Ninavyoelewa lengo la program ya RPL ni kuwasaidia wafanya kazi ambao wanataka kujiendeleza kimasomo na hatimaye kusoma na kupata shahada ya kwanza.
Kwa mfano unakuta mtu ameajiriwa kwa muda mrefu na sasa anatamani kuingia chuo ili aendelee na masomo na kupata shahada. Mara nyingi huyu mtu anakuwa ana experience ya kutosha na ukimwambia aanzie certificate au diploma kiuhalisia utakuwa unamwonea.
Kwa hivyo huyu mtu anapewa mtihani kumpima na akipasi basi anapewa nafasi ya kusoma chuo.
Hii inafanyika chini ya uangalizi wa TCU na wana centre za kufanyia hii mitihani kote nchini kwa kipindi maalum.
Samahani kwa kuandika shaghalabaghala.