Ila mama yangu keshalea mama wa kambo.

Kuna kipindi ilibaki kidogo tuletewe mama wa kambo wakati baba na mama walivyotengana.
Nakumbuka kaka zangu walikuwa wakiambizana jinsi gani watakavyomfanyia visa huyo mama akiletwa. Thank God it never happened.

Ninachoweza sema, kuna aina 2 ambazo zinamchango mkubwa sana wa mahusiano ya watoto na step parents zao.
1: watoto uliowakuta, mara nyingi chuki kwa watoto hawa huwa si kubwa sana unless the wife is a real monster.
2: watoto wakiokukuta, ingawa watoto ni honest hawana kosa lkn ni wamama wachache sana (mine included) wanaoweza ishi nao vizuri.

Sasa ni nini keinachochangia (in either cases) mama akamtreat vibaya mtoto wa mumewe.
1: mume kutukuwa na uwezo wa kuiongoza familia
2: mume kuabuse mkewe ambaye naye hutafuta mnyonge wake
3: mume kuwa malaya na kutoitimizia familia mahitaji
4: mawifi kuingilia na mara nyingi kuwapenda watoto wa kambo kuliko wa ndoa
5: tabia au roho mbaya ya mke.

Sasa nini cha kufanya.
Kabla ya kumuintroduce mtoto kwa mke na mke kwa mtoto, baba ongea nao kwa undani na kwa kutulia.

Baba uwe na muda wa kutosha na familia ikiwezekana hakikisha mnasali pamoja jioni.

Mtrust mkeo, na mwambie amlee mwanao kama wake; asiache kumkanya kisa si mwanaye.

Ongea na mtoto, amuone mama wa kambo kama mama yake na amuheshimu.

Msigombane mbele za watoto na muwashirikishe wote ktk mipango yenu ya maendeleo.

Onesheni upendo kwa maneno na matendo.

Ni hayo tu Ablessed
 
Last edited by a moderator:
Mimi nimelelewa na mama wakambo me sijui kama hawa mama wakambo wanafanya wayafanyayo kwa kupenda au ni nature ya viumbe vyote. Ilinilazimu kusoma nikiwa mtu mzima sababu ya adha za mama wakambo nimeishia darasa la tano mwaka 1991 na sikuendelea hadi mwaka 2007 nilipo anza form 1 na nina subiri tokeo la 4m6 yote sababu mama hakunipenda sababu uwezo wangu kimasomo ulikuwa juu kuliko mtoto wake ila nachofahamu hata kuku hawez kulea kifaranga cha kuku mwenziwe
Pole sana rafiki . Nimefurahi kuona comment zako maana wewe ni muhusika wa moja kwa moja. Nadhani hawa wanaofanya/kuonyesha roho mbaya pengine wengine ni kwa sababu ya jina lenyewe basi huamua kuwa wakatili au ni roho mbaya tu tuseme. Lkn umetoa experience inayoumiza kwa kweli. Naamini wapo wenye tabia nzuri lkn nao ni adimu kweli kuwapata.
 
nitawalea watoto hao iwapo baba yao ana pesa ya maana baasi if dadddy is poor am sorry sorry for them
Sijalelewa na mama wa kambo na bado sijawahi kuwa mama wa kambo ila nimekuwa mama wa yatima.
Ila mama yangu keshalea mama wa kambo.

Kuna kipindi ilibaki kidogo tuletewe mama wa kambo wakati baba na mama walivyotengana.
Nakumbuka kaka zangu walikuwa wakiambizana jinsi gani watakavyomfanyia visa huyo mama akiletwa. Thank God it never happened.

Ninachoweza sema, kuna aina 2 ambazo zinamchango mkubwa sana wa mahusiano ya watoto na step parents zao.
1: watoto uliowakuta, mara nyingi chuki kwa watoto hawa huwa si kubwa sana unless the wife is a real monster.
2: watoto wakiokukuta, ingawa watoto ni honest hawana kosa lkn ni wamama wachache sana (mine included) wanaoweza ishi nao vizuri.

Sasa ni nini keinachochangia (in either cases) mama akamtreat vibaya mtoto wa mumewe.
1: mume kutukuwa na uwezo wa kuiongoza familia
2: mume kuabuse mkewe ambaye naye hutafuta mnyonge wake
3: mume kuwa malaya na kutoitimizia familia mahitaji
4: mawifi kuingilia na mara nyingi kuwapenda watoto wa kambo kuliko wa ndoa
5: tabia au roho mbaya ya mke.

Sasa nini cha kufanya.
Kabla ya kumuintroduce mtoto kwa mke na mke kwa mtoto, baba ongea nao kwa undani na kwa kutulia.

Baba uwe na muda wa kutosha na familia ikiwezekana hakikisha mnasali pamoja jioni.

Mtrust mkeo, na mwambie amlee mwanao kama wake; asiache kumkanya kisa si mwanaye.

Ongea na mtoto, amuone mama wa kambo kama mama yake na amuheshimu.

Msigombane mbele za watoto na muwashirikishe wote ktk mipango yenu ya maendeleo.

Onesheni upendo kwa maneno na matendo.

Ni hayo tu Ablessed
 
Last edited by a moderator:
nitawalea watoto hao iwapo baba yao ana pesa ya maana baasi if dadddy is poor am sorry sorry for them

What if nawe ukirest in pieces, wanao wasilelewe kwakuwa umeacha urithi wa madeni badala ya fortune?
 
watalelewa na my young sister not step mum and i have already write the issue in my will incase anything happens to me
What if nawe ukirest in pieces, wanao wasilelewe kwakuwa umeacha urithi wa madeni badala ya fortune?
 
watalelewa na my young sister not step mum and i have already write the issue in my will incase anything happens to me

Huyo kid sis wako hataolewa au hata kuzaa. And do you think atawatreat wanao the same way atakavyowatret wake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom