Nini maana ya neno UCHOCHEZI?

Nini maana ya neno UCHOCHEZI?

makesy

Member
Joined
Jan 29, 2013
Posts
75
Reaction score
32
KWANZA SALAM,

Nimejiuliza bila majibu nini maana ya uchochezi? spika makinda amekataa hotuba ya kambi ya upinzini isiingie kwenye hansad kwakuwa eti imejaa uchochezi sasa nikawa najiuliza uchochezi ni kusema matukio yaliyofanywa na serikali lakini hayawafurahishi wananchi?

Hivi ukisema mulongo aliwatishia waandishi wa habari kwa kuwaambia wakiandika habari za kumkashifu kiongozi wanaweka maisha yao rehani huo ni uchochezi?

Uukisema serikali ilimuua Mwangosi ni uchochezi?
Ukusema usalama wa taifa walimteka Ulimboka huo ni uchochezi?

NAOMBA WAELEWA ZAIDI WANISAIDIE, HATATA WALE WANACCM MLIOKO HAPA JAMVINI MNISAIDIE
 
Hivi kuna mtu anayefurahia kuambiwa ukweli? hata wewe uliyeleta uzi wako huu, unafurahia unapoambiwa ukweli?
 
Ndg yangu kwa ccm maana ya uchochezi ni kusema ukweli. ukisema tu ukwel wakagungua umewafungua wananchi kujua ukweli lazima uitwe mchochezi
 
Wahenga waliposema "Ukweli Unauma". Siku za nyumba ilishazoeleka uwongo kufanywa ukweli, na ukweli kufanywa uongo.
 
KWANZA SALAM
Nimejiuliza bila majibu nini maana ya uchochezi? spika makinda amekataa hotuba ya kambi ya upinzini isiingie kwenye hansad kwakuwa eti imejaa uchochezi sasa nikawa najiuliza uchochezi ni kusema matukio yaliyofanywa na serikali lakini hayawafurahishi wananchi??hivi ukisema mulongo aliwatishia waandishi wa habari kwa kuwaambia wakiandika habari za kumkashifu kiongozi wanaweka maisha yao rehani huo ni uchochezi?? ukisema serikali ilimuua Mwangosi ni uchochezi?ukusema usalama wa taifa walimteka Ulimboka huo ni uchochezi?
NAOMBA WAELEWA ZAIDI WANISAIDIE, HATATA WALE WANACCM MLIOKO HAPA JAMVINI MNISAIDIE

UCHOCHEZI kwa jinsi navyofahamu mimi ni
Hali ya kushawishi watu, kundi la watu au mtu kwa njia ya kuwahadaa au kumhadaa au kudanganya kupandikiza chuki ili kuhamasisha kufanya jambo fulani la kudhuru, kuharibu mali au kuvunja sheria yeyote ile kwa lengo la kuharibu taratibu fulani. lakini kwa nchi yenye utawala wa kimsongo wa mawazo na hofu ya kutolewa madarakani Uchochezi kwao ni kuwaeleza wananchi maovu yanayofanywa na serikali yao ili wachukue njia stahiki za kuiwajibisha.

Mfano mzuri umeonyeshwa jana bungeni mimi sikuona kama ni uchochezi kuwaeleza wanachi ukweli kuhusu serikali inavyofanya kupitia vyombo vyake ya usalama. nani asiyejua kama Mwangosi aliuwawa na polisi, au nani asijua kama Dr Ulimboka alitekwa na usalama wa taifa na kufanyiwa unyama sasa ukisema hivyo serikali inaita uchochezi.
 
Itafika mahali hata kudai maji kwa wanavijiji itakuwa uchochezi maana hawana!
 
Wala tusiwe na shaka haya ni mapambano ya kifikra....fikra dhalimu dhidi ya fikra sahihi za ukombozi na kujitambua!!..

Hebu tufikiri kidogo. Msigwa kama msemaji mkuu wa kambi ya upinzani wizara ya maliasili alisema sana kuhusu ujangili wa tembo wetu na kumhusisha moja kwa moja katibu mkuu wa CCM Ndg Kinana.Kama kawaida wabunge wa CCM waling'aka wakamwita ni mchochezi, anamtuhumu mtu ambaye hayupo bungeni na hivyo hawezi kujitetea!!

Je, haya nayo ya Sugu serikali haiwezi kujitetea? Si ipo bungeni kwa nini isijitetee? Je, si ni bora wakatunga kanuni ya kusema jambo/mambo ambayo wanataka kusikia tu? Na, je tutaweza kuyafanya masikio yetu na macho kuwa selective kwamba tuone na tusikie tunayotaka tu?......tuchague kuwa vipofu au viziwi basi!...hii ndiyo option pekee salama kwao.....Otherwise tuache fikra zigongane na kukwaruzana ili kupata mwafaka na hiki ndicho chanzo cha maendeleo yeyote ya kweli!!!!

Hapa wanajamii hakuna cha uchochezi wala nini, ni uwoga wa watawala wetu tu, ni uwoga wa CCM na serikali yake tu na kwa kweli wanamfanya huyu mama Spika Makinda, mwana CCM mwenzao akiongoze chombo hicho katika mazingira mugumu sana bila sababu na wao bila kujua wanamfanya huyu mama sometimes aonekane kama zezeta....

Ni bora wakaacha bunge kikawa chombo huru cha mawazo ya wabunge.....wasiharibu Bunge letu kwa kuwafanya wabunge wetu wawe wanasema yanayowafurahisha watawala tu
 
Aliye Lala hapendi kuamshwa...!! "Sema kweli japokuwa ina uchungu"
 
Ndg. CCM wako sawa kilichokuwa kikisemwa ni uchochezi. Maana ndogo tu, uchochezi ni kusema au kufanya jambo ama kutumia kauli fulani za kuibua hisia kali za wasikilizaji, mara zote uchochezi ni jambo baya! Sasa CCM hawatofautishi jambo hili baya na UKWELI ambao daima ni mzuri. Kwahiyo ukweli mzuri wa viongozi wetu wazalendo unabatizwa uchochezi kwasababu utawaamsha watu hasa wasiojua kujua SIRIKALI yetu ilipowafikisha! Kwa namna hiyo ukweli utakuwa uchochezi. Kiti cha spika siku hizi ni mtetezi wa serikali, bajeti zinapitishwa hata kwa lazima! Balaaa
 
Kumekua na hofu nyingi ya watu kukamatwa kamatwa hasa pale wanapotoa kauli zinazoonekana na kutafsiriwa kua kinyume na na msimamo na mtazamo wa mheshmiwa Rais, kwa sababu hiyo niwaombe wenye maana sahihi ya neno lugha za kichochezi ili tukiwa na mawazo mbadala tuyawasilishe bila mashaka.
 
Uchochezi - ..enye lengo la kuleta au kuhamasisha vurugu au uvunjifu wa amani.

Labda waje wataalam wa lugha!
 
Tuache kazi zetu tuanze kujadiri uchochezi ili kumchochea nani? kwani shughuri zingine za kufanya hazipo?
 
Kumekua na hofu nyingi ya watu kukamatwa kamatwa hasa pale wanapotoa kauli zinazoonekana na kutafsiriwa kua kinyume na na msimamo na mtazamo wa mheshmiwa Rais, kwa sababu hiyo niwaombe wenye maana sahihi ya neno lugha za kichochezi ili tukiwa na mawazo mbadala tuyawasilishe bila mashaka.
Unataka umchochee nani mkuu?
Anyway, mii nafahamu lugha za kichochezi ni hizi hapa
1. kuchochea moto
2. kuchochea ugonvi
3. kuchochea mapenzi
4. kuchochea ushindani
N.K.
Sasa wewe ulitaka uchochezi upi? kwa kifupi maana ya uchechezi ni uhamasishaji
 
Tangu serukali hii ya awamubya tano iingie madarakani wamekuwa wanapenda sana kutumia neno 'uchochezi' wanapopambana na upinzani!

Badala ya kujibu hoja kwa hoja wao wanskimbilia kuwaita polisi kuwahoji na kuwafungulia kesi za uchochezi!

Tumezoea kusikia sana katika nchi za wenzetu, ambao hawaheshimu demokrasia na utawala wa sheria, wanasiasa na wanaharakati na vyombo vya habari wakimatwa na kufunguliwa kesi za uchochezi. Sasa naona hili wimbi limeshika kasi pia hapa kwetu katika awamu hii. Ni kitu ambacho hakijazoeleka katika nchi hii!

Leo ningependa kujua nini maana ya hii dhana yauchochezi!
Ni nini kina determine kwamba huu ni uchochezi na huu si uchochezi? Unawezaje kudhibitisha mahakamani kwamba kauli fulani ninya kichochezi? Je, vitabu vyetu vya sheria vinadefine vipi hii dhana ya uchochezi? Ni waksti gani ukosoaji utaonekana wa kawaida na ni wakatibgani unakuwa wa kichochezi!
Katika nazingira ya vyama vingi ambapo kuna ushindani wa vyama ambapo ni lazima kuonesha mapungufu ya serikali, huku hakuwezi kutafsiriwa kuwa ni kuchochea wananchi kuichukia serikali yao?

Dhana ya uchochezi bado inafaa kutumika katika demokrasia ya vyama vingi?
 
Chukua petroli halafu imwage kwenye moto mdogo, utaona utaelewa kuchochea maana yake.
 
Chukua petroli halafu imwage kwenye moto mdogo, utaona utaelewa kuchochea maana yake.
Ukimaanisha kuna fukuto la chinichini nchini ambalo halipaswi kumwagiwa petroli lusije kulipuka kabisa?
 
Back
Top Bottom